Rais Uhuru Kenyatta ni mlevi au?

Kuna takwimu zinatolewa humu za ajabu kweli. huyu jamaa ni mlevi na hana sifa za kuwa rais bora. Rais bora kwa sasa ni Magufuli, ukitaka kujua fuatilia nchi za wenzetu wanavyo mu admire kwa utendaji wake. mfano halisi ni WB ambayo kupitia kwa rais wake wameikubali tz chini ya uongozi wa magufuli kuwa itakua kiuchumi kuifikia dubai au zaidi ktk kipindi kifupi. vile vile ameipa tz fedha nyingi kuzidi nchi yeyote na kiwango kikubwa zaidi kuwahi kukopeshwa katika historia. Huyo ndiye magufuli.
 

Friday, 21 October 2016
JAJI MUADVENTISTA MSABATO ALIYEKATAA KUFANYA KAZI SIKU YA SABATO AMEAPISHWA RASMI KUA JAJI MKUU - KENYA.
Jaji wa kiadventista msabato DAVID MARAGA aliye kataa kufanya kazi katika siku ya Sabato(jumamosi),ameapishwa rasmi na kua jaji mkuu katika nchi ya Kenya.
Katika hafla ya kuapishwa kwake iliyofanyika katika ikulu ya Rasi wa Kenya Uhuru Kenyatta,Jaji DAVID MARAGA alimualika Rais wa kanisa la waadventista wa sabato Division ya Mashariki na kati Dr. BLASIOUS RUGURI kwaajili ya kumuombea kabla hajaanza utekelezaji wa majukumu yake mapya.
"Kama mkristo(mwadventista) niliadhimia kwamba kabla sijaanza mujukumu yangu mapya kama jaji mkuu nitamshukuru Mungu kwa kunifikisha sehemu hii ya Juu"Alisema Jaji mkuu David Maraga.
Dr.Blasious Ruguri alisema kua Jaji mkuu David Maraga ni mtu wa maombi na ni mfano wa kuigwa kwa waadventista wasabato wote.
Jaji mkuu David Maraga alisema kua itakua ni vigumu sana kwake kufanya kazi katika siku ya sabato(Jumamosi) na kwamba atamuweka Mungu mbele ya kazi yake.
Jaji mkuu David Maraga amechukua nafasi hiyo baada ya Aliye kua jaji mkuu kustaafu mwaka huu naye alikuwa na msimamo wake kama Maraga
 
Ndiye rais wa kwanza Afrika kutia saini ya mswada wa kupunguza riba huku akiwa anamiliki bank kutoka 24% mpaka 12%-14 %

Ndiye rais wa kwanza Africa ambaye sijawai kumsikia akiwakejeri wapinzani wake

Ndiye rais wa kwanza Africa ambaye sijawai kumsikia akiwakejeri majirani zake...

Ujenzi wa reli ya kihistoria kutoka Mombasa kwenda Western Kenya ....

Ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Mombasa litaenda mpaka south sudani...

Rais wa kwanza Africa aliyekubali kutengeneza tume huru akiwa madarakani bila kupepesa macho....

Rais pekee anayejichanganya na watu wa kila wawe masikini wawe matajiri

Kikubwa zaidi office ya rais nchini Kenya imetangazwa ndio ofisi pekee isiyokuwa na kiwango cha Rushwa iko chini ya 5% hasa Rushwa ya Ajira .

Ndiye pia rais pekee wa Africa ambaye safari za nje alizozifanya ndani ya mwaka huu pekee zitaongeza pato la taifa kwa 27% kwa mwaka mmoja yaani maana yake hakusafiri kwenda kushangaa au kubembea Bali ni kwa faida ya nchi yake !!

Na mengine mengi tu kiukweli nampenda sana kwa Sera zake akiwa ni msomi wa uchumi naona anaitendea haki hii taharuma yetu
Yah mkuu,nakubaliana wewe hasa bank interest rate Na tume. Kwenye ni vigumu kwa presidaa Wa kiafrika kufanya hivyo.kama anapiga urabu ni personal issue maendeleo ni muhimu zaidi.Wa kwetu ubabe tu anaua democracy
 
Back
Top Bottom