Mponjoli Njenga
Member
- Aug 16, 2016
- 43
- 56
Wadau,
Akiongea wakati wa uzinduzi wa ndege mpya mbili jana , Raisi wetu mpendwa, kipenzi cha masikini, alisema " Kuna mawziri wamepeleka wake zao ATCL, wakati wao ni mawaziri, na wanajua shirika linafanya vibaya". Aliongea haya maneno akimuagiza DG na Bodi kuwashughulikia wale wote ambao amesema hawako tayari kwenda inavyotakiwa na hawataki kubadilika. Pia aliwaagiza wafanyakazi wa ATCL wajirudi na kutubu wenyewe ili waingie kwenye ufalme wa ndege mpya.
Nina maswali kadhaa wandugu mnisaidie hapa:
1. Hao mawaziri waliopeleka wake zao huko ATCL ni kina nani?
2. Je wake zao wana sifa za kazi walizopewa?
3. Je wake hao , ni kweli walipelekwa, au waliona matangazo ya kazi wakaomba kazi kama waombaji wengine na wakapita kwa sifa zao?
4. Kama walikuwa na sifa, lini ikawa mwiko wake za mawaziri kufanya kazi wakati waume zao wakiwa mawaziri? Na je ikitokea mke ndo waziri, mume wake atatakiwa kutoajiriwa serikalini?
5. Najua mke wa Mheshimiwa Raisi ni mwalimu kitaaluma, na kwamba alistaafu majuzi tu ili aungane na Mheshimiwa Raisi kama "first Lady" kuendesha majukumu ya uraisi. Swali langu : hivi wakati wote Raisi Magufuli alipokuwa waziri serikalini, matatizo ya walimu hayakuwapo? Kama yalikuwapo , ilikuwaje yeye alimwacha Mama Janeth Magufuli aendelee kufanya kazi ilihali yeye ni waziri?
Basi wakuu, naombeni mnisaidie . Tafadhali jenga hoja...
cc: Ritz , Lizaboni , FaizaFoxy , Pasco , Ben Saanane na wengine wengi
Akiongea wakati wa uzinduzi wa ndege mpya mbili jana , Raisi wetu mpendwa, kipenzi cha masikini, alisema " Kuna mawziri wamepeleka wake zao ATCL, wakati wao ni mawaziri, na wanajua shirika linafanya vibaya". Aliongea haya maneno akimuagiza DG na Bodi kuwashughulikia wale wote ambao amesema hawako tayari kwenda inavyotakiwa na hawataki kubadilika. Pia aliwaagiza wafanyakazi wa ATCL wajirudi na kutubu wenyewe ili waingie kwenye ufalme wa ndege mpya.
Nina maswali kadhaa wandugu mnisaidie hapa:
1. Hao mawaziri waliopeleka wake zao huko ATCL ni kina nani?
2. Je wake zao wana sifa za kazi walizopewa?
3. Je wake hao , ni kweli walipelekwa, au waliona matangazo ya kazi wakaomba kazi kama waombaji wengine na wakapita kwa sifa zao?
4. Kama walikuwa na sifa, lini ikawa mwiko wake za mawaziri kufanya kazi wakati waume zao wakiwa mawaziri? Na je ikitokea mke ndo waziri, mume wake atatakiwa kutoajiriwa serikalini?
5. Najua mke wa Mheshimiwa Raisi ni mwalimu kitaaluma, na kwamba alistaafu majuzi tu ili aungane na Mheshimiwa Raisi kama "first Lady" kuendesha majukumu ya uraisi. Swali langu : hivi wakati wote Raisi Magufuli alipokuwa waziri serikalini, matatizo ya walimu hayakuwapo? Kama yalikuwapo , ilikuwaje yeye alimwacha Mama Janeth Magufuli aendelee kufanya kazi ilihali yeye ni waziri?
Basi wakuu, naombeni mnisaidie . Tafadhali jenga hoja...
cc: Ritz , Lizaboni , FaizaFoxy , Pasco , Ben Saanane na wengine wengi