Rais Kikwete na safari za nje

Itakuwa vizuri tukianza kukusanya data za safari za Mbeki na M7 ili kujua ukweli umelalia wapi. Kwa kumbukumbu zangu za haraka haraka safari za Muungwana haziwezi kabisa kulinganishwa na Mbeki na M7, VDG anajichukulia Gold medal kirahisi kabisa.
 
Siku hizi ninakuwa mtazamaji tu.... ila sijakata tamaa ...
Mkuu hata mimi huwa kuna wakati nashikwa na hasira natamani ningekuwa karibu na viongozi(wezi) hawa ningwazaba vibao.Huyu Membe anafikiri anaongea na mtoto wake wa chekechekea.

Ile Hospitali ya Milembe kazi yake ni nini? kama watu kama Membe hawapewi tiba pale
 
Ana kila sababu ya kutetea utalii wa JK kwa sababu wote huwa pamoja (JK na Membe) kwenye safari hizo.Halafu huyu Chinga asitufanye sie hatuna access na foreign media that anaweza kutughilibu kwamba Museveni na Mbeki wamesafiri mara nyingi zaidi kuliko JK.Naamini safari za Mbeki au Museveni tangu waingie madarakani miaka kadhaa iliyopita hazifui dafu kwa huyu Vasco da Gama wetu.
 
Alafu uyu waziri mi sina ata imani nae akiongea anakuwa serious kama ayaongeayo yana umakini ndani yake kumbe wapi?
Alishawai wapiga bit mabalozi eti wasiingilie siasa za nchi.
Uko nje wanakoenda solicit wawekezaji sisi ni nchi izo izo ambao mabalozi wao wamepigwa bit kutoingilia mambo ya nchi.
Problem ya Tz na Africa kwa ujumla hatuchukulii siasa as a serious discipline yaani kwetu ni blaa blaa tuu.
Ndo maana wasnii wengi wako siasani.
Leo anaongea iki kesho kile as a result ukija jumuisha alivyoongea unakuata vyote vyapingana alafu aliyeongea ni uyo uyo.
Its time to be serious hatuwezi tetea mambo yasiyo na kichwa na miguu.
Alfu JK alikuwa post ya membe kabla ya apo so ilikuwa ni suala la kusettle down na kuwasiliana na hao aliowai kutana nao alipokuwa waziri wa foreign affairs?
Ninachokiona apa ni kufukuziz 10% na kuhakikisha miradi na mines ambazo bado hazijawa expoloited anazifanyia kazi ili akingatuka nae awe mtu ktk watu
Its common sense kwamba ukitaka mkaribisha mgeni wa heshima kwako ni lazima ufanye maandalizi ya nyumba kwanza.
Unaita wawekezaji wakati huo umeme tuu sio relistic,maji ni nightmare,urasimu ni jadi.
Ah basi nsije tukana bure.
 
hao museveni na kibaki hatuna interest nao..hawatuhusu ..anayetuhusu ni jk....

lazima amteteee kwa sababu tunajua ..anaact as a president in the making ..akijua mwaka 2015 anakua rais...hilo tunajua linamsumbua kichwa kila akilala...
 
Hivi Membe ana akili kweli? Uganda na S.A wanaenda kutafuta wawekezaji kwa maana wameshaweka miundombinu sawasawa. Sasa mmungwana mambo ya muhimu kama barabara, maji na umeme yahajakaa vizuri anakimbia kutafuta wawekezaji wa nini? Nani alimwambia kuwa tunahitaji kwenda kuomba wamachinga waje Tanzania? Nenda Kariakoo ndio utajua hakuna wawekezaji kuna wamachinga wa kichina wengi tuu. Muungwana anatakiwa akae kwanza nchini aweke mambo sawa kabla hajaenda kutafuta hao wawekezaji. Hivi hata kwenye madini kuna haja ya kwenda kuwapigia watu magoti?

Kuweka hiyo miundombinu kunahitaji pesa, na hizo pesa zitapatikana kutokana na uwekezaji. Au unazungumzia miundombinu ya aina gani? Kama tungekuwa na uwezo wa kuweka hiyo miundombinu kwa hela yetu wenyewe, wawekezaji tungetafuta wa nini? Tungewekeza wenyewe tu!

Nadhani pia watu wanaokosoa safari za Rais hawajatupa hoja za maana, hawajatoa uthibitisho au ushahidi kuwa safari hizi za rais ni nje au kinyume na majukumu yake. Kulinganisha safari za Kikwete na zile walizofanya Mwinyi, Mkapa na Nyerere ni kukosa mantiki, kwani sababu za kusafiri nje wakati ule zilikuwa tofauti na sababu za kusafiri nje wakati huu. Nyerere alisafiri kwa ajili ya mambo mengi, ikiwemo kufuatilia support ya mapambano ya uhuru kusini mwa Afrika, Angola, Msumbiji etc, kazi hiyo imekwisha na sasa zipo kazi nyingine. Mkapa alisafiri sana mwaka wa mwanzo kufuatilia mambo ya Rwanda na Burundi, sasa hivi hali ni tofauti, nk. Pia safari anazofanya Museveni na Mbeki zina maudhui na uzito tofauti kwa sababu mahitaji yao huko kwao ni tofauti na yetu. Sioni mantiki yoyote ya kulinganisha mambo haya. Hoja hii imekosa mashiko sawa na ile ya wabunge waliokuwa wanadai nyongeza ya mishahara, eti kwa kuwa wenzao wa nchi za jumuiya ya madola wanalipwa zaidi! Ujinga tu! Pia inanikumbusha JKT siku moja kwenye kwata saa nane mchana afande akagundua makuruta wamelegea na wanapiga miayo ovyo, akaanza kuwafokea "Kuruta! Miayo ya nini? Njaa? Hamkula jana?" Hizi ndizo aina za fikra walizo nazo watu wanaopinga kila safari ya rais, ni aina fulani ya fikra butu na kukosa upeo kulikokithiri.
 
Kuweka hiyo miundombinu kunahitaji pesa, na hizo pesa zitapatikana kutokana na uwekezaji. Au unazungumzia miundombinu ya aina gani? Kama tungekuwa na uwezo wa kuweka hiyo miundombinu kwa hela yetu wenyewe, wawekezaji tungetafuta wa nini? Tungewekeza wenyewe tu!

Nadhani pia watu wanaokosoa safari za Rais hawajatupa hoja za maana, hawajatoa uthibitisho au ushahidi kuwa safari hizi za rais ni nje au kinyume na majukumu yake. .

Ah Kithuku!
1. Miundombinu unahitaji uwekezaji? Jamani kitu gani hii?! Hivi kodi zetu zinazokusanywa mabilioni ni za nini? Watu wanafuja tu na kutanua! Zinanunua mashangingi ya serikali na viongozi wake! Miundombinu hatakujengea mtu wa nje, kamwe! ni lazima uendeleze mwenyewe! kama utaomba msaada kama tanroads sawa, lakini ni lazima serikali i-contribute asilimia kadhaa (tena ni significant) ndivyo Mkapa alivyojenga barabara! Huyu Jk anshangaashangaa tu !
2. Eti tunaokosoa hatujatoa uthibitisho au ushahidi kwamba ni kinyume na majukumu ya Jk?! What kind of statement is this? ndiyo hiyo staili mpya eti mafisadi wasituhumiwe, watafutiwe ushahidi! Mmh! Si hivyo ndugu yangu! Rais kwa taarifa yako siyo figure head ni mtendaji mkuu! Kama angekuwa mfalme wa UK sawa, kazi ya ceremonious head ni kutembeatembea na kudumisha uhusiano. Unafikiri December alipoenda kupata tuzo feki ya Sullivan na kutumbuizwa na Boyz 2 Men alienda kunufaisha nchi? Alafu akaacha kwenda huko Portugal for the historic EU-Africa meeting? Ambapo ilikuwa ni PROTOCOL kwa head of states wote kudhuria na marais wote walikuwepo hata Mugabe! Kwani kulikuwa na dili nyingi nzito na mhimu za kimataifa! Eti kaacha safari hiyo ya maana kaenda kusikiliza Boy 2 Men!
Mtetee JK kwa mambo mengine lakini siyo katika safari zake atabaki kuitwa Vasco da Gama. Ungesikia watu wanavyomkejeli mitaani hata wamachinga, ungempa ushauri apunguze safari zake na aanze kushughulikia matatizo ya wananchi wake.
 
