RC Mbeya amtimua Mkurugenzi

Kiongozi awe mpole.

Kind words can be short and easy to speak, but their echoes are truly endless.
Mother Teresa
 
Mama Munuo chapa kazi usijali, sababu najua ulikuwa unaongea kwa mapana kuhusu matatizo ya uchafu mjini Mbeya, ambapo mkuu wa mkoa ilibidi na yeye aplay part yake kusolve tatizo.

Mama Munuo kasema bajeti imeruhusu magari 2 wakati kwa level ya uchafu inatakiwa magari 10. Sasa mkuu wa mkoa angekuwa na busara angehamasisha wananchi kupunguza kutupa uchafu kwa sababu sometimes Kinga ni muhimu, kwa hio kama uchafu ukipunguzwa labda hayo magari 2 yatatosha.
 
Sasa angalia wanasiasa wetu! wanamshupalia huyu mama badala ya kuangalia namna wanavyoweza kumwezesha kupata nyenzo za kufanyia kazi ( jiji lina magari mawili, ameomba mawili zaidi wakati anahitaji kumi.)! Au walitegemea atazunguka mwenyewe na kutoa uchafu kwa mikono yake? Wao,, ndiyo wawajibike kwa kutompa mtendaji nyenzo na support ya kumwezesha kufanya kile walichotarajia! Ndiyo yale ya kuwa na mlinzi kavaa kata mbuga na upinde halafu anapokimbia wakija watu wa kazi unamlaumu na kudai kuwa alishirikiana nao! Hatutafika kwa mwendo huu.

Pamoja na ubabe mwingi alionao Mwakipesile kwa hili la kumshupalia huyu mama yuko sahihi.Huyo mama sielewi kama anajua maana ya kuwa mkurugenzi ni nini? Ina maana kama hana hayo magari ya kuzoa takataka hayapo ya kutosha anachotakiwa kufanya ni kukaa ofisini akipokea mshahara wa kikurugenzi akisubiri miaka hiyo magari yatakapoletwa azoe hizo taka? Ina maana kazi yake yeye ya ukurugenzi ni transport officer wa magari ya takataka ambayo kama hayapo yeye hana cha kufanya kuhakikisha takataka zinazolewa?

Hawezi kufanya kazi under limited resources? Hawezi kama mkurugenzi kukaa na kubuni mbinu mbadala za kuhakikisha taka zinazolewa hata kama jiji halina gari hata moja la kuzoa taka? Ina maana huyo mama hajui kuwa kuna mbinu mbadala au kama hajui anataka nani ambunie hizo mbinu na kumpelekea yeye? Hajui kuwa ukurugenzi ni pamoja na kutafuta mbinu mbadala za utatuzi wa tatizo kama una limited resources? Kusema sababu hakuna magari na bajeti ya uzoaji takataka ni excuse ya kutozolewa takataka nadhani kunaonyesha huyu mama uwezo wake wa kufikiri na kupanga mipango ya uzoaji taka under limited resorces hana.

Iko miji haina vitendea kazi vya kuzoa takataka lakini hutumia mitindo mbadala kama ya watu binafsi kuzoa na kulipwa na wale wenye takataka.Ziko njia mbadala kibao ambazo angeitumia kuhakikisha taka zinazozolewa.

Jibu huyo mama alilompa Mwakipesile ingekuwa mimi ndio mkuu wa mkoa ningemtandika kibao huyo mama na mihasira yangu.Jibu alilotoa huyo mama liko chini ya kiwango cha mkurugenzi na msomi.Ni jibu ambalo hata mtu ambaye hakwenda shule hakustahili kulitoa.Mama kama huyu ndio wanaaibisha wasomi waonekane kuwa vituko na watu waone kuwa wasomi ni mbumbumbu wasiokuwa wabunifu kwenye kutafuta ufumbuzi wa matatizo kunapokuwa na constraint ya limited resources.

Mwakipesile simpendi sana kwa kuwa naye ana ujinga wake ulikubuhu lakini kwa hili la kumwambia aondoke mbeya akatafute kazi ingine na mimi naungana na mwakipesile.Kwa kuwa huyo mama kama anataka hadi apewe magari ya kutosha ndipo taka taka zizolewe wakati uwezekano wa kupata magari zaidi haupo basi ni vizuri huyo transport officer wa magari ya takataka aondoke mbeya aende yaliko ya kutosha au akatafute kazi ingine kama alivyosema mwakipesile.
 
...wote wapuuzi tuu ndio maana mji ni mchafu,wangekuwa na akili mji ungekuwa msafi,hakuna excuse ya magari hapo wala nini,na huyo mwakipesile he must shut the fcuk up maana mji ni mchafu na yeye ndio mkuu wa kaya,kumpandishia mama kwa mihasira isiyo na kiwango hazisaidii usafi!
 
......wataalamu wetu huwa wanakabiliana na wakati mgumu sana kutoka kwa wanasiasa...mara nyingi wanasiasa ni watu wanaoangalia sifa..kuliko ukweli halisi...

nani ambaye hajuwi kwa dunia ya leo na idadi ya watu inakuwa kwa kasi ..jiji lazima liwe na miuondombinu ya kuondoa taka ngumu na maji????

..mitaro...,magari ya maji taka,mabwawa ya maji taka[stabilization ponds or waste treatments ponds,garbage collection vehicles[ratio 1:5,000]-jiji lenye wakaazi milioni linahitaji anglau magari 20-nadhani mkurugenzi ameomba 10 kwa sababu mbeya bado wanamaeneo ya kuchimba mashimo ya taka kwenye ngazi ya familia,...mbeya watahitaji dampo la kisasa [lenye matrekta na bulldozer ya kutosha].....

.....sasa wana MBEYA bila kupata vifaa kama hivyo ..mtamfukuza kila mtu kazi..!!!....rescue plan ya kusolve tatizo la mbeya itahitaji at least 1.2bilioni..tshs...wapate lori [za kawaida tata 10-tani 18 @ 80,000,000],bulldozer lenye uwezo wa kuchimba na ku load weka kama 200m........na pesa za utekelezaji [vifaa vinginevyo ]at least 200million......that is the best you can do ..tena hapo kama watanunua vifaa moja kwa moja kwa wazalishaji[single souce]..kama watatumia tender ...ya kawaida wanaweza kujikuta wakipata vifaa kama hivyo kwa 2 billion....hapo ndio unapata uzuri na ubaya wa tenda ....

nashauri serikali inaponunua vifaa vinavyojulikana watengenezaji ni bora waende moja kwa moja bila kutumia madalali......kwani miradi mingi inakwama kwa sababu bei zinakuwa inflated sana......wenzetu kama uganda na rwanda hawezi kumpa kazi dalali ....kama kiwanda kinajulikana ...buy direct...na as you know viwanda havina muda wa kujaza tenda ...you have to aproach them direct...
 
......wataalamu wetu huwa wanakabiliana na wakati mgumu sana kutoka kwa wanasiasa...mara nyingi wanasiasa ni watu wanaoangalia sifa..kuliko ukweli halisi...

nani ambaye hajuwi kwa dunia ya leo na idadi ya watu inakuwa kwa kasi ..jiji lazima liwe na miuondombinu ya kuondoa taka ngumu na maji????

..mitaro...,magari ya maji taka,mabwawa ya maji taka[stabilization ponds or waste treatments ponds,garbage collection vehicles[ratio 1:5,000]-jiji lenye wakaazi milioni linahitaji anglau magari 20-nadhani mkurugenzi ameomba 10 kwa sababu mbeya bado wanamaeneo ya kuchimba mashimo ya taka kwenye ngazi ya familia,...mbeya watahitaji dampo la kisasa [lenye matrekta na bulldozer ya kutosha].....

..,bulldozer lenye uwezo wa kuchimba na ku load weka kama 200m........na pesa za utekelezaji [vifaa vinginevyo ]at least 200million......that is the best you can do ..tena hapo kama watanunua vifaa moja kwa moja kwa wazalishaji[single souce]...
Kwa sasa wanahitaji bulldozer kwa haraka mno, na ukirejea kikao chao kilikuwa kinahusu Barabara na sio tatizo la taka katika Jiji hilo changa. Landfill yao haina bulldozer hivyo taka hizo chache zinazokusanywa huishia kurudi tena barabarani.

