Mlyafinono
Senior Member
- Apr 6, 2012
- 177
- 47
Rais wa umoja wa vyama vya waandishi wa habari Tanzania UTPC Keny Simbaya ameshindwa kuwashawishi waandishi wa habari wa mkoa wa iringa kuandika habari za wiki ya nenda kwa usalama barabarani ambayo kitaifa inafanyika mkoani iringa.
Hatua ya waandishi wa habari kugomea kuandika habari za polisi inafuatia tukio la kikatili la kuuawa kwa mwandishi wa chanel ten Daudi Mwangosi lililofanywa na jeshi la polisi septemba 2 mwaka huu katika kijiji cha Nyololo wilayani mufindi mkoani Iringa.
Waandishi wamesema kwasasa bado wanaomboleza msiba mkubwa uliomkumba mwandishi mwenzao,na kuwataka wanaoandaa sherehe hizo kuchukua waandishi kutoka dar au mikoa mingine ya jirani.
Daudi Mwangosi aliuawa kikatili kwa kupigwa na bomu mbele ya kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda
Hatua ya waandishi wa habari kugomea kuandika habari za polisi inafuatia tukio la kikatili la kuuawa kwa mwandishi wa chanel ten Daudi Mwangosi lililofanywa na jeshi la polisi septemba 2 mwaka huu katika kijiji cha Nyololo wilayani mufindi mkoani Iringa.
Waandishi wamesema kwasasa bado wanaomboleza msiba mkubwa uliomkumba mwandishi mwenzao,na kuwataka wanaoandaa sherehe hizo kuchukua waandishi kutoka dar au mikoa mingine ya jirani.
Daudi Mwangosi aliuawa kikatili kwa kupigwa na bomu mbele ya kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda