Rais Kikwete na ziara ya kwanza Jijini Mwanza baada ya uchaguzi

Sasa nimepata picha. Zitto kabwe ni mshiriki mkubwa wa kikwete. Ni zitto aliyewakilisha mchango wa tsh 10mil kutoka kwa jk, ktk hafla ya kuchangia mfuko wa elimu, wenje akiwa muandaaji, kumbe mil 10 ilikuwa ni kisafisha njia? Jk, kwa nn amtume zitto wakat kandoro mwakilishi wake yupo? Naanza kushawishika na mawazo ya weng kuhusiana na zitto.

On the red - Spot on!

Si vizuri ku-generalise watu wa maeneo fulani lakini nashawishika kusema kwa siasa za Tanzania na hasa kwa vyama vya upinzani watu wa Kigoma wanaonekana kuwa vegeugeu - wanatoa picha ya kutoaminika. Dr.Kaborou (spelling), David Kafullila, na sasa Zitto. Pia tukumbuke baada ya uchaguzi Kikwete alisikika akilia na UDINI, Zitto naye anadakia akisema kuwa hata yeye anaamini kuna udini (including jimboni kwake).

Kwa wale waliokuwa wanasema huyu dogo karudi kwenye mstari think again. Hana jinsi, he has to do as they tell him maana alishapigwa bei a looooong time ago. Kwa kifupi Zitto yuko kwenye njia panda- sijui anapataje usingizi huyu mtoto. Kwa upande mmoja ni 'stakeholder' wa mmoja wa mapacha watatu, upande mwingine ni 'stakeholder' wa magogoni, wakati huo huo ni anajiona yeye ni mpambanaji ndani ya chadema (zitto vs mbowe vs uchagga vs udini!!!!) then anajitokeza kwa umma kama mmoja wa makamanda wa chadema!!! Mkorogo.
 
Mi sielewi umuhhimu wa mtoa mada hapa maana ishu siyo ishu bali ni umbeya tu siinui mantiki ya kutujulisha ziara hamna jipya haoa

We ndo mbea. Hiyo ni taarifa kwa wengine kama kwako sio taarifa. Na kama umeona sio taarifa then hakuna haja ya kuona maana ya safari hiyo.
 
Asante kwa taarifa mkuu Katulanda ingawa hiyo ya mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama kuwa meya haijakaa sawa.

Ni kweli kaka Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama ni Mkuu wa mkoa na meya ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Jiji, na sahihisha kaka
 
Askofu Stephan Mang'ana ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Maskofu wa kanisa la Mennonite Tanzania leo amempiga kijembe Rais Jakaya Kikwete pale alipomwambia kuwa viongozi walioshindwa kuongoza waachie ngazi na kuondoka madarakani.

Akizungumza katika Ibada ya Misa maalum ya kumsimika Askofu Mteule Albert Jella Randa, Askofu huyo alisema huu ni wakati wa viongozi wasio waadilifu kuondoka katika nafasi zao za uongozi kwa kuachia ngazi kwa vile wameshindwa kuwatumikia wananchi.

“Rais, nawaheshimu sana viongozi wetu, lakini kwa hili mtanisamehe nawaomba mtoke kwa sababu mmeshindwa kuwatumikia wananchi waliowapa dhama ya kuwa viongozi, badala yake mnaonekana wakati wa kuomba kura”alisema Askofu Mangana.

Alidai kuwa hakuna haja ya viongozi hao kung’ang’ania kuwa madarakani wakati hawana uwezo wa kuongoza na kuwatumikiwa wananchi jambo ambalo wamekuwa wakimtwisha Rais mzigo wa malalamiko toka kwa wananchi.

Alisema sifa ya viongozi ni kufahamu matatizo ambayo wanayapata wananchi na kuwa mstali wa mbele katika kutafuta ufumbuzi wake na kusisitiza viongozi wa serikali ya Kikwete wameshindwa na kuwataka kuondoka kwa kuachia ngazi.

“Kiongozi anapaswa kuelewa matatizo ya wananchi, kuyatafutia ufumbuzi na kusoma alama za nyakati,"alieleza na kutumia mfano wa Musa katika kitabu cha Mwanzo cha Biblia alipokuwa akiwaongoza wana Isael na kusema, "Kiongozi anatakiwa ajitoe kafara kwa kundi la watu anaowaongoza, lakini viongozi wa nchi hii wamekuwa wakitenda kazi zao na kuwaacha wananchi wakibaki na maswali ambayo hayana majibu juu ya ugumu wa maisha."

Alisema kama ilivyokuwa kwa Mussa, alipopiga magoti mbele ya Mungu na kumwambia kuwa hana sauti juu ya watu wanao waongoza sababu ya ‘mdomo mzito’ na kuwataka hata viongozi walioshindwa kurudi kwa Rais aliye wateua na kumwambia majukumu aliyowapa yamewashinda hivyo kuachia uongozi.

Rais Jakaya Kikwete akimpongeza Askofu Randa mara baada ya Ibada ya Kusimikwa rasmi leo jijini Mwanza
 

Attachments

  • GO9G1763.JPG
    GO9G1763.JPG
    28.5 KB · Views: 132
nakwambia huku kila dk ni ving,ora tu msafara mrefu ukiona unaweza fikiri ni Gadafi kaja mza.cjui posho na pesa wanatoa wapi manake tumeambiwa siri.kali haina pesa ya kulipa watumishi madai yao na mshahara wa mwezi huu umewahi baada ya zito kulipua cjui wamekopa wapi?au kwa mapacha watatu?
 
Askofu huyu moga ameshindwa kumpasulia ukweli kuwa aliyeshindwa ni yeye Kikwete
 
Askofu huyu moga ameshindwa kumpasulia ukweli kuwa aliyeshindwa ni yeye Kikwete
Mkuu heshima mbele sana tu!
Hapa duniani kila mtu ameumbwa na hulka yake ya kuzungumza na kufikisha ujumbe anaotaka ufike kwa mhusika kwa namna yake. Baba Askofu amefikisha ujumbe wake huenda pia ni ujumbe wa Kanisa lake kwa mkuu wa nchi. Haonekani kutumia maneno magumu na makali lakini mwenye akili ameelewa
.
 
Mahali pekee JK akienda anakuwa na wasiwasi na hotuba ni mbele ya Pengo.

JK analijua hili na hawa wengine mh, but huyu kajaribu sana japokuwa kuna kujikomba kiasi fulani.
 
Haha,kesho utasikia chadema wana wapa maneno viongozi wa dini
ili wamwambie raisi

attachment.php
 
Haha,kesho utasikia chadema wana wapa maneno viongozi wa dini
ili wamwambie raisi

attachment.php
Kuna mtu amachanganya habari ya raisi kutembelea mwanza na zito sijajua hii inahusiana vipi jamani tusiwe wavivu wa kipost topic zetu na kudakia za wengine
 
wacha akaoshe macho kidogo! kwani tangu alipokwenda kumuwekea kifua Masha, na akadondoka!hana jinsi mwacheni hana jipya na watanzania wamekwishaelimika juu ya siasa za magamba. Haaha!!!!!!
 
Dawa ya babu nadhani imefanya kazi sidhani kama atapiga zile sarakasi zake tena na mungu amuweke mahali pema huko atakapokufa na wazee wa magamba,,,,maana mwanza hawataki hata kuona pendera ya magamba ikipepea sehemu yoyote ile...
 
Safari ya Rais Kikwete Mkoani Mwanza ni dalili za kupima upepo wa kisiasa kutokana na wimbi la Chama pinzani cha Chadema kuteka Kanda ya Nyanza hivi karibuni.
  • Je atafikiwa kiwango wananchi waliohudhuria Chadema?
  • Je atasambaratisha ngome ya Chadema Mkoani Mwanza?
  • Kuchangia mfuko wa maendeleo jimboni kwa Wenje ni njia ya kujaribu kuwateka wananchi wa Mwanza?
 
Safari ya Rais Kikwete Mkoani Mwanza ni dalili za kupima upepo wa kisiasa kutokana na wimbi la Chama pinzani cha Chadema kuteka Kanda ya Nyanza hivi karibuni.
  • Je atafikiwa kiwango wananchi waliohudhuria Chadema?
  • Je atasambaratisha ngome ya Chadema Mkoani Mwanza?
  • Kuchangia mfuko wa maendeleo jimboni kwa Wenje ni njia ya kujaribu kuwateka wananchi wa Mwanza?


Naomba nirudie tena, jimbo la Wenje linatafutwa kwa udi na uvumba. Infact Mwanza yote inatafutwa so expect a lot of movement kichinichini. Kama Wenje hatobadili thinking yake, na approach ya ubunge wake katika kutatua matatizo ya wapiga kura wake,basi chadema wasahau hili jimbo. Tayari CCM-Kikwete imeshawekeza Tsh 10million kwenye jimbo la Wenje kupitia kwa Zito.
 
Naomba nirudie tena, jimbo la Wenje linatafutwa kwa udi na uvumba. Infact Mwanza yote inatafutwa so expect a lot of movement kichinichini. Kama Wenje hatobadili thinking yake, na approach ya ubunge wake katika kutatua matatizo ya wapiga kura wake,basi chadema wasahau hili jimbo. Tayari CCM-Kikwete imeshawekeza Tsh 10million kwenye jimbo la Wenje kupitia kwa Zito.

Naweza afiki point yako kutokana na Kikwete kutanguliza Sh. Millioni 10 jimboni Kwa Wenje ili kutafuta stahili ya kupokeleka, lakini je amepokeleaje? Tusubiri walioko huko watupe yatokanayo.
 
jk mjanja kweli kweli katanguliza harambee kumbe yy mwenyewe anafuata nyuma , hahahaha
 
Kama CCM bado hiyo hiyo basi labda iwe kwa nguvu za serikali. Wananchi wameshaamua na wako tayari kwa mabadiliko.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom