Rais Kikwete, mbegu uliyoipanda italitafuna taifa letu...

Actually, nimekataa jambo la mwanachma wa cdm kuongelea au kupalilia udini. nasema mtu siyo mwanachma. Kama Quality ni mwanachama wa CDM akaongelea udini, isichululiwe kuwa qulity ameongelea kwa vile ni mwanachma bali kwa vile ni quality as an individual. sababu ukimchukua kama mwanachma wa cdm unakosea maana anaweza kuwa pia mwanachama katika vikundi vingi eg mwanachma wa chama cha madaktari; mwanachma wa chama cha kuweka na kukopa n.k

I advise you to deal with issues not CDM or its members as they are members of various religiond.
Labda nikuulize hili - CHAMA ni nni? chama kinajengwa na kina nani kama sio watu? Hivi unafikiri CUF ilitokea tu kuwa chama cha Waislaam na Wazanzibar pasipo wanachama wake kuumeza mtalimbo wa CCM kueneza hisia za Udini.. Leo hii wako wapi? hata Huyo Lipumba anashndwa kujitetea maana tayari wanachama wake wamesha aminishwa kuwa CUF inatetea maslahi ya Waislaam, hivyo QUALITY anapotetea maslahi ya Wakristu na mwingine akayakubaliyakafikia kukubaliwa na wanachama walio wengi unafikiri chama hicho kitaelekea wapi?..

Mkuu wangu mwanachama wa Madaktari au mikopo hawezi kuzungumzia SIASA pasipo kuwa mtazamo wake na tutampima tu kama ni mwanachama wa chama gani na sio profession yake. You can't advise me in defence of your engagement in religious matters. Mwanaume anapozungumzia swala ya jinsia na kuusifia Mfumo dume haijalishi yeye ni Daktari au mwanasesele isipokuwa hatari ya maneno yake inaweza vipi kuwaathiri wanaume wote hasa pale anapoungwa mkono..
 
Chama ni wanachama lakini si kila mtu anafanya kwa niaba ya wanachama wote. na nakuthibitishia kuwa hakuna mwanachama yeyote akifanya jambo anawakirisha wanachama wengine. Kila mmoja anakuwa judged kwa nafasi yake, kwa kosa lake, na kwa mtizamo wake. mimi ninapoona Ponda anaongoza baadhi ya watu kuvamia viwanja na kusema anakomboa mali za waislamu, kesho Bakwata wanainuka na kusema wanalaani vitenddo vya ponda; siwezi nikakaa na kusema uislamu ni mbaya... Nitasema Ponda ana tatizo na si uislamu.

Kwa taarifa yako mimi ni Christiani, saved one. Baada ya makanisa kuchomwa, niliongea na mashekhe kama watano kuhusu mtizamo wao wa kuchomwa makanisa na walisema "tumeishi na wakristo kwa miaka mingi, hatujui haya yanatoka wapi" kwa hiyo matatizo utakayo yafanya wewe Binafsi kama Mkandala, usidha ni tutayaelekeza kwa uislamu au waislamu au CCM yatakuwa yako mwenyewe.

All the best
 
Chama ni wanachama lakini si kila mtu anafanya kwa niaba ya wanachama wote. na nakuthibitishia kuwa hakuna mwanachama yeyote akifanya jambo anawakirisha wanachama wengine. Kila mmoja anakuwa judged kwa nafasi yake, kwa kosa lake, na kwa mtizamo wake. mimi ninapoona Ponda anaongoza baadhi ya watu kuvamia viwanja na kusema anakomboa mali za waislamu, kesho Bakwata wanainuka na kusema wanalaani vitenddo vya ponda; siwezi nikakaa na kusema uislamu ni mbaya... Nitasema Ponda ana tatizo na si uislamu.

Kwa taarifa yako mimi ni Christiani, saved one. Baada ya makanisa kuchomwa, niliongea na mashekhe kama watano kuhusu mtizamo wao wa kuchomwa makanisa na walisema "tumeishi na wakristo kwa miaka mingi, hatujui haya yanatoka wapi" kwa hiyo matatizo utakayo yafanya wewe Binafsi kama Mkandala, usidha ni tutayaelekeza kwa uislamu au waislamu au CCM yatakuwa yako mwenyewe.

All the best
Mkuu wangu mbona unajikanyaga. Sheikh Ponda sio mwanachama wa Bakwata kama angekuwa na akasema hayo mnayomshirikisha nayo ingeeleweka baraza la waislaam lina msimamo gani ktk swala hilo. Na Hata hivyo Bakwata sio balozi wa Waislaam wote kama ilivyo Chadema kwa Watanzania wote, hivyo kinachosemwa na mwanachama wa Bwakata kuhusu Sheikh Ponda itachukuliwa Bakatwa inampinga Sheikh Ponda kama Chadema inavyompinga JK na CCM, na huwa ndio msimamo wa chama hata kama kasema mbunge asokuwa kiongozi au mwanachama hai na akaungwa mkono na wanachama.

Tatizo hapa ni wanachama wa Chadema kuendelea kuunga mkono maswala yanayowatenga Waislaam kama walivyokuwa wakianza CUFbaada ya uchaguzi wa mwaka 2000. Kwanza ilikuwa agenda ya CCM halafu watu wakaamini na chama kikajikuta kina wanachama wengi wanaoamini ktk Udini na fikra za kujikomboa wao toka utawala wa kikristu. Lipumba na wengine wakawa hawana pa kujikinga isipokuwa kujihami na mwisho wa siku CUF imehamia Zanzibar na kuwa chama kinachotetea Waislaam wa Zanzibar. Leo wanajaribu kila hali lakini it's too late watu wameisha wasoma.

Unafikiri Chadema ingeendekeza Uchagga wangekuwa hapa walipo, walipiga vita Ukabila wakajibu waswali mazito na kuonyesha hawana Ukabila lakini wangeendelea kusema Wachagga wana uwezo mkubwa wa kuongoza, kuhalalisjha kuwepo kwao ktk uongozi wa juu hata kwa kauli tu kweli tungefika hapa tulipo? Mkuu hata kama ni mawazo ya mtu mmoja au wawili na yakaungwa mkono wa Wachagga wengi wakiwadharau makabila mengine hudhani kama ni mbegu ya Ukabila hiyo. Umetoa mfano mzuri sana wa wale masheikh watano ulokutana nao na hata sisi hapa JF tumelaani kitendo cha Mbagala na tunawaonyesha kwamba tuko pamoja nanyi kulaani kitendo kile na hata watu kama Jussa na UAMSHO wakamatwe maana inaharibu amani yetu.

Lakini rudi kwenu ktk swala hili la MoU. hatuna zaidi isipokuwa hilo moja tu ambalo athari zake tumeziona toka Mkoloni na tumeeleza mambo mengi sana lakini wapi hamtaki kuelewa. Ebu nambie Mkristu hata mmoja ambaye anaiona sii haki hasa mwanaChadema? - Sidhani! na pengine hakuna hata maana hata viongozi wetu wamekuwa kimya ktk swala hili..Je tunapeleka ujumbe gani kwa Waiislaam?. Na kibaya kuliko yote mnakuja hapa na kujisifia mlivyoweza kufanikiwa kama Wakristu mkitumia watu kama Mohamedi Mtoi kuubeza Uislaam.. inatupeleka wapi Chadema.

Kama kuna swala lolote linalohusu Dini ya Kiislaam bora mshauriane na viongozi wa dini kwanza kabla ya kutoa maoni ama mtazamo wenu hasa pale mtu anapojitambulisha kama mwanachadema. Nimewahi kuzungumza na kiongozi wa chama juu ya swala hili na kumtahadharisha juu ya maswala ya dini kuwa ni sensitive sana and should be approached with caution and rightfully..

Naomba unielewe vizuri kutoka upande huu kwa sababu nawasoma na kuwaelewa vizuri zaidi yako..
 
Mkuu wangu mbona unajikanyaga. Sheikh Ponda sio mwanachama wa Bakwata kama angekuwa na akasema hayo mnayomshirikisha nayo ingeeleweka baraza la waislaam lina msimamo gani ktk swala hilo. Na Hata hivyo Bakwata sio balozi wa Waislaam wote kama ilivyo Chadema kwa Watanzania wote, hivyo kinachosemwa na mwanachama wa Bwakata kuhusu Sheikh Ponda itachukuliwa Bakatwa inampinga Sheikh Ponda kama Chadema inavyompinga JK na CCM, na huwa ndio msimamo wa chama hata kama kasema mbunge asokuwa kiongozi au mwanachama hai na akaungwa mkono na wanachama.

Tatizo hapa ni wanachama wa Chadema kuendelea kuunga mkono maswala yanayowatenga Waislaam kama walivyokuwa wakianza CUFbaada ya uchaguzi wa mwaka 2000. Kwanza ilikuwa agenda ya CCM halafu watu wakaamini chama kikajikuta kina wanachama wengi wanaoamini ktk Udini na fikra za kujikomboa wao toka utawala wa kikristuna Lipumba na wengine wakawa hawana pa kujikinga isipokuwa kujihami na mwisho wa siku CUF imehamia Zanzibar na kuwa chama kinachotetea Waislaam wa Zanzibar. Leo wanajaribu kila hali lakini it's too late watu wameisha wasoma.

Unafikiri Chadema ingeendekeza Uchagga wangekuwa hapa walipo, walipiga vita Ukabila wakajibu waswali mazito na kuonyesha hawana Ukabila lakini wangeendelea kusema Wachagga wana uwezo mkubwa wa kuongoza, kuhalalisjha kuwepo kwao ktk uongozi wa juu hata kwa kauli tu kweli tungefika hapa tulipo? Mkuu hata kama ni mawazo ya mtu mmoja au wawili na yakaungwa mkono wa Wachagga wengi wakiwadharau makabila mengine hudhani kama ni mbegu ya Ukabila hiyo. Umetoa mfano mzuri sana wa wale masheikh watano ulokutana nao na hata sisi hapa JF tumelaani kitendo cha Mbagala na tunawaonyesha kwamba tuko pamoja nanyi kulaani kitendo kile na hata watu kama Jussa na UAMSHO wakamatwe maana inaharibu amani yetu.

Lakini rudi kwenu ktk swala hili la MoU. hatuna zaidi isipokuwa hilo moja tu ambalo athari zake tumeziona toka Mkoloni na tumeeleza mambo mengi sana lakini wapi hamtaki kuelewa. Ebu nambie Mkristu hata mmoja ambaye anaiona sii haki hasa mwanaChadema? - Sidhani! na pengine hakuna hata maana hata viongozi wetu wamekuwa kimya ktk swala hili..Je tunapeleka ujumbe gani kwa Waiislaam?. Na kibaya kuliko yote mnakuja hapa na kujisifia mlivyoweza kufanikiwa kama Wakristu mkitumia watu kama Mohamedi Mtoi kuubeza Uislaam.. inatupeleka wapi Chadema.

Kama kuna swala lolote linalohusu Dini ya Kiislaam bora mshauriane na viongozi wa dini kwanza kabla ya kutoa maoni ama mtazamo wenu hasa pale mtu anapojitambulisha kama mwanachadema. Nimewahi kuzungumza na kiongozi wa chama juu ya swala hili na kumtahadharisha juu ya maswala ya dini kuwa ni sensitive sana and should be approached with caution and rightfully..

Naomba unielewe vizuri kutoka upande huu kwa sababu nawasoma na kuwaelewa vizuri zaidi yako..

I would like very much to understand you BUT unfortuantely you have not touched my understanding... Sorry for that. For me to understand you, your statements must be logical...

Ndugu Mkandala, I have a lot of questions about the way you present issues. Kila nilipoweka red and other clours ni maswali matupu. Muda hautosho ili kutoa nafasi kwa shughuli zingine za maendeleo lakini Ponda ni mwislamu kutokuwa mwanachma is ok lakini nadhani kama Bakwata haiwakilishi waislamu wote then kama ni muhimu kuwa na chombo kinachowaunganisha waislamu wote inaweza kuwa vizuri kama wakikiunda wenyewe. Inagwaje hata CCT na TEC haziwakirishi wakristo wote. kitu ambacho ni sawa, kikundi/dhehebu la kikristo chochote ambacho si mwanachma wa cct na tec kikiona kuna umuhimu wa kujiunga, wajiunge. I'm one of those who are not member and does not feel that its necessary for me to be.

Tatizo hapa ni wanachama wa Chadema kuendelea kuunga mkono maswala yanayowatenga Waislaam Toa mifano halisi. Maana hapa unaunganisha chama cha siasa na waislamu... Ningefurahi kama wanachama wa CDM ambao pia ni waislamu wangeeleza hapa maana ninawafahamu kwa wingi wao. Maana unachojaribu kujenga wewe binafsi hapa ni kuwa CUF ndiyo inayotetea maslahi ya waislamu (kitu ambacho si kweli na kama ni kweli kilipaswa kufutwa katika orodha ya vyama vya siasa na kusajiliwa kama chombo cha kidini "chama kikajikuta kina wanachama wengi wanaoamini ktk Udini na fikra za kujikomboa wao toka utawala wa kikristu.")

Lakini rudi kwenu ktk swala hili la MoU... Hapa sikubaliani kuwa hiyo ni really MoU ni document imeandaliwa ili kuleta ugomvi nchini. Uliona wapi MoU ya kiwango hicho haina majina ya watia sahihi? Haina Muhuri wa vyombo husika? Haina uthibitisho wa kamishena wa viapo? Hiyo ni feki zile zinazotengenezwa na Pri..n..e B g n a. Ulaghai mtupu. Siamini. Kwa uzoefu wangu wa Mou na Agreements hii ni null and void

Na kibaya kuliko yote mnakuja hapa na kujisifia mlivyoweza kufanikiwa kama Wakristu mkitumia watu kama Mohamedi Mtoi kuubeza Uislaam.. inatupeleka wapi Chadema. Ndugu Mkandala, Una kazi kubwa kweli.. Linking the dotes even those which are not related... Mtoi hakubeza bali alieleza ukweli. Simjui Mtoi lakini sijawahi kuona duniani uongo (giza) ukisshinda ukweli (nuru). Sijui kama Mohamedi Mtoi ni mkristo au ni mwanachama wa CDM ninadhani ni mtanzania ambaye anaona taifa linakoelekezwa. hatuwezi kufikia maendeleo yanayokusudiwa kwa kupitia nia ambayo wewe unapenda watanzania tuipitie.

Kwa sababu ya muda siwezi kujibu hoja zako zote lakini nipende kusema kuwa bado unahitaji kutofautisha "issues" and deal with one issue at a time. Do not link political parties with religion. If you ask me why many members of CUF are muslim, I will give you ab answer BUT the original plan of CUF was not to be islamic political Party!

May God of Islael, Jehova Bless you. Read Numbers 6: 24-26
 
Jamani ni bora tuendelee kuwa wazi. Huyu Kikwete kweli amekuwa janga la Tanzania. Anatake advantage ya wajinga wengi wanafuata mkumbo tu ilimradi kimesemwa. Mbona hatukuyaona haya yanayotokea Tanzania sasa tangu uhuru?
Huyu jamaa ni hatari sana kwa nchi yetu. Anatembelea laana kibao ikiwepo ya kuwaua watanzania wengi sana kwa maslahi yake binafsi.
Tuangalie yaliyotokea kwa Dr. Ulimboka. Umafia kama huu unawaambia nini watoto wa Tanzania? Kisha tu mtu amedai haki! Tuangalie picha za Mwangosi zilizosambaa nchi nzima. Tuangalie mauwaji ya Ally kule Morogoro. Tuangalie picha za makanisa yaliyochomwa waziwazi tena mchana kweupe.
Wapendwa ni udini ni ubinafsi ni ujinga vyote vinachanganya hapa. Hatuna kiongozi kabisa. Alijiingiza madarakani kwa nia alizojijua yeye mwenyewe na katumia ujinga wa watanzania akiwatenganisha kwa udini. Mimi nilishasema mara nyingi madhara ya uongozi wa Kikwete ni makubwa sana kwa Tanzania. Yaani yatatucost miaka mia ijayo. Yeye mwenyewe kama raisi kipofu anachekelea akidhani yuko salama. Mwenye kumpa maoni haya amjulishe kuwa hayuko salama hata kidogo. Watoto wake na wajukuu zake atateseka sana kwa mbegu hii ya ubinafsi aliyoipanda. Familia yake itasambaratika vibaya na mali yote waliyojikusanyia wakitunyima wanyonge haki yetu wala hawataifaidi. Bita za kidini hazina macho. Kikwete na familia yake wataumia kwanza ndipo sisi wengine tufuate kama vile anavyoendelea kukosa image hapa Tanzania kila kukicha.
Mungu mbariki na kumpokea peponi Nyerere aliyetuunganisha kama ndugu.
 
Mkuu Mkandara kumbe na wewe una fikra kuwa Waislamu wanaonewa, nimesikitika sana.

Awali nilikuwa napenda michango yake, akijinasibu kuwa ni Muislamu na Mfuasi wa CDM mwenye mawazo huru, lkn tangu kuibuka vurugu za Waislamu kudaiwa kuchoma Makanisa, kabadilika.
Ghafla ameanza kumpiga vita Dr Slaa, tena kwa kauli za kejeli na kuwa pro Zitto! Ati mwana CDM, Muislamu, Pro Zitto but anti Dk Slaa!
 
Kupigwa risasi kwa Padre huko Zanzibar ni moja wapo ya matunda ya mbegu iliyopandwa na Ustaadh Jakaya Mrisho Kikwete.
 
Hakika hili la UDINI limeniumiza kuliko mambo yote niliyowahi kukutana nayo kitaifa. Hakika tusisahau kamwe yale maneno ya Mwl J K Nyerere aliyosema "watanzania wote ni ndugu... bila kujali rangi, kabila wala dini zao..."

Turudishe uhusiano wetu uliotukuka wa kuheshimu imani na dini za watu wengine. Kwa sasa si muda wa kulaumu nani ni nani na nani alifanya nini, Nadhani sasa ni muda wa kujega mahusiano yaliyohitilafiwa na watu wachache wanaopenda madaraka. Ni wajibu wangu mimi, wewe na yule katika kuhakikisha tunalitokomeza hili jambo kabisa.

Ee mwenye enzi Mungu utusaidie sisi waja wako

Amen[/QUOTENadhani njia rahisi ya kuutokomeza udini ni kuitokomeza CCM kwanza kwa sababu kinga ni Bora kuliko tiba,tusiuwe mbu ila tuharibu mazingira yanayoruhusu mbu kuzaliana.
 
Kwenye siasa kote duniani kuna ujanja, hila na fitna nyingi
 
JK alikuwa tayari kumpaka matope yeyote ilimradi akwee juu kisiasa. Mambo ya Dr. Salim
 
Siyo siri kuwa muasisi wa siasa za maji taka hapa Tanzania ni JK na genge lake la wanamtandao. Mbinu hii aliizanza mapema kabla ya uchaguzi wa mwaka 2005, na wahanga wakubwa wa siasa hizi za kishenzi ni Fredrick Sumaye, Salim A. Salim, Prof.Mark Mwadosya na wengineo, na wahanga hawa walilengwa kwani walionekana kuwa tishio kwa malengo ya JK kuukwaa urais hivyo ilikuwa lazima wachafuliwe kiasi cha kutosha ili wanuke na wakati huo magazeti yakimpamba JK kwa sifa asizostahili, na kweli mbinu hii ya kishenzi ilifanikiwa na JK akawa rais.

Mwaka huu kwa vile kanuni za CCM zilikuwa zinamlinda JK asipate mpinzani toka ndani ya chama hicho hakuwa na haja ya kutumia mbinu hiyo na akawa anajiandaa kushinda kwa kishindo, lakini ghafla upepo ukabadilika baada ya mzalendo wa kweli Dr Slaa kuteuliwa na Chadema kugombea nafasi ya urais, JK baada ya kuona kuwa maji ni marefu kwake na chama chake akarudia tena mbinu yake ya maji taka na ndipo zikasikika habari za Dr Slaa kuchukuwa mke wa mtu, lakini kwa vile watanzania wa leo siyo wale wa mwaka 47, waliimpuuza JK na siasa zake hizo chafu wakaendelea kumuunga mkono Dr Slaa.

Baada ya JK na genge lake kuona kuwa mbini hii haifanyi kazi akaamua kutumia SILAHA YA MAANGAMIZI - UDINI.

Ukazushwa uvumi kuwa Dr Slaa ametumwa na Kanisa Katoliki, mbinu hii ilikolezwa na magazeti ya fisadi Rostam Aziz na mengine kama Habari Leo, AL HUDA, AL NUR, na kama haitoshi zikatumwa sms kwa mamilion ya wapiga kura kumchafua Dr Slaa na kuhusisha na udini.

Siyo siri kuwa silaha hii imeacha majeraha mengi miongoni mwa Watanzania na mfano hai ni hata hapa jamvini hangover ya siasa hizi za udini zilizo asisiwa na Kikkwete mwenyew e ipo. Dini ni jambo nyeti sana na likitumiwa vibaya linaweza kuilipua nchi nzima na hiki ndicho
alichokifanya JK.

NATOA MWITO KWA WACHA MUNGU WOTE TUOMBEE NCHI YETU IONDOKANE NA SUMU ILIYOMWAGWA NA JAKAYA MRISHO KIKWETE
acha kumsingizia jk
 
Back
Top Bottom