For the record.

Not to be defensive about JK and Portugal, but one of the strong characters we have to learn to develop is to be objective.

I remember JK chose to be home for the December 9 Uhuru celebration rather than go to Portugal.Sane minds will understand that given the day's significance, albeit ceremoniusly, to our sovereignity.

He did delegate Membe, didn't he?

I am not one to come to JK's rescue but for the Portugal issue he had a valid reason.

African Union Chairman, will this weekend lead Africa in the much publicised EU-AU Summit in Lisbon, Portugal.

The Summit, which is scheduled for December 8 and 9, will discuss contemporary global issues that affect the two continents and establish the basis for a long-term strategic partnership between Europe and Africa.

From http://www.ghana.gov.gh/ghana/presi..._lead_africa_eu_au_summit_lisbon_portugal.jsp
 
Pundit, you may have had a point if the celebrations were like in 2006, with fireworks and all the funfare! Sasa Uhuru day kulifanyika nini? Mpaka watu walijiuliza what is happening. Alafu in a few days HUYOOOOO kaenda D.C.!
Mi nadhani alijipumzikia tu or whatever, but he was saving his energy for the D.C. bash with Andy Young!
Kama asingekuwepo wakati wa uhuru tungemwona in portugal wote tungeelewa, maana kisingizio cha safari zote si ni kutafuta wawekezaji na wafadhili? this was HISTORIC! please note!
 
Mi niliona watu wa EU kuweka summit kwenye national holiday yetu ilikuwa kama dis fulani.Yaani hawakujali kuangalia calendar za watu kama vile Kikwete insignificant fulani.

Kama kusaini deals siyo lazima Kikwete aende, hatukususia mkutano ndiyo maana Membe alienda.

Ila ma gun slaute and all that jazz ya uhuru hayawezi kupigwa kama mkulu wa kaya hayupo.
 
yet jamaa kwa kuongea pumba kama hizi bado anaitwa waziri wa Tz...duh ndio maana nikasema ni hata bora kibaki ana only matapeli 19 kwake kuliko sie tuko na mijizi mingiii ila there is nothing cha muhimu wana do basi kufanya wameshindwa ndio hata kuongea wanaongea pumba kama hiziiiii??
looooh nadhani hata statement yake akimpa mwanae aisome si alimcheka na kumwambia baba hapo wawa chizi?
au ndi kama alivyosema mmoja kuwa yabidi a support as anamtetea bosi wake and most of the places anazo go mheshimiwa anakua naye???!!!!
 
Membe asilete data za uwongo.

Rais hafanyi kazi ya kutafuta wawekezaji kila kukicha kwa kuzuinguka dunia nzima miaka yote miwli. Ameweka mbalozi wa kumwakilisha katika karibu kila nchi anayotembelea ambao ndio wanatakiwa kufanya jukumu hilo.

Halafu wawekezaji gani anaoleta na kuingia mikataba ya kutuibia madini yetu? Akina Andrew Young na Barrick ndio wawekezaji?
 
You do not attract investment, foreign or otherwise, by flying all over the place. Failure to be seen to be a hands-on CEO does infact scare away intending investors. You attract investment by building a conducive environment. That is done on the ground and not in the air.

People will invest where there are ample and reasonably priced supplies of water and electricity, good communications, transport, skilled workforce, security and good policies.

Kenya attracted a lot more FID than we did during the last five years. Its president hardly traveled. Investors need to see our situation and policies rather that a face. For this, we need a good national website rather than an airborne president.
 
Tino, you have said it all. Does that mean if JK is not flying we Tanzanians are finished ? Is this exactly also planted in JK's brain ?

Anyway shame you VOTERS you needed a young good looking popular PRESIDENT. You will still pay this price up to December 2015.
 
Ana kila sababu ya kutetea utalii wa JK kwa sababu wote huwa pamoja (JK na Membe) kwenye safari hizo.Halafu huyu Chinga asitufanye sie hatuna access na foreign media that anaweza kutughilibu kwamba Museveni na Mbeki wamesafiri mara nyingi zaidi kuliko JK.Naamini safari za Mbeki au Museveni tangu waingie madarakani miaka kadhaa iliyopita hazifui dafu kwa huyu Vasco da Gama wetu.

Kwa hili waandishi wa habari na wamiliki wa redio kama Mwanakijiji wanaweza kutusadia kwa kuwasiliana na balozi za nchi husika ili wajibu haya madai ya Membe kuwa marais wao huwa wanasafiri kuliko JK, kuona kuna ukweli kiasi gani na pengine hizo balozi zingeulizwa tija ya hizo safari ili tuangalia na za JK.
 
People will invest where there are ample and reasonably priced supplies of water and electricity, good communications, transport, skilled workforce, security and good policies.

Wana JF,

Ukisikia kuna mawaziri vilaza kama some other JF members said a few weeks ago Membe is one of them. Kweli a foreign minister of a poor country like Tanzania anawezaje kulinganisha uwezo wa kusafiri wa raisi wa Tanzania na raisi wa Nigeria, Egypt, Sudan, South Africa au hata Kenya!

Kusoma kwake John Hopkins I wish mngedadisi wale walioko DC wakati anasoma ndo mngeweza ku-conclude kuwa si ajabu Membe ku articulate namna hiyo. Hayo niliyo ya nukuu hapo juu toka kwa Ndugu Augustine Membe wetu hawezi kuya articulate wala kuelewa kuwa ndizo basic factors za kujenga uchumi, na eleze wazi ni mwekezaji gani aliyeletwa na raisi kushughulikia hayo ; au Richmond na Buzwagi?

Mwisho namalizia kwa kusema kuwa safari za nje ndiyo mojawapo ya sources ya forex kwa watu kama Membe; proof juzi tu last December kashusha 2007 Nissan Patrol toka DT Dobie worth US$65,000.00 "kwa hela za mshahara na mkopo wa benki" utaambiwa hivyo. Ukweli unauma!
 
Wana JF,

Ukisikia kuna mawaziri vilaza kama some other JF members said a few weeks ago Membe is one of them. Kweli a foreign minister of a poor country like Tanzania anawezaje kulinganisha uwezo wa kusafiri wa raisi wa Tanzania na raisi wa Nigeria, Egypt, Sudan, South Africa au hata Kenya!

Kusoma kwake John Hopkins I wish mngedadisi wale walioko DC wakati anasoma ndo mngeweza ku-conclude kuwa si ajabu Membe ku articulate namna hiyo. Hayo niliyo ya nukuu hapo juu toka kwa Ndugu Augustine Membe wetu hawezi kuya articulate wala kuelewa kuwa ndizo basic factors za kujenga uchumi, na eleze wazi ni mwekezaji gani aliyeletwa na raisi kushughulikia hayo ; au Richmond na Buzwagi?

Mwisho namalizia kwa kusema kuwa safari za nje ndiyo mojawapo ya sources ya forex kwa watu kama Membe; proof juzi tu last December kashusha 2007 Nissan Patrol toka DT Dobie worth US$65,000.00 "kwa hela za mshahara na mkopo wa benki" utaambiwa hivyo. Ukweli unauma!

Mhh,

hii ya nissan Patrol ni kali. Watetezi wa ufisadi watakuambia kuwa hizo ni pesa zake binafsi ametumia!
 
Back
Top Bottom