Richmond ni kampuni ya kitapeli na hewa!

MKWECHE

JF-Expert Member
Apr 8, 2011
299
64
Wana JF
Kuna swala moja limekuwa likinikanganya sana katika ufuatiliaji wangu wa habari za Kampuni ya Richmond Development na Dowans.Swala lenyewe ni Kuwa Richmond Development ni kampuni ya Kitapeli na Hewa!
Ukiendelea kusoma habari mbalimbali juu ya sakata hili hasa za siku za karibuni unakuta Makampuni ya Richmond na Dowans yameshafunguliana kesi ya Madai kwenye Mahakama moja huko Marekani na kesi inarindima!
Kikubwa hapa Kinachonizubaisha katika haya Matukio,Je inakuwaje Richmond kampuni hewa na ya Kitapeli ifungue kesi Mahakamani, tena Mahakama za USA(Kwa watu Mahiri na Makini ktk Mambo yao)!
Jamani U-hewa wa Richmond upoje katika hili au ni ile hewa ya Jina!Au ni Hewa Tanzania Marekani Si Hewa,
Navoisikiaga Marekani(Sijawahi Fika) Huwa ni nchi ya watu wa ukweli na hawafanyagi mzaha na Fedha za Umma(walipa Kodi) hata Kidogo. Sasa inakuwaje wanakubali Makampuni hewa Yafungue kesi ya Madai kwenye ardhi yao afu kwa jambo TATA lililofanyika nchi ya Dunia ya Mwisho!
Jamani hapo kidogo jambo hili Linawekwaje sawa kwangu na Kisheria LinaHudumiwaje?Ma-Thinker wa JF!
 
Back
Top Bottom