Rais Magufuli, Usiruhusu Hospitali za Rufaa za mikoa kutolewa TAMISEMI

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,233
4,451
Hivi majuzi Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya mchapakazi, akiwa Morogoro alitoa taarifa kwamba hospitali za rufaa za mikoa zinakusudiwa kuhamishiwa Wizara ya Afya, toka mamlaka ya TAMISEMI.

Ingawa serikali ni moja, lakini kitendo cha hospitali za rufaa za mikoa kuwa chini ya TAMISEMI kinarahisisha mambo mengi sana ya kiutawala hasahasa katika kutatua kero za watumishi wa afya kama kutoa ajira, kuwaingiza watumishi haraka kwenye payroll, kulipa madai ya mishahara kwa wakati, kupandishwa vyeo kwa wakati n.k. Na pia wananchi kufikisha malalamiko yao kirahisi. Hii ni kwa sababu mamlaka zinazosimamia hospitali hizi zipo jirani na hospitali, tofauti na wizara ya afya ambayo iko centralized sana. Watumishi wa afya wa hospitali husika sasa watapaswa kusafiri kwenda Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam ili kufuatilia madai yao mbalimbali, ambayo yalikuwa yakihudumiwa vizuri na ofisi ya Katibu Tawala wa mkoa (RAS). Bahati mbaya sana hili litarejesha nyuma ufanisi wa hospitali hizi.

Ni bahati mbaya sana kwamba Wizara ya Afya imeshindwa kuzihudumia vizuri hospitali zake chache katika rasilimali watu, mfano Mirembe, Kibong'oto na hospitali ya rufaa Mbeya, sababu kubwa ikiwa ofisi yake pekee iko jijini Dar es Salaam, huku TAMISEMI ikiwa imesambaa. Chukua hospitali yoyote ya mkoa, halafu nenda kalinganishe na hospitali zilizo chini ya Wizara ya Afya uone ipi ina malalamiko mengi ya watumishi!!! Za TAMISEMI zina manung'uniko machache sana.

Lakini pia baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa Wizara ya Afya, huzitumia hospitali zilizo chini yake kufanya ubadhirifu mbalimbali. Mfano kuzihamishia pesa zisizo maelezo kwenda hospitali husika, na kisha kurejeshwa kwenye akaunti za Watumishi wasio waaminifu.

HAKUNA UMUHIMU wa kuzihamisha hospitali za mikoa kutoka TAMISEMI naamini hili hata watumishi wa hospitali hizi hawalipendi, cha muhimu wizara ya Afya na TAMISEMI wapeane ushirikiano katika kutatua changamoto zilizopo. Mkuu wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa wanatosha sana kumwakilisha Rais katika kusimamia hospitali hizi ambazo ndizo uti wa afya mikoani, Wizara ya Afya ibaki kuwa na majukumu iliyonayo sasa ikiwa ni pamoja na regulation, kama kuna mapungufu basi yanapaswa kutatuliwa.



Hospitali za rufaa za mikoa zahamishiwa Wizara ya Afya

Monday, November 27, 2017
PIC+tAMISEMI.jpg

Kwa ufupi
Tamisemi itaendelea kusimamia hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati.

By Habel Chidawali, Mwananchi hchidawali@mwananchi.co.tz
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo amekabidhi hospitali za rufaa za mikoa kwa Wizara ya Afya.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa pendekezo la Rais John Magufuli aliyetaka waziri wa Tamisemi na wa Waziri ya Afya wakae kujadili namna ya kuzifanya hospitali za mikoa kuwa chini ya Wizara ya Afya badala ya kusimamiwa na Tamisemi kama ilivyo sasa.

Jumamosi Novemba 25,2017 alipozindua Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas), kampasi ya Mloganzila, Rais Magufuli alisema kufanya hivyo kutaondoa mkanganyiko na kupanga watumishi holela kwenye hospitali, jukumu ambalo wamepewa watu wasio na utaalamu wa masuala ya afya.

Rais Magufuli alisema Tamisemi watabaki wanasimamia hospitali za wilaya na nyingine ndogo.

Waziri Jafo amesema leo Jumatatu Novemba 27,2017 kuwa tayari wameshafanya mazungumzo.

"Kuanzia leo hospitali zote za rufaa zitakuwa chini ya Wizara ya Afya na kwetu sisi (Tamisemi) tutabaki na hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati pekee," amesema.

Kuhusu madaraka ya waganga wakuu wa mikoa amesema wataendelea kuwa chini ya Tamisemi lakini waganga wafawidhi wa hospitali watapelekwa Wizara ya Afya.

Amewataka waganga hao kufanya kazi waliyokubaliana na Tamisemi ya kusimamia ujenzi wa vituo vya afya 172 nchi nzima.

Akizungumza mgongano wa madaraka kwa waganga wa mikoa, Naibu Katibu Mkuu Tamisemi (Afya), Dk Zainabu Chaula amesema hakutakuwa na shida kwa kuwa kila kitu kimewekwa sawa.

Dk Chaula amesema hata kabla ya kupelekwa huko, hospitali za mikoa zilikuwa zikipeleka taarifa moja kwa moja wizarani.

My Take
Kuna mtu hajamshauri vizuri Mheshimiwa.
 
Nadhani kuna logic katika hoja zako, japokuwa sifahamu sababu za zilizopelekea mh Waziri kuona sasa ni vizuri kwa hizo hospital kusimamiwa na wizara badala ya TAMISEMI
 
I support your arguement. Kuna conflict ya muda mrefu hapa nchini kati ya watu wa Dar na Mikoani kugombania usimamizi wa taasisi zilizopo mikoani.

Watu wa Dar wanatamani kusimamia taasisi za mikoani bila ya kujali gharama za usimamizi na mambo mengine yenye masilahi ya Taifa.

Mawaziri wengi wameingizwa mkenge wa kupigania usimamizi kuhamishiwa Dar na kujikuta wanatumia nguvu nyingi ktk hilo huku wakiacha mambo ya msingi.
 
Nasikitika kama ni kweli kuwa Waziri wetu mchapakazi kama Ummy Mwalinu naye kakubali kuingizwa mkenge kama mawaziri waliomtangulia katika suala hili.

Yeye tulitarajia ajikite kwenye mambo ya msingi aliyoanza nayo ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, vifaa tiba na vya kisasa vinapatikana kwenye hospitali zote za umma na mambo ya aina hiyo.
Nami naungana na wengine wenye nia njema kwa Waziri Ummy kumrai kuwa aachane kabisa na hiyo biashara ya kigombania usimamizi.
 
ushauri huu ni wakizalendo unapaswa kuzinatiwa na wahuska nimeguswa sana na kipenele cha udahili wa vyuo vyetu vya afya ukilinganisha na nchi za wenzetu nihatari sana
 
Wizara ya Afya ibaki na majukumu yaliyoainishwa kama overview wa Afya za watanzania.

Mambo ya Huduma za Hospital za wilaya na mikoa zibaki kwa Tamisemi kama awali.

Nakumbuka utawala wa Rais Mwinyi kuna maafisa zaidi ya 10 toka Wizara ya Afya walitimuliwa na kurudishwa kutibu wagonjwa au kufundisha baada ya ubadhirifu mkubwa pale wizarani.Tusirudi huko.

Ugomvi wa kimaslahi wa maafisa wa ngazi za juu wa Afya unaweza ukawa ndiyo chanzo cha kumpa Waziri wazo na sababu za kuhamisha hospital za mikoa kuwa chini ya Wizara.
 
Hivi majuzi Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya mchapakazi, akiwa Morogoro alitoa taarifa kwamba hospitali za rufaa za mikoa zinakusudiwa kuhamishiwa Wizara ya Afya, toka mamlaka ya TAMISEMI.

Ingawa serikali ni moja, lakini kitendo cha hospitali za rufaa za mikoa kuwa chini ya TAMISEMI kinarahisisha mambo mengi sana ya kiutawala hasahasa katika kutatua kero za watumishi wa afya kama kutoa ajira, kuwaingiza watumishi haraka kwenye payroll, kulipa madai ya mishahara kwa wakati, kupandishwa vyeo kwa wakati n.k. Na pia wananchi kufikisha malalamiko yao kirahisi. Hii ni kwa sababu mamlaka zinazosimamia hospitali hizi zipo jirani na hospitali, tofauti na wizara ya afya ambayo iko centralized sana. Watumishi wa afya wa hospitali husika sasa watapaswa kusafiri kwenda Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam ili kufuatilia madai yao mbalimbali, ambayo yalikuwa yakihudumiwa vizuri na ofisi ya Katibu Tawala wa mkoa (RAS). Bahati mbaya sana hili litarejesha nyuma ufanisi wa hospitali hizi.

Ni bahati mbaya sana kwamba Wizara ya Afya imeshindwa kuzihudumia vizuri hospitali zake chache katika rasilimali watu, mfano Mirembe, Kibong'oto na hospitali ya rufaa Mbeya, sababu kubwa ikiwa ofisi yake pekee iko jijini Dar es Salaam, huku TAMISEMI ikiwa imesambaa. Chukua hospitali yoyote ya mkoa, halafu nenda kalinganishe na hospitali zilizo chini ya Wizara ya Afya uone ipi ina malalamiko mengi ya watumishi!!! Za TAMISEMI zina manung'uniko machache sana.

Lakini pia baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa Wizara ya Afya, huzitumia hospitali zilizo chini yake kufanya ubadhirifu mbalimbali. Mfano kuzihamishia pesa zisizo maelezo kwenda hospitali husika, na kisha kurejeshwa kwenye akaunti za Watumishi wasio waaminifu.

HAKUNA UMUHIMU wa kuzihamisha hospitali za mikoa kutoka TAMISEMI naamini hili hata watumishi wa hospitali hizi hawalipendi, cha muhimu wizara ya Afya na TAMISEMI wapeane ushirikiano katika kutatua changamoto zilizopo. Mkuu wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa wanatosha sana kumwakilisha Rais katika kusimamia hospitali hizi ambazo ndizo uti wa afya mikoani, Wizara ya Afya ibaki kuwa na majukumu iliyonayo sasa ikiwa ni pamoja na regulation, kama kuna mapungufu basi yanapaswa kutatuliwa.


Napingana hoja yako....nitakueleza kwa nini.
 
Mleta mada futa kwanza kauli ya kusema Ummy Mwalimu ni mchapa kazi, yaani Ummy Mwalimu ni waziri wa Ovyo kupita maelezo, kwa sababu.
1/Ni mropokaji balaa. Yule ni zaidi ya Chiriku.
2/Ni mnafiki mno.
3/Ni mbumbu wa mambo ya Afya.
4/Ni muongo balaa.
5/Ni mvuvi.

Jaribu kuchunguza wewe mwenyewe halafu utakuja kuniambia.
 
Hivi majuzi Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya mchapakazi, akiwa Morogoro alitoa taarifa kwamba hospitali za rufaa za mikoa zinakusudiwa kuhamishiwa Wizara ya Afya, toka mamlaka ya TAMISEMI.

MAJIBU YA JINGALAO
Hili ni tamko sahihi na limefanyiwa kazi mda mrefu sana kiasi cha kuingizwa kwenye ilani ya CCM 2015..Inawezekana wakati CCM inatoa sera zake wewe ulikuwa unazungusha mikono.YAANI HOSPITALI ZA MIKOA KUPEWA HADHI YA HOSPITALI YA RUFAA ILI KUNORESHA HUDUMA NA KUACHANA NA UKIRITIMBA WA KUTEGEMEA HOSPITALI CHACHE ZILIZOKUWA ZA RUFAA AMBAPO SASA ZITAKUWA NI CONSULTANT HOSPITALS.ikumbukwe kuwa kulikuwa na msongamano mkubwa sana katika hospitali kama Mbeya,KCMC,Bugando na MNH kiasi cha kuleta malalamiko ya mara kwa mara.

Ingawa serikali ni moja, lakini kitendo cha hospitali za rufaa za mikoa kuwa chini ya TAMISEMI kinarahisisha mambo mengi sana ya kiutawala hasahasa katika kutatua kero za watumishi wa afya kama kutoa ajira, kuwaingiza watumishi haraka kwenye payroll, kulipa madai ya mishahara kwa wakati, kupandishwa vyeo kwa wakati n.k.

MAJIBU YA JINGALAO
Huu ni uongo kwani watumishi wengi walioko chini ya halmashauri wana malalamiko makubwa sana tena hayo hayo uliyoyataja.watumishi wanachelewa kupanda vyeo,hawalipwi stahiki zao kwa wakati ...hospitali hizi ingawa zinazalisha kiasi kingi cha fedha ...mara nyingi fedha hizo zinaelekezwa kwenye matumizi mengine yasiyohusu afya kisa tu RAS ndio mmiliki wa hizo fedha.Hospitali hizi zinatakiwa kupewa gawio la asilimia 20 ya mapato ya halmashauri lakini kiutendaji huwa fedha hizo hazitolewi.waeka hazina na maRAS wamekuwa ni miungu watu inapokuja suala la matumizi halali na ya muhimu kwa maendeleo ya hospitali hizo...kiasi cha kushusha ari ya ukusanyaji wa mapato.

Na pia wananchi kufikisha malalamiko yao kirahisi. Hii ni kwa sababu mamlaka zinazosimamia hospitali hizi zipo jirani na hospitali, tofauti na wizara ya afya ambayo iko centralized sana.

MAJIBU YA JINGALAO
Labda nikuulize wananchi wanawezaje kutoa malalamiko yao dhidi ya Muhimbili au bugando au KCMc?huo umbali wa kutoa malalamiko unatoka wapi katika ulimwengu huu wa teknolojia?sana sana hospitali hizi zimekuwa zikisumbuliwa sana na madiwani kwa malalamiko yasiyo na ukweli.
Watumishi wa afya wa hospitali husika sasa watapaswa kusafiri kwenda Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam ili kufuatilia madai yao mbalimbali,

MAJIBU YA JINGALAO
Hebu taja hayo malalamiko ya watumishi wa afya yanayotakiwa kwenda wizarani tuyajue.isitoshe malalamiko ya watumishi wa afya ni yale yale kuanzia ngazi ya zahanati mpaka ngazi ya consultant hospitals.

ambayo yalikuwa yakihudumiwa vizuri na ofisi ya Katibu Tawala wa mkoa (RAS). Bahati mbaya sana hili litarejesha nyuma ufanisi wa hospitali hizi.

MAJIBU YA JINGALAO
Ufanisi wa hospitali hizi umekuwa mbovu kwa miaka yote hii zikiwa chini ya RAS.
Ni bahati mbaya sana kwamba Wizara ya Afya imeshindwa kuzihudumia vizuri hospitali zake chache katika rasilimali watu, mfano Mirembe, Kibong'oto na hospitali ya rufaa Mbeya, sababu kubwa ikiwa ofisi yake pekee iko jijini Dar es Salaam, huku TAMISEMI ikiwa imesambaa. Chukua hospitali yoyote ya mkoa, halafu nenda kalinganishe na hospitali zilizo chini ya Wizara ya Afya uone ipi ina malalamiko mengi ya watumishi!!! Za TAMISEMI zina manung'uniko machache sana.

MAJIBU YA JINGALAO
Mtazamo wa sasa wa wizara na serikali ni kuondokana na suala la utegemezi kwa serikali kuu na badala yake hospitali hizi zijiendeshe mithili ya taasisi kama MNH,MOI n.k

Lakini pia baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa Wizara ya Afya, huzitumia hospitali zilizo chini yake kufanya ubadhirifu mbalimbali. Mfano kuzihamishia pesa zisizo maelezo kwenda hospitali husika, na kisha kurejeshwa kwenye akaunti za Watumishi wasio waaminifu.

MAJIBU YA JINGALAO
Halmashauri nyingi imezitumia hospitali hizi za mikoa na hata zile za wilaya kibadhirifu mno na ndio maana malalamiko ya ukosefu wa dawa na viffa ni makubwa...ten percent kwenye manunuzi imekuwa ni mwiba wa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa wakati.Ndio maana wadau wengi wa level za RAS na concils mnalilia zibakie kwenu ili muendelee kupiga hela.


HAKUNA UMUHIMU wa kuzihamisha hospitali za mikoa kutoka TAMISEMI naamini hili hata watumishi wa hospitali hizi hawalipendi, cha muhimu wizara ya Afya na TAMISEMI wapeane ushirikiano katika kutatua changamoto zilizopo. Mkuu wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa wanatosha sana kumwakilisha Rais katika kusimamia hospitali hizi ambazo ndizo uti wa afya mikoani, Wizara ya Afya ibaki kuwa na majukumu iliyonayo sasa ikiwa ni pamoja na regulation, kama kuna mapungufu basi yanapaswa kutatuliwa.

MAJIBU YA JINGALAO
Umuhimu wa kuzifanya hospitali hizi kuwa taasisi ni mkubwa sana ...hospitali ziachwe zifanye kazi na pia zitaepushwa sana na siasa za madiwani.

RAS au manispaa husika zijenge hospitali zake ili kuwahudumia watu wake wanaohitaji huduma za primary health care na sio kujificha kwenye kivuli cha RRHs.



Nadhani kwenye bold nimekujibu...
 
Mleta mada futa kwanza kauli ya kusema Ummy Mwalimu ni mchapa kazi, yaani Ummy Mwalimu ni waziri wa Ovyo kupita maelezo, kwa sababu.
1/Ni mropokaji balaa. Yule ni zaidi ya Chiriku.
2/Ni mnafiki mno.
3/Ni mbumbu wa mambo ya Afya.
4/Ni muongo balaa.
5/Ni mvuvi.

Jaribu kuchunguza wewe mwenyewe halafu utakuja kuniambia.
Kwa hili wewe ndio mkurupukaji...kaisome ilani ya ccm.
 
Nasikitika kama ni kweli kuwa Waziri wetu mchapakazi kama Ummy Mwalinu naye kakubali kuingizwa mkenge kama mawaziri waliomtangulia katika suala hili.

Yeye tulitarajia ajikite kwenye mambo ya msingi aliyoanza nayo ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, vifaa tiba na vya kisasa vinapatikana kwenye hospitali zote za umma na mambo ya aina hiyo.
Nami naungana na wengine wenye nia njema kwa Waziri Ummy kumrai kuwa aachane kabisa na hiyo biashara ya kigombania usimamizi.
Hivi wakati wagombea wanatoa sera huwa mnaangalia wasanii tu?
 
Hivi majuzi Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya mchapakazi, akiwa Morogoro alitoa taarifa kwamba hospitali za rufaa za mikoa zinakusudiwa kuhamishiwa Wizara ya Afya, toka mamlaka ya TAMISEMI.

Ingawa serikali ni moja, lakini kitendo cha hospitali za rufaa za mikoa kuwa chini ya TAMISEMI kinarahisisha mambo mengi sana ya kiutawala hasahasa katika kutatua kero za watumishi wa afya kama kutoa ajira, kuwaingiza watumishi haraka kwenye payroll, kulipa madai ya mishahara kwa wakati, kupandishwa vyeo kwa wakati n.k. Na pia wananchi kufikisha malalamiko yao kirahisi. Hii ni kwa sababu mamlaka zinazosimamia hospitali hizi zipo jirani na hospitali, tofauti na wizara ya afya ambayo iko centralized sana. Watumishi wa afya wa hospitali husika sasa watapaswa kusafiri kwenda Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam ili kufuatilia madai yao mbalimbali, ambayo yalikuwa yakihudumiwa vizuri na ofisi ya Katibu Tawala wa mkoa (RAS). Bahati mbaya sana hili litarejesha nyuma ufanisi wa hospitali hizi.

Ni bahati mbaya sana kwamba Wizara ya Afya imeshindwa kuzihudumia vizuri hospitali zake chache katika rasilimali watu, mfano Mirembe, Kibong'oto na hospitali ya rufaa Mbeya, sababu kubwa ikiwa ofisi yake pekee iko jijini Dar es Salaam, huku TAMISEMI ikiwa imesambaa. Chukua hospitali yoyote ya mkoa, halafu nenda kalinganishe na hospitali zilizo chini ya Wizara ya Afya uone ipi ina malalamiko mengi ya watumishi!!! Za TAMISEMI zina manung'uniko machache sana.

Lakini pia baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa Wizara ya Afya, huzitumia hospitali zilizo chini yake kufanya ubadhirifu mbalimbali. Mfano kuzihamishia pesa zisizo maelezo kwenda hospitali husika, na kisha kurejeshwa kwenye akaunti za Watumishi wasio waaminifu.

HAKUNA UMUHIMU wa kuzihamisha hospitali za mikoa kutoka TAMISEMI naamini hili hata watumishi wa hospitali hizi hawalipendi, cha muhimu wizara ya Afya na TAMISEMI wapeane ushirikiano katika kutatua changamoto zilizopo. Mkuu wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa wanatosha sana kumwakilisha Rais katika kusimamia hospitali hizi ambazo ndizo uti wa afya mikoani, Wizara ya Afya ibaki kuwa na majukumu iliyonayo sasa ikiwa ni pamoja na regulation, kama kuna mapungufu basi yanapaswa kutatuliwa.


Tatizo lako ni kuwa hujatuekeza malengo ya wizara ni nini?

Bila kuyatambua uimara wake na udhaifu wake unawaonea. Unawapima kwenye mizania ambayo malengo yao yamewekwa pembeni kabisa.

Hujawatendea ubinadamu.

Pili, kubwa kwa wizara ni maendeleo yanayowiana kwa hospitali zote za rufaa za mikoa.

Zikiwa chini ya Tamisemi yapo matatizo ya baadhi ya mafungu kuelekezwa kwenye vipaumbele vinginevyo.

Pia, siyo kazi ya RAS kuingilia uendeshaji wa Hospitali za rufaa za mikoa kwani hospitali hizo ili kuwa na ufanisi zinapaswa kujitegemea kiutawala kama su agencies za serikalini.

Ofisi ya mkuu wa mkoa iendelee na majukumu mengine ila ya uendeshaji wa hizi hospitali za mikoa siasa zipunguzwe
 
Nasikitika kama ni kweli kuwa Waziri wetu mchapakazi kama Ummy Mwalinu naye kakubali kuingizwa mkenge kama mawaziri waliomtangulia katika suala hili.

Yeye tulitarajia ajikite kwenye mambo ya msingi aliyoanza nayo ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, vifaa tiba na vya kisasa vinapatikana kwenye hospitali zote za umma na mambo ya aina hiyo.
Nami naungana na wengine wenye nia njema kwa Waziri Ummy kumrai kuwa aachane kabisa na hiyo biashara ya kigombania usimamizi.

Huyo waziri wana mwingiza mkenge.
Huenda kunakundi la watumishi wana mpotosha Kwa sababu zao.
Pia Ni mwaka huu alirudishwa Na Mswada Bungeni .
 
Nadhani kwenye bold nimekujibu...
Majibu yako ni sahihi asilimia 100, huyu aliyeleta hoja naona hana uelewa halisi wa hizi, hospitali, na siku zikiwa zinajiendesha km taasisi zilizochini ya wizara ya afya moja kwa moja tutaona mabadiliko makubwa sana!
Nimekuwa nikiliota na kulitamani jambo hili muda mrefu sana
 
Hospitali ndio zishahamishwa sasa. Wengi wa watumishi walioko hospitali za mikoa wanalalamika. Sasa issue zao za ajira inabidi wazifuatilie hadi Wizara ya Afya ambako kuna Maafisa Utumishi waliochoka kufanya kazi. Ningeshauri maofisa utumishi wa wizara ya afya wahamishiwe kwenye hospitali zote za wizara. Wasikae makao makuu ambapo 'DAP' anatosha sana kuhudumia watumishi waliopo.
 
Hivi majuzi Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya mchapakazi, akiwa Morogoro alitoa taarifa kwamba hospitali za rufaa za mikoa zinakusudiwa kuhamishiwa Wizara ya Afya, toka mamlaka ya TAMISEMI.

Ingawa serikali ni moja, lakini kitendo cha hospitali za rufaa za mikoa kuwa chini ya TAMISEMI kinarahisisha mambo mengi sana ya kiutawala hasahasa katika kutatua kero za watumishi wa afya kama kutoa ajira, kuwaingiza watumishi haraka kwenye payroll, kulipa madai ya mishahara kwa wakati, kupandishwa vyeo kwa wakati n.k. Na pia wananchi kufikisha malalamiko yao kirahisi. Hii ni kwa sababu mamlaka zinazosimamia hospitali hizi zipo jirani na hospitali, tofauti na wizara ya afya ambayo iko centralized sana. Watumishi wa afya wa hospitali husika sasa watapaswa kusafiri kwenda Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam ili kufuatilia madai yao mbalimbali, ambayo yalikuwa yakihudumiwa vizuri na ofisi ya Katibu Tawala wa mkoa (RAS). Bahati mbaya sana hili litarejesha nyuma ufanisi wa hospitali hizi.

Ni bahati mbaya sana kwamba Wizara ya Afya imeshindwa kuzihudumia vizuri hospitali zake chache katika rasilimali watu, mfano Mirembe, Kibong'oto na hospitali ya rufaa Mbeya, sababu kubwa ikiwa ofisi yake pekee iko jijini Dar es Salaam, huku TAMISEMI ikiwa imesambaa. Chukua hospitali yoyote ya mkoa, halafu nenda kalinganishe na hospitali zilizo chini ya Wizara ya Afya uone ipi ina malalamiko mengi ya watumishi!!! Za TAMISEMI zina manung'uniko machache sana.

Lakini pia baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa Wizara ya Afya, huzitumia hospitali zilizo chini yake kufanya ubadhirifu mbalimbali. Mfano kuzihamishia pesa zisizo maelezo kwenda hospitali husika, na kisha kurejeshwa kwenye akaunti za Watumishi wasio waaminifu.

HAKUNA UMUHIMU wa kuzihamisha hospitali za mikoa kutoka TAMISEMI naamini hili hata watumishi wa hospitali hizi hawalipendi, cha muhimu wizara ya Afya na TAMISEMI wapeane ushirikiano katika kutatua changamoto zilizopo. Mkuu wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa wanatosha sana kumwakilisha Rais katika kusimamia hospitali hizi ambazo ndizo uti wa afya mikoani, Wizara ya Afya ibaki kuwa na majukumu iliyonayo sasa ikiwa ni pamoja na regulation, kama kuna mapungufu basi yanapaswa kutatuliwa.



Hospitali za rufaa za mikoa zahamishiwa Wizara ya Afya

Monday, November 27, 2017
PIC+tAMISEMI.jpg

Kwa ufupi
Tamisemi itaendelea kusimamia hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati.

By Habel Chidawali, Mwananchi hchidawali@mwananchi.co.tz
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo amekabidhi hospitali za rufaa za mikoa kwa Wizara ya Afya.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa pendekezo la Rais John Magufuli aliyetaka waziri wa Tamisemi na wa Waziri ya Afya wakae kujadili namna ya kuzifanya hospitali za mikoa kuwa chini ya Wizara ya Afya badala ya kusimamiwa na Tamisemi kama ilivyo sasa.

Jumamosi Novemba 25,2017 alipozindua Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas), kampasi ya Mloganzila, Rais Magufuli alisema kufanya hivyo kutaondoa mkanganyiko na kupanga watumishi holela kwenye hospitali, jukumu ambalo wamepewa watu wasio na utaalamu wa masuala ya afya.

Rais Magufuli alisema Tamisemi watabaki wanasimamia hospitali za wilaya na nyingine ndogo.

Waziri Jafo amesema leo Jumatatu Novemba 27,2017 kuwa tayari wameshafanya mazungumzo.

"Kuanzia leo hospitali zote za rufaa zitakuwa chini ya Wizara ya Afya na kwetu sisi (Tamisemi) tutabaki na hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati pekee," amesema.

Kuhusu madaraka ya waganga wakuu wa mikoa amesema wataendelea kuwa chini ya Tamisemi lakini waganga wafawidhi wa hospitali watapelekwa Wizara ya Afya.

Amewataka waganga hao kufanya kazi waliyokubaliana na Tamisemi ya kusimamia ujenzi wa vituo vya afya 172 nchi nzima.

Akizungumza mgongano wa madaraka kwa waganga wa mikoa, Naibu Katibu Mkuu Tamisemi (Afya), Dk Zainabu Chaula amesema hakutakuwa na shida kwa kuwa kila kitu kimewekwa sawa.

Dk Chaula amesema hata kabla ya kupelekwa huko, hospitali za mikoa zilikuwa zikipeleka taarifa moja kwa moja wizarani.

My Take
Kuna mtu hajamshauri


Hivi majuzi Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya mchapakazi, akiwa Morogoro alitoa taarifa kwamba hospitali za rufaa za mikoa zinakusudiwa kuhamishiwa Wizara ya Afya, toka mamlaka ya TAMISEMI.

Ingawa serikali ni moja, lakini kitendo cha hospitali za rufaa za mikoa kuwa chini ya TAMISEMI kinarahisisha mambo mengi sana ya kiutawala hasahasa katika kutatua kero za watumishi wa afya kama kutoa ajira, kuwaingiza watumishi haraka kwenye payroll, kulipa madai ya mishahara kwa wakati, kupandishwa vyeo kwa wakati n.k. Na pia wananchi kufikisha malalamiko yao kirahisi. Hii ni kwa sababu mamlaka zinazosimamia hospitali hizi zipo jirani na hospitali, tofauti na wizara ya afya ambayo iko centralized sana. Watumishi wa afya wa hospitali husika sasa watapaswa kusafiri kwenda Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam ili kufuatilia madai yao mbalimbali, ambayo yalikuwa yakihudumiwa vizuri na ofisi ya Katibu Tawala wa mkoa (RAS). Bahati mbaya sana hili litarejesha nyuma ufanisi wa hospitali hizi.

Ni bahati mbaya sana kwamba Wizara ya Afya imeshindwa kuzihudumia vizuri hospitali zake chache katika rasilimali watu, mfano Mirembe, Kibong'oto na hospitali ya rufaa Mbeya, sababu kubwa ikiwa ofisi yake pekee iko jijini Dar es Salaam, huku TAMISEMI ikiwa imesambaa. Chukua hospitali yoyote ya mkoa, halafu nenda kalinganishe na hospitali zilizo chini ya Wizara ya Afya uone ipi ina malalamiko mengi ya watumishi!!! Za TAMISEMI zina manung'uniko machache sana.

Lakini pia baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa Wizara ya Afya, huzitumia hospitali zilizo chini yake kufanya ubadhirifu mbalimbali. Mfano kuzihamishia pesa zisizo maelezo kwenda hospitali husika, na kisha kurejeshwa kwenye akaunti za Watumishi wasio waaminifu.

HAKUNA UMUHIMU wa kuzihamisha hospitali za mikoa kutoka TAMISEMI naamini hili hata watumishi wa hospitali hizi hawalipendi, cha muhimu wizara ya Afya na TAMISEMI wapeane ushirikiano katika kutatua changamoto zilizopo. Mkuu wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa wanatosha sana kumwakilisha Rais katika kusimamia hospitali hizi ambazo ndizo uti wa afya mikoani, Wizara ya Afya ibaki kuwa na majukumu iliyonayo sasa ikiwa ni pamoja na regulation, kama kuna mapungufu basi yanapaswa kutatuliwa.



Hospitali za rufaa za mikoa zahamishiwa Wizara ya Afya

Monday, November 27, 2017
PIC+tAMISEMI.jpg

Kwa ufupi
Tamisemi itaendelea kusimamia hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati.

By Habel Chidawali, Mwananchi hchidawali@mwananchi.co.tz
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo amekabidhi hospitali za rufaa za mikoa kwa Wizara ya Afya.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa pendekezo la Rais John Magufuli aliyetaka waziri wa Tamisemi na wa Waziri ya Afya wakae kujadili namna ya kuzifanya hospitali za mikoa kuwa chini ya Wizara ya Afya badala ya kusimamiwa na Tamisemi kama ilivyo sasa.

Jumamosi Novemba 25,2017 alipozindua Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas), kampasi ya Mloganzila, Rais Magufuli alisema kufanya hivyo kutaondoa mkanganyiko na kupanga watumishi holela kwenye hospitali, jukumu ambalo wamepewa watu wasio na utaalamu wa masuala ya afya.

Rais Magufuli alisema Tamisemi watabaki wanasimamia hospitali za wilaya na nyingine ndogo.

Waziri Jafo amesema leo Jumatatu Novemba 27,2017 kuwa tayari wameshafanya mazungumzo.

"Kuanzia leo hospitali zote za rufaa zitakuwa chini ya Wizara ya Afya na kwetu sisi (Tamisemi) tutabaki na hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati pekee," amesema.

Kuhusu madaraka ya waganga wakuu wa mikoa amesema wataendelea kuwa chini ya Tamisemi lakini waganga wafawidhi wa hospitali watapelekwa Wizara ya Afya.

Amewataka waganga hao kufanya kazi waliyokubaliana na Tamisemi ya kusimamia ujenzi wa vituo vya afya 172 nchi nzima.

Akizungumza mgongano wa madaraka kwa waganga wa mikoa, Naibu Katibu Mkuu Tamisemi (Afya), Dk Zainabu Chaula amesema hakutakuwa na shida kwa kuwa kila kitu kimewekwa sawa.

Dk Chaula amesema hata kabla ya kupelekwa huko, hospitali za mikoa zilikuwa zikipeleka taarifa moja kwa moja wizarani.

My Take
Kuna mtu hajamshauri vizuri Mheshimiw


Hivi majuzi Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya mchapakazi, akiwa Morogoro alitoa taarifa kwamba hospitali za rufaa za mikoa zinakusudiwa kuhamishiwa Wizara ya Afya, toka mamlaka ya TAMISEMI.

Ingawa serikali ni moja, lakini kitendo cha hospitali za rufaa za mikoa kuwa chini ya TAMISEMI kinarahisisha mambo mengi sana ya kiutawala hasahasa katika kutatua kero za watumishi wa afya kama kutoa ajira, kuwaingiza watumishi haraka kwenye payroll, kulipa madai ya mishahara kwa wakati, kupandishwa vyeo kwa wakati n.k. Na pia wananchi kufikisha malalamiko yao kirahisi. Hii ni kwa sababu mamlaka zinazosimamia hospitali hizi zipo jirani na hospitali, tofauti na wizara ya afya ambayo iko centralized sana. Watumishi wa afya wa hospitali husika sasa watapaswa kusafiri kwenda Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam ili kufuatilia madai yao mbalimbali, ambayo yalikuwa yakihudumiwa vizuri na ofisi ya Katibu Tawala wa mkoa (RAS). Bahati mbaya sana hili litarejesha nyuma ufanisi wa hospitali hizi.

Ni bahati mbaya sana kwamba Wizara ya Afya imeshindwa kuzihudumia vizuri hospitali zake chache katika rasilimali watu, mfano Mirembe, Kibong'oto na hospitali ya rufaa Mbeya, sababu kubwa ikiwa ofisi yake pekee iko jijini Dar es Salaam, huku TAMISEMI ikiwa imesambaa. Chukua hospitali yoyote ya mkoa, halafu nenda kalinganishe na hospitali zilizo chini ya Wizara ya Afya uone ipi ina malalamiko mengi ya watumishi!!! Za TAMISEMI zina manung'uniko machache sana.

Lakini pia baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa Wizara ya Afya, huzitumia hospitali zilizo chini yake kufanya ubadhirifu mbalimbali. Mfano kuzihamishia pesa zisizo maelezo kwenda hospitali husika, na kisha kurejeshwa kwenye akaunti za Watumishi wasio waaminifu.

HAKUNA UMUHIMU wa kuzihamisha hospitali za mikoa kutoka TAMISEMI naamini hili hata watumishi wa hospitali hizi hawalipendi, cha muhimu wizara ya Afya na TAMISEMI wapeane ushirikiano katika kutatua changamoto zilizopo. Mkuu wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa wanatosha sana kumwakilisha Rais katika kusimamia hospitali hizi ambazo ndizo uti wa afya mikoani, Wizara ya Afya ibaki kuwa na majukumu iliyonayo sasa ikiwa ni pamoja na regulation, kama kuna mapungufu basi yanapaswa kutatuliwa.



Hospitali za rufaa za mikoa zahamishiwa Wizara ya Afya

Monday, November 27, 2017
PIC+tAMISEMI.jpg

Kwa ufupi
Tamisemi itaendelea kusimamia hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati.

By Habel Chidawali, Mwananchi hchidawali@mwananchi.co.tz
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo amekabidhi hospitali za rufaa za mikoa kwa Wizara ya Afya.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa pendekezo la Rais John Magufuli aliyetaka waziri wa Tamisemi na wa Waziri ya Afya wakae kujadili namna ya kuzifanya hospitali za mikoa kuwa chini ya Wizara ya Afya badala ya kusimamiwa na Tamisemi kama ilivyo sasa.

Jumamosi Novemba 25,2017 alipozindua Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas), kampasi ya Mloganzila, Rais Magufuli alisema kufanya hivyo kutaondoa mkanganyiko na kupanga watumishi holela kwenye hospitali, jukumu ambalo wamepewa watu wasio na utaalamu wa masuala ya afya.

Rais Magufuli alisema Tamisemi watabaki wanasimamia hospitali za wilaya na nyingine ndogo.

Waziri Jafo amesema leo Jumatatu Novemba 27,2017 kuwa tayari wameshafanya mazungumzo.

"Kuanzia leo hospitali zote za rufaa zitakuwa chini ya Wizara ya Afya na kwetu sisi (Tamisemi) tutabaki na hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati pekee," amesema.

Kuhusu madaraka ya waganga wakuu wa mikoa amesema wataendelea kuwa chini ya Tamisemi lakini waganga wafawidhi wa hospitali watapelekwa Wizara ya Afya.

Amewataka waganga hao kufanya kazi waliyokubaliana na Tamisemi ya kusimamia ujenzi wa vituo vya afya 172 nchi nzima.

Akizungumza mgongano wa madaraka kwa waganga wa mikoa, Naibu Katibu Mkuu Tamisemi (Afya), Dk Zainabu Chaula amesema hakutakuwa na shida kwa kuwa kila kitu kimewekwa sawa.

Dk Chaula amesema hata kabla ya kupelekwa huko, hospitali za mikoa zilikuwa zikipeleka taarifa moja kwa moja wizarani.

My Take
Kuna mtu hajamshauri vizuri Mheshimiwa.

Vipi Bado unahuo wasiwasi mpaka leo?
 
Back
Top Bottom