Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
Rais Jakaya Mrisho Kikwete atakuwa mgeni rasmi wa Tamasha la Pasaka litakalofanyika Aprili 24 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tamasha hilo ambae ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mshama Promotions, Alex Msama aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Rais amethibitisha kubariki tamasha hilo.
Napenda kuwaambia kwamba Rais wetu mpendwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete amethibitisha kuwa mgeni rasmi katika tamasha letu mwaka huu.
Amekubali kushirikiana na Wakristo wote kusherehekea Sikukuu ya Pasaka Diamond Jubilee, alisema Msama aliyeambatana na mshauri wa kamati ya maandalizi, Askofu Rashid Matigisa, Askofu Philemon. Wainjilisti John Benjamin na Elia Mashaka pamoj na Shemasi Benjamin.
Mshama alisema kwa niaba ya Kamati namshukuru Rais kwa kukubali mualiko wa kuhudhulia Tamasha hilo, wasanii mbalimbali wa muziki wa injili wamethibitisha kushiriki ni pamoja na Rose Muhando. Anastazia kutoka kenya.
Mwananchi march 14, 2011
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tamasha hilo ambae ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mshama Promotions, Alex Msama aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Rais amethibitisha kubariki tamasha hilo.
Napenda kuwaambia kwamba Rais wetu mpendwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete amethibitisha kuwa mgeni rasmi katika tamasha letu mwaka huu.
Amekubali kushirikiana na Wakristo wote kusherehekea Sikukuu ya Pasaka Diamond Jubilee, alisema Msama aliyeambatana na mshauri wa kamati ya maandalizi, Askofu Rashid Matigisa, Askofu Philemon. Wainjilisti John Benjamin na Elia Mashaka pamoj na Shemasi Benjamin.
Mshama alisema kwa niaba ya Kamati namshukuru Rais kwa kukubali mualiko wa kuhudhulia Tamasha hilo, wasanii mbalimbali wa muziki wa injili wamethibitisha kushiriki ni pamoja na Rose Muhando. Anastazia kutoka kenya.
Mwananchi march 14, 2011