Regia alikuwa anaendeshaje gari? Wakati mguu wake wa kulia ndio wenye ulemavu?

Poleni wote kwa msiba. Unajua nimejiuliza swali kama hili mimi binafsi na sikupata jibu. Watanzania tuna unafiki mwingi sana na double standards. Tukifika msibani wataulizana swali hili watu na minong'ono kibao, kafaje, aliendeshaje nk nk kibao.

Alipokufa kaka yangu Mr Ebbo maneno yalisemwa sana, mara ngoma mara nini. Hapa tunajua kafa kwa ajali lakini ndiyo watu wanauliza amekufa kwa ajali kivipi? Watu wana haki ya kujua. Nchi zilizoendelea swali kama hili si siri. Tena kama amekosea inasemwa kabisa na mamlaka kwamba alikosea.

Swali lijibiwe tu msikasirike. Wote tuna majonzi. Tusiitane mbwa wala paka. Hata kama litajibiwa mwezi ujao lijibiwe tu.

Poleni wote kwa msiba mzito wa dada Regia!
 
Jamani tusiwe na dabo standadi hapa, kama kuna hoja ya maana ijadiliwe.
Wamekufa wangapi na maswali kibao yakulizwa?
Kusema kweli we need to know this, je kuna utaratibu gani kwa watu wenye haloi kama yake kupata leseni na aina ya magari wanayotakiwa kuyatumia.
Itakuwa ni upuuzi kukwepa hoja ya msingi kwa kisingizio cha majonzi, na je kama majonzi hayo yameletwa na uzembe wa hoja inayoulizwa?
Kuna watu humu tayari wamesha fungua sredi eti kuna mkono wa serikali na wakaungwa mkono kwa nguvu zote, lakini inapotokea mtu akadadisi uhalisia anakua amekosea timing kipindi cha majonzi
Tujadili now, pamoja na kifo na majonzi tuliyo nayo lazima maisha mengine yaendelee, tujuwe tatizo right now kuokoa wengine na janga hili
 
Mkuu sasa hapo upuuzi wake nin mbn kauliza ki2 kizuri2! sababu huyo pia anaumia km wewe kwahiyo anatafakari mengi ndo mana kauliza
 
Kila la kijinga lisemwalo lina hoja,kwa kweli lazma tujiulize,nadhani mtoa Mada ana Mantiki
Nimesikitishwa na taarifa za msiba wa muheshimiwa Regia Mtema, inasemekana alikuwa anaendesha gari yeye mwenyewe sasa mimi najiuliza hivi gari hiyo ilikuwa ni ya buttons za kubonyeza kwa mkono maana mguu wake wa kulia ndio wenye ulemavu sasa brake accelerator angewezaje kuzikanyaga au ilikuwa LHD? ni risk sana kuendesha gari kwa mtu ambaye ni physically challenged in udadisi tu
 
Sio vyema kuanzisha mijadala kama hii wakati wa msiba,hususani inayomlenga marehemu negatively.Watanzania hatuna mila za kumlaumu ama kuuliza maswali mengi kuhusu marehemu.Tusubiri msiba upite.R.I.P Regia
 
Sasa hapo karopoka nini?na upuuzi wake ni upi?Naamini majibu ya swali lake ni muhimu sana.
Tatizo ni kwamba kauliza halafu katoa li conclusion lake la opinion..."ni risk sana kuendesha gari kaw mtu ambaye ni physically challenged." Angejaribu ku hold on to her god-awful opinion mpaka ajue ukweli ulivyokuwa.
 
mkuu kuna magari automatic special kwa vilema nadhani hata hiyo gari yake ilikuwa hivyoo sawa mkuu..

jaribu kutumia lugha nzuri, unapotumia neno "ki"lema au "vi"lema au mdhalilisha mtu. "Ki" inatumika kwa vitu. Mfano kisu,kijiko,kikombe nk. Hali kadhalika visu,vijiko,viti nk, tumia neno mlemavu. Asiyesikia(kiziwi) asiyeona(kipofu) nk. Acha kufananisha watu na vitu. Huko ni kudhalilisha.
 
Ni majonzi kwa wana JF. Tutazimiss updates na picha za matukio mbalimbali ulizokuwa unatuma hapa kwenye jukwaa la siasa! RIP sis Regia.
 
