Rais Kikwete: Nabii asiyekubalika nyumbani kwake?

Just a question for the JK apologists, Hivi JK alichaguliwa kuwa raisi ili afanye nini? Na so far aliyotakiwa kuyafanya yametekelezeka kwa % ngapi??
 
Rais Kikwete kazi yake kubwa kutembea nchi za nje tu hakuna chochote anachofanya nchi imejaa kila Ufisadi,njaa Umasikini,Ulaji rushwa umeongezeka na Ufisadi ndio huo unazidi Nchi imeuzwa ikiwa watamchaguwa tena wananchi basi wananchi wamejaa na usingizi tunachotaka ndugu zangu Wana JF Maendeleo na kipatikane chama kingine tuone mafanikio ya chama kingine kiondowe Ufisadi,Rushwa,Ujambazi,Wizi wa Mali ya Umma Tuamke ndugu zangu WaTanzania Tumelala usingizi mzito ndugu zangu Wana JF Mungu atusaidie Ameen.
 
Nilienda mahali kidogo nimerudi namuandalia majibu mlalahoi

Je huko ulikokuwa umepata confirmation kuwa waendeshaji wa jamii (jambo) forums walikamatwa na kuwekwa selo wakati wa Kikwete na sio wa Mkapa kama ulivyodai mapema?
 
Kwani Mwanahalisi lilifungiwa katika utawala upi?Kulikoni je?Na Kubenea alimwagiwa tindikali wakati wa utawala wa Nyerere?Na hao majasusi wanaokesha JF kila kukicha ni waajiriwa wa Kamuzu Banda?Ni uhayawani kufikiria kwamba JK ametupa uhuru wa kuongea wakati haki hiyo iko wazi na bayana kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano.Yani haki yako ya Katiba unaihusisha na matakwa ya mtu?Kweli safari ya kumkomboa Mtanzania bado ni ndefu sana kwa mawazo kama haya!
Na hatma ya Meremeta ni ipi hadi leo?Pinda (mteuliwa wa Kikwete) alisemaje Bungeni alipoulizwa kuhusu Meremeta?

Halafu napokuona wa ajabu ni namna unavyoweza kuonyesha bayana kuwa JK ana uwezo wa kufanya mazuri lakini unajikanganya kwa kushindwa kutueleza nini kinamkwaza kufanya mazuri kama kuwachukulia hatua mafisadi wa Kagoda,Richmond,Kiwira,IPTL,rada,nk.

Tumia busara usiendeshwe na simulizi kwani simulizi zimekuwepo tangia enzi hizo.Kwanza,nimeshakujibu kuwa huo muswada wa kutenganisha biashara na siasa ni kiini macho kwa vile CCM yenyewe inaendeshwa na wafanyabiashara wa fedha chafu.Unatarajia nini kama mwenyekiti wa kamati yake ya maadili ni jambazi wa rada Chenge?

Kwa upande wa kisheria,uamuzi huo unaweza kupingwa mahakamani kuwa unawanyima wafanyabiashara waadilifu fursa ya kushiriki katika demokrasia.Kwa taarifa yako,tatizo sio wafanyabishara kujihusisha na siasa hususan katika mfumo wa uchumi wa soko.Tatizo ni wafanyabisahara wa aina ya Rostam Aziz,Lowassa,Karamagi na mafisadi kama hao.Kwani kama Rostam anaweza kuandikisha utitiri wa makampuni kwa kutumia majina mbalimbali,atashindwaje kusema anaacha biashara na kubaki mwanasiasa asilimia 100% huku makampuni anayomiliki kwa majina mbalimbali yakiendeleza ufisadi?

Pia uanapswa kuelewa kuwa tatizo sio sera,miswada au sheria bali usimamizi na utekelezaji wake.Kwani wakati tunaingizwa mkenge wa Richmond kulikuwa hakuna sheria inayosimamia manunuzi?Je wakati tunaingia mkenge wa IPTL hakukuwa na sheria za kuhakikisha kuwa mkataba huo haugeuki kuwa loba ya mbao?

Ni kipi kinakupa matumaini kuwa sheria ya kutenganisha siasa na biashara itatekelezeka ilhali hseria nyingine zinazoweza kuzuia ufisadi zimeendelea kubaki vitabuni tu?

Na muulize huyo rafiki yako JK kwanini yeye mwenyewe hafuati sheria kwa kututangazia mali zake ili tujue kama naye si mfanyabisahara?Kwanini asimuige Pinda?



Kwahiyo kwa vile ndani ya CCM hakuna aliye bora basi tuendelee na Kikwete?Hivi unafahamu kuwa membership ya CCM ni takriban asilimia 10 tu ya population ya Tanzania?Yani unachosema ni kwamba laiti ungekuwa na mke malaya ungeendelea nae hivyohivyo kwa vile tu kwa mtizamo wako huko nje hakuna wanawake walio bora zaidi?Haya ndio yanayowaua watu kwa ukimwi.

Kumbuka kuwa uongozi wa TAIFA LETU sio divine right ya CCM pekee.Kumsifia Kikwete kuwa ni bora kwa vile tu wenzake huko CCM ni wachafu,au hakuna aliye bora zaidi yake,ni ufinyu wa mawazo.

I would say kuna watu kama Dr Slaa ambao at least wametuonyesha nini maana ya kiongozi kuwa na uchungu na nchi.



Na kwa akili yako iliyo timamu ukishakuwa na barabara nzuri hapo Dar wakati wakulima huko mahenge wanasumbuana na kivuko feki unatarajia hayo mazao yanafikaje bandarini Dar?Eti infrastructural economics!Yaani barabara za lami mijini zimekusahaulisha kabisa adha ya watanzania wenzako wanayipata huko reli ya kati na Tazara?Vipi kuhusu ATC?

Ni ulevi wa kifikra kuangalia upande mmoja wa "maendeleo" na kupuuza upande mwingine.Tegemeo la uchumi wa Tanzania ni katika kilimo,na kama unafuatilia mijadala ya bunge vizuri utakumbuka kwanini bajeti ya WIzara ya Miundombinu iliwekewa ngumu katika kikao cha bajeti kilichopita.Fuatilia hilo kisha ufanye review ya hoja yako dhaifu.

Of course,kutawala nchi sio sawa na kuongoza nyumba ndio maana hatutaki kiongozi dhaifu ang'anganie kuongoza wakati ameshindwa hata kumudu nidhamu ya baraza lake "dogo" la mawaziri waziofika 60.Kama hawezi kuwamudu hao "wachache" alowateua ataweza kumudu kuwatumikia watanzania zaidi ya milioni 40?



Unavyoongea kuwa ameingia na kukuta madudu inasomeka kana kwamba ALILAZIMISHWA KUINGIA MADARAKANI.Dont tell me kuwa hakujua madudu yalokuwepo before hajaingia madarakani because HE WAS PART YA MADUDU ALIYOYAKUTA ALIPOINGIA MADARAKANI.Kwa kumbukumbu zako,JK alianza kushika madaraka ya kitaifa lini?Mwaka 2006?Alikuwa anafahamu fika uzito wa jukumu analolipokea na akatuahidi kutupatia ufumbuzi.

Halafu baadhi ya kauli zako ni kama za KUJIPENDEKEZA.Mbona sijamsikia JK mwenyewe akisema kuwa CHANZO CHA MATATIZO YALIYOPO NI WATANGULIZI WAKE?

Kaka sikatai hapa nilikuwa najaribu kuyatafuta mazuri ya JK na sio kuwa nakubaliana na siasa na msimamo wake kwani hauridhishi but hebu tujaribu kuangalia kwanini nasema ni afadhali JK. Kwanza tukija CCM wenyewe ni chama kama cha kimafia ambacho kimekaa kuangalia nani anajaribu kukikosoa ili kimshughulikie unadhani mtazamo huo utaweza kuibadilisha uendeshaji wa chama? Au unataka kuniambia Sitta na wenzie ndio watakaobadilisha chama unakuta jibu hakuna.

Kuhusu CCM ni 10% of the population wewe ni mtu usiyeifahamu siasa ya tanzania. CCM naweza kukwambia ni 60% of the population. Vijijini huko hakuna mtu anayejua chama cha siasa zaidi ya CCM. Chadema wanajua hiki na kazi nzito kuwaelemisha watanzania kuwa CCM imekumbatia mafisadi na ndio maana nguvu ya CCM iko vijijini na sio mijini. Hivyo basi ni mimi na wewe tunaokaa katika keyboard tukaripuka hapa ndio 10% the rest wanafahamu chama ni CCM na huna vya kuwaambia hiyo ndio inayowafanya CCM wawe na nguvu. Sasa tukitazama CCM imejaa mauvundo ambao mwisho wa siku unajiuliza nani ana uafadhali yule ambaye anajali maslahi binafsi kama Lowassa au JK mpenda masifa. Ndio unakuta bora JK kwani japokuwa anapenda sifa bado ana ile damu ya uzalendo.

Tuje katika meremeta, IPTL na mengineyo. Mwafrika alinionyesha article inayosema kuwa Kikwete alisign IPTL. Come on hivi waziri anakuwa responsible kwa kusign kitu wakati chini yake kuna wanasheria, makatibu wakuu na maafisa walikuwa wapi??? Mnataka kuniambia nyie mkiwa mawaziri ukiletewa mkataba utajua kama huo mkataba ni dili?? Kwanza wewe utaangalia sheria inasemaje, pili vigezo vyote vilifatwa?, Tatu nani alifuzu unakuta vigezo vyote vimefaulu mnataka kuniambia waziri atoke aende marekani kucheki kama IPTL inaexist au la that is pathetic na ludicrous to be honest huwezi kuongoza idara kihivyo let alone wizara.

Tuje katika infrastructure. nimeshakueleza kuwa utekelezaji wa project mbalimbali unategemeana na malengo ya serikali. Unataka kuniambia waanze na barabara nzuri bunda, msata, kila eneo linazalisha aina moja ya zao halafu wakulima wawe na gharama kubwa za kusafirisha mazao ya mijini unadhani ndio akili hiyo au wewe umesoma economics ya kijijini. Wapi bora kutengeneza barabara mijini kwenye masoko ya bidhaa au kule katika kuzalishia? Kimtazamo wangu ni afadhali utengeneze kule katika mijini maana ndio kwenye viwanda na wateja then uanze kutengeneza maeneo ya wakulima kufuatana na umuhimu wa barabara. Otherwise ukifanya zote kwa pamoja barabara zinakuwa haziishi kwasababu serikali inakuwa haina hela. Likewise, ukiwa unatengeneza barabara vijijini utamaliza lini kuna maeneo haya natija ya kuwa na barabara nzuri hata ulaya kuna maeneo ukienda barabara kama bunda vijijini je unadhani wao hawakuona umuhimu wa wakulima wao kule vijijini msitake kutuzingua bwana JK amejitahidi kwa hili.

Tuje katika madudu aliyoyakuta sawa alikuwa na yeye ni mmoja katika mawaziri hivyo basi anabear part of the responsibility unasema kwanini hakusema rais aliyepita alifanya madudu.Kwanza kaa ukijua ukimcritise rais aliyepita na kumsulubu ukae ukijua na wewe jiandae kuyapata hayo hayo kama sio msafi (muulize Chiluba wa Zambia yalimkuta nini). Kwani rais si mtu ni institution iliyojengwa na watu hivyo basi akiondoka watu wake hubakia let alone mko chama kimoja unataka apate tabu kuongoza nchi. Be realistic my friend unataka kuniambia JK asimame katika mimbari kama hayawani aseme Mkapa ndio matatizo yote. I think not anajua repurcussion zake labda wewe ukishakuwa rais sema hivyo but mtu mwenye akili zake timamu hawezi hata kuthubutu kusema hilo jambo. Kawatawale jamaa zako but sio watanzania JK ana mazuri yake
 
Rafiki yangu, hayo niliyowekea red yana ukweli. Unajua ni lini mpanga wa MMEM na MMES zilianza? Yeye amefanya lipi zaidi ya kutimiza tu aliyofanya mwenzake? Kwenye hili la shule naliogopa, kwa sababu mwenzake Mkapa aliongeza shule nyingi za msingi pasipo kuathiri ubora. Yeye ameachiwa kusimamia tu hizi shule za secondary ambazo mwenzake alishakuwa na mpango kabambe ndo katutokea na ziro zaidi ya 60000. Aibu kuwapotezea muda watoto zaidi ya 60000 kwa zaidi ya miaka minne. Umeongelea kuhusu barabara, maji and the like. barabara zipi, maji yapi, hizo project zote sializianzisha Mkapa? Hili suala la kusimamia hata wewe tu unaweza kusimamia. Tunachotaka ni innovation and creativity ambazo zimeibuka wakati wake ambazo yumkini zinaviashiria vizuri kwa uchumi na ustawi wa jumla wa nchi yetu.
Napenda nimpongeze sana kuhusu chuo kikuu cha Dodoma. Katika hicho sina upinzani naye, kafanya kazi nzuri yenye maslahi makubwa kwa taifa.

Ndio uongozi ulivyo kuendelea kusimamia na kufanikisha mipango uliyokuwepo kama MMEM na MMES hata obama anaendeleza vita afghanistan na iraq aliyoikuta so huwezi kutenganisha kwamba anasimamia miradi ya mmem na mmes..

Project mpya za maji, barabara mikoani naweza kutaja kwa uchache Mbeya -Rukwa, Handeni- Msata, Arusha-Babati-Singida etc hata kama zilikuwepo ndyo ilivyo mkapa alikuta mradi wa barabara ya kwenda kusini kwa mwinyi akasimamia vizuri

Innovation na creativity ziko nyingi ndugu including kilimo kwanza, utalii (vyuo vya utalii) na mkakati ambao umeongeza watalii na Tanzania kufahamika duniani zaidi wakati wake...

Huwezi kusema hajafanya chochote huo si uchambuzi wa mambo bali upofu.
 
Kaka sikatai hapa nilikuwa najaribu kuyatafuta mazuri ya JK na sio kuwa nakubaliana na siasa na msimamo wake kwani hauridhishi but hebu tujaribu kuangalia kwanini nasema ni afadhali JK. Kwanza tukija CCM wenyewe ni chama kama cha kimafia ambacho kimekaa kuangalia nani anajaribu kukikosoa ili kimshughulikie unadhani mtazamo huo utaweza kuibadilisha uendeshaji wa chama? Au unataka kuniambia Sitta na wenzie ndio watakaobadilisha chama unakuta jibu hakuna.

Bado hujajibu swali la kuwa -- tofauti ya ufisadi wa Kikwete na ule wa Sitta au Lowassa ni upi. BTW bado nasubiria majibu yako kwa alichoandika Kibanga

Kuhusu CCM ni 10% of the population wewe ni mtu usiyeifahamu siasa ya tanzania. CCM naweza kukwambia ni 60% of the population. Vijijini huko hakuna mtu anayejua chama cha siasa zaidi ya CCM. Chadema wanajua hiki na kazi nzito kuwaelemisha watanzania kuwa CCM imekumbatia mafisadi na ndio maana nguvu ya CCM iko vijijini na sio mijini. Hivyo basi ni mimi na wewe tunaokaa katika keyboard tukaripuka hapa ndio 10% the rest wanafahamu chama ni CCM na huna vya kuwaambia hiyo ndio inayowafanya CCM wawe na nguvu.

Chadema imeshinda Tarime, Kigoma na kwingineko, je huko nako ni mijini? Je wanakoshinda CUF ni mijini tu? Get data zako mkuu maana naona leo unachemka kweli!

Sasa tukitazama CCM imejaa mauvundo ambao mwisho wa siku unajiuliza nani ana uafadhali yule ambaye anajali maslahi binafsi kama Lowassa au JK mpenda masifa. Ndio unakuta bora JK kwani japokuwa anapenda sifa bado ana ile damu ya uzalendo.

Tofauti ya ufisadi wa Kikwete na Lowassa ni upi? rudia tena alichoandika Kibanga

Tuje katika meremeta, IPTL na mengineyo. Mwafrika alinionyesha article inayosema kuwa Kikwete alisign IPTL. Come on hivi waziri anakuwa responsible kwa kusign kitu wakati chini yake kuna wanasheria, makatibu wakuu na maafisa walikuwa wapi??? Mnataka kuniambia nyie mkiwa mawaziri ukiletewa mkataba utajua kama huo mkataba ni dili?? Kwanza wewe utaangalia sheria inasemaje, pili vigezo vyote vilifatwa?, Tatu nani alifuzu unakuta vigezo vyote vimefaulu mnataka kuniambia waziri atoke aende marekani kucheki kama IPTL inaexist au la that is pathetic na ludicrous to be honest huwezi kuongoza idara kihivyo let alone wizara.

Mimi nikiwa waziri na watu wakaniletea mkataba kama wa IPTL, moto nitakaowasha hapo hakuna atakayeuzima kirahisi. Lakini nikiwa fisadi kama Kikwete, nitajifanya tu kuwa sijui kinachoendelea

Tuje katika infrastructure. nimeshakueleza kuwa utekelezaji wa project mbalimbali unategemeana na malengo ya serikali. Unataka kuniambia waanze na barabara nzuri bunda, msata, kila eneo linazalisha aina moja ya zao halafu wakulima wawe na gharama kubwa za kusafirisha mazao ya mijini unadhani ndio akili hiyo au wewe umesoma economics ya kijijini. Wapi bora kutengeneza barabara mijini kwenye masoko ya bidhaa au kule katika kuzalishia? Kimtazamo wangu ni afadhali utengeneze kule katika mijini maana ndio kwenye viwanda na wateja then uanze kutengeneza maeneo ya wakulima kufuatana na umuhimu wa barabara. Otherwise ukifanya zote kwa pamoja barabara zinakuwa haziishi kwasababu serikali inakuwa haina hela. Likewise, ukiwa unatengeneza barabara vijijini utamaliza lini kuna maeneo haya natija ya kuwa na barabara nzuri hata ulaya kuna maeneo ukienda barabara kama bunda vijijini je unadhani wao hawakuona umuhimu wa wakulima wao kule vijijini msitake kutuzingua bwana JK amejitahidi kwa hili.

Longo longo kibao lakini bado hujasema alichofanya Kikwete kwa mifano hai

Tuje katika madudu aliyoyakuta sawa alikuwa na yeye ni mmoja katika mawaziri hivyo basi anabear part of the responsibility unasema kwanini hakusema rais aliyepita alifanya madudu.Kwanza kaa ukijua ukimcritise rais aliyepita na kumsulubu ukae ukijua na wewe jiandae kuyapata hayo hayo kama sio msafi (muulize Chiluba wa Zambia yalimkuta nini). Kwani rais si mtu ni institution iliyojengwa na watu hivyo basi akiondoka watu wake hubakia let alone mko chama kimoja unataka apate tabu kuongoza nchi. Be realistic my friend unataka kuniambia JK asimame katika mimbari kama hayawani aseme Mkapa ndio matatizo yote. I think not anajua repurcussion zake labda wewe ukishakuwa rais sema hivyo but mtu mwenye akili zake timamu hawezi hata kuthubutu kusema hilo jambo. Kawatawale jamaa zako but sio watanzania JK ana mazuri yake

Kikwete hawezi kumsulubu Mkapa kwa vile wote wawili (Kikwete na Mkapa) ni mafisadi waliokubuhu.

Swali kwako - mkataba wa buzwagi umesainiwa wakati wa uongozi wa nani?
 
.....

Innovation na creativity ziko nyingi ndugu including kilimo kwanza, utalii (vyuo vya utalii) na mkakati ambao umeongeza watalii na Tanzania kufahamika duniani zaidi wakati wake...

Huwezi kusema hajafanya chochote huo si uchambuzi wa mambo bali upofu.

Ha ha ha ha ... wanathubutu hata kutaja kilimo kwanza (mabilioni ya fedha yametumbuliwa) - mradi wa kifisadi wa wana ccm
 
Bado hujajibu swali la kuwa -- tofauti ya ufisadi wa Kikwete na ule wa Sitta au Lowassa ni upi. BTW bado nasubiria majibu yako kwa alichoandika Kibanga



Chadema imeshinda Tarime, Kigoma na kwingineko, je huko nako ni mijini? Je wanakoshinda CUF ni mijini tu? Get data zako mkuu maana naona leo unachemka kweli!



Tofauti ya ufisadi wa Kikwete na Lowassa ni upi? rudia tena alichoandika Kibanga



Mimi nikiwa waziri na watu wakaniletea mkataba kama wa IPTL, moto nitakaowasha hapo hakuna atakayeuzima kirahisi. Lakini nikiwa fisadi kama Kikwete, nitajifanya tu kuwa sijui kinachoendelea



Longo longo kibao lakini bado hujasema alichofanya Kikwete kwa mifano hai



Kikwete hawezi kumsulubu Mkapa kwa vile wote wawili (Kikwete na Mkapa) ni mafisadi waliokubuhu.

Swali kwako - mkataba wa buzwagi umesainiwa wakati wa uongozi wa nani?

Good point but before i answer your question nikuulize maswali yafuatayo.
a. CCM ina majimbo mangapi vijijini ?

b. Wapinzani nao je?

c. Mkataba wa buzwagi nani alikuwa rais? Na hivi unajua kwamba Mkapa alikuwa ni Bully leader?

Acheni kujenga hoja za kwamba JK before nijibu maswali haya
 
Kaka sikatai hapa nilikuwa najaribu kuyatafuta mazuri ya JK na sio kuwa nakubaliana na siasa na msimamo wake kwani hauridhishi but hebu tujaribu kuangalia kwanini nasema ni afadhali JK. Kwanza tukija CCM wenyewe ni chama kama cha kimafia ambacho kimekaa kuangalia nani anajaribu kukikosoa ili kimshughulikie unadhani mtazamo huo utaweza kuibadilisha uendeshaji wa chama? Au unataka kuniambia Sitta na wenzie ndio watakaobadilisha chama unakuta jibu hakuna.

Kuhusu CCM ni 10% of the population wewe ni mtu usiyeifahamu siasa ya tanzania. CCM naweza kukwambia ni 60% of the population. Vijijini huko hakuna mtu anayejua chama cha siasa zaidi ya CCM. Chadema wanajua hiki na kazi nzito kuwaelemisha watanzania kuwa CCM imekumbatia mafisadi na ndio maana nguvu ya CCM iko vijijini na sio mijini. Hivyo basi ni mimi na wewe tunaokaa katika keyboard tukaripuka hapa ndio 10% the rest wanafahamu chama ni CCM na huna vya kuwaambia hiyo ndio inayowafanya CCM wawe na nguvu. Sasa tukitazama CCM imejaa mauvundo ambao mwisho wa siku unajiuliza nani ana uafadhali yule ambaye anajali maslahi binafsi kama Lowassa au JK mpenda masifa. Ndio unakuta bora JK kwani japokuwa anapenda sifa bado ana ile damu ya uzalendo.

Tuje katika meremeta, IPTL na mengineyo. Mwafrika alinionyesha article inayosema kuwa Kikwete alisign IPTL. Come on hivi waziri anakuwa responsible kwa kusign kitu wakati chini yake kuna wanasheria, makatibu wakuu na maafisa walikuwa wapi??? Mnataka kuniambia nyie mkiwa mawaziri ukiletewa mkataba utajua kama huo mkataba ni dili?? Kwanza wewe utaangalia sheria inasemaje, pili vigezo vyote vilifatwa?, Tatu nani alifuzu unakuta vigezo vyote vimefaulu mnataka kuniambia waziri atoke aende marekani kucheki kama IPTL inaexist au la that is pathetic na ludicrous to be honest huwezi kuongoza idara kihivyo let alone wizara.

Tuje katika infrastructure. nimeshakueleza kuwa utekelezaji wa project mbalimbali unategemeana na malengo ya serikali. Unataka kuniambia waanze na barabara nzuri bunda, msata, kila eneo linazalisha aina moja ya zao halafu wakulima wawe na gharama kubwa za kusafirisha mazao ya mijini unadhani ndio akili hiyo au wewe umesoma economics ya kijijini. Wapi bora kutengeneza barabara mijini kwenye masoko ya bidhaa au kule katika kuzalishia? Kimtazamo wangu ni afadhali utengeneze kule katika mijini maana ndio kwenye viwanda na wateja then uanze kutengeneza maeneo ya wakulima kufuatana na umuhimu wa barabara. Otherwise ukifanya zote kwa pamoja barabara zinakuwa haziishi kwasababu serikali inakuwa haina hela. Likewise, ukiwa unatengeneza barabara vijijini utamaliza lini kuna maeneo haya natija ya kuwa na barabara nzuri hata ulaya kuna maeneo ukienda barabara kama bunda vijijini je unadhani wao hawakuona umuhimu wa wakulima wao kule vijijini msitake kutuzingua bwana JK amejitahidi kwa hili.

Tuje katika madudu aliyoyakuta sawa alikuwa na yeye ni mmoja katika mawaziri hivyo basi anabear part of the responsibility unasema kwanini hakusema rais aliyepita alifanya madudu.Kwanza kaa ukijua ukimcritise rais aliyepita na kumsulubu ukae ukijua na wewe jiandae kuyapata hayo hayo kama sio msafi (muulize Chiluba wa Zambia yalimkuta nini). Kwani rais si mtu ni institution iliyojengwa na watu hivyo basi akiondoka watu wake hubakia let alone mko chama kimoja unataka apate tabu kuongoza nchi. Be realistic my friend unataka kuniambia JK asimame katika mimbari kama hayawani aseme Mkapa ndio matatizo yote. I think not anajua repurcussion zake labda wewe ukishakuwa rais sema hivyo but mtu mwenye akili zake timamu hawezi hata kuthubutu kusema hilo jambo. Kawatawale jamaa zako but sio watanzania JK ana mazuri yake

Tufanye hivi,endelea kumsapoti JK na ndoto zake za kutuletea maisha bora kwa kila Mtanzania,na mie nibaki na mtazamo wangu kuwa JK ni msanii,mbabaishaji na aliyeshindwa kazi.Of course,atarudi madarakani 2010-15 (na kwa sapoti ya watu kama wewe huenda mkapiga kelele katiba ibadilishwe awe rais wa milele).

Hakuna kazi ngumu kama kumshawishi mvuta sigara aache kwa vile sigara yaweza kuleta kansa.Ila akipata TB ataacha mwenyewe wala hakutakuwa na haja ya kushawishiwa.Likewise,kitakachobadili mtizamo wako sio hoja za hapa JF bali hatma ya nchi yetu.
 
Good point but before i answer your question nikuulize maswali yafuatayo.
a. CCM ina majimbo mangapi vijijini ?

b. Wapinzani nao je?

Kulinganisha na nini? Ukilinganisha mijini vs vijijini, wapinzani wana majimbo mengi vijijini kuliko mijini.

c. Mkataba wa buzwagi nani alikuwa rais?

Na hivi unajua kwamba Mkapa alikuwa ni Bully leader?

Acheni kujenga hoja za kwamba JK before nijibu maswali haya

Aliyekuwa raisi wakati mkataba wa buzwagi ukisainiwa (hotelini) ni Kikwete. Kikwete alimtuma rafiki yake kipenzi Karamagi kwenda kuuza nchi kwa wazungu kule ulaya kwani waliona aibu kufanya hivyo ndani ya Tanzania.
 
Ha ha ha ha ... wanathubutu hata kutaja kilimo kwanza (mabilioni ya fedha yametumbuliwa) - mradi wa kifisadi wa wana ccm

Fedha zimefika kila wilaya na matrekata yamenunuliwa kama hutaki kushiriki kujenga nchi endelea kulalamika

Another innovations: JK loans, wajasiriamali wadogo wadogo wamepewa mkopo wengi wa access funds kuendesha project zao..
 
Ha ha ha... independent voter anayemtetea Kikwete kwa nguvu zote. Unaweza kufanya spin zako kwenye vijiwe vya kahawa lakini sio hapa

Kwisha habari ukirudi utaanza kutukana maana ukikosa hoja ndio kimbilio lako..
 
Fedha zimefika kila wilaya na matrekata yamenunuliwa kama hutaki kushiriki kujenga nchi endelea kulalamika

Another innovations: JK loans, wajasiriamali wadogo wadogo wamepewa mkopo wengi wa access funds kuendesha project zao..

Komiko Ali wa baghdadi bwana, hawezi hata kuweka data kusapoti anachoandika!
 
Kwisha habari ukirudi utaanza kutukana maana ukikosa hoja ndio kimbilio lako..

Angalia kiroja ulichoandika hapa ... hizi ndizo mnaita hoja huko madrassa!? kutetea mafisadi kama Kikwete kwataka moyo yahe
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom