Indume Yene
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 2,948
- 709
Rais mtarajiwa wa Afika ya Kusini Bw. Jacob Zuma huenda akapandishwa kizimbani kwa mara nyingine kwa makosa yaleyale ambayo yalitupiliwa mbali na mahakama ya chini mwezi Septemba mwaka 2008.
Kesi hii ambayo imechukuwa muda mrefu kusikilizwa ambayo ilisababisha kuanguka kwa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Bw. Thabo Mbeki.
Jaji Chris Nicholson aliitupilia mbali mashitaka dhidi ya Zuma kwa kudai kuwa upande wa mashitaka hawakumpa nafasi mtuhumiwa kueleza kile ambacho alikuwa anakifahamu.
Pamoja na ushindi wa Zuma katika kesi hiyo, jaribio lingine linakuja baada ya Jaji wa Mahakama Kuu nchini humo Bw. Louis Harms kudai kuwa mahakama hiyo ya chini nayo ilienda beyond na mamlaka yake katika hiyo kesi. Hivyo kulingana na maamuzi haya, upande wa mashitaka unaangalia ni tarehe gani iweze kumpandisha Bw. Zuma kizimbani kwa mara nyingine. Bw. Zuma anakabliwa na makosa 16.
Swali linakuja hapa: Je vita hii kati ya Zuma na serikali itaisha lini. Hii kesi ilikuwa na msisimko wa aina yake nchini humo, vilevile ilizidisha chuki ndani ya chama cha ANC na kufikia kiwango cha kumegeka. Nafikiri ndoto ya baadhi ya watu/viongozi ANC ni kuhakikisha Zuma harudi tena kwenye ulingo wa siasa especially kwenye KIRINGE
Source: Nytimes.
Kesi hii ambayo imechukuwa muda mrefu kusikilizwa ambayo ilisababisha kuanguka kwa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Bw. Thabo Mbeki.
Jaji Chris Nicholson aliitupilia mbali mashitaka dhidi ya Zuma kwa kudai kuwa upande wa mashitaka hawakumpa nafasi mtuhumiwa kueleza kile ambacho alikuwa anakifahamu.
Pamoja na ushindi wa Zuma katika kesi hiyo, jaribio lingine linakuja baada ya Jaji wa Mahakama Kuu nchini humo Bw. Louis Harms kudai kuwa mahakama hiyo ya chini nayo ilienda beyond na mamlaka yake katika hiyo kesi. Hivyo kulingana na maamuzi haya, upande wa mashitaka unaangalia ni tarehe gani iweze kumpandisha Bw. Zuma kizimbani kwa mara nyingine. Bw. Zuma anakabliwa na makosa 16.
Swali linakuja hapa: Je vita hii kati ya Zuma na serikali itaisha lini. Hii kesi ilikuwa na msisimko wa aina yake nchini humo, vilevile ilizidisha chuki ndani ya chama cha ANC na kufikia kiwango cha kumegeka. Nafikiri ndoto ya baadhi ya watu/viongozi ANC ni kuhakikisha Zuma harudi tena kwenye ulingo wa siasa especially kwenye KIRINGE
Source: Nytimes.