Re: Hotuba ya mr. President

werema01

Member
Feb 10, 2010
47
0
Mr president anaonesha wao kama chama cha ccm wana nia ya wazi ya kuwapa wanawake nafasi muhimu za uongozi nchini kama sehemu ya kuwawezesha.... Na hili anasema ndo maana wakamteua mama makinda agombee uspika.

Najiuliza maswali

1. Kwanini asingeacha kutetea nafasi yake nawamteue mwanamke na badala yake akawa ndugu six?

2. Kwanini ndani ya ccm ni wanawake hawapewi nafasi lakini serikalini na kwenye mambo mazito ya kitaifa ndo wanapewa nafasi?
Mfano: 1. Halimashauri kuu ni wanaume watupu nafasi zote za juu kutoka m/kiti, makamu m/kiti wawili na ma-makamu m/vyiti wao na katibu mkuu.
2. Kamati kuu (cc) ina wanawake (wajumbe wa kawaida) 15% tu.

Hapa pana nia ya kweli au kugarashia tu? Tujadili nia ya kweli ya watu hawa kuleta tanzania yenye neema kama wanavyosema
 
Back
Top Bottom