Hakuna anayesema kuwa hoja iliyotolewa kwa njia ya swali haina mashiko, ni vizuri jibu likapatikana na wakati wa kulia ukaheshimiwa kwanza. Polisi watakuja na taarifa na wataeleza
 
Yapo magari ambayo yametengenezwa maalum kwa ajili ya watu ambao wana ulemavu. dada Regia kama mlivyotujuza alikuwa na ulemavu wa mguu mmoja wa kulia. Kwa ulemavu huoo anaweza asihitaji gari maalumu maana kila kitu ni mafunzo na mazoea. wapo watu ambao hawana miguu yote na wanaendesha magari maalumu kwa ajili yao. Mengine yana vitufe vya kubofya na linamfanya dereva alimiliki kwa mikono yake. Kwa hio swali la msingi Je gari alilokuwa akiliendesha lilikuwa maalumu kwa ajili ya ulemavu wake?
Wahusika wa usalama barabarani wanahitaji kutuelekeza namna ya kuwafanya walema mbalimbali wenye uwezo au wanaotaka kuendesha magari , magari yao yawe na viwango/options zipi. Hii pia ni mahsusi kwa leseni zao.
Teknolojia imesonga mbele kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu kwani hata wasio na uwezo wa kumudu miguu na mikono yao wanatumia tu macho yao kuelekeza computer kufanya wanayotaka!!!!
Dada Regia Ulale pema peponi. Kazi uliyotumwana na Muumba wako umeikamilisha. Tuliyobaki tuendeleze ndoto zako njema.
 
ni kweli inatakiwa tujibu hoja, lakini naona mleta mada pia angekishirikisha zaidi kichwa chake, mh. ana leseni, asingeweza kupata leseni km hawezi kuendesha hiyo gari, waonaje hapo?

hiyo sio justification nzuri,kuna watu kibao hawajui hata kuendesha magari na wana leseni wamekata kabisa ili wakija kununua magari wasihangaike!!!hii ndio tz labda kama we mwenzetu uliondoka siku nyingi sana tz.Sema tu timing ya kuhoji inaweza kuwa haikua nzuri sana lakini swali la jamaa linahitaji majibu yanayojitosheleza zaidi kutoka kwa great thinkers kuliko hilo lako,may be limetokana na jazba ya kufiwa.Tusameheane sote wakati tulio nao unaeleweka.
 
kunyamaza si dawa ndo hawa mtu ana ukimwi tunafanya siri mpaka utuue wote,iwekwe wazi tu na inawezekana kabisa hicho ndo kilisababisha ajali.mke wa ngugi wa thiongo alibakwa wakati wa ujambazi polisi walificha alipotoka hospitali alisema hadharani nimebakwa,ukweli hauwi uwongo hata usiposemwa_mahatma gadhi
 
We ****** unauliza swali gani filauni mkubwa wewe,ajari inamtokea yoyote yule hata wewe inaweza kukutokea hata kesho,acha upuuzi kabisa watu tupo kwenye maombolezi wewe unaleta ujinga!
 
muhimu kujua,kwani ingekuwa mguu wa kushoto si mbaya... Ila ndiyo maana waheshimiwa,hata Amina Chifupa,pamoja na udogo wake,alikuwa akiendeshwa... Mguu wa kulia kuwa incapable na tena automatic RHD ni ......
 
Birigitta:
mkuu, swali la huyu bwana ni la kijinga na la maudhi at this perticular time. Anisamehe kama nimemkwaza, kwa bahati mbaya wengine wetu kifo chake kimetugusa kiasi ambacho discusion ya namna hii inaweza ikapelekea kichapo kama angekuwa karibu.

Si busara kwa sasa kuanza kujadili hali aliyokuwa nayo kwani jamii nzima ya wapendwa wake tuna msiba mzito na unaotugusa haswa. inasikitisha, inauma na inatuwia vigumu kuamini jambo hilo limetokea ingawa tunaitwa kulipokea kwa shukurani kwa Mungu aliyetujalia kumpata shujaa wetu huyu na ambaye kwa mipango yake mwenyewe ameamua kumwita akapumzike. Binti yule alikuwa fahari yetu sisi wa Mkoa wa Morogoro na hakika tumeumizwa mno lakini yafaa tu tuseme Bwana alitoa, Bwana ametwaa Jina lake lihimidiwe. RIP dada yetu Regia Mtema.
It is unbelievable but it has happened. An icon of opposition women activists has gone to rest so soon. We pray God to give us another person to continue from where she left.
Poleni wana Kilombero kwa kuondokewa na mwanamapinduzi wa kweli, poleni wana Morogoro wenzangu kwa kuondokewa na hili ua lililokuwa fahari yetu, na poleni wana CHADEMA na wana mageuzi wenzetu popote nchi nzima. Tumuenzi kwa kudumisha dhamira yake ya K4C yaani Kilombero for Change. RIP Regia.
 
Tutumie - watu wenye ulemavu badala ya vilema. Na pia physically challenged badala ya disabled. Nadhani sijakosea
 
Ukiitwa mchawi sijui utasemaje! Hujajiuliza kwa nini huo mguu wake unaoujua sana usisababishe hatari njia yote aliyopita hadi kufika eneo la ajali. Shame on you, watu wa aina yako hawana courage, wanaona obstacles at every opportunity. You poor soul!
 
R I P Regy. Alikuwa ni taa kwetu vijana.

Lakini tujadili uhalisia hawa wabunge pia wanaposho za madreva wao. Hii nayo imekaaje.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom