Regia adai kiwango cha elimu kimeshuka; PhD bungeni sawa na BA?

Mkuu,
Hii dunia ngumu sana, hawa watu wa mataifa yaliyoendelea wanapoleta project zao huwa wa nani ya kurudisha pesa zao kwao.Mfano wanapo ipa nchi fulani masaada wanaipa na masharti kwamba consultation lazima apewe mtu kutoka kwao na tena kwa dau kubwa.Hii ni kuhakikisha tu 80% inarudi kwao.

Lazima uelewe kuwa uelewa wa mwenye phd ni narrow band but sharp. wakati walio chini ni broad but butu. Na hata hivyo experience kubwa kazini nayo unaweza kuwa awarded phd. Na mambo ya consultation yana miono mingi sana kiuchumi,u active wa mtu husika kwa vitendo ktk hiyo kazi inayohitaji consultation nk.
Na hata hivyo je ulishawahi pia kujuuliza kwamba project za RESEARCH hawa unaowataja wanaowaletea consultation huwa mnaletewa pia ninyi undergraduate? Na pia ipi kati ya hizo ina uzito mzito?

Mkubwa,

Sasa naona tunaanza kukubaliana na ninachosema. Lakini kabla ya kukisema naomba nikusisitize kwamba sifanyi kazi kwenye kampuni ambayo ni aid oriented. Na mimi sijatoa mfano kwenye institution ambayo ni aid oriented. Hizo zinaangukia kulekue kwenye NGOs. Nimefanya kwenye service na production oriented.

Kumbuka kampuni za siku hizi ni globa oriented. Kampuni iko Tz lakini imesambaa nchi kadhaa duniani. Ninachowafahamisha hapa wenzangu ni kuwa kampni siku hzi zimeamzisha academic institutions zao kwa ajili ya trainings mbalimbali. Zingine zinatoa hadi degree kwenye discpline ya eneo au biashara hiyohiyo inayoendeshwa.

Tuje kwenye point yako nzuri. Umesema kuwa experience ya kazni inaweza kuwa PhD. Hili ndilo wengi duniani ambalo hawajaliona. Kuna kampuni zimeanzisha research department baada ya kutambua wameajiri vijana wazuri kwa research. Sasa kama mtu ndani ya kampuni amefanya research kadhaa na zikaongeza efficiency kwenye kampuni kwa nini kampuni isimuone ni equivalent na PhD kama unavyosema.

Nimesema kuwa mimi nina graduate na sina hata masters. Si kwamba siwezi kusoma masters bali hata pesa ya kujilipia au mwajiri kunilipia si tatizo. Lakini kutkana na ukweli aliosema Regia na ninaoufhamau kuwa niende University kuingiza nini kichwani ambacho nikikaa chumbani kwangu ninashindwa kukielewa nikikisoma?

Maoni yangu ni nini? Maoni yangu ni kwamba tukubali kwamba assesment mode zimekuwa nyingi na ndiyo maana hata wewe unasema dunia imekuwa ngumu. Assesment ya zamani ilikuwa ni University na huko award unayopata ni masters, Phd na Uprofessa. Sasa hivi assesors ni wengi wakiwemo employers, viwanda na centre nyingi za production.

Watakaoendelea kulinganisha PhD na upreofessor kama nguzo pekee za performance basi waendelee hvyohivyo kulala usingizi wa pono watajikuta wamechelewa kuamka. Tena wataamka na kugundua kuwa hata watumie mbio zipi wameshachelewa.

Kuna jamaa hapa juu kasema darasa la saba anajenga nyumba wakati proffessa anashindwa. PhD zijiuze kokote zishiishie kwenye Academic Institutons, NOG na Public Organs. Waje na hizo PhD zao tushindane kwenye soko la ajira watuthibitishie ukali wao.

Nakubaliana na wewe kuwa PhD ni narrow lakini sharp. Hiki ndicho kimewaua. Mtu anapata PhD anajifungia chuoni. Phd is about research. Kupata Phd ni kwamba umefanya research. Maana yake ni kwamba you are capable of conducting a convicing research. Sasa kama wako hivyo waje huku kwenye makampuni. HUku kuna maeneno mengi yanahitajia resrach.

Lakini wakiishia kujifungia vyuoni wakisubiri wafuatwe matokeo yake tutawaona wanatembea na ndala na kuishia kunywa pombe kila siku kwa frustrations.

Nasubiri mchango wako.
 
Ina maana hata wewe una phD? basi ndio maana thinking capacity yako inashindwa kupambanua maana ya kudanganya na ukweli.

Regia yuko right kwani hujaona mtu mwenye first degree au diploma wakiweza kuchambua mambo kuliko maprofesa ? Na wewe hutakiwi kuambiwa tumia tu akili ya kawaida kuona hili

Regia big up!!!!!!!!!!!!!!!!!
Mkuu wewe umesema vizuri zaidi kuliko yeye.Pia tatizo kubwa humu JF tulilo nalo sasa ni ushabiki tu na hilo linasababisha upofu wa kifikra!
Mh mbunge kawadhalilisha wote wenye Phd pamoja na first degree,tena sana sana amewadhalilisha zaidi wenye first degree kwa kumaanisha kwamba hawawezi kuchambua mambo kama wenye Phd,at the same time, wenye Phd sasa ndio wanachambua mambo kama wenye first degree....Kwamba wenye Phd wamerudi level ya chini inapokuja kwenye uwezo wa kufikiri.
Jaribu kusoma btn the lines,hili ni tatizo kubwa sana humu JF nowadays!Ushabiki tu.
 
Mh.Regia Mtema mbunge wa viti maalum wa CHADEMA wakati akijadili hotuba ya Rais katika kipaumbele cha Elimu amezungumzia kushuka kwa elimu nchini Tanzania.

Akitoa mfano wa kushuka kwa elimu amedanganya kwa kusema eti hakuna tofauti kati ya mtu mwenye PhD na mwenye digrii ya kwanza katika 'thinking capacity'.

Nawasilisha..
ulitaka asemaje?
 
Mkubwa,

Sasa naona tunaanza kukubaliana na ninachosema. Lakini kabla ya kukisema naomba nikusisitize kwamba sifanyi kazi kwenye kampuni ambayo ni aid oriented. Na mimi sijatoa mfano kwenye institution ambayo ni aid oriented. Hizo zinaangukia kulekue kwenye NGOs. Nimefanya kwenye service na production oriented.

Kumbuka kampuni za siku hizi ni globa oriented. Kampuni iko Tz lakini imesambaa nchi kadhaa duniani. Ninachowafahamisha hapa wenzangu ni kuwa kampni siku hzi zimeamzisha academic institutions zao kwa ajili ya trainings mbalimbali. Zingine zinatoa hadi degree kwenye discpline ya eneo au biashara hiyohiyo inayoendeshwa.

Tuje kwenye point yako nzuri. Umesema kuwa experience ya kazni inaweza kuwa PhD. Hili ndilo wengi duniani ambalo hawajaliona. Kuna kampuni zimeanzisha research department baada ya kutambua wameajiri vijana wazuri kwa research. Sasa kama mtu ndani ya kampuni amefanya research kadhaa na zikaongeza efficiency kwenye kampuni kwa nini kampuni isimuone ni equivalent na PhD kama unavyosema.

Nimesema kuwa mimi nina graduate na sina hata masters. Si kwamba siwezi kusoma masters bali hata pesa ya kujilipia au mwajiri kunilipia si tatizo. Lakini kutkana na ukweli aliosema Regia na ninaoufhamau kuwa niende University kuingiza nini kichwani ambacho nikikaa chumbani kwangu ninashindwa kukielewa nikikisoma?

Maoni yangu ni nini? Maoni yangu ni kwamba tukubali kwamba assesment mode zimekuwa nyingi na ndiyo maana hata wewe unasema dunia imekuwa ngumu. Assesment ya zamani ilikuwa ni University na huko award unayopata ni masters, Phd na Uprofessa. Sasa hivi assesors ni wengi wakiwemo employers, viwanda na centre nyingi za production.

Watakaoendelea kulinganisha PhD na upreofessor kama nguzo pekee za performance basi waendelee hvyohivyo kulala usingizi wa pono watajikuta wamechelewa kuamka. Tena wataamka na kugundua kuwa hata watumie mbio zipi wameshachelewa.

Kuna jamaa hapa juu kasema darasa la saba anajenga nyumba wakati proffessa anashindwa. PhD zijiuze kokote zishiishie kwenye Academic Institutons, NOG na Public Organs. Waje na hizo PhD zao tushindane kwenye soko la ajira watuthibitishie ukali wao.

Nakubaliana na wewe kuwa PhD ni narrow lakini sharp. Hiki ndicho kimewaua. Mtu anapata PhD anajifungia chuoni. Phd is about research. Kupata Phd ni kwamba umefanya research. Maana yake ni kwamba you are capable of conducting a convicing research. Sasa kama wako hivyo waje huku kwenye makampuni. HUku kuna maeneno mengi yanahitajia resrach.

Lakini wakiishia kujifungia vyuoni wakisubiri wafuatwe matokeo yake tutawaona wanatembea na ndala na kuishia kunywa pombe kila siku kwa frustrations.

Nasubiri mchango wako.

Mchango wako mzuri, lakini nafikiri unashindwa kuheshimu mgawanyo wa kazi na kuheshimu maeneo yao. Wewe unataka kuwajaribu eti mje kushindana nao ili uone kama ni mahili ama la! na pia nataka kujulishe kuwa pamoja na digrii yako kuna mtu hata hakwenda darasa la saba naye atakukaribisha ktk maeneo yake na kukwambia kama unaweza njoo huku tushindane tuone kama kweli una digrii.Na kibaya kabisa hutoweza mshinda huyo jamaa wa std 7 ktk maeneo yake.

Na hata hivyo ni hulka ya kibinadamu anapofanikiwa hasa kipesa, kuona ambaye hajafanikiwa kuwa hafai ama mjinga na anachomiliki si tija. Ni hulka hiyohiyo kwa wazungu wengi kwa vile wameona wanamafanikio kuona wana akili ama Mungu ni wao.

Ni mwendelezo huo huo, ya kwamba mtu mwenye mapesa na mtazamo mfinyu haoni sababu ya kwenda shule kama wewe unavyoona huna sababu zaidi yakuendelea kupata phd.
 
hajakosea hata kidogo kama Tanzania tuna wasomi vyeti wengi,huwezi ukawa una phd na unakuwa na maamuzi ya ki puuzi yasiyo na kichwa wala nini kwa Taifa lako ndio mana Mwalimu Nyerere alikuwa sio Proffesor lakini alikuwa na elimu ya utambuzi kwani elimu bila utambuzi unakuwa useless tu kama Dr wakutunukiwa na madokta wenzake wa ccm.
 
ulitaka asemaje?
Angesema tu "thinking capacity" ya wenye Phd haiendani na kiwango cha elimu yao period!
Kusema ni kama ya wenye degree ya kwanza ni kuwadhalilisha wenye degree ya kwanza ambao wana thinking capacity inayoendana na elimu waliyo nayo.
Think.
 
Regia Mtema mjanja sana,anataka aambiwe akadhibitishe ili sasa apate wasaha wa kukaa na kinerugaba msemakweli ili wawataje tena Fake PhDz bungeni. Mh.spika umewakomboa phd fake holders ambao kama ungedai ushaidi wangeumbuka! Alaf mh.spika mchezo wa kudai ushaidi utakucost,sasa ona ulivotaka kumuharibia Wazir.mkuu. Cheza na akili za wanaCDM makinda!
 
Regia Mtema mjanja sana,anataka aambiwe akadhibitishe ili sasa apate wasaha wa kukaa na kinerugaba msemakweli ili wawataje tena Fake PhDz bungeni. Mh.spika umewakomboa phd fake holders ambao kama ungedai ushaidi wangeumbuka! Alaf mh.spika mchezo wa kudai ushaidi utakucost,sasa ona ulivotaka kumuharibia Wazir.mkuu. Cheza na akili za wanaCDM makinda!
Gsana uko nje ya hoja completely!Na kama that isn't the case,then una tatizo ambalo ni very serious!Hivi ni kweli umepost ili kujibu hii mada ama umekosea thread?
Sasa wewe unamaanisha kuwa wenye fake Phd ndo wana thinking capacity ya wenye degree za kwanza ambazo ni halali?Duh!
 
...

Akitoa mfano wa kushuka kwa elimu amedanganya kwa kusema eti hakuna tofauti kati ya mtu mwenye PhD na mwenye digrii ya kwanza katika 'thinking capacity'.

Nawasilisha..

Hajadanganya, ila ametoa hoja dhanifu. Mtu akifikia kiwango cha elimu ya digrii ya kwanza tayari anakuwa amepata nyenzo kubwa sana ya kumuwezesha kufikiri na kuchambua masuala mbalimbali ya kitaaluma na kijumla duniani. Kinachobakia ni jinsi anavyojishughulisha kutumia nyenzo hiyo. Ndicho kinachotofautisha umahiri wa watu. Digrii ya pili (Masters) na ya tatu (PhD) sanasana zinamuongezea ubingwa kwenye taaluma yake tu na zinazolingana nayo. Digrii hizo (Masters na PhD) zina nyongeza ndogo (marginal) tu katika uwezo wa kuchambua na kufikiri masuala ya ujumla.

