ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
HII NDIO TOFAUTI YETU:
RIDHIWANI, sijajua vigezo vilivyotumiwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (The Tanzania Education Authority) kuwapata wahamasishaji wa kuchangia mfuko wa kununulia vifaa kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum (students with disabilities) na hata pia mazingira ya kuandalia matangazo haya ambayo yanaonyesha hali halisi ya utofauti wa maisha katika familia za watanzania (ukiwa katika ofisi ambayo ina kila dalili ya neema na vitendea kazi).
Labda pengine katika hali njema kama hapo ulipo, ebu jaribu pia kutupa jicho lako binafsi huko chini ili kuona tofauti ya matabaka tunayojaribu kuyatengeneza katika nchi hii ambayo ina zaidi ya miaka arobaini ya kujitawala, ebu waone pia hawa ambao ni watanzania kwa kuzaliwa na wamekuwa wakiitumaini Serikali hii hii ambayo inawawezesha wengine kuwa na hali bora hata ya kuweza kuonekana katika mazingira ya gharama: ZUNGUMZA NASI KWA MZINGIRA HALISI YA KITANZANIA ILI IMAANISHE KWELI TUPO PAMOJA NA "KWA PAMOJA IWEZEKANE KWA KILA MMOJA WETU KUFURAHIA MATUNDA YA UHURU WETU KWA MAANA YA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA!!":
Wanafunzi wa shule ya Msingi Kinole, katika halmashauri ya wilaya ya Morogoro, wakiwa wamekaa chini kutokana na uhaba mkubwa wa madawati unaoikabili shule hiyo
Mwalimu, Albert Juakali wa shule ya msingi Iboma iliyopo kijiji cha Udinde Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya akifundisha wanafunzi wa darasa la kwanza chini ya Mti wa Mbuyu
Shule ya Msingi Juhudi - Kigoma Vijijini, Tanzania
RIDHIWANI, sijajua vigezo vilivyotumiwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (The Tanzania Education Authority) kuwapata wahamasishaji wa kuchangia mfuko wa kununulia vifaa kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum (students with disabilities) na hata pia mazingira ya kuandalia matangazo haya ambayo yanaonyesha hali halisi ya utofauti wa maisha katika familia za watanzania (ukiwa katika ofisi ambayo ina kila dalili ya neema na vitendea kazi).
Labda pengine katika hali njema kama hapo ulipo, ebu jaribu pia kutupa jicho lako binafsi huko chini ili kuona tofauti ya matabaka tunayojaribu kuyatengeneza katika nchi hii ambayo ina zaidi ya miaka arobaini ya kujitawala, ebu waone pia hawa ambao ni watanzania kwa kuzaliwa na wamekuwa wakiitumaini Serikali hii hii ambayo inawawezesha wengine kuwa na hali bora hata ya kuweza kuonekana katika mazingira ya gharama: ZUNGUMZA NASI KWA MZINGIRA HALISI YA KITANZANIA ILI IMAANISHE KWELI TUPO PAMOJA NA "KWA PAMOJA IWEZEKANE KWA KILA MMOJA WETU KUFURAHIA MATUNDA YA UHURU WETU KWA MAANA YA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA!!":
Wanafunzi wa shule ya Msingi Kinole, katika halmashauri ya wilaya ya Morogoro, wakiwa wamekaa chini kutokana na uhaba mkubwa wa madawati unaoikabili shule hiyo
Mwalimu, Albert Juakali wa shule ya msingi Iboma iliyopo kijiji cha Udinde Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya akifundisha wanafunzi wa darasa la kwanza chini ya Mti wa Mbuyu
Shule ya Msingi Juhudi - Kigoma Vijijini, Tanzania
Last edited by a moderator: