Rais Magufuli, Fumua Bodi na Mamlaka za Utalii

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,240
4,466
Huwa naumia sana, majirani wasemapo:
Mlima Kilimanjaro upo kwao.
Sasa Olduvai Gorge ipo kwao pia.
Na hata Diamond Platinum ati anatoka kwao.
Bado kidogo tu watasema Magufuli mtu wao.

Huwa najiuliza, wale wazee wa mamlaka za utalii, wanafanya nini kuutangaza utalii wetu? Wamewajaza watu waliokula siku zao wakashiba, wengine wakiwa mabalozi, na sasa hawana hata motivation.

Wawekeni vijana wabunifu, style za akina Nehemiah Mchechu; wasaidie kuongeza pato la Taifa kupitia utalii.

Nani atuamshe kwenye huu usingizi mzito?!!!!
 
Maadam JPM yuko Arusha na Uhuru kwenye mkutano wa EAC, amweleze live kuwa hako kamchezo kanakofanywa na ndugu zetu Wakenya si kazuri. Amweleze kuwa wawe wazi, wasijifanye vivutio vyetu viko kwao. Amwambie kuwa tabia hiyo ni wizi na wakiendelea atawatumbua.
 
Maadam JPM yuko Arusha na Uhuru kwenye mkutano wa EAC, amweleze live kuwa hako kamchezo kanakofanywa na ndugu zetu Wakenya si kazuri. Amweleze kuwa wawe wazi, wasijifanye vivutio vyetu viko kwao. Amwambie kuwa tabia hiyo ni wizi na wakiendelea atawatumbua.
Ukiwambia hivyo matasema Magufuli ni ndogo wake Odinga
 
Inawauma kuanzia lini mbona vivutio vingi tu vinajulikana viko kenya, na bado hadi mikumi tutasema iko kenya
 
Hata Nyerere wanasema alikuwa ni wao sie wanatupa eti Mwai kibaki ndo Alikuwa rais wetu,,

Hawa watani zenu wanajifanya kama wanatania kumbe wanafanya kweli tupu.
 
Huyo Nehemia msechu anaufahamu utalii? haya ndio yale ya Juma Nature kuwa balozi wa okoa tembo wakati hamjui hata tembo mwenyewe kuna watu wanafanya katika tasinia ya utalii wapewe nafasi wa weke wazi kila kitu,Hawa wafunga milegezo mkae nao
 
Back
Top Bottom