Tatizo la Tanzania hasa kwa wanasiasa, wapo wenye digrii (hadi PhD) zisizo na viwango (zinapatikana kwa fujo siku hizi) huku walio na digrii za uhakika hawajishughulishi na mambo ya kitaaluma (kutokan na dhiki nyingi) na pia wapo walioamua kuziweka pembeni ili kukidhi/kutumikia viongozi wasio na visheni. Sasa hapo kuipata tofauti ya viwango vya usomi ni kazi sana.

Lakini hata katika mazingira ya kawaida, si lazima mwenye digrii ya kwanza (kama kweli anajituma) azidiwe na mwenye PhD. Nilipokuwa nasoma Masters Uingereza baadhi ya masomo nilisimamiwa na mwalimu mwenye BSc ambaye pia alikuwa akiwasimamia baadhi ya jamaa waliokuwa wakichukua PhD. And he was really good.
 
Mh.Regia Mtema mbunge wa viti maalum wa CHADEMA wakati akijadili hotuba ya Rais katika kipaumbele cha Elimu amezungumzia kushuka kwa elimu nchini Tanzania.

Akitoa mfano wa kushuka kwa elimu amedanganya kwa kusema eti hakuna tofauti kati ya mtu mwenye PhD na mwenye digrii ya kwanza katika 'thinking capacity'.

Nawasilisha..

Siku nyingine unapoanzisha Thread iweke iwe neutral, halafu chini yake post your opinion badala ya kutupa taarifa ya mtazamo wako wewe. Ulichotakiwa kufanya ni kutoa sababu ambazo nina hakika kuwa alizitoa katika kutoa tathmini yake hiyo. Otherwise your thread is nothing but biased ab initio.
 
Mh.Regia Mtema mbunge wa viti maalum wa CHADEMA wakati akijadili hotuba ya Rais katika kipaumbele cha Elimu amezungumzia kushuka kwa elimu nchini Tanzania.

Akitoa mfano wa kushuka kwa elimu amedanganya kwa kusema eti hakuna tofauti kati ya mtu mwenye PhD na mwenye digrii ya kwanza katika 'thinking capacity'.

Nawasilisha..

yaaa. hakuna tofauti kati yangu na Dr.[jina kapuni] in terms of thinking.

au nimemzidi.
 
Mchango wako mzuri, lakini nafikiri unashindwa kuheshimu mgawanyo wa kazi na kuheshimu maeneo yao. Wewe unataka kuwajaribu eti mje kushindana nao ili uone kama ni mahili ama la! na pia nataka kujulishe kuwa pamoja na digrii yako kuna mtu hata hakwenda darasa la saba naye atakukaribisha ktk maeneo yake na kukwambia kama unaweza njoo huku tushindane tuone kama kweli una digrii.Na kibaya kabisa hutoweza mshinda huyo jamaa wa std 7 ktk maeneo yake.

Na hata hivyo ni hulka ya kibinadamu anapofanikiwa hasa kipesa, kuona ambaye hajafanikiwa kuwa hafai ama mjinga na anachomiliki si tija. Ni hulka hiyohiyo kwa wazungu wengi kwa vile wameona wanamafanikio kuona wana akili ama Mungu ni wao.

Ni mwendelezo huo huo, ya kwamba mtu mwenye mapesa na mtazamo mfinyu haoni sababu ya kwenda shule kama wewe unavyoona huna sababu zaidi yakuendelea kupata phd.

Na kama ndiyo uelewa huu tunaoonyesha hapa Jf basi tatizo linaweza kuwa kubwa. Kwanza hoja ya msingi kama nilivyomsikia Regia ni kwamba alitumia maneno kuwa "Phd kwa hali ya sasa hakuna tofauti katik thinking capacity na graduate".

Kumbuka kwamba hakuna chuo hapa duniani kichojaza watu thinking capacity. Chuo hata kiwe the best duniani kinafundisha kutumia thinking. Thinking capacity ni uwezo binafsi wa mtu kujaza ubongo wake kwa kadiri anavyoweza.

Nakubaliana na wewe kabisa kuwa mimi ni graduate lakini kuna form six nawaheshimu kwa masuala ambayo hata mimi ni proffessional. Mdogo wangu ni form six lakini namkubali kwa utaalamu. Kwa sababu ninaheshimu mabadiliko ya dunia kwamba yamefanya watu waweze kujua jambo lolote kama una nia. Yale niliyoyasoma University kwa miaka kadhaa yanapatikana kwa urahisi na hayazuiliki kuingia kichwani kwa mtu yeyote.

Sasa kama hayazuiliki kuingia kichwani basi maana yake anayeyasomea kama master program yatamuingia kichwani. Lakini vilevile aliyekaa kwenye internet chumbani akiyasoma yanamuigia vilevile. Mwenye masters au PhD au uprofeessor hana hati miliki ya kuzuia material yasiingie kwa mwingine.

Inawezekana naeleza kwa kirefu hadi nisielweke lakini nikiweka kwa kifupi ni kwamba si busara kudhani vichwa vyenye ceritifaction ya Masters au PhD ndivyo pekee vyenye best solutions za issue.

Masters, PhD na Uprofessor ni certifications. Ni alama kwamba kuna institution imekukubali kwamba unajua au unaweza jambo fulani. Na wakati mwingine na hasa mara nyingi hivyo vinapatikana kwa kudesa. Waajiri wameligundua hilo siku nyingi.

Kwenye interview siku hizi huulizwi maswali ya Chuoni. Unaulizwa maswali yanayo-face industry. Mfano unaulizwa "likitokea tatizo fulani hapa utali-tackle vipi". Hapa ndipo panapowapiga chenga wengi. Nimeshuhudia interview nyingi mtu ana first class au upper second anashindwa swali dogo kama hili tena linalohitaji majibu ya proffession yake.

Niliposema waje huku tuwaone kwenye industry niliweka wazi kwamba waje kwenye yaleyale ambayo nao ni field yao. Na nimeeleza kuwa huku nako kuna research nyingi tena zaidi kuliko kwao. Kuna research za ku-reduce cost. Waje tuwapime, mbona walitupima tukiwa chuoni.

Mimi sioni ajabu kuitwa nikapimwe na kazi anayofanya mtu wa darasa la saba. Maadamu nipewe rsource zote zilizomfanya awe mzuri kama muda, training na working tools. Ndiyo maana ya competition neno ambalo hata lisipopendwa bado litatamalaki.

Na wewe pia hapa hukuelewa dhamira yangu ya kutotaka kusoma. Ile kutamka nina hela za kujisomesha sasa unataka ugeuze mada kwamba ninajifanya tajiri sitaki kusoma. NIlijua utakuja kihivyo na kwanza nashukuru hukuniiita fisadi.

Lakini nilisema wazi ninasita kwenda postgraduate kwa sababu kama ni kuingiza vitu vipya kichwani ninaviingiza kila siku ninaponunua vitabu mbalimbali na ninaposoma website nyingi.

Unaponijibu hutakiwi kunikebehi baada ya kueleza hivi. Unatakiwa unieleza kuwa anayekwenda darasani kuchukua Masters au Phd ananizidi nini kwa kilichoingia kichwani mwake.

Nilidhani hilo litakuwa rahisi sana kwako.
 
Mkubwa,
Nimesema kuwa mimi nina graduate na sina hata masters. Si kwamba siwezi kusoma masters bali hata pesa ya kujilipia au mwajiri kunilipia si tatizo. Lakini kutkana na ukweli aliosema Regia na ninaoufhamau kuwa niende University kuingiza nini kichwani ambacho nikikaa chumbani kwangu ninashindwa kukielewa nikikisoma?

Manufaa ya kwenda full time shuleni si kupata knowledge ya vitabu tu; PhD is more than books....hata ile how to argue/discuss with your promoter ni part ya impartation ya Phylosophy ya PhD....Kuwa subjected under harsh and stressfull environment ukaweza ku persavere na yet to come up with a thesis is the quality ambayo huwezi kuipata mtaani au kazini....Uliza waliopitia PhD wakwambie what it means na ni mara chache sana PhD material from reputable university akawa na argument zisizoeleweka; ukiona hivyo tafuta aliko soma....Something should be wrong with the institution na siyo PhD kama qualification.
 
Watanzania wengi tunasoma lakini hatuelimiki. So, Regia yuko sahihi 90%. Mifano mingi imetolewa ya mikataba mibovu iliyopitishwa na hao wasomi lakini wasio na hizo phd wakaja baini udhaifu mkubwa.
Kama huwezi kutumia elimu yako kuwakwamua wananchi hakika umesoma lakini hujaelimika; na mtu aliyeelimika thinking capacity yake ni kubwa.
Afterall, Regia amesema hayo ni maoni yake; na wewe unaweza kuwa na maoni yako, na hili ndilo linatuweka hapa JF. Maoni tofauti na hatimae tufikie conclusion ambayo yaweza kuwa muafaka au kutoafikiana.
Halafu hoja ya Regia isijadiliwe kwa kusema PHD na Bachelor, bali kama alivyosema mwenyewe, thinking capacity ya Phd holder na Bachelor holder.
Katika nchi nyingine vyuo vikuu ndipo mahali pa utafiti na tafiti nyingi za kisayansi hufanyika huko na kutoa mambo ya kusaidia maendeleo ya wananchi. Angalia Embryonic stemcell researches zinafanyika wapi, angalia global climate changes zinafanyika wapi; nyingi ni vyuoni - je TZ phd wetu wanafanya nini?
Inawezekankana Phd wetu wameacha fani zao wakaenda kwenye siasa, na huko ni kweli hawafanyi tafiti, siyo fani yao na ndiyo maana wanaburuzwa na hao wenye vyeti vya chuo cha ccm murutunguru. Hivyo Regia atakuwa sahihi maana Phd wa electronics anapaswa ang'ang'anie fani yake, kama ni malipo adai akiwa huko na aonyeshe kuwa kama ataiacha basi taifa litaathirika, siyo kukimbia. Msomi aliyeelimika halikimbii tatizo bali hutafuta dawa au suluhu; phd wetu wanapokimbia matatizo kwenye fani zao na kuingia kwenye siasa wakidhani huko watapata suluhu ya matatizo ya fani zao, hawana tofauti na mkulima asiyejua maana ya kutumia mbolea ambaye shamba likianza kutoa mazao kidogo analikimbia badala kuweka mbolea.
As great thinkers, let us think greatly!
 
Mh.Regia Mtema mbunge wa viti maalum wa CHADEMA wakati akijadili hotuba ya Rais katika kipaumbele cha Elimu amezungumzia kushuka kwa elimu nchini Tanzania.

Akitoa mfano wa kushuka kwa elimu amedanganya kwa kusema eti hakuna tofauti kati ya mtu mwenye PhD na mwenye digrii ya kwanza katika 'thinking capacity'.

Nawasilisha..
Sasa kadanganya kitu gani?its so obvious hayo yote anayosema.Nakumbuka wakati wa Zain Challenge iliyoonyeshwa ITV/TBC nimesahau wapi,ilikuwa aibu kwa wasomi wetu.Mazingira tu hayo ya chuo kikuu hayafai kwa kuboresha elimu.
 
Ule ni uongo wa graduate wa SUA,amejawa fitna kuliko kuwa mkweli,sishangai sana lakini manake kama Mhonga(CHADEMA) ana degree ya UDSM na kashindwa na Buyogela mwenye elimu ya msingi kwenye kujieleza wakati wa kuwania nafasi za ukamishna wa tume ya bunge basi degree yaweza kuwa haina maana!!!

Umegusa palepale, uliona wtofauti ya kujieleza kati ya Mhonga masters graduate na Agripina darasa la saba ndo ujue.
 
Kumbuka kwamba hakuna chuo hapa duniani kichojaza watu thinking capacity. Chuo hata kiwe the best duniani kinafundisha kutumia thinking. Thinking capacity ni uwezo binafsi wa mtu kujaza ubongo wake kwa kadiri anavyoweza.

Ukitueleza alitumia vigezo gani kupima Thinking Capacity na kwa kutumia sample ya ukubwa wa kiasi gani utatusaidia sana.
 
Mh.Regia Mtema mbunge wa viti maalum wa CHADEMA wakati akijadili hotuba ya Rais katika kipaumbele cha Elimu amezungumzia kushuka kwa elimu nchini Tanzania.

Akitoa mfano wa kushuka kwa elimu amedanganya kwa kusema eti hakuna tofauti kati ya mtu mwenye PhD na mwenye digrii ya kwanza katika 'thinking capacity'.

Nawasilisha..
Inabidi afute kauli yake na aniombe radhi mimi binafsi halafu awaombe radhi wote waliosoma 'PhD za ukweli'. Nawasilisha
 
Back
Top Bottom