The Analyst
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 464
- 246
Baadhi ya watanzania hawataki kujifunza kutokana na makosa yao wenyewe. Wanatumia muda mwingi kweli kushabikia nani awe rais badala ya kutumia muda huo na juhudi zao kuwabana viongozi wetu watimize wajibu wao na kushinikiza waondoke madarakani kama hawawezi au hawataki kutekeleza wajibu huo.
Hivi hamkumbuki mambo ya watu waliotamani kuwa rais yanavyoigharimu Tanzania mpaka dakika hii?. JK ni rais leo kwa kuwa alitamani kuwa rais na kujipanga akisaidiwa na wanamtandao wenzake kama EL, RA, SS, B.Membe, nk. Hawa jamaa walijipanga zaidi kujiremba ili wapendeze machoni pa watu na kuchafua wenzao ili waweze kuchaguliwa. Hata siku moja hawakuwaza wakiingia madarakani watafanya nini kuwasaidia wapigakura wao. Kama mnabisha chunguzenu utendaji na utekelezaji wa sera zao. Very poorly organised!
Baadhi ya wanamtandao wanaendelea kuandaa kuchaguliwa kwao miaka ijayo na kwa ujinga wa baadhi yetu tuko busy kushangilia mara Membe, mara Sitta mara nani.....2015 wengine wanajipanga kutawala nchi kwa karne kibao kupitia vizazi vyao vijavyo na bado wanashabikiwa.
Swali: Hawa watu wamefanya nini hata mkadhani wataweza?
Ushauri: Kwa nini tusipime watu kwa uwezo wao na kushinikiza vyama vyao kuwapendekeza kwa staili ile ya CDM na Dr. Slaa. Naamini Mbowe anapenda kuwa rais lakini alipima umakini wa Slaa ambao umeonekana wazi na kusikia sauti ya umma na kumwomba agombee. Upande wa magamba naona mtu mwenyewe anaanza kutafuta fedha anaitumia kujitangaza na kuchafua wenzake kisha anataka aonekane anaweza.
Mpaka dakika hii nawaogopa watu wanaotajwatajwa ndani ya magamba kwa kuwa ukweli ni wao wenyewe wanaotaka urais na si watu wengi wanawapendekeza.
Wakuu naomba tulijadili hili.
Hivi hamkumbuki mambo ya watu waliotamani kuwa rais yanavyoigharimu Tanzania mpaka dakika hii?. JK ni rais leo kwa kuwa alitamani kuwa rais na kujipanga akisaidiwa na wanamtandao wenzake kama EL, RA, SS, B.Membe, nk. Hawa jamaa walijipanga zaidi kujiremba ili wapendeze machoni pa watu na kuchafua wenzao ili waweze kuchaguliwa. Hata siku moja hawakuwaza wakiingia madarakani watafanya nini kuwasaidia wapigakura wao. Kama mnabisha chunguzenu utendaji na utekelezaji wa sera zao. Very poorly organised!
Baadhi ya wanamtandao wanaendelea kuandaa kuchaguliwa kwao miaka ijayo na kwa ujinga wa baadhi yetu tuko busy kushangilia mara Membe, mara Sitta mara nani.....2015 wengine wanajipanga kutawala nchi kwa karne kibao kupitia vizazi vyao vijavyo na bado wanashabikiwa.
Swali: Hawa watu wamefanya nini hata mkadhani wataweza?
Ushauri: Kwa nini tusipime watu kwa uwezo wao na kushinikiza vyama vyao kuwapendekeza kwa staili ile ya CDM na Dr. Slaa. Naamini Mbowe anapenda kuwa rais lakini alipima umakini wa Slaa ambao umeonekana wazi na kusikia sauti ya umma na kumwomba agombee. Upande wa magamba naona mtu mwenyewe anaanza kutafuta fedha anaitumia kujitangaza na kuchafua wenzake kisha anataka aonekane anaweza.
Mpaka dakika hii nawaogopa watu wanaotajwatajwa ndani ya magamba kwa kuwa ukweli ni wao wenyewe wanaotaka urais na si watu wengi wanawapendekeza.
Wakuu naomba tulijadili hili.