Rais ni Taasisi, Magufuli LAZIMA aheshimiwe!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,260
33,857
Kuna mambo yanatokea kuuzunguka Urais wa Magufuli, ni lazima kama Raia wenye wajibu wa kikatiba wa kulinda hadhi ya taasisi hiyo kubwa sana na yenye heshima ya hali ya juu katika nchi yetu,tuchukue hatua kuilinda.

Kwa mfano shindano linaloitwa la kumpata mtu maarufu (Siyo kiongozi maarufu) Afrika kumshirikisha Rais wetu, kama watanzania tungepigana kuliondoa jina la Rais wetu kwenye shindano hilo. Hivi inaeleweka kwamba huwezi kushindanishwa na wale usio nao kwenye daraja moja? Yaani hadhi ya Rais wetu kweli inaweza kufanana na ya Mfanyabiashara Dewji?

Yaani tuona ni sawa tu kwa Rais wetu kushindanishwa na watu ambao hata kwenye nchi zao hawafahamiki kiasi cha kulingana sifa na Rais wetu? Badala ya Rais wetu kushindanishwa na marais wenzake wa Afrika anashindanishwa na wafanyabiashra na viongozi wa taasisi zisizo za serikali? Kweli ni jambo la kujivunia hili?

Wasadizi wa Rais ambao wengi ni wateule wa Rasi wanaposema ama kufanya vitendo vya kijinga si wanamdhalilisha Rais mwenyewe? Waziri anaposema kuna viwanda 52,000 bila ya kunyumbulisha viwango vya viwanda hivyo si anamdhalilisha aliyemteua?

Hata kama hatumkubali Magufuli kama binadamu lakini ni lazima tukumbuke kwamba yeye ni Rais wetu na ni lazima taasisi ya Rais anayoiongoza iheshimiwe. Ni lazima Rais aheshimiwe na wale wanaoshusha hadhi ya ofisi anayoingoza wajifunze kujiheshimu.
 
The irony is, our system is made up of the top degree graduates from reputable uni versities....profs, docts, ma,msc etc
Excuse me sir, what is your point?
 
Mkuu, hizo tuzo hawashindanishwi Marais. Tuzo hizo huenda kwa mtu ambaye ametoa mchango mkubwa katika jamii hasa suala la ukuaji wa uchumi. Wote waliopata tuzo hizo ukiwaangalia hakika mchango wao ni mkubwa kuliko hata mchango wa marais wengi wa Afrika. Chukulia mfano wa Dangote au hata huyu wa kwetu MO
 
Hivi chadema mtaacha lini upumbavu?

Hivi hizi ndio hoja mbadala wa ccm kweli ambazo wananchi wanapaswa kuzichukua?

Huyo Yeriko kaleta uzi kwamba hizo tuzo ni uongo, na wewe umeamua kuleta kituko kwamba rais kashushwa hadhi? Aisee naona aibu mm kuwa na upinzani wa kipumbavu hivi!
 
Tangia twaweza wawe wanapika data za kumtukuza mtukufu ili kujipendekeza na hao wana Lumumba wakaiga ili kumtaftia kiki, kumbe wamemzalilisha kumlinganisha na watu wa vichochoroni. Magufuli alinganishwe na Rais ka Buhari, Nkurunziza and so on. Ila kwa vile awamu hii ni ya kupenda sifa walichekelea kweli
 
Hivi chadema mtaacha lini upumbavu?

Hivi hizi ndio hoja mbadala wa ccm kweli ambazo wananchi wanapaswa kuzichukua?

Huyo Yeriko kaleta uzi kwamba hizo tuzo ni uongo, na wewe umeamua kuleta kituko kwamba rais kashushwa hadhi? Aisee naona aibu mm kuwa na upinzani wa kipumbavu hivi!
Naona hii mada hata bavichaa hawachangii.
 
Mkuu, hizo tuzo hawashindanishwi Marais. Tuzo hizo huenda kwa mtu ambaye ametoa mchango mkubwa katika jamii hasa suala la ukuaji wa uchumi. Wote waliopata tuzo hizo ukiwaangalia hakika mchango wao ni mkubwa kuliko hata mchango wa marais wengi wa Afrika. Chukulia mfano wa Dangote au hata huyu wa kwetu MO
Pia kuna rais wa Mauritius. Hawa bavichaa wamegonga mwamba.
 
Hadhi ya urais nchi hii haipo tena, yaani rais wa nchi anashindanishwa na mtu asiyejulikana hata wilaya yake atokako kwenye nchi yake! Hlf tunakuja hapa na kupiga makofi ya kushangilia, huu ni uendawazimu! Ashindanishwa na watu wenye hadhi sawa na yake.
 
Heshima ni two way traffic hata kama ni Rais wa nchi. Huwezi kuidharau katiba ya nchi halafu utegemee wananchi wanaoiheshimu katiba ya nchi yao pamoja na mapungufu yake makubwa wakuheshimu.

Huwezi kuwadharau wananchi kwa kuwaita vil.aza halafu eti utegemee wananchi hao wakuheshimu.

Huwezi kukiuka sheria za ajira nchini kwa kuwafukuza wafanya kazi wa Serikali wa ngazi za chini ambao hawana makosa yoyote bila kuwapa nafasi ya kujitetea halafu utegemee heshima kwako.

Huwezi kuita kampuni kubwa kama Tanesco ambayo kwa kiasi kikubwa imehujumiwa na watendaji wa juu Serikalini kwa kuingia mikataba chungu nzima ya kifisadi mashetani halafu utegemee uheshimiwe.

Huwezi kuwanyanyasa na kuwapa msongo mkubwa wa mawazo Wafanyakazi Serikalini kwa kuzuia nyongeza za mishahara na promotions zao zaidi ya mwaka bila ya kuwa na maelezo yanayojitosheleza kisha eti utegemee heshima.

Huwezi kuwadharau wahanga wa maafa ya tetemeko Kagera pamoja na kukusanya zaidi ya bilioni 15 toka ndani na nje ya nchi uendelee kuzikumbatia pesa za wahanga hao bila ya kuwepo sababu za msingi za kufanya hivyo kwa wiki ya saba sasa halafu utegemee uheshimiwe.

Huwezi ukaongoza nchi kwa vitisho vikubwa kila kukicha bila sababu ya msingi bali tu kutaka kuwa dikteta uchwara halafu ukategemea wananchi wakuheshimu.

Kuna mambo yanatokea kuuzunguka Urais wa Magufuli, ni lazima kama Raia wenye wajibu wa kikatiba wa kulinda hadhi ya taasisi hiyo kubwa sana na yenye heshima ya hali ya juu katika nchi yetu,tuchukue hatua kuilinda.

Kwa mfano shindano linaloitwa la kumpata mtu maarufu (Siyo kiongozi maarufu) Afrika kumshirikisha Rais wetu, kama watanzania tungepigana kuliondoa jina la Rais wetu kwenye shindano hilo. Hivi inaeleweka kwamba huwezi kushindanishwa na wale usio nao kwenye daraja moja? Yaani hadhi ya Rais wetu kweli inaweza kufanana na ya Mfanyabiashara Dewji?

Yaani tuona ni sawa tu kwa Rais wetu kushindanishwa na watu ambao hata kwenye nchi zao hawafahamiki kiasi cha kulingana sifa na Rais wetu? Badala ya Rais wetu kushindanishwa na marais wenzake wa Afrika anashindanishwa na wafanyabiashra na viongozi wa taasisi zisizo za serikali? Kweli ni jambo la kujivunia hili?

Wasadizi wa Rais ambao wengi ni wateule wa Rasi wanaposema ama kufanya vitendo vya kijinga si wanamdhalilisha Rais mwenyewe? Waziri anaposema kuna viwanda 52,000 bila ya kunyumbulisha viwango vya viwanda hivyo si anamdhalilisha aliyemteua?

Hata kama hatumkubali Magufuli kama binadamu lakini ni lazima tukumbuke kwamba yeye ni Rais wetu na ni lazima taasisi ya Rais anayoiongoza iheshimiwe. Ni lazima Rais aheshimiwe na wale wanaoshusha hadhi ya ofisi anayoingoza wajifunze kujiheshimu.
 
Mkuu, hizo tuzo hawashindanishwi Marais. Tuzo hizo huenda kwa mtu ambaye ametoa mchango mkubwa katika jamii hasa suala la ukuaji wa uchumi. Wote waliopata tuzo hizo ukiwaangalia hakika mchango wao ni mkubwa kuliko hata mchango wa marais wengi wa Afrika. Chukulia mfano wa Dangote au hata huyu wa kwetu MO

Naomba uingie hapa Forbes Africa Magazines uniambie ni wapi JPM kaandikwa.
 
Back
Top Bottom