Rais Magufuli: Suluhu ya Zanzibar ni Uchaguzi wa marudio

yaan hili la Zanzibar limewakalia vibaya sana ccm kweli wizi unamwisho ujanja ujanja wa ccm naona kama umegota.sasa leo rais magufuli kaamua kufunguka waziwazi kuwa Zanzibar ni nchi inakila kitu chake! wakati pinda alivyoulizwaga bungeni alisema ni moja ya kipande cha tanzania yaa mkoa.leo rais amethibitisha! kaenda mbali eti cuf warudie kuthibitisha ushindi wao!hiv kumbe ukishinda huwa unatakiwa kurudia uchaguz tena bila kampen! na hizo pesa za marudio nan atatoa?na aliye haribu uchaguzi yuko magereza au? tume wako wamoja au wamegawanyika? eee mungu simama upande wa haki yetu sisi wazanzibar
Nakubaliana kabisa na hoja yako.

Hao CCM walikurupuka 'kumuamrisha' Jecha aufute uchaguzi ule na kutangaza uchaguzi wa marudio bila kuangalia impact yake.

Hao CCM waliamini ya kuwa haiwezekani CUF wakasusia uchaguzi wa marejeo.

Kitendo cha CUF kuendelea na msimamo wao wa kususia uchaguzi huo, kunafanya mkwamo huu wa kisiasa kutoweza kumalizika hata kama watalazimisha kufanya uchaguzi huo wa marejeo hiyo tarehe 20/03/2016.

Kwa kuwa kwenye makubaliano ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa [SUK] ambayo yameingizwa kwenye Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, limewekwa sharti la vyama viwili vinavyounda SUK, ni lazima iwe kwa chama kilichoshinda na chama kilichopata ushindi wa pili, kwa sharti la kupata angalau asilimia 10 ya kura zote zilizopigwa na angalau kiwe kimepata viti 5 kwenye Baraza la wawakilishi.

Kwa mujibu ya matokeo yaliyokuwa yamebandikwa vituoni kwenye majimbo yote 54 ya Unguja na Pemba kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 25/10/2015, hivyo vyama vingine vyote vya upinzani zaidi ya 10 vilivosimamisha wagombea Urais na wajumbe wa Baraza la uwakilishi, wagombea wote wa Urais kwa ujumla wao waliambulia kura chini ya asilimia moja!

Kwa upande wa Baraza la Uwakilishi hakuna chama chochote kati ya hivyo zaidi ya 10 vinavyojiita vyama vya upinzani kilichoambulia angalau kiti kimoja kwenye Baraza la Uwakilishi!

Kwa kuwa hali ya kisiasa ya Zanzibar inajulikana ni ya vyama viwili vikuu vya CCM na CUF pekee, ambavyo ndivyo vinavyoweza kupata zaidi ya asilimia 10 ya kura za Urais na ndivyo pekee vinavyoweza kupata wajumbe kwenye Baraza la Uwakilishi.

Hiyo tafsiri yake ni kuwa hata kama hao CCM watalazimisha huo uchaguzi wao,hata hivyo baada ya kumalizika uchaguzi huo na matokeo yatakapotoka, mkwamo wa kisiasa utakuwa umesalia vile vile na tena ndiyo utakuwa umeongezeka maradufu.
 
Wapi imeandikwa event ya mabalozi ifanyike Ikulu hata kama ni waziri ameandaa!

Serikali inabana matumizi wakati serikali nzima imesafiri kwa gharama za umma kwenda shughuli za vikundi binafsi! ebo!

Ulinzi, magari, madereva, wasaidizi n.k. unadhani vinatolewa na CCM

Red: Wapi imeandikwa event ikifanyika kwenye eneo la Ikulu ni lazima rais ahudhurie! Na una rahisi anaweza ku-delegate Waziri wake wa mambo ya kigeni akamuakilisha kwenye event kama hiyo ya mabalozi?


Green: Serikali nzima maana yake nini? Serikali nzima ina watu wangapi?

Blue: Mbona viongozi wa kitaifa wakiwemo wastaafu na waliojuzulu kwa kashfa bado wanapewa usafiri na ulinzi hata wakiwa kwenye harambee za kusaidia makanisa? Defination yako ya kubana matumizi inahitaji kupitiwa upya!
 
Watanzania wana shauku kujiridhisha kama CCM walishinda. Na kama walishinda watashinda tena.

Watanzania wa wapi hao wanaotaka kujiridhisha na ushindi wa CCM? Huku kwetu mambo ni shwari hatuwezi kutaka kujiridhisha pasipokuwa na makosa. Mambo yaliyofanyika Zanzibar kipindi cha uchaguzi ndio yanaipa nguvu Tume na yanawapa watu nguvu kuwataka CUF kuthibitisha ushindi wao.
 
Watanzania wa wapi hao wanaotaka kujiridhisha na ushindi wa CCM? Huku kwetu mambo ni shwari hatuwezi kutaka kujiridhisha pasipokuwa na makosa. Mambo yaliyofanyika Zanzibar kipindi cha uchaguzi ndio yanaipa nguvu Tume na yanawapa watu nguvu kuwataka CUF kuthibitisha ushindi wao.
Kwanza tambua Tume haina mamlaka ya kufuta uchaguzi uliokamilika. Kama unamaanisha "nguvu" kwa maana ya JWTZ na Polisi hilo ndio lililotokea kutumia nguvu kuvuruga uchaguzi wa Zanzibar.

Kwenu CCM?

Link CHADEMA yawasilisha barua NEC kupinga matokeo ya kura za Uchaguzi Mkuu 2015 - wavuti

Link Lowassa awasilisha malalamiko yake Tume ya Uchaguzi
 
The Boss , Nonda Tulisema watakwama kutokana na kutokuwa na sababu za mashiko
Balozi na mwanadiplomasia Cisco anasema 'Sherry Party' ni utaratibu uliopo hasa kwa commonwealth
Ni muda Rais anakutana na mabalozi kueleza sera za nje

Kasema katika hafla hiyo kuna Mchapalo na hapo kuna maongezi mawili matatu

Msemaji wa Ikulu anasema Rais alikuwa nje ya Dar es Salaam

Yaani anataka tuamini hafala hiyo ni dharura na haikuwa imepangwa

Lakini pia anatueleza kuwa Rais wetu hana mshika Kalenda

Kwamba Rais hajui nini kitatokea kesho au keshokutwa kiasi kwamba hakujua kuna hafla na mabalozi. Rais hana diary!

Hii ni aibu sana na tukisema serikali Inafeli baadhi yetu wanakereka! KUFELI ndiko huku
Wala hili si jipya, wengine tuliliona mapema sana! Felia ipo wazi haihitaji ramli

Hawana sababu na wanajua wamechemka.

Hoja inayomkimbiza Rais ni baada ya tamko la kuwazuia mabalozi wasifanye shughuli na hofu ya suala la ZNZ

Pia wenye hoja nyingine zinazidi kupata nguvu kwa utetez huu! pengine communication skills etc

Halafu wapo waliokamata mapambio wakiimba #Hapakazi , fikirieni tena hii felia kisha mjiulize kuna kuna kazi wakati watu hawaonekani kazini? Wanakimbia !

Nyani Ngabu
 
.. Tulisema watakwama kutokana na kutokuwa na sababu za mashiko
Balozi na mwanadiplomasia Cisco anasema 'Sherry Party' ni utaratibu uliopo hasa kwa commonwealth
Ni muda Rais anakutana na mabalozi kueleza sera za nje

Pia wenye hoja nyingine zinazidi kupata nguvu kwa utetez huu! pengine communication skills etc

Halafu wapo waliokamata mapambio wakiimba #Hapakazi , fikirieni tena hii felia kisha mjiulize kuna kuna kazi wakati watu hawaonekani kazini? Wanakimbia !
Kama communication skills ni tatizo, amtafute huyu atamsaidia.

 
The Boss hii jambo ni zito, watetezi wa #Hapakazi wakiwemo ''46 wanaofikiriwa'', nawaona wanyoonge! Sura zimeswajika, wamekumbwa na mfadhaiko, simanzi tele huku wakiwa wametunduwaa

Wanajiuliza waanzie wapi kutetea hili.
Nafikiri Abdul Mtiro kaliongelea vizuri hili
ni mara ya kwanza Rais anaaalika watu ikulu na yeye haupo
kashangaa sana....kiukweli ni big blunder ...
 
Pia wenye hoja nyingine zinazidi kupata nguvu kwa utetez huu! pengine communication skills etc

Hilo la uwezo wa mawasiliano ni dhahiri shahiri kabisa.

Hayuko vizuri kwenye hilo eneo.

Hata akiongea Kiswahili ni rahisi sana kubaini kwamba mawasiliano si eneo analolimudu vizuri.

Sasa ukiongeza na ile lugha ya kigeni ndo kabisaaa inakuwa karibu majanga.

Ila kweli kualika watu nyumbani kwako halafu mwenyeji unaenda AWOL haijakaa vizuri.
 
Magufuli ni janga la taifa. Ni mnafiki wa kutupwa. Ila hili za Zanzibar safari hii weanalo. Yaani kuanzia sasa wajianda kwenda kwa mtindo wa kusigina katiba na sheria hadi kieleweke. Sioni ni kwa namna gani watakavyo-justify hayo madhila waliyoyaanzisha. Lazima itafika mahali watajuta kumtuma Jecha kufuta matokeo yote ya uchaguzi Zanzibar.
 
Magufuli ni janga la taifa. Ni mnafiki wa kutupwa. Ila hili za Zanzibar safari hii weanalo. Yaani kuanzia sasa wajianda kwenda kwa mtindo wa kusigina katiba na sheria hadi kieleweke. Sioni ni kwa namna gani watakavyo-justify hayo madhila waliyoyaanzisha. Lazima itafika mahali watajuta kumtuma Jecha kufuta matokeo yote ya uchaguzi Zanzibar.
Mimi naona Magu anataka kupakaa rangi nyekundu mikononi mwake kama alivyofanya Mkapa. Magu ikumbuke kauli yako, Mungu hapendi wanafiki, kumbuka usiposema ukweli na kutenda haki utakuwa ni mnafiki. Ee Mungu Muepushe hii kiumbe yako na unafiki, mtie nguvu atende haki na akutangulize Wewe Mungu,muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake mbele.
Magu tunakuombea, usituangushe sisi wadanganyika ambao tunaiogopa CCM kama ukoma.
 
Magufuli ni janga la taifa. Ni mnafiki wa kutupwa. Ila hili za Zanzibar safari hii weanalo. Yaani kuanzia sasa wajianda kwenda kwa mtindo wa kusigina katiba na sheria hadi kieleweke. Sioni ni kwa namna gani watakavyo-justify hayo madhila waliyoyaanzisha. Lazima itafika mahali watajuta kumtuma Jecha kufuta matokeo yote ya uchaguzi Zanzibar.
Janga la taifa ni wewe sio Magu
 
Nimeamini kweli kila chenye mwanzo kina mwisho.

Utawala huu wa CCM tokea mwaka 1992 iliutangazia Ulimwengu kuwa inaendesha mfumo wa vyama vingi.

Dunia ikaamini kuwa Tanzania inaendesha mfumo wa vyama vingi.

Lakini kilichotokea Oktoba 28 mwaka jana kwa mtu anayeitwa Jecha kujitokeza kwenye ZBC na kusoma taarifa ya kuufuta uchaguzi uliokuwa umekamilika na matokeo yake kubandikwa kwenye kuta za vituo vya upigaji kura kwenye majimbo yote 54 ya Unguja na Pemba.

Kitendo hicho cha Jecha kuufuta uchaguzi huo wa Zanzibar, baada ya 'kuamrishwa' na watawala wa CCM ndiyo kimeuthibitishia Ulimwengu kuwa kumbe Tanzania bado ipo kwenye mfumo wa Chama kimoja.

Kwa kuwa hakuna uwezekano hata kidogo inapotokea chama kingine zaidi ya CCM kinaposhinda uchaguzi hapa nchini, kwa ZEC au NEC yenye ubavu wa kumtangaza mgombea wa upinzani kwa nafasi ya Urais kuwa ameshinda Urais.

Badala ya nchi yetu kuendelea na unafiki huu wa kupindukia wa kufanya 'maigizo' ya kujifanya kuwa ipo kwenye mfumo wa vyama vingi, wakati in reality bado tupo kwenye mfumo wa Chama kimoja, ni vyema sasa Bunge letu likapelekewa muswada ya kuwa nchi yetu imerejea rasmi kwenye mfumo wa chama kimoja.

Kwa kuwa ni dhambi kubwa inayofanywa na watawala wetu kwa kuwapanga mamilioni ya wananchi wake kwenye foleni wanazokaa masaa kadhaa, wananchi hao wakiamini kuwa kura zao kwenye sanduku la kura ndizo zinazomchagua Rais wa nchi hii, wakati kwenye vikao vyao vya 'siri' watawala wetu walishaamua kuwa Tanzania hii hadi itakapofika mwisho wa dunia haitakuja kutokea kamwe mpinzani aingie Ikulu!
 
Ikitokea Magufuli akafuata ushauri 'mbovu' wa Mwanasheria wake mkuu Masaju na Mwenyekiti wa NEC Jaji Lubuva kuwa yeye hapaswi kuingilia mambo ya Zanzibar yanayohusiana na kufutwa kwa uchaguzi kulikofanywa na Jecha Salim Jecha.

Lakini wakati huo huo akafuata ushauri wa 'kipuuzi' wa wanasheria hao wawili waliobobea kuwa Magufuli atapaswa kuingilia Zanzibar na akaamua kuutumia Uamiri Jeshi wake mkuu na kuamua kupeleka vifaru vya kijeshi viwaponde ponde wazanzibari watakaokuwa wamejitokeza mitaani kupinga udhalimu wa watawala wa CCM, walioamua kuibaka demokrasia kwa kuyakataa maamuzi yao waliyoyafanya kupitia sanduku la kura hapo Oktoba 25 mwaka jana.

Ikitokea hivyo itafanya hata ile 'allergy' yake Mkulu ya kutopanda ndege kwenda nje ya nchi itatoweka ghafla na atapandishwa kwenye ndege chapuchapu na atapelekwa The Hague Uholanzi ambako Bensouda swali lake la kwanza atamuuliza imekuwaje Mheshimiwa Mkuu uingilie masuala ya Zenji ambayo washauri wako na wewe mwenyewe ulibainisha kuwa hupaswi kuyaingilia?!
 
....Katika hotuba hiyo, Rais Magufuli amewaeleza mabalozi hao kuwa licha ya Tanzania kuwa nchi moja, Zanzibar ina mfumo wake wa siasa, ina serikali yake, Katiba yake na pia tume yake ya uchaguzi inayojitegemea.
Amesema tume hiyo ilifuta uchaguzi kutokana na mapungufu yaliyojitokeza kisiwani Pemba, na kwamba tayari tarehe mpya ya uchaguzi wa marudio imekwisha tangazwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar.
Amesema mazungumzo ya kutatua mgogoro huo yalifanyika bila mafanikio ambapo chama kikuu cha upinzani (CUF) kimeendelea kupinga uchaguzi wa marudio huku vyama vingine kikiwemo chama tawala vikionesha uhitaji wa uchaguzi huo wa marudio.

Amesema kwa hali ilivyo, busara inahitajika ili kunusuru suala hilo, na kwamba kususia uchaguzi siyo suluhu bali kutumia nafasi iliyopo sasa kujadili namna ya kuufanya uchaguzi wa marudio kuwa huru na wa haki. ......
“Tunakiasa chama cha CUF kama ambavyo watanzania wengi wangependa kuona, kuthibitisha madai ya ushindi wao katika sanduku la kura, hakuna jinsi nyingine ya kutatua suala hili zaidi ya kukubali kufanya uchaguzi wa marudio” imesema sehemu ya hotuba hiyo.
.
Bado Rais Magufuli hajatolea maelezo changamoto aliyopewa. Kuelezea kwa ushahidi kasoro za uchaguzi wa Zanzibar. Badala yake ameibuka na kauli ya "uhitaji(mahitaji ya CCM) wa uchaguzi wa marudio. CCM inapoangukia pua upo uhitaji wa kubaka demokrasia na uhitaji wa kurudia uchaguzi ili CCM ichakachue matokeo katika uchaguzi wa marudio ambao ni kinyume na katiba.

“Tunamtaka Rais Magufuli kuonyesha uongozi wake kupitia mgogoro huu wa kisiasa kwa kuingilia kati na kutafuta usuluhishi baina ya vyama vikuu kuhakikisha amani pande zote," ilisema sehemu ya tamko hilo.
Tamko hilo pia lilieleza kuwa hakuna ushahidi wa moja kwa moja kuwa uchaguzi wa Oktoba 25, mwaka jana, ulikuwa na kasoro zilizoelezwa na kwamba waangalizi wa kutoka Jumuiya ya Madola, Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Afrika Mashariki, EU, Marekani na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) waliridhika na mwenendo wa uchaguzi huo.

Link Ulaya wamgomea Magufuli

Uchaguzi wa marudio ni kukiuka katiba, huwezi kufuta uchaguzi na matokeo yake wakati Tayari kuna wawakilishi na madiwani wateule. Wote walishapewa vyeti vya ushindi. Kiashiria na uthibitisho kuwa uchaguzi ulishakamilika.
Link Uchaguzi Zanzibar: Hongera Rais Magufuli kwa msimamo sahihi
Link2. Uchaguzi Zanzibar: Hongera Rais Magufuli kwa msimamo sahihi
Link3. Uchaguzi Zanzibar: Hongera Rais Magufuli kwa msimamo sahihi

Baada ya NEC/ZEC kutangaza matokeo ya uchaguzi ni mahakama pekee inayoweza kuyatengua/kuyafuta. Jecha hakuwa na hana mamlaka ya kufuta uchaguzi uliokamilika au kufuta matokeo ya uchaguzi baada ya kutangazwa na msimamizi wa jimbo.

CCM iache unafiki. Rais Magufuli aache kudanganya umma wa watanzania.
Magu ujitafakari na kujitathmini kama kweli unamtanguliza Mungu mbele na kama unasema ukweli na kusimamia haki ya kila mtanzania. Mungu hapendi wanafiki.
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
 
Ila kwakuwa wazanzibar ni wanafiki acha wapashwe moto kidogo ndo watakuwa wamoja.
wanakaa kwao wanapanga yao baadae anatokea NYANI mmoja anaanza kujikomba anawageuka wenzake,acha dhambi iwatafune
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom