RE: Hatua za kufungua biashara ya Insurance Agent

newazz

JF-Expert Member
Mar 28, 2009
843
780
Nina azima ya kusajili kampuni ili nifanye biashara kama insurance agent, nilipotazama kwenye TIRA website, nikaona masharti yameanishwa na mengine yananitaka nifanye mambo kadhaa, ikiwemo ya kuwa na principal officer. Ukiangalia masharti yanaonekana kuwa makubwa sana kwa insurance agent , sina uhakika kama ni hivyo au imechanganya na masharti ya insurance brokers!!

Je hili sharti la details za principal officer ni hata kwa insurance agent au kwa brokers tu.

Naomba ushauri kama kuna mtu ambaye, ameshafanya mchakato huu na kuanzisha insurance agent. Asante kwa ushauri wa hatua ulizopitia.
 
Mkuu hilo suala la kuwa na "principal officer" ni sharti kwa watu wote, Agent or broker, mwezi mmoja uliopita nilikuwa nina mchakato kama wako, ila hilo suala la kuwa na huyo mtu lisikukwamishe sana, hapo unatakiwa umtafute mtu aliyesomea masuala ya insurance, mkubaliane utumie cheti chake wakati wa kupeleka usajili wako kwa ofisa wa bima. Na sio lazima awe ana bachelor, hata mwenye certificate anatosha. Na sidhani kama unahitaji kuwa na usajili wa kampuni, hayo masharti ukiyatizama yanaonekana makubwa ila yanatekelezeka bila vikwazo
 
Mkuu che wa Tz,

Asante sana kwa ushauri murua, maana biashara naiona ipo , ila nilikuwa nakwaza na mambo madogo madogo, kama hayo.

Sikuamini kweli JF nzima hakuna mtu ambaye amepitia issue kama hiyo, long live JF ni sehemu nzuri ya kuconnect, nikihitaji jambo nitakupm, asante kwa mara nyingine.
 
Back
Top Bottom