Rais Magufuli na yoote mazuri ila hapa sijakuelewa

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,785

Bado natafakari na nashindwa kupata majibu ya ujenzi wa daraja kwa mujibu wa Hotuba yako ya jana litakalo pita baharini likitokea Coco beach mpka Hospitali ya Aga Khan, najaribu kukokotoa mahesabu yanakataa kabisa, na mimi sijisifu lkn niko vizuri kiasi fulani na namba lkn kwa hili bado nashindwa kupata jibu embu ngoja nililalie labda kesho asubuhi nitapata jawabu lkn mpaka sasa hivi nimeshindwa!

Hili daraja ni la nini?
Mambo ambayo nimekuwa najiuliza wakazi wote wa Masaki na Oysterbay ni wachache sana lakini na zaidi ya hapo Masaki na O'bay kunagota yaani hakuendelei hivyo ina maana ni br. itakayaotumiwa na watu wale wale tu kila siku na isitoshe wakazi wa hayo maeneo ni kati ya watu ambao foleni kwao siyo tatizo kubwa kama wengine leo hii kama wanaingia kazini saa moja na nusu wanaondoka saa moja kamili dakika 15-20 wako mjini na kurudi karibia hivyo hivyo sasa mahesabu yangu hayanipi kabisa kama nilivyosema ngoja niliache mpaka kesho asubuhi labda nitapata jawabu!
 
Njoo tena,sijui kama wengi watakuelewa ulichoandika..Inawezekana una ujumbe mzuri wa kueleza
 
Huwa mara kadhaa napenda unavyofanya reasoning without being clouded or gurded na ushabiki.
Katika hili nakuunga mkono, ingawa ulitaka kujarubu kum block kwa kumjibu Msulibasi katika thrwad aliyoianzisha, ukaamua kumjibu kwa kumpinga katika mengine na ukaona anahoja katika hili na umeamua kukubakiana naye kwa kulufungulia uzi kabisa.
 
Lile daraja likijengwa litapunguza foleni ya pale salenda maana magari ya Masaki, Oyesterbay hayatalazimika kupita salenda bbadala yake yataunga moja kwa moja kutoka coco beach na kutokea Agakhan na hivyo kupunguza msongamano wa magari yanayopita barabara ya Ali Hassan Mwinyi kwenda mjini.
 
Na lenyewe watakuwa wanalipia?maana la kigamboni tutalipia kuvuka na magari.
 
Kwa Waliowahi|Wanaopita Hiyo Njia Utakubaliana Na Mleta Mada Bila Ushabiki Maana Haina Hitaji La Kujenga Njia Ya Gharama Kubwa Hivyo
 
Lile daraja likijengwa litapunguza foleni ya pale salenda maana magari ya Masaki, Oyesterbay hayatalazimika kupita salenda bbadala yake yataunga moja kwa moja kutoka coco beach na kutokea Agakhan na hivyo kupunguza msongamano wa magari yanayopita barabara ya Ali Hassan Mwinyi kwenda mjini.
Kama nimemuelewa mleta mada yeye anataka kujua economuc impact yake hilo daraja. Ndiyo maana ameingelea population ya wakaaji wa masaki na oysterbay ukilinganisha na maeneo mengine ya jiji ambayo yana population ya kufa mtu.
Ferries zingetosha sana kuhudumia wakaazi wa oyesterbay/masaki wajao mjini.
Maana hiyo barabara haitakuwa na kuchepuka, ni moja kwa moja and so is ferry. Hiyo pesa ingekua relocated maeneo mengine .
 
Mimi nashangaa rais wangu JPM ameelekeza nguvu zote Dar ambako hawakumpa kura wakati sehemu zingine za nchi hajui kuwa barabara zote zimekatika mvua zimezidi, watoto sio tu kukaa chini hata darasa hawana. Yeye na Dar sana sana alienda Arusha ambako pia hawakumpa kura. Anyway ndio kwanza ana siku 100 ngoja tusubiri
 
Lile daraja likijengwa litapunguza foleni ya pale salenda maana magari ya Masaki, Oyesterbay hayatalazimika kupita salenda bbadala yake yataunga moja kwa moja kutoka coco beach na kutokea Agakhan na hivyo kupunguza msongamano wa magari yanayopita barabara ya Ali Hassan Mwinyi kwenda mjini.
Kwahiyo foleni inahama toka Salender kuja Agakhan?
 
Kwa Waliowahi|Wanaopita Hiyo Njia Utakubaliana Na Mleta Mada Bila Ushabiki Maana Haina Hitaji La Kujenga Njia Ya Gharama Kubwa Hivyo

Miaka sita mbele ndio mtajua umuhimu wa hilo daraja mji unakuwa huo surrender inasababisha mji aufunguki. .
 

Bado natafakari na nashindwa kupata majibu ya ujenzi wa daraja kwa mujibu wa Hotuba yako ya jana litakalo pita baharini likitokea Coco beach mpka Hospitali ya Aga Khan, najaribu kukokotoa mahesabu yanakataa kabisa, na mimi sijisifu lkn niko vizuri kiasi fulani na namba lkn kwa hili bado nashindwa kupata jibu embu ngoja nililalie labda kesho asubuhi nitapata jawabu lkn mpaka sasa hivi nimeshindwa!

Hili daraja ni la nini?
Mambo ambayo nimekuwa najiuliza wakazi wote wa Masaki na Oysterbay ni wachache sana lakini na zaidi ya hapo Masaki na O'bay kunagota yaani hakuendelei hivyo ina maana ni br. itakayaotumiwa na watu wale wale tu kila siku na isitoshe wakazi wa hayo maeneo ni kati ya watu ambao foleni kwao siyo tatizo kubwa kama wengine leo hii kama wanaingia kazini saa moja na nusu wanaondoka saa moja kamili dakika 15-20 wako mjini na kurudi karibia hivyo hivyo sasa mahesabu yangu hayanipi kabisa kama nilivyosema ngoja niliache mpaka kesho asubuhi labda nitapata jawabu!
wewe si ndio unashinda humu kwa kumsifia leo imekuaje?
 
Yaonekana huendagi posta asubuhi kupitia alhassan mwinyi road,salender bridge ni padogo kuhimili magari yanayotokea kinondoni, alh.mwinyi road yenyewe na hii ya baharini kutoka Coco sijui inaitwaje,
So likijengwa daraja kutoka Coco to agakhan linapunguza huo wingi wa magari salender bridge
 
Back
Top Bottom