Mkuu wa Mkoa na Mkurugenzi wake wanahitaji japo kukodi bulldozer kwa muda kuondoa taka zilizojuu katika Landfill yao. Na Iwapo Jaa hilo limejaa, ni vema kutafuta sehemu nyingine.
 
...mwakipesille au mkuu wa mkoa hana ubavu wa kumfuta kazi mkurugenzzi...hawa wote bosi wao mmoja....

..huyu mama kasema kweli ila lugha aliyotumia haikuwa muafaka...ila amewambia ukweli unaouma...kama hakuna resources ni ngumu kufikia malengo..thats not romours...

Mama Munuo ni experienced officer ambaye kaacha record nzuri sehemu zote alizofanyakazi. RC huyo anajulikana kwa jazba na ubabe unaotokana na background yake ya upolisi (konstebo) na umeneja wa muda mrefu wa baa za DDC Dar es Salaam. Alifanyakazi na babangu huyu jamaa - jazba ile mbaya! Hana uzoefu mzuri wa uongozi, yeye ngumi tu za DDC Kariakoo. Pole Mama Munuo, usikate tamaa. Hao ndo appointees wa mzee wa mtandao!
 
Hawezi kufanya kazi under limited resources? Hawezi kama mkurugenzi kukaa na kubuni mbinu mbadala za kuhakikisha taka zinazolewa hata kama jiji halina gari hata moja la kuzoa taka? Ina maana huyo mama hajui kuwa kuna mbinu mbadala au kama hajui anataka nani ambunie hizo mbinu na kumpelekea yeye? Hajui kuwa ukurugenzi ni pamoja na kutafuta mbinu mbadala za utatuzi wa tatizo kama una limited resources? Kusema sababu hakuna magari na bajeti ya uzoaji takataka ni excuse ya kutozolewa takataka nadhani kunaonyesha huyu mama uwezo wake wa kufikiri na kupanga mipango ya uzoaji taka under limited resorces hana.

Iko miji haina vitendea kazi vya kuzoa takataka lakini hutumia mitindo mbadala kama ya watu binafsi kuzoa na kulipwa na wale wenye takataka.Ziko njia mbadala kibao ambazo angeitumia kuhakikisha taka zinazozolewa.

Jibu huyo mama alilompa Mwakipesile ingekuwa mimi ndio mkuu wa mkoa ningemtandika kibao huyo mama na mihasira yangu.Jibu alilotoa huyo mama liko chini ya kiwango cha mkurugenzi na msomi.Ni jibu ambalo hata mtu ambaye hakwenda shule hakustahili kulitoa.Mama kama huyu ndio wanaaibisha wasomi waonekane kuwa vituko na watu waone kuwa wasomi ni mbumbumbu wasiokuwa wabunifu kwenye kutafuta ufumbuzi wa matatizo kunapokuwa na constraint ya limited resources.

We, Netanyahu, we! Usitake kutudanganya. Tuambie ni Jiji gani ambalo limeweza kutatua tatizo la taka kwa kutegemea magari mawili? Hata hayo kumi anayoyasema ni under-estimate kama unataka kutatua tatizo hilo.

Unadai itafutwe mbinu mbadala ya ku-privatise au ku-outsource hili suala. Lakini hao watu binafsi unaowasema wana uwezo gani? Na ni nani atakaye-guarantee kuwa watalipwa kwa kazi hiyo? Lingine ni uwezo wa watumiaji kulipia gharama za huduma hiyo. Mwisho, kwa nini wakazi walipishishwe kwa ajili ya huduma hiyo wakati wanalipa kodi ya maendeleo? Unfortunately, jibu lako linaonyesha upeo wa kufikiri wa wanasiasa na wengi wa wanaojiita wasomi nchini kwetu.

Hao wanasiasa badala ya kumkejeli huyu mama, wangekaa na kuangalia wapi wanaweza kumsaidia. Utakuta kwenye hizo unazoziita limited resources kuna matumizi kibao yasiyo na maana yanayowafaa wao! Kwa mfano, bila shaka kwa kukaa kwenye hicho kikao wanategemea kibahasha. Kwa nini wasianze kwa kuondoa vibahasha hivyo ili fedha zitakazookolewa zisaidie katika kutoa huduma? Utakuta humo humo kwenye bajeti kuna matumizi kibao ya safari na huduma zinazolenga vibosile hao! Kwa nini wasijiangalie wao kwanza na mchango wao katika kufuja resources za jiji?

Kitu cha kwanza na cha muhimu ambacho hao wanasiasa na watu kama wewe mnachohitaji kujua ni kuwa "there are no free lunches in this world". Usomi si uungu kwamba unaweza kulisha maelfu kutokana na vipande vichache vya mkate!

BTW kumtandika kibao mwenzako kungekufikisha lupango. Ubosi haukupi haki ya kuwa abusive. Viongozi wenye mawazo kama yako ndiyo waliotufikisha hapa tulipo.
 
operesheni sio kazi.... kazi inahitaji mipango. Hii ni hata kwa ukusanyaji wa taka. Wengi wanaiga opereshi za usafi katika Jiji la DSM. Hili ni kosa, tena kosa kubwa sana katika utendaji. Si Munua wala Mwakipesile mwenye kosa hapa. Tatizo ni hao Wadiwani ambao wanawajibu wa kupisha bajeti na ndio watunga sera.

Mkurugenzi wa Jiji anafuata sera za madiwani, na iwapo Waheshimiwa Madiwani wameamua kuwa wachafu - "we can do nothing about that.."

Na huyo Mkuu wa mkoa aibu ya uchafu ipo juu yake vilevile... Mbeya kuna JKT, Mageraza, Polisi na asasi binafsi ambao wanaweza kutoa magari yao kukusanya taka.. aidha makontraka wanaweza kutoa bulldozer kuhakikisha Jaa kuu lipo katika hali nzuri...

Ukirudi kwenye ushirikishwaji wa wananchi katika tatizola taka utaona wazi kuwa kuna uzembe fulani katika watendaji wa idara ya afya...

Hebu wasafiri kidogo hadi Iringa na waone mafanikio yao.. au waende hadi Kilimanjaro na kuangalia juhudi zao katika taka... Mwisho wanaweza hata kutembelea Jiji la Mwanza na kujifunza namna ya kukusanya taka katika kiwango cha upungufu wa vitendea kazi.

Au wanaweza kwenda katika halmashauri ya Mji wa Kinondoni na kusoma namna ya ukusanyaji wa taka kwa kuwashirikisha wananchi.

Iwapo ni tatizo la sehemu ya kutupia taka hizo, ni vema wakawasiliana na Halmashauri ya mji wa Zanzibar, ambao kwa upeo mkubwa wameweza kutatua tatizo kama hilo...

Mantiki ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ni tabia ambayo ipo kwa viongozi wengi ambao kwa namna moja ama nyingine wameshindwa kukubali kuwa kuna tatizo katika suala zima la ukusanyaji na utupaji wa taka katika Miji mingi ya Tanzania. Hiki ni kiburi cha hali ya juu na ulimbukeni wa madaraka.

Iwapo Jiji la Mbeya linasimamiwa na Mkuu wa Mkoa, Meya na Mkurugenzi, huku Waheshimiwa Madiwani wakiwa ndio watunga sera, ilikuwa ni jambo la busara kwa Mkuu huyo wa Mkoa kutuma shutima zake kwa Madiwani badala ya Mkurugenzi wa Jiji...

Kilio cha Madiwani kuajili Mkurugenzi wanaomtaka wao, kinafaa sana kulinganishwa na tukio hili. Huu ni wakati wa serikali kuu kuona ukweli wa matakwa ya Madiwani kudai kuajili Mkurugenzi wao badala ya kusubiri ateuliwe na Rais...
 
Last edited:
operesheni sio kazi.... kazi inahitaji mipango. Hii ni hata kwa ukusanyaji wa taka. Wengi wanaiga opereshi za usafi katika Jiji la DSM. Hili ni kosa, tena kosa kubwa sana katika utendaji. Si Munua wala Mwakipesile mwenye kosa hapa. Tatizo ni hao Wadiwani ambao wanawajibu wa kupisha bajeti na ndio watunga sera.

Mkurugenzi wa Jiji anafuata sera za madiwani, na iwapo Waheshimiwa Madiwani wameamua kuwa wachafu - "we can do nothing about that.."

Na huyo Mkuu wa mkoa aibu ya uchafu ipo juu yake vilevile... Mbeya kuna JKT, Mageraza, Polisi na asasi binafsi ambao wanaweza kutoa magari yao kukusanya taka.. aidha makontraka wanaweza kutoa bulldozer kuhakikisha Jaa kuu lipo katika hali nzuri...

Ukirudi kwenye ushirikishwaji wa wananchi katika tatizola taka utaona wazi kuwa kuna uzembe fulani katika watendaji wa idara ya afya...

Hebu wasafiri kidogo hadi Iringa na waone mafanikio yao.. au waende hadi Kilimanjaro na kuangalia juhudi zao katika taka... Mwisho wanaweza hata kutembelea Jiji la Mwanza na kujifunza namna ya kukusanya taka katika kiwango cha upungufu wa vitendea kazi.

Au wanaweza kwenda katika halmashauri ya Mji wa Kinondoni na kusoma namna ya ukusanyaji wa taka kwa kuwashirikisha wananchi.

Iwapo ni tatizo la sehemu ya kutupia taka hizo, ni vema wakawasiliana na Halmashauri ya mji wa Zanzibar, ambao kwa upeo mkubwa wameweza kutatua tatizo kama hilo...

Mantiki ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ni tabia ambayo ipo kwa viongozi wengi ambao kwa namna moja ama nyingine wameshindwa kukubali kuwa kuna tatizo katika suala zima la ukusanyaji na utupaji wa taka katika Miji mingi ya Tanzania. Hiki ni kiburi cha hali ya juu na ulimbukeni wa madaraka.

Iwapo Jiji la Mbeya linasimamiwa na Mkuu wa Mkoa, Meya na Mkurugenzi, huku Waheshimiwa Madiwani wakiwa ndio watunga sera, ilikuwa ni jambo la busara kwa Mkuu huyo wa Mkoa kutuma shitima zake kwa Madiwani badala ya Mkurugenzi wa Jiji...

Kilio cha Madiwani kuajili Mkurugenzi wanamtaka wao kinafaa sana kulinganishwa na tukio hili. Huu ni wakati wa serikali kuu kuona ukweli wa matakwa ya Madiwani kudai kuajili Mkurugenzi wao badala ya kusubiri ateuliwe na Rais...

Hivi wewe Kibs lugha inapanda kweli maana sijawahi hata siku moja kusoma bandiko lako lililo ktk lugha ya kiingereza. Dizaini lugha haipandi wewe.....
 
Hivi wewe Kibs lugha inapanda kweli maana sijawahi hata siku moja kusoma bandiko lako lililo ktk lugha ya kiingereza. Dizaini lugha haipandi wewe.....
Nyani wacha utani wako, kwani hii mada imekuja kwa lugha gani?
 
Last edited:
Mkuu wa Mkoa hana ubavu wa kumfukuza kazi mteule wa Rais, kumbuka wakurugenzi ni presidential appointee hivyo anayeweza kumfukuza kazi ni Waziri wa TAMISEMI baada ya kupata kibali cha Rais.

Mnuo kama ninavyomjua mimi ni mtendaji mzuri, ebu watu wa Iringa waseme hapa maana kabla ya kuhamishiwa Mbeya alikuwa Manispaa ya Iringa.

Hapa mwandishi anakuza tu mambo ili kumharibia mtu either mama Mnuo au Mwakipesile. Hizi politics za Tanzania, zisizo angalia ujenzi wa Taifa na kujikita katika mifarakano, fukuza fukuza nk, haziwezi kutusaidia kujenga nchi.

Tatizo letu tunaweka siasa mbele kuliko taaluma.
Ahsante
 
Back
Top Bottom