Re: Jamani Housegirl wangu Huyu!!!Ananitafuta ubaya! (STRICTLY KWA WANAUME TU)-PART II

Gugwe

Senior Member
Jul 25, 2011
122
54
Wana jamvini ripoti pokeeni.

Kwanza kabisa nashukuru sana kwa ushauri wenu-yote yenye mitazamo tofauti, kwa kweli imeniwezesha kujitazama upya kama tatizo na si kumwangalia mtu mwingine. UAMUZI NIMECHUKUA. Kwa wale wote walionishauri chapa ilale nawashukuru sana lakini nasikitika kuwataarifu kuwa ushauri wenu nimeuweka kapuni, wale wenye ushauri tofauti na huo wenye malengo ya kuheshimu ndoa yangu, familia yangu, watoto wangu na mke wangu nawashukuru maradufu na huo ndio ushauri nilioamua kuufuata katika mazingira yafuatayo;
  1. Kwanza kabisa, sitamtimua/kumfukuza kazi katika mazingira ya hisia za kumtega bosi wake. Kwa ushauri wenu nimeweza kujitazama zaidi na kuamini katika kushinda majaribu
  2. Nimemuita na kumkanya juu ya mitego yake isiyokuwa na tija, pia kuongea nae kuhusu maisha kwa ujumla na maisha yake. Seriously nimemkanya na kumuamuru aniheshimu kama muajiri wake na si vinginevyo. Mkutano huu nimeufanya nikiwa na mdhamini wake wa kazi ambaye ilibidi nimuite aje tuweze kuliongelea hili tukiwa wote. Sikumshirikisha wife katika hatua hii kwa sababu sipendi apate maumivu yoyote juu ya mapenzi hasa kwa wakati huu, pia nilihisi akijua hata kwa nia njema lazima angedemand kumfukuza kazi, jambo ambalo niliona kwamba si haki katika hatua hii ambayo inaongozwa na hisia. Katika kuongea nae alishindwa kukiri au kukataa, lakini akaomba sana msamaha kama alikuwa katika mienendo inayokwaza
  3. Nimempatia muda wa probation wa miezi mitatu-katika muda huo nitakuwa namchunguza tabia na mienendo yake, akikengeuka kazi hana on the spot na hilo nitalisimamia mimi mwenyewe katika namna ninayojua kuhakikisha adhabu inatekelezeka
  4. Katika kuongea nae, tulimuuliza juu ya future ya maisha yake badala ya kutegemea/kuamini katika kupata mwanaume ndio maisha yaende, naye alisema anapenda kupata msaada wa kuendelea kielimu-elimu ya Hotel Management. Maamuzi niliyofikia, akimaliza muda wa miaka mitatu bila matatizo, nitamgharamia elimu hiyo aliyopendekeza au nyingine kwa kipindi na wakati husika
Nashukuru sasa ninaishi kwa amani, pia shukurani zangu ziwaendee wachangiaji woooote katika thread hii, kuwakumbuka wachache tu-Mr. Rocky, Shantel, Dinnah, Sangara, Mjasiria, La Jeneral, Ndaki, Katavi na wote wengine. Pia nawashukuru akina dada mlioamua kuvamia thread hii kimabavu kwa kweli ushauri wenu pia umekuwa ni wa manufaa sana.

Cheers!
 
Afadhali umeamua kuweka msimamo wako na kujali zaidi familia yako na maisha ya watoto wako. Pia kumjali mke wako na kuamua kuweka msimamo wa kuijenga familia yako. Ila muhimu kuwa makini sana na angalia sana isije ikawa mtego kwako wa kukusababishia maumivu kwa siku za mbele. Kama ni msimamo uwe nao haswa kama baba mwenye nyumba na ile kutaniana au kuangaliana na msichana wa kazi kama mwanamke ndani ya nyumba uishe la sivyo huo muda wa probation hautaisha vituko vitakuwa vimezidi
Hongera sana kw auamuzi wako na maamuzi uliyochukua
 
Jina la bwana libarikiwe.... Umeshinda kama Yusufu wala hukuwa kama Daud.
 
Mkuu part one sikuweza ku comment kwa ukosefu wa nafasi,lakini nimeisoma kwa mapana na marefu.Acha kuutega moyo wako,sisi wanaume kwenye suala la ngono ni dhaifu hatuna mipaka.So long ulishapata matamanio hiyo ni sumu tayari na the longer unakaa naye hamu itaongezeka.Run man run ondoa huyo mtoto nyumbani kwako haraka,kama ni chuo basi mpeleke kesho akasome na atokee kwao.Take it from me ukiendelea kukaa naye piga ua utamlamba tu.Kibaya zaidi eti umekaa naye kikao ,seriously unakaa kikao na house girl eti mnajadili mambo ya nonino,halafu eti ulimficha mkeo taarifa za kikao,unadhani hatajua,duniani siri ya wawili hakuna itakuwa ya watatu? acha hizo bana kama vipi basi tangaza ndoa ya pili kijulikane,usitufunge wala wewe mwenyewe kujifunga kamba!
 
gugwe samahani sana tena sana. lakini wewe si ndio uliotoa issue ya kujivua gamba kwenye jukwaa maalum?{la kikubwa}kule uliandika vitu vya ajabu,ambavyo kama uliona sifa fulani kwa unayoyafanya nyumba ndogo.na huku ni kama uonekani msafi huwezi kumtendea vibaya mke wako.nikueleweje?
 
gugwe samahani sana tena sana. lakini wewe si ndio uliotoa issue ya kujivua gamba kwenye jukwaa maalum?{la kikubwa}kule uliandika vitu vya ajabu,ambavyo kama uliona sifa fulani kwa unayoyafanya nyumba ndogo.na huku ni kama uonekani msafi huwezi kumtendea vibaya mke wako.nikueleweje?
Kisukari, swala hapa lilikuwa kutembea na msichana wa kazi, ambako tuliona kama ni kumkosea adabu mkewe na family nzima, kama anafanya nje pia si kitu kizuri ila ni afadhali huko kuliko ndani kabisa ya nyumba
 
Hongera kwa kushinda majaribu, ishi kwa amani sasa na huyo msichana nafikiri ungeanza mapema kumtafutia kitu cha kufanya ili aondoke hapo mapema kushakuwa na doa
 
Narudia tena UKOME yaani akuoshee vyombo miaka yote 3 ndo umpeleke shule!!!
hehe heheh
 
Kisukari, swala hapa lilikuwa kutembea na msichana wa kazi, ambako tuliona kama ni kumkosea adabu mkewe na family nzima, kama anafanya nje pia si kitu kizuri ila ni afadhali huko kuliko ndani kabisa ya nyumba
kwa aliyoyaandika kule,kiukweli simuamini vizuri
 
Big up kwa kushinda hayo majaribu.....ni wachache sana wanaoamua hivyo!
 
Narudia tena UKOME yaani akuoshee vyombo miaka yote 3 ndo umpeleke shule!!! <br />
hehe heheh
<br />
<br />
Maria, hiyo ya kupelekana shule ni kama bonus tu wala haipo kwenye mkataba au wewe ulikuwa unapendekeza baada ya muda gani!?
 
Big up kaka, but hiyo miaka mitatu mingi sana, huyo binti inabidi asome, ipo siku atanufaika na kusoma na atakushukuru kwa hilo..bora ungefanya hata mwaka mmoja! Ni wazo langu tu mjomba.
 
Ni vizuri kuleta feedback baada ya kuomba ushauri hapa na kuufanyia kazi. Huwa sifurahishwi na watu ambao wanaleta mada ya kuomba msaada wa kimawazo, kisha wanaishia mitini. Matokeo yake watu hatujui kama ushauri wetu ulimsaidia chochote au lah!
 
Chamsingi kinachotakiwa hapo cha msingi we umuite na umuite na umpe ushauli na kumuelimisha na matatizo yake jambo la hekima ajue mazala yake na faida yake asitamani mambo ambayo yapo juu ya uwezo wake.hongela kwa msimamo wako mzuri hapo tanzania bila ukimwi itawezekana
 
Back
Top Bottom