Hii tabia ya rais kukaa kimya wakati wananchi wanahitaji kusikia tamko la mkuu wa nchi linanikanganya sana. Hivi kweli kwa ali ilivyo Tanzania, ili tatizo la umeme ni lakufumbia macho? Umeme umekuwa kero kwa wafanyabiashara, wananchi wa kawaida na ata kwa hao wanaoitwa investors. TRA wanashindwa kukusanya mapato kama ilivyotakiwa, wanafunzi wanashindwa kusoma, viwanda havizalishi alafu rais anaenda kutafuta wawekezaji. Naogopa sana muda si mrefu umeme utazimika Tanzania nzima. Mbona baba wa Taifa Hayati Mwl Julius Nyerere alikuwa anasema wazi kama ni kipindi cha mavuno au kujifunga mkanda? Rais Kikwete tukueleweje?