Rais Kikwete, toa tamko kuhusu mafuta: Tunaumia wananchi!

Kwanini watz tusiandamane kuisapoti ewura kusimamia msimamo wake wa kutoshusha bei??
 
Napata uchungu sana napoona serikali yetu ilivyo dhaifu, kiasi hata inashindwa kusimamia maagizo yake.

Serikali ilitoa agizo la kushushwa kwa bei ya mafuta. Tena agizo likasisitiza kuwa wafanyabishara wa mafuta watakaofunga vituo kwa kisingizio chochote watakiona.

Lakini wiki moja imekwisha bila agizo hilo kutekelezwa. Vituo vimefungwa na serikali badala ya kuchukua hatua eti inawaomba wamiliki wa vituo wapunguze bei.

Nimemsikia afisa mmoja wa EWURA akisema "tunatoa wito vituo vyote viuze mafuta." alitoa kauli hii baada ya kutembelea vituo tisa na kukuta ni vitatu tu vyenye kutoa huduma.

Hivi Serikali huwa inatoa wito au huwa inaagiza? Serikali inayoshindwa kutekeleza maagizo yake ni serikali ya hovyo sana.

Jamani, Serikali hii haina sababu ya kuendelea kuwepo.

Nafikiri ungeanzia hatua moja nyuma, yaani CCM inashindwa kusimamia maagizo inayotoa kwa serikali yake, kama inashindwa basi serikali yake haiwezi pia. Iweje JK kama mwenyekiti ajiamulu kama Rais?
 
Eti hii ni strategy wamebuni kupunguza foleni barabarani, CCM bana, ningekuwa daktari wake ningeichomolea mashine ya kupumulia ijifie rasmi.
 
Rais yuko busy anafuturisha! mafuta wzr si yupo? Mulizeni kulikoni
 
big bon sinza kwa remmy watu wanagombania mafuta,..kwa ufupi biashara yake ya mafuta inalipa kipindi kama hiki...utasubiri tamko mpaka uchoke,..after all..a poor old man doesn't even know what to comment,..mambo ya uchumi sio mchezo..theory of the firm...
 
Jamani eeeh si alishasema kuwa na magari ni maendeleo, kwahiyo hata kukosa mafuta kwake ni maendeleo.
 
Bei za mafuta haziwezi kushushwa kwa matamko, serikali lazima ishughulikie uchumi. Katika karne hii uchumi hauongozwi kwa matamko ya Nape NNauye na CCM! Ikiwa shilingi inadhoofika kila kukicha, waagizaji mafuta lazima wauze bei itakayowawezesha kuagiza stock nyingine.

Bei za mafuta hazifuati kodi tu, au bei iliyopo sokoni bali inatazama mwelekeo wa shilingi dhidi ya fedha za kigeni! Inachotakiwa serikali sio kutoa maagizo bali kushughulikia uchumi, kudhibiti mfumuko wa bei, na kuifanya shilingi stable ili waagizaji wa mafuta waweze kukadiria gharama na faida na hapo ndipo bei zita-stabilize.

Sasa matamko ya wakina Nape, kulazimisha serikali kushusha bei huku wakijua kuwa uchumi uko taabani matokeo yake ndiyo hayo! Total chaos! Watanzania tusikubali kudanganywa na matapeli wa CCM. Uchumi wa zamani wa Chama kushika hatamu na kutoa matamko hauwezekani tena kwa sasa!

Kiasi Fulani uko sawa,
Serikali ni ya CCM, sisiem imeilalamikia serikali kuhusu tatzizo la umeme, mwenyekiti wa sisiem ndiye rais wa Tanzania na ndiye Kiongozi mkuu wa serikali, na alikuwepo kwenye kikao hicho cha Kamati kuu ya CCM. Kazi ya chama ni kupanga sera ambazo serikali huzitekeleza, sera mbovu hudumuza uchumi.

EWURA ni mamlaka iliyo chini ya serikali, serikali ambayo inaundwa na CCM.Kodi zimezidi kwenye mafuta, kama ilivyo ada serikali kupitia TRA Kila mwaka imekuwa na tabia ya kupandisha PAYE, Kodi ya Magari, Kodi ya Mafuta, Sigara na Bia .Kwa Mtaji huu uchumi utakuwa kweli?

Rais yuko busy akizunguka zunguka uku na uko akiombaomba misaada, nchi haiwezi kuendelea kwa misaada!!
Wala wawekezaji!! hawa ni wanyonyaji tu.
 
Kiasi Fulani uko sawa,
Serikali ni ya CCM, sisiem imeilalamikia serikali kuhusu tatzizo la umeme, mwenyekiti wa sisiem ndiye rais wa Tanzania na ndiye Kiongozi mkuu wa serikali, na alikuwepo kwenye kikao hicho cha Kamati kuu ya CCM. Kazi ya chama ni kupanga sera ambazo serikali huzitekeleza, sera mbovu hudumuza uchumi.
EWURA ni mamlaka iliyo chini ya serikali, serikali ambayo inaundwa na CCM.Kodi zimezidi kwenye mafuta, kama ilivyo ada serikali kupitia TRA Kila mwaka imekuwa na tabia ya kupandisha PAYE, Kodi ya Magari, Kodi ya Mafuta, Sigara na Bia .Kwa Mtaji huu uchumi utakuwa kweli????
Rais yuko busy akizunguka zunguka uku na uko akiombaomba misaada, nchi haiwezi kuendelea kwa misaada!!
Wala wawekezaji!! hawa ni wanyonyaji tu.

Huwa najiuliza kwanini mzigo wote huu wa kodi huwa hawaupeleki kwenye madini? utakuta ni kodi yamafuta , vileo nk ndo huwa inaongezeka lakini madini acha bana!
 
Duu!! Za siku nyingi da Pretta, za wapi vile?

Ama kweli shida huibua watu toka kusikojulikana!!! Afadhali nijisemee asante Mh Kikwete kwa makali haya ya maisha na hasa haya ya hivi sasa ya ukame wa mafuta zote za vyombo vya moto maana bila hivo mie ningemkuta wa Pretta kama si haya matatizo tu kumuibua huko maficho?

Kwa mara nyingine asante sana Mhe Kikwete kwani naamini haya MAISHA DUNI KWA KILA MTANZANIA MMATUMBI yakiendelea zaidi nchi pengine huenda nikakutana na marafiki zangu wengi kibao vipenzi KULEE TAHRIR SQUARE MNAZI MMOJA pale shida zetu zitakapotulazimisha bila ajizi kwenda kuwatimulia kivumbi maponjoro, ma********* na maburushi wanyonya nchi.

Oya uncle, usiogope CHADEMA kulazimishwa jina katika haya yote kwani shida hizi zilizotufikia pomoni kamwe hazifaha cha chama wala dini isipokua rangi za ngozi zetu kama ambavyo tulivyolazimishiwa kwa mara ya kwaanza Tanzania na baadhi za tawala zetu hizi.

mhhh......twende zetu kule kwenye tabia za wanyama mpenzi......hapa sio kabisa
 
Atoe tamko wakati mwenzenu anajiandaa kwenda Washington dc kushereke uhuru watanganyika, mbna nyinyi wa'tz mnapenda kumsumbua mzee wa watu mwenzenu ndoto yake ilkuwa aje kuwa rais kafanikiwa hayo mengne ni yenu.
 
Back
Top Bottom