Raisi Kikwete pole sana, lakini napenda ulifahamu hili

Ng'wanapagi

JF-Expert Member
Sep 18, 2013
9,125
8,627
Naomba mlifikishe hili suala kwa raisi kwani wasaidizi wake wapo kupiga dili tu. Tangu mwaka jana niliamua kufuata bidhaa Kampala hasa nguo na vipodozi.

Tangu nimeanza hii biashara ndugu zangu nimejifunza kuwa hii inchi kamwe tusitegemee kuwa inchi ya maendeleo ama kutoka hapa tulipo na kusonga mbele.

Ukifika Kampala bidhaa karibu zote ukiongea na wafanyabiashara watakwambia zinapitia bandari ya Dar es salaam lakini bei zake ni ndogo sana tofauti na bidhaa zilizoko nchini mwetu huku bidhaa za Waganda zikiwa nzuri sana.

Mwanzo nilidhani kwa vile niko Mwanza huenda ukaribu na Uganda umenifanya nichukue bidhaa Kampala,lakini nikajikuta nakutana na wafanyabiashara kutoka Dar es salaam kwa wingi wakifuata bidhaa hizi hizi Kampala.

Rais wangu mimi kama Mtanzania ninayeamini nchi yetu inastahili kuwa na maendeleo kama Afrika Kusini,inaniuma sana pesa zangu/zetu kuziacha Uganda kwa vile tu Wafanyabiashara wakubwa nchini mwetu serikali yako inawatoza ushuru mkubwa kiasi kwamba inawabidi wapandishe bei kwa sisi wenye mitaji midogo.

Rais wangu hebu fikri kama bidhaa tunazochukua Uganda zinakuwa nafuu na huku wakitumia Bandari yetu ya Dar! Tutendeeni haki sie Watanzania tusio na ndoto za kuwa wanasiasa ambao wanatumia siasa kujitajirisha huku wakituwekea masharti magumu katika biashara tofauti na nchi zingine ikiwemo Uganda ambayo kibiashara iko juu sana mheshimiwa.
 
Yani mali inakupita pale pale dar,unaifata ugenini,hayo Ndio matatizo ya sukar ya kuagizwa na ya ndani.siku moja chini ya watu makini watanzania tutajivunia rasilimali tulizonazo ikiwemo bahari
 
Mr. Kikwete yuko busy na deal zake za kuhujumu uchumi wetu, hii habari yako hana time nayo kabisa.
 
Naomba mlifikishe hili suala kwa raisi kwani wasaidizi wake wapo kupiga dili tu. Tangu mwaka jana niliamua kufuata bidhaa Kampala hasa nguo na vipodozi. Tangu nimeanza hii biashara ndugu zangu nimejifunza kuwa hii inchi kamwe tusitegemee kuwa inchi ya maendeleo ama kutoka hapa tulipo na kusonga mbele. Ukifika Kampala bidhaa karibu zote ukiongea na wafanyabiashara watakwambia zinapitia bandari ya Dar es salaam lakini bei zake ni ndogo sana tofauti na bidhaa zilizoko inchini mwetu huku bidhaa za Waganda zikiwa nzuri sana. Mwanzo nilidhani kwa vile niko Mwanza huenda ukaribu na Uganda umenifanya nichukue bidhaa Kampala,lakini nikajikuta nakutana na wafanyabiashara kutoka Dar es salaam kwa wingi wakifuata bidhaa hizi hizi Kampala. Raisi wangu mimi kama Mtanzania ninayeamini nchi yetu inastahili kuwa na maendeleo kama Afrika Kusini,inaniuma sana pesa zangu/zetu kuziacha Uganda kwa vile tu Wafanyabiashara wakubwa nchini mwetu serikali yako inawatoza ushuru mkubwa kiasi kwamba inawabidi wapandishe bei kwa sisi wenye mitaji midogo. Raisi wangu hebu fikri kama bidhaa tunazochukua Uganda zinakuwa nafuu na huku wakitumia Bandari yetu ya Dar! Tutendeeni haki sie Watanzania tusio na ndoto za kuwa wanasiasa ambao wanatumia siasa kujitajirisha huku wakituwekea masharti magumu katika biashara tofauti na nchi zingine ikiwemo Uganda ambayo kibiashara iko juu sana mheshimiwa.

Pole sana ndugu kwa kupigia mbuzi gitaa!
 
Siasa chafu huleta fedha chafu na fedha chafu huleta bei chafu. Ni kweli kabisa bidhaa Kampala ni rahisi kuliko Tanzania
 
Lakini ni vizuri tukayaweka hadharani yanayotusibu.
PROBABLY,yatashughulikiwa,ujue kama tungekuwa na mifumo mizuri na innovative na motivated bas hizi tuitazo land locked countries zingekua zinanunua magar kwenye yard za Tanzania badala ya wao kuagiza Ujapani na kwingineko,ila sasa is it possible?
 
PROBABLY,yatashughulikiwa,ujue kama tungekuwa na mifumo mizuri na innovative na motivated bas hizi tuitazo land locked countries zingekua zinanunua magar kwenye yard za Tanzania badala ya wao kuagiza Ujapani na kwingineko,ila sasa is it possible?

Inasikitisha sana hata ukifika Mtukula jinsi TRA wanavyotusurubu.
 
Mtoa mada ametoa haja nzuri sana, naomba tusichoke kuzungumza kwa kusema kwamba hizi habari hazisomi amini wapo wengi wanaosoma habari hizi na hapa ndiyo tuition yao ilipo, tutumie ujunzi na utaalamu wetu kuwaeleza yale ambayo tuna data sahihi na tuna mapendekezo yenye tija kwa ajili ya taifa hili, tuseme tu kwa busara na hekima watasoma na misumari itawachoma moyoni. Tusichoke jamani tupaze sauti zetu na JF itakuwa ni mkombozi wa wanyonge
 
Back
Top Bottom