Rasimu ya Mswada wa Sheria ya Kuandika Katiba Mpya - The Proposed Constitutional Review Act

We cannot solve our problems with the same thinking we used when we created them. - Albert Einstein
Einstein.jpg
 
Wadau,
Baada ya kuukataa muswada wa sheria ya uundwaji wa tume maalum itakayoshughulika na kukusanya maoni ya wananchi ili kuleta katiba mpya, Serikali imeandaa muswada mwingine ambao ndio utawasilishwa bungeni hivi karibuni.
Muswada huu mpya umeingiza mambo kadhaa ambayo wadau waliyalalamikia kama vile:
1. Ushiriki sawa wa rais wa Zanzibar katika uteuzi kama ilivyo kwa rais wa muungano.
2. Muswada kuwa katika lugha za kiswahili na Kiingereza.
3. Kuwepo kwa bunge la katiba(japo wamelichanganya na wabunge wa sasa na wajumbe wa baraza la wawakilishi wa sasa).
4. Time frame zinazoeleweka kidogo n.k

Tatizo kubwa ambalo tunalikataa na bado serikali imelirudisha ni madaraka ya rais katika uundaji wa katiba mpya. u-Rais wa Tanzania ni cheo kinacholalamikiwa kuwa na madaraka makubwa mno, na sasa katika uandikaji wa katiba ya watanzania wote bado rais anapewa kusimamia kila kazi inayohusiana na katiba hii.

Tume ya taifa ya uchaguzi NEC na tume ya taifa ya uchaguzi ya Zaznibar ZEC bado zinapewa mamlaka yaleyale ya kusimamia masuala ya kura za maoni za wananchi wakati wa kupitisha katiba.

Serikali ya CCM ina kichwa kigumu sana, haisikii wala kusikiliza. Yaani tume ile ile inayochakachua matokeo ya uchaguzi kila kukicha ndiyo inapewa kazi ya kusimamia suala muhimu la katiba. Tume ya rais, katiba ya rais,nchi ya rais.

Ati mkuu wa wilaya, mtendaji wa kata,mtendaji wa kijiji na mtendaji wa mtaa ndio wanapewa kazi ya kusimamia taratibu za ukusanyaji wa maoni ngazi ya chini, ARE WE SERIOUS?

Kwani mpaka watu wabebe bunduki ndiyo serikali ione wananchi wanahitaji katiba mpya ya wananchi na siyo ya rais, DC,WEO,VEO,NEC,ZEC n.k?

Hivi ikulu ina hofu gani ikitengeneza utaratibu wa uhakika na wa haki wa kuleta katiba mpya? Kwa nini kila jambo katika kuleta katiba anapewa rais, kwa nini tusiunde tume maalum itakayoteuliwa kwa utaratibu maalum ikiwa na watu maalum ambao hata upatikanaji wao utatokana na uadilifu wao na watu hao watahojiwa kikamilifu live mbele ya watanzania wote katika televisheni n.k?

Kuna biashara gani katika ku-complicate hivi suala la katiba? Kwani serikali haijui ma-WEO, VEO, NEC, ZEC, DC, RAIS na kadhalika ni watu ambao wamelaumiwa sana kwa udhaifu mkubwa ambao wamekuwa wakiuonesha katika chaguzi mbalimbali na katika utendaji wao kwa ujumla kwa maana ya kuisaidia CCM?

Hivi sasa nchi inayumba sana kiuchumi, mfumuko wa bei, matatizo ya umeme na mauchafu kedekede, kwa nini rais wetu asishughulikie haya suala la katiba likawekwa katika mikono ya watu safi wanaoaminiwa na jamii ya watanzania?

Wasiwasi wangu ni kwamba, CCM wana hofu kuwa tukipata katiba ya haki ya ukweli ya maadili ya dira safi - wanajua wataondoka madarakani immediately. Lakini njia ya mwongo ni fupi sana, hii katiba ya RAIS na IKULU yake na chama CHAKE, tutaipinga kwa nguvu zote.

Kwa bahati mbaya hapa duniani, tangu ulimwengu uumbwe, haijawahi kutokea SERIKALI na MAJESHI yaliyowashinda wananchi wenye kiu ya haki na mabadiliko ambavyo ni haki yao.

TEMBELEENI TOVUTI YA BUNGE ,SOMENI KWA MAKINI - SOTE TUCHUKUE HATUA KWANI KATIBA HII SIYO YA MTU MMOJA NA FAMILIA YAKE NA MARAFIKI ZAKE, NI KATIBA YETU SOTE, WATANZANIA!

Julius Mtatiro,
26 Oktoba 2011.

mtatiro hao ndo watu mlioingia nao ubia kuifilisi nchi
 
Wanasiasa bwana! Kwanza CCM haikuwa na wazo la katiba mpya kwenye ilani yake,bali hili wamelikubali kutokana na joto kali ili waendelee kuaminika.Hivyo CCM na serikali yake wamekubali lakini wameweka limitations ili kujilinda,kamwe hawawezi kupeana talaka na NEC au ZEC.

Mbali na CCM ukweli ulio wazi ni kuwa wapinzani wakubwa CHADEMA,CUF na NCCR ambao ni wapiga debe wa katiba mpya, hawa wote hawana jipya zaidi ya uchaguzi ili kuingia ikulu tu! Kila wakati utasikia tume huru ya uchaguzi na kwa hili naomba kusema wapinzani wamerogwa na uchaguzi, kwani kila wakilala wanawaza na kuota uchaguzi.

Slaa na Mtatiro hebu tuambieni juu ya rasilimali zetu na sio mauchaguzi.Hakuna kati ya ccm,chadema wala cuf wanaosema katiba mpya rasilimali zetu tuzilindeje na tuzitumieje au vipaji vya wazalendo juu ya ugunduzi na sayansi tuvitumieje na tuvihifadhije ili tusiendelee kutegemea wazungu na teknolojia zao,badala yake wanalia na uchaguzi.

Kama itakuwa hivi hata katiba mpya ikipatikana maisha ya mtazania wa kawaida hana chake. Jamani tuwaangalie sana wanasiasa!kwan katiba sio yao bali ni yetu wananchi.
 
Bwana Itatiro, ni kweli mswada mpya una mapungufu ila angalao wamerekebisha baadhi ya mambo. Mapungufu ninayoyaona kkwa haraka ni haya:

(a) Marais kuteua tume na sekretariat. Angalao kwa vile wameweka vigezo vya wateuliwa, itakuwa si rahisi kuteua watu wa CCM, ila tujaribu kujadili njia nzuri ya kuteua watu huru kama ipo

(ii) Tume za uchaguzi, hapa kuna tatizo maana hawajasema kama kutakuwa na waangalizi wa vyama au interest groups. Nadhani kama watu wakipata nafasi ya kujiandikisha na kukiwa na waangalizi wanaweza kusimamia tu maana katiba mpy ndio itaunda tume mpya ya uchaguzi. Kama tunaweza kuwa na tume ya muda itasaidia zaidi.

(iii) Swala la Zanzibar ni tatizo. Kwanza nikuulize Mtatiro, vipi katiba ya Zanzibar haina tatizo? nafikiri kama CUF mkiona ina matatizo mshinikize kuundwe sambamba katiba ya Znz. Mimi naungana na Tundu Lissu alitoa maelezo mazuri sema tu watu hawachambui vizuri

(a) Znz wanahusika tu na mambo ya muungano maana wana katiba yao. Kuwahusisha katiba nzima hasa ukizingatia watakuwa na 1/3 kwenye bunge la katiba ni tatizo

(b) Wajumbe wa bunge la katiba Znz lazima 2/3 waunge mkono ili katiba ipite. Hii katiba si ya Znz ni ya wabara kwa kiasi kikubwa. Nadhani wangesema Znz wapigie kura mambo ya muungano tu na 2/3 waunge mkono ili ipite

Nakushauri Itatiro, kwa jinsi mswada ulivyokaa CUF imepata nguvu nzuri na bila CUF katiba haitapita. Kwanini? Tunahitaji 2/3 ya wabunge wa znz waunge mkono, 50% ya wazanibari waunge mkono kwenye referandum.

Sasa ni nafasi ya CUF kushinikiza mambo fulani kama serikali tatu, tume huru ya uchaguzi nk yaingizwe kwenye katiba mpya la sivyo mtaipinga na kweli haitapita.

Hata Chadema watakuwa na nafasi kubwa ya kukwamisha katiba kama haitaweka vitu kama serikali tatu, tume huru, nk maana si rahisi CCM kupata 2/3 majority bunge la katiba
 
Wanasiasa bwana! Kwanza CCM haikuwa na wazo la katiba mpya kwenye ilani yake,bali hili wamelikubali kutokana na joto kali ili waendelee kuaminika. Hivyo CCM na serikali yake wamekubali lakini wameweka limitations ili kujilinda,kamwe hawawezi kupeana talaka na NEC au ZEC. Mbali na CCM ukweli ulio wazi ni kuwa wapinzani wakubwa CHADEMA, CUF na NCCR ambao ni wapiga debe wa katiba mpya, hawa wote hawana jipya zaidi ya uchaguzi ili kuingia ikulu tu!

Kila wakati utasikia tume huru ya uchaguzi na kwa hili naomba kusema wapinzani wamerogwa na uchaguzi, kwani kila wakilala wanawaza na kuota uchaguzi. Slaa na Mtatiro hebu tuambieni juu ya rasilimali zetu na sio mauchaguzi. Hakuna kati ya ccm, chadema wala cuf wanaosema katiba mpya rasilimali zetu tuzilindeje na tuzitumieje au vipaji vya wazalendo juu ya ugunduzi na sayansi tuvitumieje na tuvihifadhije ili tusiendelee kutegemea wazungu na teknolojia zao, badala yake wanalia na uchaguzi.

Kama itakuwa hivi hata katiba mpya ikipatikana maisha ya mtazania wa kawaida hana chake. Jamani tuwaangalie sana wanasiasa!kwan katiba sio yao bali ni yetu wananchi.

rasilimali hazilindiki ni kwa sababu ya madhaifu ya katiba iliyopo. wote wanahusika na rasilimali, wamechaguliwa na magamba ya ccm. kwa hali hii unategemea kulinda rasilimali zetu? suluhisho ni katiba, ndiyo itakayofuta sheria zote kamndamizi za madini, uwekezaji, kodi na nyingine nyingi zinazofanikisha uporaji wa rasilimali zetu.

katiba mpaya, tunaitaka ili pia itoe mwongozo wa namna ya kupatikana sheria yoyote ile. ikiwezekana sheria zote kabla ya kutumika, zipate baraka za umma na ziwe kwa lugha umma unayoiweza kuliko sasa hivi kila kitu ni siri hata yasiyotakiwa kuwa siri, yamefanywa siri
 
]Ngoja nirekebishe miwani nisome vizuri[/B]

Hivi unaweza kuwa serious sometimes au muda wote kwako ni wa mchezo?!! Watu wanajaribu kuchambua suala la msingi wewe unajaza nafasi kwa kuandika hivyo hapo juu kwanini usingerekebisha miwani ukasoma kabisa ili ukipost kiwe ni kitu chenye kujenga?!!!!!!
 
Hivi hii ya Rais wa ZNZ na Tanzania kushirikiana kuteua imekaaje?? Hivi ina maana Wazanzibar hawamtambui Rais wa nchi kuwa ni Rais wao pia?? Kwa mtizamo huu hii katiba surely inahitaji serikali tatu ili usawa uwepo!!!

Anyway, kwa jinsi Mtatiro alivyotudokeza inaelekea tunafanyiwa mazingaombwe hapa. Sasa kituo cha haki za binadamu na TLS kazi tunawachia nyinyi!! Badala ya kupigania malipo ya Dowans naona hii ni ya maana zaidi kama kuna kuchagua!!
 
Kama watu wanaona kuwa mambo muhimu hayamo kwenye mswada huu ni wa kuukataa tu. Ni bora watu wasubiri chama ambacho kitakuja kuandika katiba mpya kwa misingi ya uwazi, usawa, demokrasia na utu wa Watanzania kuliko kuburuzwa kwa sababu watu wanataka Katiba Mpya. Tusiburuzwe kwani tutakachoandika ndio urithi wetu kwa kizazi kijacho.

Hapo kwenye red sijakupata kabisa. Maana kama inakuwa vigumu kuruhusu uwepo wa mambo ya msingi katika ukuaji wa taifa...ni lini itaonekana kuwa inafaa kuwepo na chama kingine? Just thinking loudly!
 
Wanasiasa bwana! Kwanza CCM haikuwa na wazo la katiba mpya kwenye ilani yake,bali hili wamelikubali kutokana na joto kali ili waendelee kuaminika.Hivyo CCM na serikali yake wamekubali lakini wameweka limitations ili kujilinda,kamwe hawawezi kupeana talaka na NEC au ZEC.

Mbali na CCM ukweli ulio wazi ni kuwa wapinzani wakubwa CHADEMA,CUF na NCCR ambao ni wapiga debe wa katiba mpya, hawa wote hawana jipya zaidi ya uchaguzi ili kuingia ikulu tu! Kila wakati utasikia tume huru ya uchaguzi na kwa hili naomba kusema wapinzani wamerogwa na uchaguzi, kwani kila wakilala wanawaza na kuota uchaguzi.

Slaa na Mtatiro hebu tuambieni juu ya rasilimali zetu na sio mauchaguzi.Hakuna kati ya ccm,chadema wala cuf wanaosema katiba mpya rasilimali zetu tuzilindeje na tuzitumieje au vipaji vya wazalendo juu ya ugunduzi na sayansi tuvitumieje na tuvihifadhije ili tusiendelee kutegemea wazungu na teknolojia zao,badala yake wanalia na uchaguzi.

Kama itakuwa hivi hata katiba mpya ikipatikana maisha ya mtazania wa kawaida hana chake. Jamani tuwaangalie sana wanasiasa!kwan katiba sio yao bali ni yetu wananchi.
Huwezi kwepa umuhim wa uchaguzi katika katiba mpya ati kisa rasilimali. Hao wanaopitisha na kusaini mikataba wanapatikana kwa uchaguzi huo huo. Au hulioni hilo?
 
Asante Mwankijiji,

Kwakweli muswada bado ni mbaya na kama ni mbaya basi waliouandaa wanataka ipatikane katiba mbaya. Naomba watanzania wote tuungane kuwapinga ili wasipate nafasi hiyo.

Pamoja na mapungufu mengine yaliyotajwa kuna upungufu mmoja mkubwa ambao ni chombo au baraza/mkutano wa kuandika katiba mpya. Hiki ni chombo muhimu cha wataalamu, Kenya walikuwa na The Bomas huu muswada hauzngumzii lolote kuhusiana na hilo, badala yake kazi imepewa tume ya kukusanya maoni. Na chombo hiki ndugu zangu ndicho kilistahili kupokea taarifa au maoni ya wananchi kutoka kwa tume, lakini badal yake ripoti anapewa Rais, kituko cha karne. Kwa hiyo kama Watanzania tnataka katba nzuri sana tutakayoifurahia lazima chombo hki kiwepo na chenyewe ndiyo kiwasilishe muswada wa katiba mpya kwenye bunge la katiba ambalo nalo lazima liwe na wajumbe huru ambao watachaguliwa kutoka katika kila wilaya za sasa na ambao hawana uhusiano na vyama vya siasa.

Kwa hiyo, ndugu zangu naomba tsikubali ujanjaujanja na usanii wa serikali ambao unonekana wazi wazi katika muswada huu. Lazima wananchi wapate nafasi kubwa na sio viongozi walioingia madrakani kwa kuchakachua uchaguzi.

Asante sana wakuu.
 
Slaa na Mtatiro hebu tuambieni juu ya rasilimali zetu na sio mauchaguzi.Hakuna kati ya ccm,chadema wala cuf wanaosema katiba mpya rasilimali zetu tuzilindeje na tuzitumieje au vipaji vya wazalendo juu ya ugunduzi na sayansi tuvitumieje na tuvihifadhije ili tusiendelee kutegemea wazungu na teknolojia zao,badala yake wanalia na uchaguzi.

Utakuwa unakosea unapoitenga siasa na rasilimali zetu na uchaguzi. Kumbuka bila siasa safi hakuna uchaguzi safi na hapatakuwa na kiongozi safi mwenye uwezo wa kusimamia sheria na hatimaye rasilimali zetu kuwa salama. Hivyo ni vizuri kuizungumzia katiba kutilia maanani kwamba mwisho wa siku ni kumpata kiongozi mzuri atakayewajibika kwa wananchi na kutenda kwa matakwa ya wananchi. Vinginevyo katiba haina maana, kwani ni sawa na kutokuwa na taifa! Kimsingi katiba ni utawala/uongozi.
 
Shukran MM
Kimsingi muswada bado haujakaa sawa kabisa. Bado kuna mapungufu mengi sana. Katiba bado itakuwa ni ya raisi si ya wanannchi. Pia suala la Zanzibara kushiriki kwa 1/3 katika masuala ya bara ni tatizo. zanzibar wana katiba yao kwa nini washiriki kupitisha katiba ya bara? Kwenye masuala ya Muungano ni sawa ila kwanye masuala yasiyokuwa ya muungano hapa muswada bado ni mbichi kabisa. Kitu kingine ambacho nimeona ni bunge la kawadia kuunda bunge la katiba na zaidi sana kanuni za bunge la sasa kutumika. Tumeshuhudia kanuni za ajabu kabisa zikitumia kupitisha vitu vya ajabu ajabu pale bungeni kwa kusema, "wanaosema ndiyo.!!!!," "wanaosema hapa...... Sheria hizi zitatumika kwenye bunge la katiba. Nadhani sehemu hii inahitaji marekebisho. Kanuni za ndiyo na siyo zitatumika kwa sababu hiyo naomba kanuzi za kuchambua katiba mpya ziundwe na si zile za ndiyoooooo, siyoooooo.
Nawataka warudishe mswada huu wakaupitie tena bado haufai.
 
Kuna thread nzuri ya kuhusu katiba ilianzishwa na Julius Itatizo asubuhi nimeisaka sana bila mafanikio. Mod ameiondoa au na ni sababu gani?
 
CCM bado inadhana ya chama kushika hatamu...Nadhani tupiganie kwanza hilo pengine tuwawekee wale watakao kuwa highly costed na mabadiliko haya certain future maana naona wanaogopa kuachia power...

Kikubwa hapo ni huyo mdudu dominant system CCM thru ideology yao ya chama supremacy ambayo ikazaa serikali ya ki aina fulani dictator ndiyo maana utasikia mabalozi wa mtaa sijui wawilaya, wakuu wa wilaya mpaka juu Rais mwenyewe hiyo yote ni system ya CCM ambayo kwa sura ya kura zisizo huru ikajipa mamlaka ya kuunda serikali. Unapo gusa mboni ya jicho lao hilo hawako tayari kwa garama yoyote ile.

Tanzania ni ya kila mtanzania mwana CCM na sasiye amini katika chama chochote hii kufanya watu wa ideology moja kutuamulia future yetu tuikatae kwa nguvu zote. Walipewa nafasi wameitumia kwa miaka 50 sasa we want a change too bad for them kama hiyo miaka haikuwatosha. Hakuna tena chama kushika hatamu tunataka raia kushika hatamu for theirs and our own goods and bads.
 
Wanasiasa bwana! Kwanza CCM haikuwa na wazo la katiba mpya kwenye ilani yake,bali hili wamelikubali kutokana na joto kali ili waendelee kuaminika.Hivyo CCM na serikali yake wamekubali lakini wameweka limitations ili kujilinda,kamwe hawawezi kupeana talaka na NEC au ZEC.

Mbali na CCM ukweli ulio wazi ni kuwa wapinzani wakubwa CHADEMA,CUF na NCCR ambao ni wapiga debe wa katiba mpya, hawa wote hawana jipya zaidi ya uchaguzi ili kuingia ikulu tu! Kila wakati utasikia tume huru ya uchaguzi na kwa hili naomba kusema wapinzani wamerogwa na uchaguzi, kwani kila wakilala wanawaza na kuota uchaguzi.

Slaa na Mtatiro hebu tuambieni juu ya rasilimali zetu na sio mauchaguzi.Hakuna kati ya ccm,chadema wala cuf wanaosema katiba mpya rasilimali zetu tuzilindeje na tuzitumieje au vipaji vya wazalendo juu ya ugunduzi na sayansi tuvitumieje na tuvihifadhije ili tusiendelee kutegemea wazungu na teknolojia zao,badala yake wanalia na uchaguzi.

Kama itakuwa hivi hata katiba mpya ikipatikana maisha ya mtazania wa kawaida hana chake. Jamani tuwaangalie sana wanasiasa!kwan katiba sio yao bali ni yetu wananchi.

Kafikirie upya juu ya Policy na decision makers! Wanapong'ang'ania uchaguzi wanamaana wanataka ridhaa ya watanzania waweze kuwaongoza juu ya matakwa yao ambayo mara nyingi yanaamuliwa na wawakilishi wao halali waliochaguliwa kwa kuzingatia matakwa ya wengi. Sasa wasipofikiria uchaguzi watapataje nafasi ya kutimiza matakwa ya wengi?
 
Kama mswada umeandaliwa na watu walewale na wenye mawazo yaleyale tuliyoyakataa mwanzo unafikiri kuna dhana ya kukidhi matarajio ya Tanzania mpya "over my dead body"
 
Mkuu 2nashukuru kwa hii nakala ingekua ni hapa kenya hata kwny magazeti binafsi ungechapishwa. kwa huko bongo sijajua kama wamefanya hivyo. Basi wahariri wanapaswa wauweke kwny magazeti yao ili uweze kuwafikia wananchi wengi zaidi waone wenyewe ulivyo chaka
 
Back
Top Bottom