Rais Kikwete na mazungumzo na ujumbe wa CHADEMA




  • Wakutana uso kwa uso Ikulu
  • Mjadala mzito, waahirishwa mpaka leo


Kulwa Karedia na Maregesi Paul

"

Nilitamani sana kuwaeleza kilichojadiliwa, lakini nashindwa kuwaambia kwa sababu mazungumzo hayakumalizika, kwa hiyo tutatoa taarifa kamiliki baada ya mazungumzo kumalizika,
"Kwa kifupi tu ni kwamba tulikutana na Rais, mawaziri na wasaidizi wake saa 9:30 mchana Ikulu mpaka saa 12 jioni, kikao kilipoahirishwa.

"Tumefanikiwa kumweleza Rais hoja zetu zote ambazo tulizokuwa nazo, miongoni mwa hoja hizo ni nini kilichosababisha wabunge wa Chadema kususia mjadala wa Katiba mpya katika kikao cha Bunge kilichomalizika wiki iliyopita,"Hoja nyingine tumemtaka Rais asisaini Muswada huo kabla ya Desemba Mosi kama alivyokuwa ameahidi wakati akizungumza na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam,
"Tumeona kama akisaini Muswada huo, ni wazi utaligawa taifa kwa sababu kuna baadhi ya watu wanadai haukufuata taratibu zilizokuwa zinahitajika.

"Baada kutoa hoja zetu, tumemwachia Rais na wasaidizi wake, wakazijadili na tutapoonana kesho (leo), watatupa majibu na majadala utaendelea zaidi,"kilisema chanzo chetu.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, mawaziri waliohudhuria ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Steven Wasira,Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Mathias Chikawe na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Emannuel Nchimbi.


Kwa upande wa Chadema, waliongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.

Mbowe pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na ni Mbunge wa Hai.
Wengine ni Makamu Mwenyekiti Bara, Said Amour Arfi, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, Said Issa Mohamed, Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Mbali na hao, waliokuwapo Mbunge wa Ubungo, John Mnyika ambaye pia ni Katibu wa Wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Halmashauri na Bunge, John Mrema na makada wa chama hicho, Profesa Abdallah Safari na Profesa Mwesiga Baregu.


Kikao hicho, kimefuatia ombi la Chadema kutaka kuonana na Rais Kikwete ili kumueleza kasoro zilizopo kwenye Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba, ambao yatari umepitishwa na Bunge na sasa unasubiri kusainiwa na Rais ili kuwa sheria.


Itakumbukwa wakati wa majadala wa Muswada huo, wabunge wa Chadema na wale wa Chama cha NCCR-Mageuzi, walisusia na kutoka nje ya ukumbi wa Bunge, kwa madai kuwa hawakutendewa haki.


Wakati huo huo, Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ilitoa taarifa kwa vyombo vya habari ikisema Rais Jakaya Kikwete na ujumbe wa Serikali walikutana na ujumbe wa CHADEMA na kufanya mazungunzo Ikulu.


Taarifa hiyo ilisema kuwa, mazungumzo hayo yalifanyika katika mazingira ya urafiki na kwa ujumbe wa CHADEMA kuwasilisha mapendekezo kuhusu mchakato wa Katiba mpya ya Tanzania.


"Serikali imepokea mapendekezo hayo, hata hivyo, pande zote mbili zimekubaliana kukutana tena asubuhi ya kesho (leo), ili kuipa nafasi Serikali iweze kutafakari mapendekezo hayo.


"Lakini, pande hizo mbili zimekubaliana kuwa, Katiba ya sasa ni Katiba nzuri iliyolilea taifa kwa miaka 50 iliyopita kwa sababu ni Katiba ya sasa iliyoliwezesha Taifa la Tanzania kuwa na amani, utulivu na kupata maendeleo makubwa ambayo nchi yetu imepata mpaka sasa.


"Pia pande zote mbili zimekubaliana kuhusu umuhimu wa kutunga Katiba mpya kama Rais Kikwete alivyoliahidi taifa wakati wa salamu zake za mwaka mpya Desemba 31, mwaka jana, Katiba ambayo italiongoza Taifa la Tanzania kwa miaka mingine 50 ijayo.



