Vawulence
JF-Expert Member
- Jan 4, 2009
- 1,928
- 2,101
Makamu mwenyekiti wa REDET Dr. Benson Benza amelalamikia kitendo cha mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA Dr. Wilbrod Slaa kudai kuwa yeye ni mshauri wa Rais aliyemaliza muda wake Bwana Jakaya kikwete (for the sake of education simwiti doctor). Pia amekanusha madai kuwa yeye ni mteule wa rais na kudai kuwa nafasi yake si ya kuteuliwa.
Katika mahojiano yaliyofanyika Star tv ya jijini Mwanza,Dr. Benson alizungumzia matokeo ya REDET na kudai kuwa matokeo yale yalikuwa ni ya muda mfupi tu. Pia alidai kuwa haikuwa sahihi kwa vyama vya siasa kulaumu matokeo ya utafiti ikiwemo ccm kwani utafiti wao ni wa kisayansi na machapisho yao hutafutwa na vyuo vya Oxford na Havard.
Katika hali iliyoonesha kuwa anataka kumshitaki Dr. Slaa , Dr. Benson alisema "Nilikuwepo Mwanza wakati Dr. Slaa aliposema kuwa mimi nafasi yangu nimeteuliwa na rais Kikwete na pia mimi ni mshauri wa rais.....ningekuwa mwanasiasa ningelizungumzia hili jukwaani ila kama political analyist NITALIWEKA HILI SAWA BAADA YA UCHAGUZI."
MY TAKE
Ataliwekaje hili sawa?
Katika mahojiano yaliyofanyika Star tv ya jijini Mwanza,Dr. Benson alizungumzia matokeo ya REDET na kudai kuwa matokeo yale yalikuwa ni ya muda mfupi tu. Pia alidai kuwa haikuwa sahihi kwa vyama vya siasa kulaumu matokeo ya utafiti ikiwemo ccm kwani utafiti wao ni wa kisayansi na machapisho yao hutafutwa na vyuo vya Oxford na Havard.
Katika hali iliyoonesha kuwa anataka kumshitaki Dr. Slaa , Dr. Benson alisema "Nilikuwepo Mwanza wakati Dr. Slaa aliposema kuwa mimi nafasi yangu nimeteuliwa na rais Kikwete na pia mimi ni mshauri wa rais.....ningekuwa mwanasiasa ningelizungumzia hili jukwaani ila kama political analyist NITALIWEKA HILI SAWA BAADA YA UCHAGUZI."
MY TAKE
Ataliwekaje hili sawa?