Ramadhani & Zarina Madabida na ARVs FEKI (Miradi ya CCM...?)

Phillemon Mikael

Platinum Member
Nov 5, 2006
10,517
8,582
Locally manufactured HIV/AIDS drugs launched, Arusha-based Tanzania Pharmaceutical Industry (TPI) has scored first in East Africa by manufacturing some of the first line drugs used in HIV/AIDS treatment.

The drugs, Stavudine, Lamivudine and Nevirapine or a cocktail of the three (TT-VIR), were launched last weekend by Dr. Krisana Kraisintu, a consultant at the plant and TPI Managing Director, Ramadhani Madabida.

Manufacturing of the drugs in Arusha is a relief to the about 1.6 million Tanzanians living with HIV/AIDS. The drugs when distributed for wider use, after approval by the government, will cost between Tsh.15,000 to Tsh.20,000 for a month's dose.

An estimated 50 to 60 per cent of hospital beds in Tanzania are occupied by patients with AIDS- related illness. With training in pharmaceutical chemistry, Dr. Kraisintu was formerly the director of Research and Development Institute of Thailand's Government Pharmaceutical Organization.

Unable to garner the support of his governmental colleagues, he directed his own organization's research funds to develop and produce generic versions of AIDS medications.

Dr. Kraisintu's homegrown pharmaceuticals proved themselves both medically viable and cost effective were later supplied to patients in Laos, Cambodia and Vietnam. Over 100,000 patients are now able to receive treatment in South East Asia.

With partnership with the German Medical Aid Organization, Dr. Kraisintu has now successfully reproduced his formula on to fight HIV-AIDS on a larger scale, especially in sub-Saharan Africa.

The President of Mount Holyoke College, South Hadley, Massachusetts, Dr. Joanne V. Creighton has hailed him as the "AIDS Warrior" praising his efforts to provide AIDS treatment to those who would otherwise be denied.

"You have revitalized public health efforts around the world to fight the spread of HIV/AIDS", she noted in a statement of appreciation dated 22nd May, 2005.

My Take:
Je Hivi ni aina ya vitega uchumi tunavyohitaji kuwapa makada wa chama ....ili wakichangie chama mapesa kwenye uchaguzi .....kwa kuwauzia watanzania dawa feki za Ukimwi? Ni wangapi wameshakufa?

.....wakurugenzi wa MSD wamechukuliwa hatua...though hao ni scape goats tu. Je, Madabida ..amechukuliwa hatua gani?..au kwa kuwa pesa zilikuwa zinanufaisha CCM.....?

 
Aiseee! Sasa naona jinsi gani ilivyo ngumu kutenganisha CCM na UFISADI... maana hawa jamaa akina Madabida ndio wenyewe kwenye CCM
 
Waathirika nao wanatakiwa waifikishe mahakamani serikali,huu ni uuaji jamani
 
kama wachina waliwanyonga ,wamiliki wa kiwanda cha kutengeneza maziwa feki! hawa kwanini wasishitakiwe

Huu ni mradi wa Lumumba kama ule wa SUKITA....

Nape ..aje hapa atuambie ...,tunajuwa makampuni mengi tu ambayo yanamilikiwa na ccm kupitia makada wake kwa mgongo wa nyuma kwa minajili ya kukiwezesha chama kiuchumi....Green Company Limited ..etc ambayo nayo inaagiza madawa nje kati ya shughuli nyingine..., Pia kuna MWANANCHI GOLD COMPANY ....Ambayo ilichota pesa benki kuu kwa ajili ya kujenga gold refinery or similar stuff...

Na hii Tanzania Pharmaceuticals ambayo ni mwavuli wa kukiwezesha chama na vigogo kiuchumi kupitia tatizo la UKIMWI ambalo limeshaadhiri kila kaya...hapa nchini ...pasipo na shaka yeyote....watu wameamua kutupa wananchi au wananchi wenzetu wenye matatizo haya ...vidonge vya uwongo [Placebo] ....ili wajichotee fedha za Millenium Goal ambazo zimetoka kununulia wagonjwa ARV ,Za Wafadhili wengine pamoja na za bajeti ya nchi...

Fungueni kitabu cha bajeti muone ni bilioni ngapi zimetengwa kwa ajili ya kununua ARV toka basket fund..its billions...!!
 
Kwa nchi wenzetu hawa jamaa waliohusika na hili sakata na kupatikana na hatia walikuwa wanahukumiwa kunyongwa au kifungo cha maisha Yao yote hapa duniani.

Inasikitisha sana kuona hata mgonjwa anayeishi kwa matumaini Mafisadi wanataka kuyanyakua matumaini yake kwa ARVs feki..duuh! Bongo hippopotamus(kiboko).
 
Guninita hii ndio nafasi yako ya kumpiga mweleka Madabida katika kugombea Uenyekiti wa Magamba Dar es salaam.
 
Kwahiyo kumbe hizo dawa feki zimetoka Arusha katika kiwanda hicho? This is very sensitive matter,can someone who is committed and couraged to stand for the rights of the people and benefit of the people,come out and reveal all this scandal!

Anayeua kwa Upanga atakufa kwa Upanga,what is this? Au ndio maisha bora kwa kila mtz (Single ya ccm 2005)
 
Hiyo ndio serekali ya ccm na kuna siku utakuja kusikia wameingiza dawa za kulevya ili tu wapate pesa za kampeni
 
Tanzania Pharmaceutical Industry (TPI)


TPI was established in 1977 as a state-owned pharmaceutical company, assisted by the Finnish government. Lack of operating capital and other financial constraints led to closure in the early 1990s, and it was then privatised in 1995 with 40% government ownership. Since then TPI has undergone re-engineering to become Good Manufacturing Practices (GMP) compliant. In 2009 it was the second largest pharmaceutical industry in Tanzania, accounting for about 20% of the value of pharmaceutical production.


TPI, with Action Aid Medeor (a charitable non-governmental medical aid organisation based in Germany that depends on donor support to provide services globally), implements two projects:

 manufacturing affordable artemisinin-based anti-malarial drugs for adults and paediatrics, (started in 2003); and
 producing good quality and affordable ARV fixed-dose combination, TT-virus (started in
2005).

ARV production is a €6 million project, financed through a €5 million grant from the EU Aid for Poverty-Related Diseases in Developing Countries and TPI’s €1 million contribution. The TTvirus is a generic antiretroviral drugs (ARV) fixed-dose combinations, which the World Health Organisation (WHO) has chosen as the first regimen treatment for HIV and AIDS patients in poor countries. TPI imports APIs from China, formulates the off-patent triple combination product, and packages the ARVs, so there are no significant TRIPs implications. The drug developer, Dr Kraisintu, provided technical assistance and know-how to TPI, which contributed to reducing ARV prices to affordable levels for developing countries.

Besides building local manufacturing capacity for anti-malarials and ARVs, the TPI and Medeor partnership facilitates building technical expertise, creates incentives for technical cooperation, and warms up the local market. Local manufacturing capacity building takes place through a contractual arrangement which specifies that ARVs produced will be made available to the public health sector at low cost for 40 months, after which the facility will be handed over to TPI.

Capital flow (donor money) into TPI has focused on achieving public value. Its investment and marketing strategies are focused on realising the national health policy and, particularly, drug policy objectives — ensuring that all people have access to adequate medicines, at an affordable price and acceptable quality. TPI’s focus on producing anti-malarials, ARVs and antiTB drugs at affordable prices and the 100% local marketing of drugs, supports this claim.
 
UONGOZI ndani ya CCM unauzwa na kununuliwa kama bidhaa nyingine yoyote ile. Mwalimu aliwaogopa sana wafanyabiashara kwenye uongozi wa CCM na NCHI. Akajikinga kwa Azimio la Arusha.
 
syndicate inayohusika ni kubwa sana...kubwa mno..kusimamishwa kwa mkurugenzi wa MSD kunakiuka taarifa iliyotolewa..taarifa inataka hata hao kina madabida na wenzake wakamatwe mara moja lakini kwa kuwa kikundi hicho kipo mpaka sebuleni kwa ''mwenye nyumba'' basi hakuna kingine zaid kitakachotokea..
 
dah! Hawa magamba mbona watatumaliza? Hv ni madaraka 2 ndo yanawafanya wawalinde hawa wahain au kuna jambo nyuma ya pazia?
 
Huyu Madabida anaonekana kuwa hicho kiwanda ata mtaji wenyewe mgogoro.


Mjumbe wa NEC CCM matatani



na Happiness Katabazi

*


MAHAKAMA Kuu Kitengo cha Biashara jijini Dar es Salaam, imemwamuru mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (CCM), Ramadhani Madabida na wadaiwa wengine wanne kulipa zaidi ya sh milioni 699 walizojipatia kama mkopo kutoka Benki ya Stanbic jijini Dar es Salaam.

Uamuzi huo ulitolewa hivi karibuni na Jaji Frederick Werema, ambaye alisema amefikia uamuzi huo baada ya kuridhishwa na hoja na ushahidi uliotolewa na mlalamikaji, Dilip Kesaria na Meneja wa benki hiyo, Charles Daniel.

Kwa mujibu wa nakala ya hukumu hiyo, wadaiwa wengine mbali na Madabida ambao nao wametiwa hatiani baada ya kushindwa kurejesha sh 699,860,717 kama mkopo walioupata kutoka kwa benki hiyo ni Kampuni ya Pharmaceutical Investment, Mpewani Trading, Global Trading na Mkurugenzi wa Kampuni ya Pharmaceutical, Salum Shamte.

*Jaji Werema alisema mbali ya kuwaamuru wadaiwa hao kurejesha mkopo huo, pia amewaamuru walipe fidia ya asilimia 15 kwa mwaka, kuanzia Septemba mosi 2007 hadi Mei 22, mwaka huu, ambapo hukumu hiyo ilitolewa, na asilimia saba tangu siku ya kutolewa kwa hukumu.

Aidha, Jaji Werema amemtaka Madabida na mwenzake kulipa gharama za uendeshaji wa kesi hiyo kwa Benki ya Stanbic, ambaye ndiye mlalamikaji katika kesi hiyo.

Ilidaiwa kuwa Benki ya Stanibic katika shughuli zake za kibenki ilitoa mkopo kwenye Kampuni ya Pharmaceutical na baada ya Madabida na wenzake kuweka dhamana (guarantee). Hadi kufikia Oktoba 31, 2003 deni lilifikia sh 1,110,444,611 na baadaye kupunguzwa na kufikia sh 971,861,074/-.

“Pamoja na hayo, benki ilipunguza tena deni hilo na kufikia sh milioni 800 Mei 2004 . Na kwakuwa Kampuni ya Pharmaceutical haikuwa na uwezo wa kulipa deni hilo, benki ilipunguza tena deni hilo na kufikia sh milioni 529 ambazo zingelipwa kwa miezi 24, ambapo kila mwezi wadaiwa wangelipa sh 25,649,436 pamoja na faida.*

Hata hivyo, wadaiwa walishindwa kurejesha deni hilo, hali iliyosababisha benki kutoa taarifa kadhaa za kuwakumbusha wadaiwa kulipa deni hilo na ilipofika Agosti mosi 2007 deni lilifikia sh 699,807,717, jambo ambalo liliilazimu benki hiyo kufungua kesi katika mahakama hiyo.

Katika hukumu yake, Jaji Werema alisema ameridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo kuwa Benki ya Stanibic ilitoa mkopo kwa Kampuni ya Pharmaceutical, hivyo kutokubaliana na wadaiwa, ambapo Madabiba na wadaiwa wengine walipinga vikali kuhusika na deni hilo.

“Baada ya kupitia kwa hoja na ushahidi uliotolewa na pande mbili katika kesi hii nimebaini kuwa kulikuwepo na majadiliano kadhaa kati ya pande zote mbili, ambapo nyaraka zilizoletwa mbele yangu zimebainisha kuwapo kwa mkopo ambao ulipunguzwa na kufikia sh milioni 529, ambazo zingelipwa kwa kipindi cha miezi 24.

Aidha, Jaji Werema alisema katika nyaraka hizo zimeonyesha makubaliano ambayo yalisainiwa na Madabida kama Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Pharmaceutical ambayo ndiyo ilikuwa mkopaji mkuu na pia Madabida alisaini kama Mkurugenzi na mtoa dhamana (guarantor) wakati Shamte na mkewe Madabida anayeitwa Zarina Madabida, ambaye ni Mwenyekiti wa UWT-CCM Mkoa wa Dar es Salaam, ambao wote ni wakurugenzi wa kampuni hiyo walisaini kama watoa dhamana (guarantors).

*Kwenye utetezi wao, wadaiwa kupitia Madabida walikana kuhusika na deni hilo na badala yake alidai benki ndiyo iliyopaswa kumlipa fidia ya dola za Marekani 105,000, ambazo alitozwa na Medical Store Department (MSD), baada ya benki hiyo kuchelewa kufungua kile alichokiita Local Letters of Credit.

Alidai kuwa Kampuni ya Pharmaceutical iliingia mkataba na MSD ya kusambaza au kuwapatia dawa mbalimbali za thamani ya dola za Marekani milioni 5.1, ambazo wangeziagiza kutoka nje ya nchi na kwa kuwa kampuni hiyo haikuwa na mtaji wa kutosha, iliiomba MSD ifungue hiyo Local Letters of Credit ambapo wangeitumia kufungua kile alichokiita ‘Slave Letters of Credit’.

Madabida aliiambia mahakama kuwa MDS ilitimiza utaratibu huo mwaka 1997 lakini Benki ya Stanbic ilikataa utaratibu huo na baadaye kubadili uamuzi wake na kuikubalia MSD kufungua hiyo Local Letters of Credit mwaka mmoja baadaye na hivyo kuchelewesha usambazaji wa dawa hizo, kitendo kilichoigharimu kampuni na kutozwa kiasi hicho cha pesa kama fidia.




juu
 
Ramadhani Madabida alishawahi kuwa Meneja wa RTC na mke wake Zarina Shamte Madabida alikuwa Meneja wa kampuni ya tAIFA YA MADAWA (NAPCO) makampuni hayo yote yamekufa katika hali ya kusikitisha kifisadi, wanafamilia hawa wamechelewa sana kujiingiza katika siasa, lakini baada ya kuwaona wenzao waliokuwa nao katika system enzi za Board of Internal Trade (BIT) Akina Mwapachu, Salome Mbatia , Henry Shekiffu, Athuman Janguo na wengine wameingia katika siasa na kupata mafanikio na wao wakaamua kuingia kwa kutumia nguvu nyingi ili kujinufaisha kupitia CCM, Zarina ni mwenyekiti UWT DSM na Mbunge viti maalum CCM, Ramadahani Madabida ligombea ubunge (CCM) Jimbo la Kilwa akangushwa na jamaa wa CUF, ........ lakini kwa wale waliowahi kufanya nao kazi ni watu wanaoijua pesa, ni wajanja wajanja, kile kiwanda cha Arusha, wanamiliki wao Mke ndio mtaalam wa Madawa mume ni mtu wa masoko na utawala na kuna kila la uwezekano wameamua kutafuta pesa za ziada kwa njia yoyote kama hii ya kudhuru maisha ya binadamu wenzao,..... ninaamini serikali hii haitawafumbia macho na itawachukulia hatua stahili
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom