Rais wa Tanzania kufanya mahojiano na MSNBC-Andrea Mitchel

Mara 1000 ningeona rais anafanya jambo la maana kwa kuitisha mkutano wa kitaifa unaojumuisha watu mbalimbali wa matabaka mbalimbali na kujadili namna ya kuondoa umaskini. Ifike mahali sasa kama taifa tuwaambie viongozi wetu waache kutuabisha na kutafuta majawabu kwa wanyonyaji.

Watanzania ndio wanaokumbana na adha ya umaskini, lakini kwa hakika ni watanzania hawa hawa maskini ndio wenye majawabu juu ya namna ya kutokomeza umaskini. Tatizo tulilo nalo ni kasumba mbaya kwa viongozi wetu kujadili with the wrong people.

Hii campaign ya nutrition imeletwa na Marekani. It is not coming from us, na kwa mtu mwenye akili timamu Marekani wamebuni hii campaign kama njia mojawapo ya kupambana na influence ya China Africa. Wanajua watu wengi bado hawana chakula cha kutosha, na mchina yeye haongei mambo ya chakula, sasa wanacheza na akili za viongozi wetu. Na campaign inaongozwa na shirika lao USAID. kila anapokwenda Kikwete anakumbana na mkurugenzi wa USAID! Inakuwaje? Mbona hao USAID hawawagandi wakenya? Au Tanzania wana shida ya chakula kuliko Kenya?

Unaonesha una ubongo wa kumbukumbu mfupi sana. Kukukumbumsha tu naomba pitia hizi links:

Tanzania to Host a Regional Ministerial Conference on ''Poverty Reduction and Rural Growth in Eastern and Southern Africa''

IMF Survey: Amid Crisis, Africa Calls for Stronger Partnership With IMF
NEW031109A-4.jpg
Tanzanian President Kikwete (r) addresses media with IMF Managing Director Strauss-Kahn after Dar es Salaam conference (photo: Stephen Jaffe/IMF)

http://www.changes-challenges.org/pdf/tanzania_brochure.pdf
 
yaani huyu mzee jamani...yaani anajiona jabali kujisifia nchi masikini wakati ina kila kitu cha kuifanya iwe tajiri....daaaah

Mairha bora kwa kila mTz ndo hayo anayoyapaisha huko!
 
Tatizo la viongozi wetu ni waoga sana linapokuja swala la hao weupe. Hata kama huna tatizo mweupe wa ulaya akituambia tuna tatizo huwa tunawakubalia. Hapo ndipo mwanzo wa matatizo kwa vile, ni kama mganga wa kienyeji, chochote akitakacho tunawapa ili mradi atuhakikishie kuwa atatuondolea tatizo letu ambazo sisi wenyewe hatulijui ila yeye.

Nakubaliana na wewe kabisa. Viongozi wetu wanatoa ajenga nje ya nchi. Ni nani hasa ameanza hii ajenda ya Nutrition? Ni Tanzania? Yaani barani Afrika hizo nchi nne ndio zina tatizo la nutrition and food security?

Pamoja na kwamba tunalima kwa kutumia jembe la mkono, Tanzania hakuna shida ya chakula. Tatizo ni distribution. Mikoa ya kusini mahindi yanaozea ndani kwa sababu (a) hakuna soko au/na (b) wakulima wanakatazwa kuuza mazao yao kwa jinsi wanavyotaka. Pili, ni vigumu sana kutoa mazao toka upande mmoja wa nchi kwenda upande mwingine kwa sababu ya miundo mbinu e.g barabara na reli.

Na pengine tujiulize, kama wakulima wanatumia hizi zana za ujima lakini wanavuna na kupata ziada, ingekuwaje kama wangepewa zana za kisasa? Ni lini serikali imeshirikiana kwa karibu na wakulima kwa kuwapa zana bora i.e matreka, mbolea na mbegu bora (sio fake) halafu watu wakashindwa kulima?

Sasa ninapoona rais anakazana kwenye uzalishaji wakati mazao yanozea ndani unashindwa kuelewa nani kampa hiyo ajenda? Hao wakulima wakubwa wakija watasafirisha mazao kwa kutumia migongo yao?
 
wewe ni malalamikaji tu,hebu jiulize wewe umefanya nini kuondoa umaskini wa watanzania zaid ya kubeza wanayofanya wengine.

Kajikimu kimaisha na angepata nafasi kama ya jk Tz nadhani maendeleo tusingeyasikia yakihubiriwa majukwani wakati wa campain tu bali yangekuwa kwa vitendo
 
Naona hamuielewi lugha ndio maana hamjui mnachokiongea humu.

Bono hapo anamsifu Kikwete kwa kuonesha mfano bora na anasema huyu si kiongozi wa Tanzania tu bali ni wa Kontinenti zima, ambalo kwa mazuri na mabadiliko aliyoyafanya kwa muda mchache inabidi wengi wajifunze kutoka kwake.

Mtakufa navyo vijiba vya roho!
 
Naona hamuielewi lugha ndio maana hamjui mnachokiongea humu.

Bono hapo anamsifu Kikwete kwa kuonesha mfano bora na anasema huyu si kiongozi wa Tanzania tu bali ni wa Kontinenti zima, ambalo kwa mazuri na mabadiliko aliyoyafanya kwa muda mchache inabidi wengi wajifunze kutoka kwake.

Mtakufa navyo vijiba vya roho!

Watu wanaanza kwa kuponda tu as long as it is Kikwete bila hata kusikiliza contents!
 
Nakubaliana na wewe kabisa. Viongozi wetu wanatoa ajenga nje ya nchi. Ni nani hasa ameanza hii ajenda ya Nutrition? Ni Tanzania? Yaani barani Afrika hizo nchi nne ndio zina tatizo la nutrition and food security?

Pamoja na kwamba tunalima kwa kutumia jembe la mkono, Tanzania hakuna shida ya chakula. Tatizo ni distribution. Mikoa ya kusini mahindi yanaozea ndani kwa sababu (a) hakuna soko au/na (b) wakulima wanakatazwa kuuza mazao yao kwa jinsi wanavyotaka. Pili, ni vigumu sana kutoa mazao toka upande mmoja wa nchi kwenda upande mwingine kwa sababu ya miundo mbinu e.g barabara na reli.

Na pengine tujiulize, kama wakulima wanatumia hizi zana za ujima lakini wanavuna na kupata ziada, ingekuwaje kama wangepewa zana za kisasa? Ni lini serikali imeshirikiana kwa karibu na wakulima kwa kuwapa zana bora i.e matreka, mbolea na mbegu bora (sio fake) halafu watu wakashindwa kulima?

Sasa ninapoona rais anakazana kwenye uzalishaji wakati mazao yanozea ndani unashindwa kuelewa nani kampa hiyo ajenda? Hao wakulima wakubwa wakija watasafirisha mazao kwa kutumia migongo yao?

Kama ulivyosema hapo juu mkuu. Solutions za matatizo yetu zipo hapa hapa. Ukiondoa hivyo vikwazo ambazo ziko wazi kabisa, bado kuna tatizo kubwa ya namna serikali inavyo simamia sekta ya kilimo. Hakuna coordination kati ya vyuo vya kilimo (technical expertise)na wakulima. Kwanza hadi majuzi tu ndo tume aanza kuwa na database ya wakulima nchi nzima. Kwa miaka mingi serikali imekuwa ikifanya kazi under the assumption kuwa kila mtu kijijini ni mkulima wakati sio kweli. Ifikie wakati sasa serikali iaanze ku-engage wananchi wake pamoja na wataalamu wa ndani kutafuta solutions za kilimo hapa hapa nchini.Matatizo mengi katika sekta ya kilimo yana sababishwa na either bad government intervention au usimamizi mbovu wa sekta mbali mbali kama sekta ya pamba. Hivi bodi ya mazao kwanini zisi simamiwe na wakulima wenyewe? Rais anavyo fanya uteuzi ana washirikisha wadau kwenye sekta husika? Je hizo bodi kwanini hazina performance contracts? Kwenda kila siku kuomba msaada G8 na nchi zinazo endelea inaonyesha kuwa serikali na mfumo wake mzima umeshindwa kuuelewa complexities za matatizo ya kilimo. Na hili ndo tatizo kubwa. Kwa sababu kama ni masoko, kuna masoko makubwa tu, nchi za jirani na hata hapa nchini, utaalamu upo, viwanda vya fertilizer vipo. Tunarudi kwenye yale ambayo mkuu FJM ameainisha kwenye post yake.
 
Naona hamuielewi lugha ndio maana hamjui mnachokiongea humu.

Bono hapo anamsifu Kikwete kwa kuonesha mfano bora na anasema huyu si kiongozi wa Tanzania tu bali ni wa Kontinenti zima, ambalo kwa mazuri na mabadiliko aliyoyafanya kwa muda mchache inabidi wengi wajifunze kutoka kwake.

Mtakufa navyo vijiba vya roho!

Bono na wenzie wanaweza kumsifia Kikwete kutokana na what they benefit from us. Watanzania walio wengi hawawezi kumsifia Kikwete kutokana na kuteseka/kupigika zaidi kimaisha kutokana na uongozi wake. Nafikiri hii haihitaji kufikiri sana kuielewa!
 
Naona hamuielewi lugha ndio maana hamjui mnachokiongea humu.

Bono hapo anamsifu Kikwete kwa kuonesha mfano bora na anasema huyu si kiongozi wa Tanzania tu bali ni wa Kontinenti zima, ambalo kwa mazuri na mabadiliko aliyoyafanya kwa muda mchache inabidi wengi wajifunze kutoka kwake.

Mtakufa navyo vijiba vya roho!

Manufacturing of teachers!!......
 
Hapa anazungumza vitu ambavyo ni so general utadhani anawakilisha Umoja wa Africa badala ya Tanzania. He's shown himself to be a huge embarrasement kwa kweli everytime he opens his mouth to answer questions in the English language. Bora hata angekuwa anajibu kwa Kiswahili kama Wachina wanavyojibu Kichina kwenye interviews kama hizi. He surely qualifies as the least intelligent and capable of all presidents The Republic of Tanzania has had thus far.
 
Masikini Tanzania tunajivunia umasikini!!!, Hivi tutaishi kuombaomba mpaka lini!! JK please, na maraisi wengine mtakaokuja njia pekee ni kuwekeza na kuwezesha watanzania wenyewe kuondoka na umasikini, hakuna njia nyingine, kuombaomba sana tutakuwa tunajidhalilisha na tutaendelea kuwa watumwa na kunyonywa na nchi ambazo zimeendelea, Je siku tukipatwa na majanga makubwa tutaomba nini!!. Mambo tunayoweza kufanya wenyewe tufanye wenyewe!!.
 
Kushughulikia kilimo ni swala lililo ndani ya uwezo wetu

Muhimu hapo alichotakiwa kuongea ni kuwa serikali yake wa waTz watafanya kilimo anaomba soko tuu .

Watutaki wawekezaji mpaka kwenye kilimo tunataka soko ...hu ni mpango wa kumilikisha wengine ardhi yetu.

Nahisi Rais anania nzuri towe positive jamani kaongea vema kiasi
 
Back
Top Bottom