Rais Kikwete: Watanzania wanataka adhabu ya kifo iendelee

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,079
Kikwete%201.jpg

Rais Jakaya Kikwete.



Rais Jakaya Kikwete amesema kwamba idadi kubwa ya Watanzania wanapinga kufutwa kwa adhabu ya kifo na wanataka iendelee kuwapo katika vitabu vya sheria.
“Hili ni jambo lililoulizwa na Kamati ya Jaji Nyalali. Watu walikataa kufutwa kwa adhabu ya kifo. Tanzania kwa muda mrefu haijapata kunyonga mtu hata kama Sheria ya Kunyonga imeendelea kuwapo katika vitabu vyetu,” alisema na kuongeza:
“Majuzi nilibatilisha kiasi cha hukumu 75 za vifo kuwa vifungo vya maisha. Lakini bado waliohukumiwa kifo kwenye magereza yetu ni wengi, pengine kufikia watu 200, hata kama sijahesabu.”
Rais Kikwete alitoa msimamo huo Jumanne wiki hii, wakati wa chakula cha usiku katika makao makuu ya Jumuiya ya Kilei ya Kanisa Katoliki Duniani ya Mtakatifu Eggidio, jijini Rome, Italia.
Sheria ya adhabu ya kifo inapingwa na jumuiya ya kimataifa pamoja na Jumuiya ya Eggidio.
Katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete pia alisema kuwa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini, siyo tu ni mauaji ya kusikitisha bali ni mauaji ya kijinga kabisa kutokea katika dunia ya leo ya sayansi na teknolojia.
Rais Kikwete alisema kuwa katika moja ya mambo yaliyoiabisha zaidi taifa la Tanzania katika muda mfupi ni mauaji na “kijinga” ya albino.
“Kwamba watu wanaweza kuwa wajinga kuamini kuwa ukipata kidole cha albino utatajirika ni jambo gumu sana kuamini katika dunia ya leo ya sayansi na teknolojia.
“Lakini napenda kuwahakikishieni kuwa sasa Serikali imeyadhibiti mauaji haya,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:
“Tuliendesha kura ya maoni. Watu wengi wametiwa mbaroni na wengine wako mahakamani. Kati yao wengine wamehukumiwa kunyongwa.”
Aidha, Rais Kikwete alirejea onyo lake kuwa vyombo vya habari kuwa haviwezi kutumia uhuru wake kwa madhumuni ya kuvuruga amani na kuvunja umoja wa kitaifa, na bado vikaachiwa kuwa huru kuendelea na shughuli zake bila kuchukuliwa hatua.
Hata hivyo, Rais Kikwete alisema kwa vyombo vya habari vyenyewe lazima vijirekebishe na kuwa na wajibu ambao ni sehemu muhimu ya uhuru huo wa habari
“Kama nilivyowaambia pale Musoma majuzi wakati wa kuadhimisha miaka 10 ya kifo cha Mwalimu Nyerere, huu hauwezi kuwa uhuru wa kuvunja taifa, uhuru wa kugawa watu, uhuru wa kuchochea maasi na magomvi kati ya dini mbalimbali, kati ya makabila, kati ya watu wenye rangi mbali mbali,” alikumbusha.
Alisema kuwa: “Baadhi ya vyombo vyetu havina wajibu kabisa. Vinachochea maasi ya kuvunja nchi na kuleta mfarakano kati ya watu wetu. Vinajaribu kugawa watu wetu, kugawa mataifa yetu na kusababisha maafa makubwa. Hatuwezi kuvumilia vyombo vya habari vya namna hiyo vinavyotumia uhuru kuleta balaa kwa watu.”
Viongozi wa Mtakatifu Eggidio walimwambia Rais Kikwete kuwa wanaipenda Tanzania kwa sababu ni mfano wa jinsi watu wanavyoishi kwa amani duniani bila kusukumwa kuvunja nchi na sababu za kikabila, kidini ama hata rangi.
Rais Kikwete na viongozi hao wa Jumuiya ya Mtakatifu Eggidio pia walijadili migogoro inayoendelea katika Afrika. Jumuiya hiyo ilishiriki katika majadiliano ya kuleta amani katika nchi za Burundi na Msumbiji.
Ujumbe huo wa Mtakatifu Eggidio uliongozwa na mwanzilishi wa Jumuiya hiyo, Profesa wa Historia katika Chuo Kikuu cha Rome, Andrea Riccardi, na msaidizi wake wa kiroho, Padre Matteo Zuppi.
Ujumbe wa Tanzania kwenye mazungumzo hayo uliwajumuisha Waziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula, Steven Wassira na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Seif Iddi.
Rais Kikwete ambaye alikuwa Italia kuhudhuria Mkutano wa wakuu wa nchi na serikali kujadili Usalama wa Chakula Duniani, alirejea nchini jana.



CHANZO: NIPASHE
 
Ila nabiidi niulize swali moja. Na nadhani hili ni tatizo kubwa nchini kwetu, kusema vitu bila supporting evidence. Ni Watanzania wapi waliosema wanataka adhabu ya kifo iendelee? Wali survey watu? Ni Watanzania wangapi walisema kuwa wana taka adhabu ya kifo iendelee? Siyo data zozote raisi anazo toa zinazo onyesha kuwa Watanzania idadi hii wameulizwa na asilimia hii wamesema wana taka adhabu ya kifo iendelee. Sisemi kuwa ni uongo lakini ikibidi can he back up that statement with proof?
 
Ila nabiidi niulize swali moja. Na nadhani hili ni tatizo kubwa nchini kwetu, kusema vitu bila supporting evidence. Ni Watanzania wapi waliosema wanataka adhabu ya kifo iendelee? Wali survey watu? Ni Watanzania wangapi walisema kuwa wana taka adhabu ya kifo iendelee? Siyo data zozote raisi anazo toa zinazo onyesha kuwa Watanzania idadi hii wameulizwa na asilimia hii wamesema wana taka adhabu ya kifo iendelee. Sisemi kuwa ni uongo lakini ikibidi can he back up that statement with proof?
Huyo nadhani atakuwa katoa maoni yake, na si ya waTZ wote
 
Huyo nadhani atakuwa katoa maoni yake, na si ya waTZ wote

Ndicho ninacho hisi hata mimi mkuu. Ata semaje Watanzania wanataka adhabu ya kifo iendelee bila kutoa data za kuthibitisha hilo?Kama huu ndiyo mtindo wa serikali yetu basi nina mashaka sasa kwamba mambo mengi tunaambiwa tu kutokana na maoni ya viongozi na siyo facts. Lakini kama ana toa maoni yake mwenyewe na kutumia "Watanzania" tuna weza kusema huko ni kujaribu kudanganya umma.
 
tatizo kubwa ni kuwa msimamo wa kiongozi huyu wa nchi katika masuala makubwa hataki kuuweka hadharani, anaogopa sana kuwaudhi baadhi ya watu
 
Ila nabiidi niulize swali moja. Na nadhani hili ni tatizo kubwa nchini kwetu, kusema vitu bila supporting evidence. Ni Watanzania wapi waliosema wanataka adhabu ya kifo iendelee? Wali survey watu? Ni Watanzania wangapi walisema kuwa wana taka adhabu ya kifo iendelee? Siyo data zozote raisi anazo toa zinazo onyesha kuwa Watanzania idadi hii wameulizwa na asilimia hii wamesema wana taka adhabu ya kifo iendelee. Sisemi kuwa ni uongo lakini ikibidi can he back up that statement with proof?


Mimi nafikiri kikwete ana haki ya kusema hivyo,pamoja na kutotoa takwimu lakini watanzania wengi wanataka adhabu ya kifo iendelee,na mimi pia ni mmojawao. kila kitu data data!!!! mambo mengine ni yanajidhihirisha yenyewe.
 
Ila nabiidi niulize swali moja. Na nadhani hili ni tatizo kubwa nchini kwetu, kusema vitu bila supporting evidence. Ni Watanzania wapi waliosema wanataka adhabu ya kifo iendelee? Wali survey watu? Ni Watanzania wangapi walisema kuwa wana taka adhabu ya kifo iendelee? Siyo data zozote raisi anazo toa zinazo onyesha kuwa Watanzania idadi hii wameulizwa na asilimia hii wamesema wana taka adhabu ya kifo iendelee. Sisemi kuwa ni uongo lakini ikibidi can he back up that statement with proof?



mkuu ilikujiridhisha na aliyosema mh.Rais wetu ni vyema ukapata ripoti ya jaji nyalali maana hata yeye amezungumza hivyo basing on that ripoti.

it's not good to negative in everything.bravo JK
 
Ndicho ninacho hisi hata mimi mkuu. Ata semaje Watanzania wanataka adhabu ya kifo iendelee bila kutoa data za kuthibitisha hilo?Kama huu ndiyo mtindo wa serikali yetu basi nina mashaka sasa kwamba mambo mengi tunaambiwa tu kutokana na maoni ya viongozi na siyo facts. Lakini kama ana toa maoni yake mwenyewe na kutumia "Watanzania" tuna weza kusema huko ni kujaribu kudanganya umma.

Mkuu unajua tume ya jaji Nyalali? Huyo unayetaka kumuonesha kuwa ni mjinga kiasi cha kuongea sentesi kali kama hiyo ni Rais aliyechaguliwa na watanzania wengi tu, next time unapotaka kumtukana jaribu ku keep hiyo in mind.
 
mkuu ilikujiridhisha na aliyosema mh.Rais wetu ni vyema ukapata ripoti ya jaji nyalali maana hata yeye amezungumza hivyo basing on that ripoti.

it's not good to negative in everything.bravo JK

Nafikiri kuna kajitabia ka watu kujisahau wanapokuwa nyuma ya monitor zao kuanza kutukana bila sababu za msingi, sitegemei huyu bwana hafanyi hivi kwa makusudi. Huyu ni mfano tu watu wachache wanaodhani ili waonekane ni lazima wa mtusi JK.
 
Ila nabiidi niulize swali moja. Na nadhani hili ni tatizo kubwa nchini kwetu, kusema vitu bila supporting evidence. Ni Watanzania wapi waliosema wanataka adhabu ya kifo iendelee? Wali survey watu? Ni Watanzania wangapi walisema kuwa wana taka adhabu ya kifo iendelee? Siyo data zozote raisi anazo toa zinazo onyesha kuwa Watanzania idadi hii wameulizwa na asilimia hii wamesema wana taka adhabu ya kifo iendelee. Sisemi kuwa ni uongo lakini ikibidi can he back up that statement with proof?

MwanaFalsafa:

Jamaa si amenukuu kutoka kwa tume ya jaji Nyalali? Sasa unataka supporting evidence gani? Matokeo ya tume ni reference inayokubalika.
 
Mkuu unajua tume ya jaji Nyalali? Huyo unayetaka kumuonesha kuwa ni mjinga kiasi cha kuongea sentesi kali kama hiyo ni Rais aliyechaguliwa na watanzania wengi tu, next time unapotaka kumtukana jaribu ku keep hiyo in mind.

Onyesha wapi nimemtukana.
 
MwanaFalsafa:

Jamaa si amenukuu kutoka kwa tume ya jaji Nyalali? Sasa unataka supporting evidence gani? Matokeo ya tume ni reference inayokubalika.

Sikatai mkuu. Kareference tume ya jaji Nyalali so I assume kaisoma right? Sasa kama alisoma alitakiwa aseme tume ilihoji idadi hii ya watu na asilimia hii wakasema hivi. Hiyo itaonyesha kweli ni wantanzania wana taka adhabu iendelee. Sasa kumquote mtu bila kutaja ushahidi wa huyo mtu kama vile una assume kila mtu kaisoma haimake sense.
 
Nafikiri kuna kajitabia ka watu kujisahau wanapokuwa nyuma ya monitor zao kuanza kutukana bila sababu za msingi, sitegemei huyu bwana hafanyi hivi kwa makusudi. Huyu ni mfano tu watu wachache wanaodhani ili waonekane ni lazima wa mtusi JK.

Nadhani haujui maana ya maneno matusi. Pole kama ime kutouch sana. Don't take it too personally.
 
Sikatai mkuu. Kareference tume ya jaji Nyalali so I assume kaisoma right? Sasa kama alisoma alitakiwa aseme tume ilihoji idadi hii ya watu na asilimia hii wakasema hivi. Hiyo itaonyesha kweli ni wantanzania wana taka adhabu iendelee. Sasa kumquote mtu bila kutaja ushahidi wa huyo mtu kama vile una assume kila mtu kaisoma haimake sense.

Mkuu:

Matokeo ya tume ya Nyalali si ni sehemu ya public domain? Kama ni public domain basi assumption kuwa kila mtu kaisoma ni valid.
 
Adhabu ya kifo ni alama ya primitive societies, Tanzania as a society bado tyuko primitive na huenda tunahitaji hii adhabu ya kifo iwepo, lakini rais kusema Watanzania wamesema hivyo bila kuback up na data wala kuogopa kunaonyesha ni jinsi gani society yetu ilivyo primitive na labda ku justify capital punishment in a circular way.

But it is wrong to pull things out of thin air, or without sufficient citation, Mr. President. Au ndiyo mambo ya degree za student government DARUSO?
 
Mkuu:

Matokeo ya tume ya Nyalali si ni sehemu ya public domain? Kama ni public domain basi assumption kuwa kila mtu kaisoma ni valid.

I don't think so mkuu. JF ni public domain kwa hiyo nikienda kuongea na watu is it safe to assume kila mtu ame soma yanayo endelea humu? Na je wewe umesha isoma au kuiona?
 
Back
Top Bottom