...Kuna kila sababu ya kutilia mashaka "utajiri wa kutupwa" wa Bwana Mdogo Ridhwan - mtoto wa Mheshimiwa Jakaya bin Mrisho wa Kikwete kutoka Msoga. Ridhiwan, kwa ujumla ni mtoto mdogo katika umri wa kazi na kinyume chake kijana huyu ametokea kumiliki utajiri mnono unaotia mashaka. Pamoja na sababu nyingi zifuatazo ni sehemu ya kutilia mashaka juu ya utajiri wake.
- Anamiliki akaunti zaidi ya mbili kwenye benki kubwa nchi ambazo hajui "salio" lake; hii inaonyesha kijana huyu akaunti zake ni nono na zimeshiba hasa!
- Anaonekana akitanua matanuzi ya gharama kubwa pamoja na kutumia magari ya kifahari na yenye thamani kubwa kuliko uwezo wake!
- Ana uhusiano na wafanyabiashara wenye kumiliki biashara nene na kubwa zenye mafungamano ya fedha nyingi na chafu!
- Baba yake (JK) anamtumia kama "chaka" la kuendesha biashara kwa mgongo wa IKULU huku akipewa "ulinzi = immunity" na baba yake!
- Amejenga "kiburi" na "jeuri" ya fedha hata kuwatukana watu na au kuwafanyia hila na mizengwe kwa utumizi wa fedha chafu!