"Katika mazungumzo hayo, Rais aliwahakikishia wajumbe hao wa CHADEMA ambao waliongozwa na Mwenyekiti wao Mbowe kuwa ni dhamira yake na ya Serikali kuhakikisha Tanzania inapata Katiba mpya.

"Katika mkutano huo, pande zote mbili zimekubaliana kuwa, ni jambo muhimu sana kwa mchakato mzima wa kutungwa kwa Katiba mpya kuendeshwa kwa namna ya kulinda na kudumisha tunu za taifa za amani, utulivu na umoja wa kitaifa.


"Aidha, pande zote mbili zimekubaliana kuwa, mchakato huo uendeshwe kwa kuzingatia misingi ya mambo mengine muhimu kwa Taifa la Tanzania kama vile kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani, kuligawa taifa kwa misingi ya udini na ukabila ama kutugawa kwa misingi ya maeneo," ilisema taarifa hiyo.



 
Jamani hebu nijuzeni what is going on huko white house hii leo, waheshimiwa wameshapewa juice?
 
Nilitamani sana kuwaeleza kilichojadiliwa, lakini nashindwa kuwaambia kwa sababu mazungumzo hayakumalizika, kwa hiyo tutatoa taarifa kamiliki baada ya mazungumzo kumalizika
Mbona Ikulu walitoa taarifa?Tena wakasema walikubaliana kuwa hii ya sasa pia ni nzuri?
 
Jamani hebu nijuzeni what is going on huko white house hii leo, waheshimiwa wameshapewa juice?

Daah kaka unajua tunalipia internet wengine sasa kitendo cha kufungua hii thread umekula bytes zangu za bure, anyway nakusamehe bure
 
Twende taratibu Pasco, unaanza kuharibu hali ya hewa hapa. Mpaka sasa wafuasi wa CDM hawaelewi kinachoendelea.

Sio kweli mkuu'shida yenu mnapenda ku undermine ukweli'mimi kama chadema najua chama changu kinataka kutafuta amani ili tupate katiba nzuri
 
[h=3]KURUGENZI NA MEYA JIJI LA MBEYA KUCHUKULIWA HATUA KISA, KUWA VINARA WA VURUGU ZA MWANJELWA NA KUMSINGIZIA KANDORO [/h]
MKUU WA MKOA WA MBEYA ABBAS KANDORO

* N i kutokana na kupimana nguvu za maamuzi

Na, Gordon Kalulunga, Mbeya

MAASKOFU,Wachungaji na wanataaluma mkoani Mbeya wametoa tamko la kumtaka Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, kuwachukulia hatua za kinidhamu Meya wa Jiji la Mbeya, Athanas Kapunga na Mkurugenzi wa Jiji hilo Juma Idd kutokana na kuwa chanzo cha vurugu zilizotokea jijini hapa hivi karibuni


Tamko hilo limetolewa leo katika Kongamano la kujenga mkakati wa maendeleo ya Mkoa wa Mbeya ambalo liilifanyika katika ukumbi wa Kanisa la Winners lililopo jijini hapa kutoka makanisa yote yaliyopo mkoani Mbeya ambalo Mkuu wa Mkoa alikuwa mgeni rasmi.

Mchungaji William Mwamalange, ambaye pia ni Mkurugenizi wa taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya kuhifadhi Mazingira mkoani Mbeya (MRECA) alisema maaskofu na wachungaji wanasikitishwa na vurugu zilizotokea eneo la Mwanjelwa Jijini Mbeya na kwamba hata Meya na Mkurugenzi wa Jiji wachukuliwe hatua za kinidhami kutokana na kuwa chanzo cha vurugu hizo.

Alisema ''Vurugu zilizotokea haikuwa ni siasa bali ni maamuzi mabaya yaliyofanywa na viongozi waAndamizi wa Jiji la Mbeya katika kushughulikia tatizo la wamachinga wanaouza bidhaa zao eneo la Mwanjelwa''

“Tukiwa na uongozi wa uongo jiji halitasonga mbele kimaendeleo, vurugu zilizotokea kimsingi pale siyo siasa bali ni maamuzi mabaya ya baadhi ya watu, “alisema Mwamalange huku akishangiliwa na mamia ya viongozi wa dini walioshiriki kongamano hilo.

Alisema maaskofu na wachungaji wanasikitishwa na kitendo cha baadhi ya watu kumsingizia Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Kandoro kwamba yeye alikuwa ndiye chanzo cha vurugu hizo wakati siku ya tukio alikuwa katika ziara wilayani Mbozi kukagua miradi ya maendeleo.

Mchungaji Mwamalange alisema kimsingi viongozi wa Jiji la Mbeya hasa Meya na Mkurugenzi hawawezi wakakwepa katika suala la vurugu za Mwanjelwa kwasababu walikiwa na nafasi ya kuzungumza na wamachinga kwa utaratibu ambao usingezua vurugu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro alisema anashangaa na baadhi ya watu wanaomsingizia kwamba alishiriki kuchochea vurugu za wamachinga wakati siku vurugu zinatokea alikuwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo wilayani Mbozi na kwamba Serikali inawatambua wamachinga kama sehemu ya jamii na haiko tayari kukaa nao mbali na katika soko linalojengwa Mwamnjelwa watapata nafasi.

Kandoro alisema tangu ateuliwa hajawahi kumwagiza mtu au kiongozi yeyote wa Jiji la Mbeya achukue hatua yeyote dhidi ya wamachinga na kusababisha kutokea vurugu.
“Sijawahi kumwagiza mtu achukue hatua yeyote iliyosababisha vurugu na kimsingi sina sababu maana kwanza ilikuwa ni mapema mno kuchukua maamuzi hayo maana sisi wageni unapofika katika mkoa unahitaji kwanza kusoma mkoa na siyo ghafla unaanza kuchukua hatua,”alisema Kandoro

Kandoro alisema hata hivyo Halmashauri ya Jiji la Mbeya ipo katika mpango wa kuweka utaratibu mzuri wa kuwafanya wamachinga kufanya biashara zao.

Aliongeza kuwa kinachotakiwa ni kuwajengea mazingira wamachinga kufanya biashara zao na pia kufufua viwanda vilivyosimama uzalishaji ili waweze kupata ajira katika viwanda hivyo.

Tamko hilo limekuja wiki moja tu tangu Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya kilipotoa tamko la kuchukua maamuzi magumu ya kuwachukulia hatua kali za kinidhamu viongozi wandamizi na watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya walioshindwa kutimiza wajibu wao na kupelekea kutokea kwa vurugu zilizozua mapambana kati ya wamachinga na polisi jijini hapa.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya, Nawab Mullah alitoa tamho hilo tamko hilo kwa kusema kuwa CCM haiwezi kuacha viongozi wachache ndani ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya wawe chanzo cha vurugu hizo na kusababisha kuvunjia kwa amani kwa maslahi yao binafsi na kupelekea wananchi kuilaumu serikali ya CCM.


“Kutokana na vurugu za Mwanjelwa CCM baada ya kutafakari kwa kina suala hili na kufanya utafiti wake wa jinsi vurugu zilivyokea na wananchi wa ndani na nje ya mkoa wanavyolizungumzia kimeazimia kuchukua hatu kali kwa viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya walioshinda kutimiza wajibu wao,”alisema Mullah katika tamko hilo.

Mullah alisema CCM ni chama makini ambacho kinawajali na kuwapenda wananchi wake kwa hiyo italazimika kuchukua maamuzi hayo magumu kwa kuhakikisha wale wote wanaoharibu sifa ya Jiji la Mbeya wanaondolewa ili kurejesha imani ya wananchi kwa jiji na serikali ya CCM.


Alisema wananchi lazima watambue kuwa vurugu ni kama mvua zinanyesha na kuleta mafuriko ambayo huleta madhara makubwa kwa kusomba kila kitu ambapo nchi kadhaa za Afrika zikiwemo Libya,Misri na Somalia zimeingia katika machafuko ya vita ambayo chanzo chake ni baadhi ya vyama vya siasa kutaka madaraka kwa nguvu kwa kuwashinikiza wananchi kufanya maandamano na vurugu.


Mullah alisema kwa kuwa CCM na serikali yake vipo makini kitaendelea kudumisha amani ya nchi hasa kwa kutambua kuwa hakuna nchi dunia iliyofanikiwa kujenga amani kwa kuvurugu hivyo wanaokuwa chanzo cha kutaka kuvunjika kwa amani watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Vurugu hizo za wamachinga waliokuwa wakipinga kuhamishwa maneeo yao ya kufanyiwa biashara zilianza tangu Novemba 11 mwaka huu na kudumu kwa takribani siku tatu zilisababisha kifo cha mtu mmoja, watu 17 kujeruhiwa kati yao watano kwa kupigwa risasi za moto ambapo polisi walifanikiwa kuwatia mbaroni watu zaidi ya 300 wanaosadikika kushiriki katika vurugu hizo.


Hata hivyo wamachinga hao walisitisha mapambano hayo ambayo pia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) lililazimika kuingilia kati baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi kuwasili mjini hapa akitokea mkoani Dodoma ambako alikuwa akihudhuria vikao vya bunge na kuwaomba kusitisha vurugu ambapo walimsikiliza na kuacha kuendelea na vurugu.







 
[h=3]SERIKALI MBARALI YAMTEGA KANDORO NA USALAMA WA TAIFA [/h]
MKUU WA MKOA WA MBEYA ABBAS KANDORO

OFISI ya Mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya imempa kazi nzito ya kutatua migogoro Mkuu wa mkoa Abbas Kandoro na idara ya usalama wa Taifa ikihofia kusutwa na wananchi wakiwemo wananchi wa kijiji cha Isunura, imebainika.


Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa ofisi hiyo imekuwa ikipelekewa malalamiko na wananchi juu ya utendaji mbovu wa viongozi wake lakini haitaki kuchukua hatua zozote mpaka imefikia hatua wananchi kuanza kujichukulia hatua mikononi kudhibiti viongozi wabadhilifu wa mali za umma.

Wakizungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki, wananchi wa kijiji cha Isunura chini ya baraza la wazee wa kijiji hicho walisema kuwa kwa sasa kijiji chao hakina uongozi wa Serikali ya Kijiji jambo ambalo limesababishwa na ofisi hiyo ya Mkurugenzi wa wilaya ya Mbarali.

Mwenyekiti wa baraza hilo Chifu Victory Mpalile alisema kuwa, kijiji hicho kimekuwa kikiyumbishwa mara kadhaa na ofisi ya Mkurugenzi hali ambayo imekuwa ikizorotesha maendeleo ambapo mpaka sasa zaidi ya miezi kumi hakuna shughuli zozote zinazoendelea kutokana na Serikali kutoweza kutoa maamuzi yaliyo wazi ya kijiji hicho kuwa katika kata ipi kati ya kata ya Igava na Mawindi.

''Wialaya hii rushwa imezidi na wananchi wanapodai haki tunaonekana ni wakorofi kwasababu hatukubaliani na mambo yao ya kutuburuza na kutokana na hilo mpaka sasa hatuna uongozi wa Serikali ya kijiji kwasababu hawa waliokuwepo wamevuliwa uongozi kutokana na vitendo vyao vya rushwa'' alisema Chifu Mpalile.

Alisema Novemba 20, mwaka huu, wananchi wa kijiji hicho baada ya kuiandikia ofisi ya Mkurugenzi barua na mihutasari tangu mwanzoni mwa mwaka huu juu ya malalamiko ya kutokuwa na imani na Ofisa mtendaji na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Silivyo Mbishila na kupuuzwa waliamua kuchukua funguo za ofisi na mihuri ya Kijiji hicho chini ya uangalizi wa Jeshi la Polisi.

''Tulipochukua mihuri hiyo tukawaambia Polisi waliokuwa wamekuja kuwa tunawahitaji Mkuu wa wilaya au Mkurugenzi lakini mpaka sasa wameshindwa kuja kutokana na kutambua makosa yao ya kuwalinda watendaji hawa mafisadi'' alisema Mpalile.

Sanjari na hayo alimuomba Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro na idara ya usalama wa Taifa kufika kijijini hapo na kuwasikiliza kilio chao ili pia waunde serikali ya muda kwa ajili ya huduma za kijamii za Kijiji hicho.

Kwa upande wake Katibu wa baraza hilo la wazee Vitus Mbishila alisema kuwa kilichowapelekea wananchi hao kuchukua mihuri kwa maandamano kutoka kwa ofisa mtendaji na Mwenyekiti wake ni kutokana na kuwepo mazingira ya kuuza ardhi yao zaidi ya kilomita 3.
''Unajua tuliamua kuchukua mihuri hiyo kwasababu viongozi hawa walitaka kuuza ardhi kwa wafugaji wa Kijiji cha Ikanutwa Novemba 21, mwaka huu hivyo tungechelewa tungeuzwa lakini viongozi wilayani hawalioni hili'' alisema Mbishila.

Mwenyekiti wa wafugaji wa Kijiji hicho Nicorous Kikwembe alisema kuwa kabla ya suala hilo, baadhi ya wafugaji walikamatwa katika kijiji hicho na kupelekwa mahakamani lakini kutokana na Mwenyekiti huyo kutokuwa mwaminifu alienda kuwa shahidi wa wafugaji hao hatimaye wafugaji wakashinda kesi.

Kwa upande wao Josephine Mdimilage ambaye ni Mwenyekiti wa kitongoji cha Luvalanda, Bibi kizee Ashura Nguluva (90) walisema kuwa eneo hilo lililotaka kuuzwa na viongozi hao lina hati miliki ya mawe na hata wilaya pia wanalijua hilo.

Aidha mbali na hilo waliiomba Serikali kufanya hima kutatua matatizo baina ya hicho na Serikali ya wilaya hiyo kwasababu kutokana na Serikali kukisusa kijiji hicho imefikia wanawake wajawazito kukosa hata huduma za kliniki katika zahanati iliyopo Kijijini hapo ambapo hulazimika kutembea zaidi ya kilomita Nane mpaka eneo la Rujewa.


Juhudi za kumpata Mkurugenzi mtendaji wa wilaya hiyo George Kagomba ziligonga mwamba baada ya kufika ofisini kwake na kuelezwa na katibu muhtasi wake kuwa alikuwa nje ya ofisi.


 
Haya tena wandugu vikao vya mwafaka kati ya ccm & CDM ndo vishaanza jana na leo kitaendelea tena. Nijuavyo vikao vya miafaka haviishi siku moja vitaanza kupangiwa tarehe hapo.

Kwani CHADEMA wametoa mapendekezo yao jana leo watapewa majibu na mapendekezo ya ccm na wataambiwa waende kuyatafakari na watapangiwa muda wa kurudi tena siajabu miezi 3 ijayo vikao hadi 2015 inaingia. Hata CUF walianza hivyo hivyo mwisho wakawa wabia wa ccm.

CHADEMA washaanza sasa tusubiri tupate mwafaka mwingine wa ccm/cdm ambao vikao vimeanza na utafikiwa ikaribiapo 2015 [angalizo CDM Kuwa macho]

Ama kweli kukutana huku kwa Rais na kundi fulani la wananchi wake kutaitwa kila aina ya Jina. Nijuavyo mimi huu si muafaka wa vyama vya siasa ambao mara nyingi hufanywa na watendaji wakuu wa vyama hivyo kutoa tofauti zao hasa pale kunapokuwa na mgogoro wa kisiasa, watu hawasalimiani, watu hawazikani na wakati mwingine hata kutupiana vinyesi kama ilivyokuwa Zanzibar. Lengo kuu ni kuwafanya wananchi hawa wenye itikadi tofauti waishi pamoja.

Katika mazungumzo haya simuoni Dr Slaa wala Mukama ambao ni watendaji wakuu wa vyama vyao, sasa muafaka huu utaingiwaje bila ya watendaji kuwepo?. CHADEMA wanaonana na rais wa nchi kufikisha ujumbe wao na rais halazimiki kuukubali ila tu pale atakapoona kuwa sasa anahitaji kuongoza nchi na hivyo ni busara kuongoza Katiba ya kitaifa siyo ya kiitikadi za vyama.

Vyovyote tutakavyo spin, huu si muafaka ambao kwa kawaida mwisho wa siku huhitaji kutiliana saini na sherehe, huku ni kufanya kazi pamoja kwa ajili ya mustakabali wa Taifa.

Nice try Kivia but we got you
 
Strategies za CDM nazikubali!!! Hapa CDM kuna kitu wanataka kufanya,bila shaka wameamua kumpa changamoto J.K. na kujua msimamo wake kabla ya kuamsha nguvu ya umma.Viva CDM songeni mbele.PAMOJA TUNAJENGA NCHI.
 
Back
Top Bottom