Rais Kikwete ndiye anayefaa kuongoza – Dk. Mwakyembe

Kidudu Mtu

Member
Nov 7, 2009
64
0
MBUNGE wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe amesema Rais Jakaya Kikwete ndiye anayefaa kuongoza nchi na ni mhimili mkubwa katika vita ya ufisadi ila baadhi ya wasaidizi wake wanamrudisha nyuma katika vita hiyo.

Alisema hayo jana katika kongamano la miaka 10 Bila ya Baba wa Taifa lililoandaliwa na wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini na kufanyika katika Chuo cha Ustawi Jamii (ISW).

Mwakyembe alikuwa akijibu swali la mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) anayesoma shahada ya elimu, Chagona Deogratias aliyetaka kufahamu iwapo hoja alizokuwa akitoa Dk. Mwakyembe katika kongamano hilo alikuwa akiogopa kumsema Rais.

“Mimi kwangu namuona Rais anafaa kuongoza…bali tunapaswa tumuondolee baadhi ya watu wanaomchafua,” alisema Dk. Mwakyembe huku akiwataka watu wasimfikirie vibaya anapotoa hoja zake kuwa ni mbwembe bali anajiamini kutokana na elimu aliyonayo na hivyo anajivuna.

Alisema kuwa wananchi kwa ujumla wanapaswa kumsaidia Rais Kikwete katika mapambano ya ufisadi na vitendo vingine viovu katika jamii ili nchi ipige hatua za maendeleo.

Akizungumzia suala la mikataba mibovu, Mwakyembe alidai imekuwa ikisababishwa na ushamba wa wataalamu wetu katika masuala ya mikataba hali ambayo inaigharimu nchi na kuchangia kurudi nyuma kimaendeleo.

Kwa upande wake kada wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) aliyeshiriki katika mkutano huo Nape Nnauye, alisema kuwa kelele za ufisadi zinazopigwa nchini na baadhi ya watu hazimaanishi kwamba nchi nzima imeoza, bali kuna baadhi ya matatizo yanayotakiwa kushughulikiwa ili yasizidi na kuenea na hatimaye kuidhoofisha nchi.

Alisisitiza umuhimu wa kukomesha rushwa wakati wa kugombea nafasi katika uchaguzi mbalimbali la sivyo taratibu za uchaguzi zitaendelea kuharibika na kuwaasa wenye tabia hizo waache.

Mbunge wa Kishapu kupitia CCM Fred Mpendazoe, alisema kuwa umasikini unasababishwa na uongozi mbovu na kushauri miiko ya uongozi ipewe kipaumbele.

Katika hatua nyingine alisisitiza umuhimu wa kuongezeka kwa viwanda vingi vya usindikaji wa vyakula na matunda kama ilivyokuwa wakati wa utawala wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ili falsafa ya Kilimo Kwanza itekelezwe kwa vitendo.

...................................

Is Mwakyembe serious?
 
Ukisikia utapeli wa kisiasa ndio huo, uma puliza, nenda zako; kazi kugombanisha watu badala ya ku-address the real problem. Ipo siku watanzania watawashtukia na kuwasuta!
 
Ukisikia utapeli wa kisiasa ndio huo, uma puliza, nenda zako; kazi kugombanisha watu badala ya ku-address the real problem. Ipo siku watanzania watawashtukia na kuwasuta!

we Kitila ushakuwa politician mzee, from Daruso to "na apana ahidi mbele ya chama mapinduzi nitakulinda mpaka kufa!
 
hakuna cha wapiganaji wala nini...watu wanachanganya changanya mambo tuuu..matoleo yake hawaeleweki

mambo ya siasa tz hayatabadilika mpaka pale wabunge watakapopigana kuwapigania wana vijiji waliowachagua na sio ccm iliyowapa ticket ya kuingia bungeni
 
Ukisikia utapeli wa kisiasa ndio huo, uma puliza, nenda zako; kazi kugombanisha watu badala ya ku-address the real problem. Ipo siku watanzania watawashtukia na kuwasuta!
.
Kwenye thread ya Mwanakijiji, "Wapiganaji walioko CCM Wanapigania Nini", nilimjibu baadhi wanapiganaji sio wapiganaji chochote, ni ma-oportunist wanaopigania nafsi zao. Japo bado namuaminia kijana Nape ni mpiganaji wa kweli tatizo ni aliance anayoikumbatia kwa sasa inamjengea umaarufu kwa free ride kwenye press ya mrengo wao with airtime bonus kwenye TV ya mrengo wao, when the time comes, asipojiangalia, atakwenda na maji pamoja na aliowadhania ni wapiganaji.
 
Baada ya kuhojiwa na Takukuru tutaona na kusikia mengi kutoka kwa waheshimiwa hawa 'wapiganaji'..lolz
 
Nilishasema siku nyingi hapa, Mwakyembe ni msanii tu, tena ni bora akazuiwa na kuumbuliwa mapema kabla hajafikia ukomo wa ambitions zake.
 
Ukisikia utapeli wa kisiasa ndio huo, uma puliza, nenda zako; kazi kugombanisha watu badala ya ku-address the real problem. Ipo siku watanzania watawashtukia na kuwasuta!


kaka yangu Kitila nilishakuambia rudi nyumbani CCM.Naomba nisikie tafadhali
 
Mimi kwangu namuona Rais anafaa kuongoza…bali tunapaswa tumuondolee baadhi ya watu wanaomchafua," alisema Dk. Mwakyembe huku akiwataka watu wasimfikirie vibaya anapotoa hoja zake kuwa ni mbwembe bali anajiamini kutokana na elimu aliyonayo na hivyo anajivuna.


Duh, masikini Mwakyembe hakika unatia huruma, heri hata mimi ambaye sikuona ndani ya darasa - nilistaajabu ya Musa, kumbe ya Firauni bado. Kwa tamko lako hili hakuna tofauti kati yako na Makamba - wote mwajuana kwa vilemba. Heri Makamba, hakanushi kumpikia chai kipenzi chake, wewe wakataa hujaingia jikoni huku macho yote mekundu kwa moshi. Lililo wazi ni kuwa hatutapata shida kuwasaka kwani tutawatambua kwa hayo macho yenu.

 
Wote lao ni moja tu...ni kuilinda CCM not matter what. Siamini kama hawa jamaa ni kweli wapiganaji. Muda utayafunua wanayokusudia kwa undani.
 
Mlitaka Dr. Mwakyembe asemeje? Kule kwake Kyela kwenye CCM kumeota majani, wapinzani na nyie hamumtaki. Kilichobaki ni kujipendekeza kwa rais ili amsaidie sasa na hata asipomsaidia basi akibwangwa Kyela, mheshimiwa asimtupe kabisa kama akina Njelu Kasaka.

Huo ndio umalaya wa siasa ambao yeye sio wa kwanza na tutaendelea kuushuhudia hapa JF.
 
Si kila aliyesoma kama Mwakyembe ana uwezo kuweka mambo sawa kwa mapana yake, hivyo Mwakyembe kuringa kwa elimu aliyonayo ni bure tu. Kwenye tume alionyesha ubora, lakini umepita muda kidogo tu tayari kesha onyesha weakness yake.

Eti Mwakyembe anasema yeyote JK aweza kua raisi mzuri ili mradi ukimwondolea wanaomchafua. Kwani uliyemzuia JK kuondoa wanaomchafua ni nani.
 

........Alisema kuwa wananchi kwa ujumla wanapaswa kumsaidia Rais Kikwete katika mapambano ya ufisadi na vitendo vingine viovu katika jamii ili nchi ipige hatua za maendeleo........



Duh Hii part ni nzito tena sana, Unapo waambia wananchi kumsaidia rais ktk vita ya ufisadi,!
kwanza wananchi katka sakata hili la kupinga vita juu ya ufisadi wamepewa kipaumbele gani? wanathaminiwa na kusikilizwa hoja zao kwanzaaa??

Pili hali ya kimaisha ya watanzania ni duni sana elimu ni ndogo sana rushwa imeyapakaaaaa mpaka vijijini viyu vidogo vidogo tu kama matibabu mahospitalini ni mpaka umuhonge nesi amsaidie wakati ni wajibu wa nesi kutoa service kwa mgonjwa, serikali ilipaswa kuboresha kwanza maeneo yenye myanya ya rushwa jamani tusipende kutangulisa politics mbele.

Tatu viongozi waloko juu wao waanze kujisafisha kwanza na kuwepo na true democracy na kusiwe na propaganda eg kiongozi umekutwa na kashfa au umeusika kana namna fulani katika iyo scandal hakuna tena mjadala he/she must step down haraka sana hata kama ni viongozi wake wa chini walihusika wote they must step down immediately ili kukuza democracy ya kweli na ndipo nidhamu ya uongozi itarudi na maadili ya uongozi yatakuwa kwenye mstali ulio nyooka. eg nilisikia padri mmoja akisema mnyone mnyongeni ila haki yake mpeni haka kamsemo hata rais aliwakukasema ila napenda kuwajurisheni kama watuhumiewa wanadhani wameonewa na bado wako kwa madaraka kwanini wasikae kando kwanza i mean wa step down kwanza kama Jacob Zuma(SA President) alivyo fanya wakati wa kesi ya yake ya silaha.alijiuzuru kwanza nyadhifa zake zote na akamaliaza kwanza kesi sasa leo yuko wapi???

 
...Huyu Mwakyembe ni mganga njaa asiye na msimamo.......Hili ni tatizo la kufikiria kutumia tumbo...
 
Naona Mwakyembe hapa anaonyesha dhahiri kuwa amefikishwa kwenye kona na sasa anasubiri kutiwa vyombo tu!

Sisi ndio tunaotakiwa kumuondolea JK hao waliozumnguka, kwa taratibu zipi za kisheria? Kama yeye JK hawaoni kuwa ni tatizo ila kwetu tuliomweka rais madarakani kupitia hao wanaomzunguka tunaona ni tatizo, sio kweli kuwa rais ndiye tatizo.

Poor mwakyembe! Kweli hizi naziona kama njaa vile.
 
Nilishasema siku nyingi hapa, Mwakyembe ni msanii tu, tena ni bora akazuiwa na kuumbuliwa mapema kabla hajafikia ukomo wa ambitions zake.

Huyu na hao anaowaita mafisadi hawana tofauti wote ni wachumia tumboni; isipokuwa wakina Lowassa waliwahi na hawa wakachelewa!!! Mwakyembe ni mtoa rushwa kwa wapiga kura na mpokea rushwa vile vile; abishe kama hakupokea rushwa toka kwa Masaburi wakati wa uchaguzi wa wabunge wa Afrika Mashariki!!!
 
Inafurahisha kuona jinsi watu wanavyohamaki kwa kuzikiliza muziki wasio upenda!
 
Inafurahisha kuona jinsi watu wanavyohamaki kwa kuzikiliza muziki wasio upenda!

Wewe na hakika ni mzanzibari unapenda ushindani usiokuwa na maana nani kakuambia hatupendi kusikia habari tusizozitaka??? Tunachosikitika ni kukosekana msimamo among viongozi wa Tanzania. Mara MWakyembe anajiita champion wa ufisadi mara serikali inafanya kazi nzuri ila baadhi ya watendaji sio wazuri.

Usanii kama huu unarudisha maendeleo ya nchi mwisho wake wananchi watakosa imani na serikali yao. Nilishawahi kusema zamani kuwa an unjust law is similar to a no law!!!!! There will a be rise in a considerable degree of lawlessness in our country!!!
 
Si kila aliyesoma kama Mwakyembe ana uwezo kuweka mambo sawa kwa mapana yake, hivyo Mwakyembe kuringa kwa elimu aliyonayo ni bure tu. Kwenye tume alionyesha ubora, lakini umepita muda kidogo tu tayari kesha onyesha weakness yake.

Eti Mwakyembe anasema yeyote JK aweza kua raisi mzuri ili mradi ukimwondolea wanaomchafua. Kwani uliyemzuia JK kuondoa wanaomchafua ni nani.

Baba yao na Mama yao CCM
 
Back
Top Bottom