REINFRED MASAKO kugombea Ulanga Magharibi

Masako ameshajifanyia nini yeye mwenyewe na familia yake mpaka sasa anadhani anaweza kuwafanyia chochote wengine? Yeye aseme amegundua kuwa ubunge ni ajira yenye kulipa vizuri, na mara nyingine Rais anaweza kukuongeza ulaji - ama uwaziri, ukuu wa mkoa au wilaya, ubalozi, uenyekiti wa bodi nk. Umefika wakati wanasiasa wa Tanzania waache usanii, wawe wakweli. Hakuna anayeomba kugomembea ubunge kwa tiketi ya CCM, anayefanya hivyo kwa 'sababu ana nia ya kumfanyia yeyote chochote.
 
Nimegundua kwa nini nchi yetu haiendelei. Watu wenye uwezo wa kufikiria mambo kwa kina jinsi ya kuliendeleza Taifa wanaogopa kujitokeza kugombea nafasi hizo kwa sababu ya watu wenye vichwa butu kuendekeza mambo ya Bagamoyo. Hawa wanabagamoyo wakishapata uongozi hawajui la kufanya inakuwa kama mbuzi kafunguliwa uwanja wenye majani mengi na mazuri kila akila hapa anaona mwenzake pale anafaidi na yeye kumbilia akifika pale anaona hata yule wa pale anafaidi anajikuta kazunguuka uwanja wote bila kufanya la maana. Hawa watu wanaoendekeza bagamoyo ni kama mtu asiyejua kuendesha gari halafu anapewa funguo ya gari na kuambiwa tupeleke matokeo yake anajifanya anajua na kutumbukiza Taifa kwenye mtaro. Watu wenye uwezo jitokezeni. Vinginevyo tusipige kelele za kuongozwa na vihiyo wakati ndiyo wanaojitokeza kuomba kuchaguliwa.

Ushauri kwa JK: Najua atatangazwa mshindi na tume ya uchaguzi iwe isiwe, cha kufanya ni kuwa miaka mitano ya mwisho itadefine uongozi wake kama ni mjasiliamali ama mpiganaji, nakuomba acha uswahiba kama fadhila umeshazilipa sasa tuwafanyie wananchi Kazi, mawaziri wengi si ufanisi wa serikali bali ni kuongezea mzigo wananchi. Nakuomba Chagua wabunge wako 10 kama katiba inavyokupendelea miongoni mwa watu wasio wanasiasa, I mean wapenda maendeleo bila kujali itikadi zao wape uwaziri hao tu, tuwe na mawaziri wasiozidi 15. Wanaogombea ubunge wote ni walafi hawana la ziada kuwapa uwaziri ni kupoteza nafasi za bure. Chagua watu kama kina Mwanakijiji, Ulimwengu, J.Mashaka na wengineo wape nafasi ya kuonesha vipaji vyao bila kujali "UWENZETU" ndani ya CCM. Huu ndiyo unaididimiza nchi.
 
hebu tumwache naye ajaribu bahati yake,you never know anaweza kula shavu astaafu vizuri si unajua tena umri umesogea...
 
Ninaamini kuwa mzee masako hajashauriwa vizuri katika hili, hafanani na siasa za ulanga west ila ni vema tuone msuguano huu 2010 utaifundisha nini jamii yetu. As far i know waliojitokeza either hawana agenda zinazoendana na mahitaji ya jimbo, wamekosa hoja za kushawishi umma wao kwa sababu agenda kuu kwao ni mbunge aliyepo, wanamtuhumu kuwa hajafanya lolote, amekaa muda mrefu, amezeeka n.k lakini wanasahau ni ccm hiyohiyo ndio iliyouza ilani ambayo wao wanaiponda kutofanikiwa lakini wanaitaka tikiti hiyo hiyo, ccm wanasema wako vizuri kwani wana mafanikio ya kujivunia jimboni!!!

Waliojitokeza kwa sasa ni vijana simon ngonyani yuko ktk project fulani za maji hapo wizarani, yassin njayagha- kijana aliyekuwa marekani na kutambulishwa kwa rais wetu muungwana jk 2006 kama rais wa watz wanaoishi Amerika kwa influence ya mbunge wa sasa, dr.romuald mbwasi-yuko na mradi maduka madogomadogo ya dawa unao supportiwa na wamerekani, mponda hajji wa wizara ya afya, na sasa tunae mshikaji masako, kazi kwerikweriii.

Nway, siasa ina wenyewe na sisi tunafurahi kuwa hawa jamaa nao wakiingia ktk mchakato kwa mara ya kwanza, tatizo langu ni kwa vijana wenzangu, wameingiza siasa za mapesa sasa sijajua nani yuko nyuma yao kiufadhiri na kama watazirejesha vipi hizi fedha wazitumiazo.

Kila la heri 2010 ulanga west
 
Jana nimemsoma kaka kiyawike naye naye ametangaza nia ndani mwananchi na wamerudia nipashe. Kiyawike ni mhitimu mzamili mwaka huu na ni mkaguzi fedha mzoefu ktk wizara mbalimbali last year alikuwa kwa magufuli nadhani sasa yuko madini kitu kama hicho, siyo politician na siioni positive impact nyuma ya dhamira but acha jamii ipokee watu wao ktk sura tofauti.

Again ninawatakia ulanga west kila la heri ktk mchakato huu, mungu atubariki sana.
 
  1. Simon Ngonyani yuko ktk project fulani za maji hapo wizarani
  2. Yassin Njayagha- kijana aliyekuwa marekani na kutambulishwa kwa rais wetu muungwana jk 2006 kama rais wa watz wanaoishi Amerika kwa influence ya mbunge wa sasa,
  3. Dr Romuald Mbwasi-yuko na mradi maduka madogomadogo ya dawa unao supportiwa na wamerekani,
  4. Dr Mponda Hajji wa wizara ya afya
  5. Kiyawike -mhitimu mzamili
  6. Dr Juma Nghasongwa- Mbuge wa sasa mwenye kashfa za ufisadi na mdini
  7. Manfred Masako, Mtangazaji ITV, huyu mzee hana hata nyumba huko
Hili jimbo moto utawaka, wote hawa wanagombea kupitia CCM? Nadhani wapinzania wakisimamisha mgombea anayekubalika anabeba jimbo.
 
Kuna haja ya JF kuweka online Dictionary.Maana mambo mengine dah!
 
hebu tumwache naye ajaribu bahati yake,you never know anaweza kula shavu astaafu vizuri si unajua tena umri umesogea...

...So, now it is about kujaribu bahati, kula shavu na kustaafu vizuri na sio about kuwatumikia Wananchi, eh? :confused3:
 
Back
Top Bottom