Re: THANKS TO JF

Nimekupata. Kweli kabisa huwezi kutumia ubongo pekee bila kushirikisha mwili, ila sikumaanisha hivyo: Umewahi kusikia au kuona watu wanatumia mwili zaidi ya ubongo vyuoni na makazini ili kujirahisishia/kuweka njia nyeupe? sasa hayo yapo na kuna mabosi wanaendekeza hayo. Hope umenipata vilivyo nini namaanisha.


You bet nimekupata, ila sikulelewa kuwa tegemezi, namuomba Mungu aendelee kunipa bidii binafsi. Najua hayo yanatokea, ila kwa Elimu niliyonayo amabayo nimeipata kwa juhudi na msaada wa Mungu, no one can mess up with my carrier in such a dirty way.

Asante kwa ushauri once again.
 
Hongera kwa kupata kazi na kushiriki nasi katika kutupa ushuhuda. Je umeolewa? Nahisi nimeanza kukupenda ghafla.
 
Hongera sana inatia moyo kusikia watu wanapata kazi.

Wapendwa Sina jinsi ya kuielezea furaha yangu. Nimekuwa member wa JF kwa takriban mwaka sasa. Mie huwa si msomaji wa magazeti, na taarifa nyingi muhmu huzipata kupitia hapa JF. Kwa mara ya kwanza hii forum imenisaidia na nimeyaona matunda yake.

Nimefanikiwa kupata kazi, amabayo kwa mara ya kwanza niliiona hapa JF, katika forum ya "Nafasi za Kazi na Tenda". Mwanzoni sikuamini kama nami naweza pata kazi serikalini bila kuwa na mtu wa kunishika mkono, lakini leo imewezekana. Ni kweli kuna uwazi na ukweli na usawa kupitia Sekretariatiya Ajira na Utumishi. Tuliitwa watu saba na nafasi ilikuwa moja tuu.

Nimepata,

Namshukuru Mungu na WanaJF, Tuendelee kulijenga Taifa letu. Big up JF, LIVE LONGER.

Kwa wengine, Msikate tamaa, endeleeni kuomba kazi bila kuchoka, ipo siku mtafanikiwa, na tusipuuze kazi, na tufanye kazi kwa bidii na kutumia nafasi zetu kwa manufaa ya umma.

Asanteni.
 
Hongera kwa kupata kazi na kushiriki nasi katika kutupa ushuhuda. Je umeolewa? Nahisi nimeanza kukupenda ghafla.

Lol, Nimeipenda hii Post ghafla. wacha nkaoge nibadilishe na nguo, niweke makeup, then ntakuja rasmi kuijibu tehe
 
Hongera sana mwanangu kupata kazi na kukumbuka kumshukuru Mungu kwamba yeye pekee ndiye ameruhusu kwa wakati wake muafaka umepata kazi
Wahi kazini na waheshimu wakubwa wako utapata mafanikio na upatapo mshahara usisahau kurudisha fungu la kumi la mapato yako utabarakiwa
Pia umefanya vyema kuwashukuru pia JAmiiforums nasi wanachama wenzio tumefurahi. Mimi binafsi nina mambo kazaa ninawashukuru jamii forums nimefanikiwa kadhaa
 
Hongera sana mwanangu kupata kazi na kukumbuka kumshukuru Mungu kwamba yeye pekee ndiye ameruhusu kwa wakati wake muafaka umepata kazi
Wahi kazini na waheshimu wakubwa wako utapata mafanikio na upatapo mshahara usisahau kurudisha fungu la kumi la mapato yako utabarakiwa
Pia umefanya vyema kuwashukuru pia JAmiiforums nasi wanachama wenzio tumefurahi. Mimi binafsi nina mambo kazaa ninawashukuru jamii forums nimefanikiwa kadhaa

Asante kwa pongezi na nasaha zako. Watu wengi hudhani kuwa vyeti pekee vyatosha kupata wakitakacho, mie naamini wakati na bahati humpata yeyote, kwa wakati alioupanga mtoaji wa yote. Mungu ni mwema namwomba anijalie uvumilivu na uadilifu kazini, kama alivyonisimamia na kuniongoza tangu mwanzo.
 
hongera sana. hakika umevuka kikwazo kimoja (kutafuta ajira), naamini
vikwazo utakavyovikuta huko uendako utavikabili kwa mtazamo chanya
na kuvivuka bila wasiwasi,
 
Hongera kijana, fanya kazi kwa bidii huko serikalini usaidie kupunguza urasimu usiwe na wewe mmoja wa wale wanaonyanyasa wananchi unafika asubuhi hadi saa tano unasoma magazeti wakati sisi tumepanga foleni toka saa moja asubuhi tunahitaji huduma.

Hongera
 
hongera sana. hakika umevuka kikwazo kimoja (kutafuta ajira), naamini
vikwazo utakavyovikuta huko uendako utavikabili kwa mtazamo chanya
na kuvivuka bila wasiwasi,

Asante kwa pongezi my dear godfrey Tajiri. Naamini Mungu ataniongoza na kunisimamia, na hatimaye nitavivuka vikwazo na kutwaa taji la ushindi.
 
Last edited by a moderator:
Bado nasubiria ujue!!!

Just wait there thereee, usiondoke. Nguo nliyotegemea kuvaa imechomeka na Pasi, ngoja nianze kunyoosha ingine.
Nakuja baby, just wait and you won't regret, coz nimeambiwa JIMSHAHARA ni NONOOOOO.:wink2:
 
Hongera kijana, fanya kazi kwa bidii huko serikalini usaidie kupunguza urasimu usiwe na wewe mmoja wa wale wanaonyanyasa wananchi unafika asubuhi hadi saa tano unasoma magazeti wakati sisi tumepanga foleni toka saa moja asubuhi tunahitaji huduma.

Hongera

Tick, tick mkuu.
 
Pongezi nyng zikufikie,nenda kawe mtumwa mwema.najiskia furaha sana kuona mwenzangu umepata kazi kwani najua na mie zam yang ndio inakaribia,Thank God for that.
Sasa imebaki zamu yetu
 
Wapi wewe mfanyakazi wa sekretarieti unajifanya umepata kazi.Sema unataka uwaosheee nenda Fb huko kawadanganye wenzio sio hapa

Haya ndo majitu yaliyoathiliwa na ukosefu wa ajira kwa muda mrefu sasa makashfa ya nini?
 
Hongera sana, inabidi mshahara wa kwanza tukajengee heshima bar sawa?
kweli akili ni nywele,...... badala ya kusema mshahara wa kwanza anunue vocha mojamoja za mitandao tofautitofauti na awe akiziweka katikati ya mada yoyote mpaka ziishe, wale wanaosoma na kufuatilia mada za JF watafaidi kila mtu kwa kadiri ya anavyojituma kuitumia JF. :dance:
 
Back
Top Bottom