OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 428
Katika hili nimeamua kumfunga paka kengere,liwalo na liwe hata kama namgusa mtoto wa mpendwa Rais Jakaya Kikwete,Ridhiwan Kikwete
Niseme Wazi kiwa mimi kuwa mimi ni shabiki wake damudamu kiasi cha kuwa tayari kumwaga damu yangu kupambana na wale wanaomwonea wivu kwa ulaji anaoupata kutokana na kuzaliwa na kijiko cha dhaabu kwenye nasaba ya kifalme na Mzee kukupigia ''vuvuzela'' ili hapo baadaye naye aule.
Binafsi sioni ubaya kwa mwana kubebwa na baba au mwana kumpigia mdogo mdogo baba hata kuanza kujaribu kuvaa viatu vyake akiwa hai kama anavyofanya kikwete na Mwanae.
Sioni ubaya ukizingatia kuwa anachofanya Kikwete kwa Ridhwan ni kama walivyofanya watangulizi wengine kama vile mzee Abeid mwinyi,Hassan Mwinyi,John Malecela,Yusuph Makamba na wengine ambao wemevitengenezea vitegemezi vyao ulaji kwenye siasa.
Maana huo ni mfumo mzuri tuliokopa kwa wahindi ambao wametutawala kiuchumi nchini.Bila hiyo wale watoto wa wakubwa waliotuhumiwa hata kughushi wangekuwa wameishachukuliwa hatua.Lakini ni nyani gani anaweza kumsulubu ngendere wakati wote wala mahindi?
Sina nia ya kumtaka Ridhwan asijihusishe na mambo ya siasa wala mengine ya kijamii,lakini kasi ya mtoto huyo wa Rais inatisha na akiendelea hivyo ,gharama zake mambo anayofanya sasa ,zitabebeshwa kwa Rais kikwete tena kwa kuanzia kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Nimeamua kumwambia ukweli kwa sababu kubwa mbili za msingi,Mosi ni kwamba yeye ni mtoto wa Rais aliyoko madarakani na kama atashinda tena kwenye uchaguzi mkuu ujao .basi anaweza kuendelea ingawa safari hii,so rahisi kwake kushinda kama alivyofikiri.
Kwa Kutambua kwamba Ridhwan ni mtoto wa Rais ,Jamii inamwona kama kioo cha jamii kwa kila jambo alifanyalo.
Pili NimeMUA Kimwambia yanayozungumzwa hata na makada wenzake wa CCM ,kwani naamini hakuna anaweza kumwambia ukweli mtoto huyo wa Rais kutokana na tabia ya unafiki ya baadhi ya watu wa CCM ya kujikomba na kufikia hata hatua ya kulamba iatu vya wakubwa wa aina ya Ridhwan.
Nianze kwa kumpongeza kwa kazi kubwa kuhangaika kusaka wadhamini wa mzee wa Nchi nzima haikuwa kazi Nyepesi.Ni heshima na jukumu la pekee kwake na kwa vijana wote wa Taifa hili.
Pili Nimpongeze pia kwa kufanikisha Kimezengwe uchaguzi mkuu wa klabu ya soka ya Yanga hivi karibuni .Malalamiko yanaoendelea sasa dhidi yake kuhusu uchaguzi huo.
Nawajua vizuri sana wana yanga jinsi walivyo mahodari kuzungumza kwani baadhi wamefikia hatua ya kuamini kwamba Ridhwan alipata Maelekezo ya baba Yake (Rais Kikwete) ambaye naye ni Mnazi wa Yanga Kuhakikisha wagombea fulani hawapati nafasi Yanga.
Leo hii uchaguzi huo unalalamikiwa sana na sana baadhi ya wanachama wanatishia kwenda mahakamani na lawama nyingi zinaelekezwa kwa Ridhwan.
Yanayozungumzwa na kundi la wanayanga wanaopinga mgombea wao kufanyiwa fitna hadi kujitoa ,wanasema eti serikali ilihingilia uchaghuzi na wakati mwingine wanashindwa kumungunya maneno na kusema Ikulu ilihingilia Kati uchaghuzi wao.
Hii maan yake ni kwamba wamefika hatua ya kuamini Baba (Kikwete) kamtuma mwana kusimika viongozi anaowapenda wakati yawezekana Ridhwan aliyoyafanya hayana hata chembe ya mkono wa Rais Kikwete
Tatu nimpongeze kwa kuchangia kwa kiasi kikubwa kuachia ngazi kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (uvccm) Masauni Yusuph Masauni hatimaye kiyi hicho sasa kinakaliwa na rafiki yake wa karibu aliyeemuunga mkono kwenye harakati za kuwania nafasi ya uenyekiti wa UVCCM Beno malisa ,kabla baba yake kuamuru nafasi hiyo iende Zanzibar.
Ridhwan ni shaidi katika hilo kwani mengi yaliandikwa kwenye vyombo vya habari juhu ya kuhusika kwake na mpango wa iliyomngoa masauni Madarakani.
Ridhwani mwenyewe amepata kukaririwa na baadhi na baadhi ya vyombo vya habari akikanusha,lakini wapo wanaoamini hasa wajumbe wa Baraza kuu UVVCCM Kutoka Zanzibar kwama alihusika kuwapoka kiti hicho.kama anabisha ajaribu kwenda Zanzibar.
Binafsi naomba nikupe ushauri wa bure.Ridhwan hebu angalia mifano ya watoto wa viongozi waliopita.wapo ambao hawakijulikana hata kwa majna yao na hili lilitokana na wao kutokuwa mbele kwenye shughuli za Baba zao walipokuwa Marais.
Ridhwan leo uko mbele ya kila kitu cha baba yako ,utadhani wewe ni Rais mdogo wa Nchi .wapo watu wanaohoji ukwasi wako wa sasa unaokufanya usione umuhimu wa kazi yako uliosomea ya kuvaa jihoo la uwaki naa kubishana na majaji mahakamani kutetea watuhumiwa.
Nakushauri ,achana na mambo hayo ,Vinginevyo utamponza Baba yako na kama unabisha subiri muda si Mrefu utajua ninacholisema
Niseme Wazi kiwa mimi kuwa mimi ni shabiki wake damudamu kiasi cha kuwa tayari kumwaga damu yangu kupambana na wale wanaomwonea wivu kwa ulaji anaoupata kutokana na kuzaliwa na kijiko cha dhaabu kwenye nasaba ya kifalme na Mzee kukupigia ''vuvuzela'' ili hapo baadaye naye aule.
Binafsi sioni ubaya kwa mwana kubebwa na baba au mwana kumpigia mdogo mdogo baba hata kuanza kujaribu kuvaa viatu vyake akiwa hai kama anavyofanya kikwete na Mwanae.
Sioni ubaya ukizingatia kuwa anachofanya Kikwete kwa Ridhwan ni kama walivyofanya watangulizi wengine kama vile mzee Abeid mwinyi,Hassan Mwinyi,John Malecela,Yusuph Makamba na wengine ambao wemevitengenezea vitegemezi vyao ulaji kwenye siasa.
Maana huo ni mfumo mzuri tuliokopa kwa wahindi ambao wametutawala kiuchumi nchini.Bila hiyo wale watoto wa wakubwa waliotuhumiwa hata kughushi wangekuwa wameishachukuliwa hatua.Lakini ni nyani gani anaweza kumsulubu ngendere wakati wote wala mahindi?
Sina nia ya kumtaka Ridhwan asijihusishe na mambo ya siasa wala mengine ya kijamii,lakini kasi ya mtoto huyo wa Rais inatisha na akiendelea hivyo ,gharama zake mambo anayofanya sasa ,zitabebeshwa kwa Rais kikwete tena kwa kuanzia kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Nimeamua kumwambia ukweli kwa sababu kubwa mbili za msingi,Mosi ni kwamba yeye ni mtoto wa Rais aliyoko madarakani na kama atashinda tena kwenye uchaguzi mkuu ujao .basi anaweza kuendelea ingawa safari hii,so rahisi kwake kushinda kama alivyofikiri.
Kwa Kutambua kwamba Ridhwan ni mtoto wa Rais ,Jamii inamwona kama kioo cha jamii kwa kila jambo alifanyalo.
Pili NimeMUA Kimwambia yanayozungumzwa hata na makada wenzake wa CCM ,kwani naamini hakuna anaweza kumwambia ukweli mtoto huyo wa Rais kutokana na tabia ya unafiki ya baadhi ya watu wa CCM ya kujikomba na kufikia hata hatua ya kulamba iatu vya wakubwa wa aina ya Ridhwan.
Nianze kwa kumpongeza kwa kazi kubwa kuhangaika kusaka wadhamini wa mzee wa Nchi nzima haikuwa kazi Nyepesi.Ni heshima na jukumu la pekee kwake na kwa vijana wote wa Taifa hili.
Pili Nimpongeze pia kwa kufanikisha Kimezengwe uchaguzi mkuu wa klabu ya soka ya Yanga hivi karibuni .Malalamiko yanaoendelea sasa dhidi yake kuhusu uchaguzi huo.
Nawajua vizuri sana wana yanga jinsi walivyo mahodari kuzungumza kwani baadhi wamefikia hatua ya kuamini kwamba Ridhwan alipata Maelekezo ya baba Yake (Rais Kikwete) ambaye naye ni Mnazi wa Yanga Kuhakikisha wagombea fulani hawapati nafasi Yanga.
Leo hii uchaguzi huo unalalamikiwa sana na sana baadhi ya wanachama wanatishia kwenda mahakamani na lawama nyingi zinaelekezwa kwa Ridhwan.
Yanayozungumzwa na kundi la wanayanga wanaopinga mgombea wao kufanyiwa fitna hadi kujitoa ,wanasema eti serikali ilihingilia uchaghuzi na wakati mwingine wanashindwa kumungunya maneno na kusema Ikulu ilihingilia Kati uchaghuzi wao.
Hii maan yake ni kwamba wamefika hatua ya kuamini Baba (Kikwete) kamtuma mwana kusimika viongozi anaowapenda wakati yawezekana Ridhwan aliyoyafanya hayana hata chembe ya mkono wa Rais Kikwete
Tatu nimpongeze kwa kuchangia kwa kiasi kikubwa kuachia ngazi kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (uvccm) Masauni Yusuph Masauni hatimaye kiyi hicho sasa kinakaliwa na rafiki yake wa karibu aliyeemuunga mkono kwenye harakati za kuwania nafasi ya uenyekiti wa UVCCM Beno malisa ,kabla baba yake kuamuru nafasi hiyo iende Zanzibar.
Ridhwan ni shaidi katika hilo kwani mengi yaliandikwa kwenye vyombo vya habari juhu ya kuhusika kwake na mpango wa iliyomngoa masauni Madarakani.
Ridhwani mwenyewe amepata kukaririwa na baadhi na baadhi ya vyombo vya habari akikanusha,lakini wapo wanaoamini hasa wajumbe wa Baraza kuu UVVCCM Kutoka Zanzibar kwama alihusika kuwapoka kiti hicho.kama anabisha ajaribu kwenda Zanzibar.
Binafsi naomba nikupe ushauri wa bure.Ridhwan hebu angalia mifano ya watoto wa viongozi waliopita.wapo ambao hawakijulikana hata kwa majna yao na hili lilitokana na wao kutokuwa mbele kwenye shughuli za Baba zao walipokuwa Marais.
Ridhwan leo uko mbele ya kila kitu cha baba yako ,utadhani wewe ni Rais mdogo wa Nchi .wapo watu wanaohoji ukwasi wako wa sasa unaokufanya usione umuhimu wa kazi yako uliosomea ya kuvaa jihoo la uwaki naa kubishana na majaji mahakamani kutetea watuhumiwa.
Nakushauri ,achana na mambo hayo ,Vinginevyo utamponza Baba yako na kama unabisha subiri muda si Mrefu utajua ninacholisema