Rasilimali za Tanzania zazidi kutafunwa: JK achekelea tu...

The Informer

Senior Member
Jun 14, 2010
119
29
Mwezi Mei mwaka huu, Kikwete alienda Serengeti kupokea vifaru watano waliokuja kwa ndege kutoka Afrika Kusini huku akichekelea kama kawaida yake. Akiwa huko Serengeti, alikutana hotelini na rafiki yake mbunge Lazaro Nyalandu akiwa ameongozana na mamiss. Kikwete hakurudi Dar siku hiyo akalala hotelini Serengeti. Nyalandu sasa ni naibu waziri.

Hiyo ni chombeza tu, lakini issue hapa ni kuwa kifaru mmoja kati ya watano waliokuzwa kwa gharama kubwa Afrika Kusini na kusafirishwa kwa ndege mpaka Tanzania kauliwa na majingili.

Hii ina maana kuwa serikali ya Kikwete inashindwa kulinda rasilimali za nchi. Mimi naona bora hao vifaru wabaki huko huko Afrika Kusini mpaka WILLIBROD SLAA akiwa Rais 2015 na kuunda serikali makini itakayotunza vizuri rasilimali za taifa.

Poachers kill rare black rhino in Tanzania: minister

Thu Dec 16, 2010

By Fumbuka Ng'wanakilala

DAR ES SALAAM (Reuters) - Poachers have killed one of five critically endangered east African black rhinos that were relocated to their natural habitat in Tanzania's Serengeti park from South Africa in May.

The rhino was killed just seven months after its arrival in the Serengeti, despite being implanted with an electronic chip and protected by an elite ranger task force specially trained to guard the animals.

Rampant poaching in the Serengeti -- famed for its sweeping planes and Africa's most spectacular wildebeest migration -- in the 1960s and 70s saw the population of black rhinos in Tanzania plummet from over 1,000 to just 70, denting tourist arrivals.

"We received information on Sunday that one of the five rhinos that arrived from South Africa was missing after a special tracking gadget fitted on the animal went inactive," Ezekiel Maige, Tanzania's Minister for Natural Resources and Tourism told Reuters in a telephone interview on Thursday.

"The rhino's carcass was found in the Serengeti National Park on Tuesday, with the horn cut off. This was clearly the work of a group of poachers."

Rhinos are heavily poached for their horns, which are highly sought-after in parts of the Middle and Far East. It is believed in some cultures that powdered rhino horn has powerful medicinal properties, although this has never been proven.

The five rhinos flown to Tanzania are part of a larger group of 32 animals being reintroduced to Tanzania from a 50-strong herd. The rhinos were bred from seven animals that were relocated to South Africa in the early 1960s.

The remaining 27 rhinos are expected to be returned to their native country in stages over the next two years under the Serengeti Rhino Repatriation project.

The rhinos were flown from South Africa to Tanzania in a chartered Hercules C-130 cargo plane.

Conservation experts had hoped extra protection for the rhinos would also help other species in the park.

Organisers said the relocation was part of a new drive by African governments to protect the "big five" mammals -- lions, rhinos, elephants, leopards and buffalo -- that make up one of the continent's main tourist attractions.

"We have commissioned a serious manhunt to trace the whereabouts of the poachers behind this incident. We are using every means at our disposal," said Maige.

"We are also in talks with the Frankfurt Zoological Society to ensure closer monitoring and surveillance of the animals and the build-up of the necessary resources."

Both Tanzania and Kenya have suffered a spike in poaching, particularly of elephants and rhino, in the past few years. Kenya lost at least six rhinos last year, conservationists say.
 
Hao walio uwawa ni kwa sababu mnawakumbuka walikuwa watano. Ni wanyama wangapi msio na hesabu yao wanateketea.
 
Mkuu,

Kukukumbusha tu Dr,alisema anagombania nafasi ya Urais mara moja tu.

Hili la kuuawa kwa wanyama ni katika mlolongo tu wa mambo mengi ambayo katika Tanzania yetu yanatufanya tuwaze sana na kupata mvi kwa haraka.

Watu,wananchi wengi wanakufa, wanauliwa ovyo ovyo tu,mahospitali kwa ukosefu wa dawa na zana za matibabu. Barabarani kutokana na kutozingatiwa kanuni za kutumia barabara, ujambazi na kwa umaskini kwa ujumla.

Kwa hiyo hapa TZ kila kitu kinauliwa, juzi juzi nimesoma vigogo wanauwa miti Mufindi. Kwa hiyo kifo kimetuzunguka, bandugu !
 
Kwa faida ya wale ambao hawakuipata TAARIFA KAMILI YA CHADEMA
Najua kuna wengi huenda hawakuipata hii. Nimeitafuta sijaiona jamvini baada ya rafiki kuniambia niitafute. Ila nimeikuta feacebook yake. Wanaoitafuta kama mimi, hii hapa

Msimamo wa Chadema haujabadilika

by Dr. Wilbrod Slaa on Tuesday, December 14, 2010 at 7:29pm



Kuna taarifa ambazo zimekuwa zikiandikwa na kuripotiwa na vyombo vya habari ambavyo zinaashiria kuwa Chadema tumebadili msimamo wetu kuhusu masuala ya uchaguzi.

