Rais kikwete mlezi wa mafisadi?

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,138
Nimewwiwa kusema haya baada ya kusoma gazeti moja la mwanahalisi, hii imenifanya kuona kumb e hata zile kesi pale mahakamani yawezeknaa watu wameonewa ama ni mchanga wa macho.

CCM imeunda kamati amabayo imekuwa ikisaini mshiko kila siku tena kwa pesa za kodi ya wananchi;matokeo yake mzee mwinyi akaamua kutoa maoni yake nini cha kufanya ni kuwaondoa hawa mafisadi

Leo hii rais anathubutu kuwaita wakina mwinyi kama watoto wadogo na kuwaambia nendeni mkamalizane nao hao mafisadi muda wa uchaguzi huu.

Akiambiwa pesa za EPA ndizo zimemuingiza madarakani hataki kuamini sasa hawa mafisadi anaowapeleka mahakamani anamaana gani?

Huyu rais kwangu ndie kinara wa mafisadi naamini hii vita ni ngumu kama huyu bwana akiwa madarakani;lolote watanaznia tusimwamini kabisa maisha yake yako mikononi mwa mafisadi hakuna haja ya kumsaidia hata kimawazo nilihisi ata tukiandika nini cha kufanya kuhusu mafisadi anaweza kusaidika lakni kwa style hii never

KILA LA KHERI JK
 
BAHATI MBAYA UMEKAWIA KUTAMBUA sanaa za JK nz wenzake pale jumba jeupe na kesi zao.

Nakwambia hakuna wakumfunga paka kengele, chama kizima wote ni manyang'au, wamepungukiwa utukufu wa bwana, wanahitaji toba.

na kwataarifa yako hakuna wakutubu pale, ni lazima tuwalazimishe, tuwang'oe madarakani.
 
Ungeweza kuiweka hiyo habari ya Mwanahalisi hapa ingekuwa vyema. Hata hivyo, kama Lowasa, Rostam, Karamagi ni watu wake wa karibu unategemea nini? Huwezi ukawa na marafiki wezi, wewe ukawa si mwizi, naturally utawakwepa ukigundua ni wezi.
 
mzinzi awezi kumlinda mzinzi mwenzake hata siku moja
kazi ipo
nchi imevamiwa
 
Nimewwiwa kusema haya baada ya kusoma gazeti moja la mwanahalisi, hii imenifanya kuona kumb e hata zile kesi pale mahakamani yawezeknaa watu wameonewa ama ni mchanga wa macho.

CCM imeunda kamati amabayo imekuwa ikisaini mshiko kila siku tena kwa pesa za kodi ya wananchi;matokeo yake mzee mwinyi akaamua kutoa maoni yake nini cha kufanya ni kuwaondoa hawa mafisadi

Leo hii rais anathubutu kuwaita wakina mwinyi kama watoto wadogo na kuwaambia nendeni mkamalizane nao hao mafisadi muda wa uchaguzi huu.

Akiambiwa pesa za EPA ndizo zimemuingiza madarakani hataki kuamini sasa hawa mafisadi anaowapeleka mahakamani anamaana gani?

Huyu rais kwangu ndie kinara wa mafisadi naamini hii vita ni ngumu kama huyu bwana akiwa madarakani;lolote watanaznia tusimwamini kabisa maisha yake yako mikononi mwa mafisadi hakuna haja ya kumsaidia hata kimawazo nilihisi ata tukiandika nini cha kufanya kuhusu mafisadi anaweza kusaidika lakni kwa style hii never
KILA LA KHERI JK


Umechelewa sana kumgutukia, lakini upo absolutely right. Yeye ndiye rais, serikali ni yake. Yeye ni mwenyekiti wa chama chake cha CCM. Wananchi tumempa capital yote katika uchaguzi, kuna la ziada???? Wezi mafisadi wamejihifadhi humo humo ndani ya chama chake, wanaendelea kukamata madaraka waliyonayo kupitia chama chake, na yeye bado kawang'ang'ania tu wala haoni uvundo, kwa hakika sio mjinga huyu wa kutoyaona hayo, anafanya makusudi, kama mkweli huyu basi angalau angewafukuza/angewakurupusha kutoka kwenye maficho ya kwapa/chama chake CCM, halafu tukaona kama vyombo husika visifanye kazi zake.

Na visifanye kazi zake kwanini??? Hakuna chombo kisichokuwa chini ya wizara na mawaziri wa serikali yake, aliyowateua yeye mwenyewe.

Kweli mtu anaetuhumiwa kwa wizi/ufisadi wa Billioni 133, yaani 133,000,000,000/= milioni laki moja na halafu bado kabakia katika chama chako??? na kupitia chama chako anaendelea kuwa mbunge??? na bado anaongezewa vyeo??? uvundo wa kiasi cha najisi hasa, karaha hata kufikiria.
 
mzinzi awezi kumlinda mzinzi mwenzake hata siku moja
kazi ipo
nchi imevamiwa

Jakaya ndio fisadi namba moja; hawa wakina Lowassa, rostam, Karamagi na Chenge wasingekuwa wanatamba kama huyu bwana hakuwa nao. Katika kuonesha solidarity na hawa mafisadi ndio maana katika hafla nyingi za serikali hata juzi wakati wa sherehe za mapinduzi Zenj, Lowassa alikuwa mbele mbele beneti na Jakaya!! Waswahili husema KUNGURU HAWEZI KURUKA NA NJIWA LAZIMA ARUKE NA KUNGURU WENZIE!! Kikwete, Lowassa, Rostam, Chenge na Karamagi wote kabila ya FISADI!!
 
Ni wapiga kura ndio watakoamua kama tatizo la ufisadi ni kubwa kiasi gani,jambo ambalo REDET wangeweza kuwauliza wananchi kwa kufanya poll. Je,wananchi wanaliona tatizo la ufisadi ni tatizo kubwa kiasi gani? Inawezekana wapiga kura wakaitosa CCM,kwa sababu ya ufisadi,au wakaitosa CCM ikimweka Kikwete kugombea? Je kuna wananchi ambao hawaamua watampgiai kura nani,isipokuwa wameshaamua kwamba hawampigia kura Kikwete?
Kama wananchi wanaona hitilafu katika Serikali ya sasa,je wana imani kwamba mabadiliko ya uongozi yanaweza kuleta Serikali bora zaidi?
 
Back
Top Bottom