akelu kungisi
Senior Member
- Apr 2, 2012
- 115
- 19
Jana usiku katika kipindi cha malumbano ya hoja kinachorushwa na ITV, mwanaharakati na mzalendo wa ukweli Ndg Renatusi Mkinga aliendelea kudhihirisha na kuonyesha uwezo katika kujenga hoja zenye uzalendo na ukombozi kwa nchi yake.
Si jana tu, Ndg Renatusi Mkinga ni maranyingi kwa muda wa miaka mingi amekuwa akiwajambisha magamba kwa hoja zake mara apatapo nafasi ya kufanya hivyo! Mengi yanaweza kusemwa kuhusu yeye, lakini lililo kubwa zaidi ni kumuomba aanze kufanya maandalizi ya mapema katika harakati za kuingia mjengoni mwaka 2015. Huyu jamaa nina aminim kuwa kama atafanikiwa kuingia pale basi magamba watamkoma!
Nakumbuka Lisu kabla hajawa mbunge, naye alikuwa kama huyu mzee Mkinga, nionavyo mimi mawazo yake yatakuwa na maana zaidi iwapo atayatoa katika mfumo sahihi unaotambuliwa kisheria( bunge) kuliko huko aliko kwani magamba wanamuona mpayukaji.
Renatusi kama unachungulia humu JF naomba uyachukue na kuyapima mawazo yangu juu yako then yafanyie kazi ikibidi.
Si jana tu, Ndg Renatusi Mkinga ni maranyingi kwa muda wa miaka mingi amekuwa akiwajambisha magamba kwa hoja zake mara apatapo nafasi ya kufanya hivyo! Mengi yanaweza kusemwa kuhusu yeye, lakini lililo kubwa zaidi ni kumuomba aanze kufanya maandalizi ya mapema katika harakati za kuingia mjengoni mwaka 2015. Huyu jamaa nina aminim kuwa kama atafanikiwa kuingia pale basi magamba watamkoma!
Nakumbuka Lisu kabla hajawa mbunge, naye alikuwa kama huyu mzee Mkinga, nionavyo mimi mawazo yake yatakuwa na maana zaidi iwapo atayatoa katika mfumo sahihi unaotambuliwa kisheria( bunge) kuliko huko aliko kwani magamba wanamuona mpayukaji.
Renatusi kama unachungulia humu JF naomba uyachukue na kuyapima mawazo yangu juu yako then yafanyie kazi ikibidi.