Rais Kikwete na Waziri Karamagi; wamenunua mgodi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Kwa vile hakuna sheria inayomkataza Rais kufanya biashara akiwa Ikulu au hata kushirikiana na mmoja wa mawaziri wake kuingia ubia wakiwa madarakani kufanya ujasiriamali. Kwa vile mara nyingi habari za biashara za Rais akiwa madarakani hazitoki hadi akitoka madarakani; miye nimeamua kuuliza tu hivi tunapopiga kelele na porojo zetu inawezekana kabisa kuwa Kikwete na Karamagi wameanzisha kakampuni kao ka "B2MPOWERS RESOURCES"? Je, ni tutajuaje kama Rais sasa hivi hafanyi biashara yoyote Ikulu au hajaanzisha ka mradi ka pembeni ka kumuingizia kipato akitumia connection yake na access yake ya information za uwekezaji?

Binafsi naomba tuambiwe tu Rais ana hisa kwenye makampuni ya madini au nishati? na pia Waziri wake ana hisa gani kwenye kampuni gani kwani tunajua yeye ni mfanya biashara? Hivi Barrick Gold inauhusiano wowote wa kibiashara na kampuni za Karamagi?
 
Kwa vile hakuna sheria inayomkataza Rais kufanya biashara akiwa Ikulu au hata kushirikiana na mmoja wa mawaziri wake kuingia ubia wakiwa madarakani kufanya ujasiriamali. Kwa vile mara nyingi habari za biashara za Rais akiwa madarakani hazitoki hadi akitoka madarakani; miye nimeamua kuuliza tu hivi tunapopiga kelele na porojo zetu inawezekana kabisa kuwa Kikwete na Karamagi wameanzisha kakampuni kao ka "B2MPOWERS RESOURCES"? Je, ni tutajuaje kama Rais sasa hivi hafanyi biashara yoyote Ikulu au hajaanzisha ka mradi ka pembeni ka kumuingizia kipato akitumia connection yake na access yake ya information za uwekezaji?

Binafsi naomba tuambiwe tu Rais ana hisa kwenye makampuni ya madini au nishati? na pia Waziri wake ana hisa gani kwenye kampuni gani kwani tunajua yeye ni mfanya biashara? Hivi Barrick Gold inauhusiano wowote wa kibiashara na kampuni za Karamagi?

Wakati mwingine kama huna cha kuandika kuwa msomaji basi....

Ni ushauri tu...
 
Wakati mwingine kama huna cha kuandika kuwa msomaji basi....

Ni ushauri tu...

Na wewe kama huna cha kushauri, kaa kimya.

Kama kuna wenye nyeti za Muungwana kufanya biashara ikulu atumwagie.

Hili swali la Mwanakijiji kama lingeulizwa wakati wa kipindi cha utawala wa Mkapa, pengine angeonekana chizi...japo ukweli tunaujua sasa.
 
Masatu kama huna information mbona unarukia hoja? Acha wenye info waweke mambo wewe soma hadi pale ambapo utakuwa na wasiwasi na msosi. Shambulia hoja.
 
Binafsi sitaki kusubiri hadi 2016 to find out Kwamba rais mpendwa aliyechaguliwa kwa kura nyingi sana amefanya kwa ari, kasi, na guvu mpya biashara akiwa Ikulu. Kama hakuna kilichomzuia Mkapa kitu gani kinamzudia Kikwete?
 
Hii kitu ina nikumbusha habari fulani ikisema hivi the ''Sinclair connection'' samahani kama kumbu kumbu zangu si sahihi.
 
Na pia inatukumbusha kwamba yeye mwenyewe, Kikwete alisema biashara haiwezi alipoulizwa mambo ya Mkapa.

Lakini tunajua sasa pia kwamba 'credibility' yake inaendelea kudidimia. Sio rahisi tena kuamini akisemacho.

Huo utakuwa ni mgodi wa 'Buzwagi?'
 
natumaini waandishi watapata nafasi ya kumuuliza a pointed question kuhusu hili la hisa kuwa yeye kama mwananchi mwingine ana hisa kwenye makampuni gani na kati ya hizo ni zipi zinamfanya awe na haki ya mmiliki? Hata hivyo majibu ya Karamagi ndiyo nina uhakika yatawavutia...
 
labda anafikiria ni jinsi gani anaweza kutetea haki ya Rais Kikwete na Waziri wake kujipatia mgodi kama wakitaka bila mtu yeyote hata kuhoji hadi pale watakapotoka madarakani.
 
wakati fulani nilisikia tetesi kwamba muungwana na white head wanamiliki kampuni fulani kwa hisa na fifte fifte, na kampuni hiyo iliwahi kuwa na hisa katika hoteli moja inayobadili jina lake kila grace period inapoisha. na walikuwa wanapata kifungua kinywa pamoja ktk hoteli hiyo kila ahsubuhi. nilisikia tetesi hizo wakati akiwa hajapata kura nyingi.

naamini wapo wanaojua hili, wakubwa leteni data
 
Yeye alishasema hawezi kufanya biashara baada ya 40 kwa ushauri wa rafiki yake mzungu wa Uingereza
 
Kitila,

Unayaamini maneno ya JK? Asipofanya biashara atakuwa mjasiriamali kama BWM. Maana Mkapa kaonyesha ujasiriamali wake kwa mfano tena wa kuigwa na ndiyo maana anaendelea kuendesha vibanda vyake vya magenge/viosk huku akiendelea kulipwa pensheni na serikali na kulipiwa huduma zote. Sasa sijui huo ujasiriamali wake ni kwa ajili ya nini????
 
Yeye alishasema hawezi kufanya biashara baada ya 40 kwa ushauri wa rafiki yake mzungu wa Uingereza


Yawezekana hilo ndilo jibu lake, lakini tunajua Rais ana hisa wapi ambazo ziko chini ya uangalizi wa mtu mwingine? Je kuna agizo lolote linalozuia mawaziri wake kufanya biashara na makampuni yaliyo chini yao? Kama kwenye halmashauri za miji kuna baadhi ya watendaji wa halmashauri wana vikampuni pembeni ambavyo vinashinda tenda kwenye halmashauri hizo bila ushindani wa maana, kwanini tusiamaini kuwa hilo linawezekana hata ikulu? Kuna ubaya wowote kwa Rais kusema kuwa hana hisa kwenye kampuni yoyote au kutuambia tu kuwa jamani na mimi nina "tuhisa" fulani kwenye kampuni so and so ili kampuni hiyo inaposhinda tenda tujue imeshinda kwa haki na siyo kwa kubebwa.
 
Maswali la nyongeza:
1-Kwa kuwa wakati Karamagi anasaini mkataba wa Buzwagi hotelini London, Rais alikua amefikia hoteli hiyo hiyo, na kwa kuwa Waziri Mkuu aliponusa kuna dili London, akaenda haraka lakini hakufikia hoteli hiyo bali alikwenda tu kusalimia jamaa zake, na kwa kuwa wasaidizi wa rais wamesema kwamba Karamagi hakumjulisha Rais kwa kuwa halazimiki kufanya hivyo, na kwa kuwa wasaidizi wa Waziri Mkuu nao wamesema bosi wao hahusiki kwani hakuna mahali aliposaini, Je, Waheshimiwa wanaweza kutueleza kulikua na MVUTO gani pale London kipindi hicho? Je, Rais na Waziri Mkuu ni nani kati yao anayehusika na Buzwagi? Je, kama Rais na Waziri Mkuu hawahusiki, KARAMAGI ATACHUKULIWA HATUA GANI?
 
kasheshe limeanza upyaaa
mie nasubiri 2010 nimkute mtu ananiibia kura yangu atakiona.... ingawa sina milioni tano za rufaa nitajua pa kushtaki

nina wasiwasi saaana na hiyo kamati ya madini kama itaweza kubadili ule mkataba wa buzwagi maana ule ni mojawapo ya mifano mingi ya mikataba mibovu kuhusu rasilimali nchini. labda pia tuangalie na suala la TRC nani kahusika pale? na kwa nini majibu ya hoja nzito yanajibiwa kwa uwepesi mno? je hii ni kudharau tuhuma au wnajua ujinga wetu utadumu kama fikra za...?
 
Hutu ndugu aliyeanzisha hii hoja nafikiri ni kweli amebore. Kuna critical issues zinazoendelea kuhusu haya mambo na migodi na madini yake ambayo kwa sasa kumhusisha rais Kikwete ni mapema mno. Mzee wa waatu hii ni tume ya pili ameunda; ngoja tusubiri tuone matunda yake. Si vizuri kuanza kumpaka matope wakati tunaona juhudi zake kwenye hili. Ndugu yangu kwa upande wangu bado naona kuwa Kikwete amelivalia njuga jambo hili, na akili yangu bado iko mbali kabisa kumhusisha na mambo ya ku-own migodi.
 
Back
Top Bottom