Hakuna mahali popote Chadema imebadili msimamo wake na kusema kuwa Kura hazijaibiwa au kuchakachuliwa. Taarifa niliyotoa jana kwa TBC ilieleza wazi kuwa Kamati Kuu, ilipokea na kujadili na kuridhia mapendekezo yote yaliyowasilishwa na Sekretariat ya Chama kuwa Chadema imekataa matokeo ya Uchaguzi kutokana na irregularities 15. Chadema inaamini kuwa iwapo Katiba ya nchi isingelikuwa imezuia kuhoji matokeo ya uchaguzi Mkuu wa Rais mahakamani, matokeo hayo yangeliweza kubatilishwa. Kwa vile Katiba inakataza kuhoji matokeo kuhojiwa mahakamani, basi japo Kikwete's Presidency ni Lawful it is Illegitimate.

Chadema ilitumia maneno ya kiingereza kuonyesha tofuati kubwa kati ya maneno hayo mawili. Huo ndio msimamo wa Chadema toka mwanzo na haijawahi kuyumba, japo maneno ya kiswahili yamekuwa yakipewa tafsiri tofauti na watu mbalimbali. Ni kwa msingi huo, Kamati Kuu ikasisitiza " Kuundwa kwa Tume Huru" kuchunguza Dosari " Irregularities" hizo kubwa katika uchaguzi. Nasisitiza, Chadema ni Chama ambacho toka mwanzo ilisisitiza kuwa "Haiko Tayari kuingia Ikulu kwa kumwaga Damu ya Watanzania".

Inawezekana wanaopenda na kufurahia vurugu, Chadema haiko tayari kwa hali hiyo. Tunasukumwa sana na wapenzi na wanachame wetu kutoka mitaani na kuandamana, na ndicho pia wanachotaka ndugu zetu akina Mwanakijiji. Maandamano, (ya amani au ya kushinikiza), kwa watu wanaojua mchakato wa demokrasia ni hatua ya mwisho kabisa baada ya njia zingine zote kushindikana. Pili, ili Tanzania isiingie katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015 kwa Katiba na Sheria mbovu kama tuliyonayo leo, Chadema inasisitiza upatikanaji wa Katiba mpya, Shirikishi na ya Wananchi.

Upatakanaji wa Katiba hii utakuwa na mchakato, na kama Serikali haitaki, basi Chadema kwa kushirikiana na wadau na watu mbalimbali wakiwemo wananchi itatutumia njia zote zinazoweza kuipatia nchi Katiba ya Wananchi. Yote haya ni mchakato, na kwa mtu yeyote anayoamini kuwa mchakato huchukua muda, basi atakuwa mvumilivu. Hakuna sababu ya kutumia lugha kali, kukashifiana na kutukanana japo jamvi letu ni mahali ambapo "we dare to speak". Tukivumiliana na kuheshimiana tutafika salama bandarini.

Tukikurupuka tunaweza pia tusifikie lengo tunalotaka. Hekima na busara vikitawala na kuongoza matunda yatakuwa mazuri kwa Taifa letu. Taifa ni letu tukilibomoa hatuna pengine pa kwenda, labda tukiamua kulowea penginepo. Tukikurupuka tunaweza kuwaumiza wanaohusika na wasiohusika. Uvumilivu na Busara daima huvuta heri.




Source: Gonga hapa Msimamo wa Chadema haujabadilika | Facebook


NYONGEZA: Kuna thread imewekwa hapa chini na Mwanajamii mmoja (Chapakazi) anauliza tofauti ya maneno haya mawili (Lawful na Legitimate). Kwa uelewa wangu. Naomba niiongeze hapa kwa mtiririko sahihi. Unaweza toa usahihi zaidi


Moja ya tafsiri za legitimate zilizoko kwenye link hii define: legitimate - Google Search


Zinasema kitu
legitimate ni kile ambacho kiko affirmed to be just na in accordance with recognized or accepted standards or principles.


Na kitu
lawful ni kitu ambacho kiko recognized or sanctioned by law(lawful: meaning and definitions — Infoplease.com.


Kwa upeo wangu hii inamanishaa kitu kinaweza kuwa recognize na sheria lakini kisiwe just kwa sababu hakikiendana na accepted principles



Tukitumia mfano wa tukio lenyewe naweza kusema hivi,

Sheria inasema Raisi ni Raisi kwa kutangazwa na tume (lawful) lakini ili atangazwe lazima kanuni (principle) kadhaa zifuatwe.


Hivyo kama kanuni hazikufuatwa lakini katangazwa (kama sheria inavyotaka) na tume ya uchaguzi basi ni lawful kwa sababu katangazwa kisheria na tume yenye mamlaka ya kisheria kutangaza lakini kama kanuni za kufuatwa ili atangazwe zimevunjwa tunasema ni illegitimate kwa sababu principle s zimekiukwa.


Kwa msaada zaidi gonga hili link uone mfano kule Georgia

http://georgiandaily.com/index.php?o...2829&Itemid=68
 
Back
Top Bottom