SAGAI GALGANO
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 43,707
- 60,756
Mheshimiwa Rais Kikwete, imekuwa kawaida sasa kwa wanachama wa CCM kufanya vurugu kwenye chaguzi ndogo na hata kufanya mauaji. Hali hii haitokei kwa bahati mbaya kwani ni kawaida ya CCM kila kwenye chaguzi ndogo hizi kupeleka vijana kwenye makambi na kuwapa mafunzo ya kigaidi kwa baraka za uongozi wa juu wa chama ambacho wewe ni mwenyekiti wake.
Yalitokea Tarime, Biharamulo,Busanda,Igunga ambapo makada wawili wa Chadema waliuawa kikatili na vijana hawa wanaopewa mafunzo ya kuua watu.
Arumeru Mashariki wametekwa watu na kuteswa mpaka kuharibiwa sehemu za siri, Mwanza wabunge wawili wa Chadema wamecharangwa mapanga, katika matukio yote haya hatujasikia wahusika wakichuliwa hatua za kisheria kwa uhalifu huu, kibaya zaidi ni ukimya wako juu ya ugaidi unaofanywa na wanachama wako. Ukimya wako Mh. Rais ni kiashiria kuwa umebariki vitendo hivi vya kigaidi ili kulinda utawala wenu dhalimu.
Ushauri wangu kwako Mh. Rais uvifute vyama vyote ibaki CCM peke yake ili kuokoa maisha ya watu wasiokuwa nahatia. Ukishindwa kuvifuta vyama hivi na kuendelea kukalia kimya ugaidi huu ujue nchi itaingia kwenye umwagaji mkubwa wa damu kwa ajili ya uroho wenu wa kubaki madarakani, na damu za watanzania hawa zitakuwa juu ya kichwa chako.
Yalitokea Tarime, Biharamulo,Busanda,Igunga ambapo makada wawili wa Chadema waliuawa kikatili na vijana hawa wanaopewa mafunzo ya kuua watu.
Arumeru Mashariki wametekwa watu na kuteswa mpaka kuharibiwa sehemu za siri, Mwanza wabunge wawili wa Chadema wamecharangwa mapanga, katika matukio yote haya hatujasikia wahusika wakichuliwa hatua za kisheria kwa uhalifu huu, kibaya zaidi ni ukimya wako juu ya ugaidi unaofanywa na wanachama wako. Ukimya wako Mh. Rais ni kiashiria kuwa umebariki vitendo hivi vya kigaidi ili kulinda utawala wenu dhalimu.
Ushauri wangu kwako Mh. Rais uvifute vyama vyote ibaki CCM peke yake ili kuokoa maisha ya watu wasiokuwa nahatia. Ukishindwa kuvifuta vyama hivi na kuendelea kukalia kimya ugaidi huu ujue nchi itaingia kwenye umwagaji mkubwa wa damu kwa ajili ya uroho wenu wa kubaki madarakani, na damu za watanzania hawa zitakuwa juu ya kichwa chako.