Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Mheshimiwa Rais Kikwete,
Leo hii nakuja na ushauri kwako, tena ukiamua kukaa chini na kutafakari, yawezekana ukaleta mabadiliko makubwa sana ya kuifanya Tanzania iwe fanisi na kupiga hatua kujinasua kutoka umasikini.
Mheshimwa Rais Kikwete, nakusihi Ukaze Mkanda, Bana Matumizi na Punguza Ukubwa wa Serikali ya Jamhuri ya Tanzania.
Serikali yetu na mfumo wake ni kubwa sana na haina ufanisi na ni gharama kubwa kwa Taifa letu. Kwa maoni yangu, asilimia 45 (45%) ya Serikali ya Tanzania na Taasisi zake (ikiwa ni Serikali Kuu, Wizara, Idara, Mikoa, Wilaya na Taasisi nyingine) ni mzigo ambao hauna manufaa na ni gharama zisizo la lazima. Nasema sehemu hii inatokana na kuundwa kwa mfumo huu kwa kutumia Usiasa zaidi na kuridhishana na si kutafuta Ufanisi halisi.
Kama unataka ufanisi na kuimarika kwa utendaji, kinachohitajika ni Uimara kutoka kwenye uongozi wako na Viongozi na watu unaowapa dhamana ya kufanya kazi hiyo. Ufanisi na Maendeleo yatapatikana kama utakuwa mfuatiliaji mzuri, mchapa kazi na mwajibishaji bila woga kwa wale wanaoshindwa kufanya kazi kwa kufuata malengo, maelekezo na kutumia bajeti vizuri.
Si suala la Ufisadi, au matumizi mabaya pekee ya fedha kuwa yakisahihishwa basi tutaanza kupiga hatua mpya au tutapata fedha na uwezo wa kupiga hatua za kimaendeleo.
Tatizo letu ni Unene na Ubwanyenye wa kunona wa Serikali yetu ambako kunatufanya tuwe dhaifu, wavivu, wazito na kutegeana.
Angalia kama inavyojulikana, mtu mwembamba ni mwepesi mwenye uwezo wa kufanya mambo kwa haraka na ufanisi bila kuchoka, lakini mtu mnene kwanza ni mvivu, anafanya mambo pole pole, anapumua kwa shida na kila mara ni mwepesi kuugua na huishia kujiliwaza kwa kuendelea kunenepa na kula kwa ulafi akidhani kuwa akiongeza mlo, basi matatizo yatajipotelea.
Wewe ulikuwa mwana michezo, wasifu wako unasema ulikuwa mwanamichezo mahiri. Nafikiri utakubaliana nami kuwa staha yako ilikuruhusu si siku zile tuu, bali mpaka leo hii kuwa na siha ambayo inakuruhusu kukimbia bila kuchoka, kwa furaha na ukimaliza kufanya mazoezi una nguvu na upeo mzuri wa kufanya kazi na hulemewi na uchovu. Sasa ukiangalia mtu Kibonge, najua jibu unalo, mtu huyu ni goigoi, anategemea watu wengine wamsaidie au wafanye kazi kwa niaba yake na kwenye timu, mtu huyu kila siku yeye ni wa mwisho kwa maana hajiwezi, unene unamumbua na mbaya zaidi mtu huyu kila siku anavyoendekea kuwa mnono, ndivyo anavyoongeza uwezekano wa yeye kupata shinikizo na kuanguka chini puu, marehemu!
Sasa Serikali ya Tanzania ni kama huyu Kibonge, Bongisa, Bwanyenye ambaye akitembea tumbo, mat ako, mapaja, mikono na shingo vinanesanesa vikiwa vimejaa mafuta makubwa na hata uwezo wa kufanya kazi au kuaminiwa kuwa atafanikiwa ni haba. Unene wa Serikali yetu, kama vile unene wa Mwanadamu, ni wazi kuwa ni ziada isiyo na manufaa, ni ziada isiyo lazima na isiyo na ufanisi.
Serikali yetu imeiga mfumo wa Kikoloni, na hicho kilifanywa na Mkoloni ili kutudhibiti. Lakini sisi tumeendeleza utamaduni huu na hata kuufanya ni jambo la kisiasa na bila kufikiria, tumekuwa tunatumia pesa zaidi kujishibisha kwa kuipanua Serikali eti tukidai tunaongeza na kusambaza huduma za maendeleo kila kona.
Ukweli ni huu Mheshimiwa Kikwete, tatizo la sisi kushinda kupiga hatua za kimaana kimaendeleo ni kutokana na ukosefu wa Tija na uongozi Imara ambao uko tayari kufanya kazi kwa bidii na maarifa, kama vile mkimbiajiwa mbio ndefu anavyoweza kimbia kwa masaa mawili, sawa na mkimbiaji wa mbio fupi anayeweza kimbia mita 100 kwa Sekunde 9!
Tuna Mawaziri na Wizara nyingi kupita kiasi na hazina ufanisi. KUna makatibu wakuu wengi lakini hatuoni uwajibikaji. Tuna Wakuu wa Mikoa na wilaya ambao nao wamepewa wasaidizi wengi kwa majina ya Wakurugenzi, Waratibu na hata Wabunge, lakini kinachoishia ni matumizi kuongezeka lakini hakuna manufaa wala ufanisi.
Kama tukipunguza ukubwa wa Serikali yetu kwa asilimia nilizozipendekeza kwako hapo juu, basi bajeti na fedha ambazo zimeendelea kutumika kulea unono maiti wa Serikali, zingetumika kwa kupeleka maendeleo na huduma kwa wananchi, iwe ni Afya, Elimu, Maji hata kuboresha Miundo Mbinu.
Punguza Wizara, punguza Mawaziri, punguza Manaibu, punguza Makatibu na Wakurugenzi. Wazungu wanasema "Consolidate", basi unganisha chini ya mwamvuli mmoja na kuwa na watu maalumu kusimamia kila nyanja na utakayemteua kuwa kiongozi mkuu wa idara au wizara, ni bora ajue kuchapa kazi na si talalile na kubembea. Nawe uwe makini kumpumulia mtendaji huyu kwenye shingo yake, ukimdai ripoti na matokeo chanya. Wala usimruhusu akatumia madaraka au fedha kinyume na fungu au kilichopangwa.
Tena watendaji hawa usiwape madaraka wafanye kazi tuu, bali wajue kujibana na kuweka akiba na si kufuja kila senti kisa fedha zipo!
Punguza utitiri wa Watendaji wa Mikoa na Wilaya! hakuna maana ya kuwa na kivuli cha kila cheo kutoka Waziri Mkuu, Mkoa na Wilaya! Huku ni kuongeza matumizi yasiyo na maana. Leo kuna DC, DDD, DEO, DRD, na DDDDDD kila sehemu sawa na RC, RDD, RAO, na RRRRR nyingi.
Kila kazi na cheo tunachokitengeneza, kinahitaji mshahara, gari, nyumba, marupurupu, watumishi na mambo megine mengi tuu. Hayo ni gharama hasa ukizingatia kuwa mfumo huu tumeutumia tangu tupate Uhuru na hatupigi hatua kama Taifa bali kama wateuliwa wa nafasi hizi, tunapata maendeleo kibinafsi ya kuwa matajiri, lakini Taifa linazidi kukwama kwenye tope la mfinyanzi wa Umasikini!
Hata Ubunge, nao tumeufanya ni suala la kuzidiana kura na si suala la kuleta maendeleo. Hivi kwa nini kuna wilaya ambazo zimemegwa vipande na kuunda magharibi na mashariki?
Je Iramba, Same, Rungwe, Arumeru na nyinginezo kama Kinondoni ilivyogawanywa kuwa Kawe, Ubungo na Kinondoni, zimeleta maendeleo gani ukifanya utafiti wa kina kama si kuongeza matumizi?
Kama waliopewa madaraka na dhamana ya kuongoza wakati wilaya hizi zikiwa ni kitu kimoja si Magharibi, Mashariki, Kusini au Kaskazini walishindwa kazi na kuleta matunda, kwa nini waliendelea kuaminiwa kuwa iko siku watafanikiwa hasa kwa wale ambao wamekaa kama Wawakilishi na Watendaji zaidi ya miaka 20 na bado wanang'ang'ania eti wataweza kazi?
Ni wakati wa kufanya mambo kisayansi na kuelekea katika mfumo wa kisasa kama vile uzalishaji mali ulivyoongezeka kutumia teknolojia ambako kumepunguza gharama na uwingi wa watu kufanikisha kazi.
Hebu fikiria mishahara, nyumba, magari na marupurupu mengine, gharama za kiofisi, samani, na vifaa vya maofisi tunazozitumia kisa tuna watu wengi lakini hakuna ufanisi?
Kazi ya wewe kuratibu na kupunguza Serikali tena sasa hivi itakuwa ni Rahisi! Tuna Kompyuta na mtandao wa kompyuta ambao utafanikiwa pindi huu mkonge wa nyuzi optiki ukikamilika na hata ule mradi wa Vitambulisho vya Taifa.
Naomba ulitafakari hili unapojiandaa kuanza ngwe yako ya pili ya Utawala (nasikitika kukubali huna mshindani iwe ni ndani ya chama chako CCM au nje kupitia Upinzani mpaka dakika hii nikikuandikia salamu hizi) baada ya uchaguzi, basi uanze kampeni mpya ambayo itatumia sayansi kuboresha kauli mbiu yako ya Ari, Kasi na Nguvu Mpya!
Wafundishe Watanzania kwa matendo kuwa tunaweza Kukaza Mkanda, Kubana Matumizi na kupunguza Ukubwa wa Serikali na kupata mafanikio hata yakatiririka katika nafsi zetu kama mtu mmoja mmoja, familia na jamii kwa ujumla.
Kama Obama alivyosema "ndiyo, tutaweza" naamini nawe ukiwa na nia ya kizalendo bila woga au kujishuku na kutokujiamini, nawe utaweza pamoja na mapingamizi utakayopata kutoka kwa wale kupe, mbung'o na hata mchwa kama Mzee Mwinyi alivyotuambia majuzi ambao ni wanyonyaji na wamezoea vya kunyonya na vya urahisi na ndio maana wamenenepa kupita kiasi na kila siku wana mashinikizo na viugonjwa vinavyowalazimu kuiacha Muhimbili na kukimbilia India Bondeni na Ulaya Ulaya kwa matibabu.
Mchungaji anakuambia Mheshimiwa, kama Mwalimu Nyerere alivyosema na kutukumbusha, Uwezo tunao, Sababu tunayo, je mwenzangu utajumuika na kuwa na Nia hii ambayo ninayo? Waswahili walisema penye Nia kuna Njia!
"Ndiyo, Tutaweza" Yes, We Can!
Leo hii nakuja na ushauri kwako, tena ukiamua kukaa chini na kutafakari, yawezekana ukaleta mabadiliko makubwa sana ya kuifanya Tanzania iwe fanisi na kupiga hatua kujinasua kutoka umasikini.
Mheshimwa Rais Kikwete, nakusihi Ukaze Mkanda, Bana Matumizi na Punguza Ukubwa wa Serikali ya Jamhuri ya Tanzania.
Serikali yetu na mfumo wake ni kubwa sana na haina ufanisi na ni gharama kubwa kwa Taifa letu. Kwa maoni yangu, asilimia 45 (45%) ya Serikali ya Tanzania na Taasisi zake (ikiwa ni Serikali Kuu, Wizara, Idara, Mikoa, Wilaya na Taasisi nyingine) ni mzigo ambao hauna manufaa na ni gharama zisizo la lazima. Nasema sehemu hii inatokana na kuundwa kwa mfumo huu kwa kutumia Usiasa zaidi na kuridhishana na si kutafuta Ufanisi halisi.
Kama unataka ufanisi na kuimarika kwa utendaji, kinachohitajika ni Uimara kutoka kwenye uongozi wako na Viongozi na watu unaowapa dhamana ya kufanya kazi hiyo. Ufanisi na Maendeleo yatapatikana kama utakuwa mfuatiliaji mzuri, mchapa kazi na mwajibishaji bila woga kwa wale wanaoshindwa kufanya kazi kwa kufuata malengo, maelekezo na kutumia bajeti vizuri.
Si suala la Ufisadi, au matumizi mabaya pekee ya fedha kuwa yakisahihishwa basi tutaanza kupiga hatua mpya au tutapata fedha na uwezo wa kupiga hatua za kimaendeleo.
Tatizo letu ni Unene na Ubwanyenye wa kunona wa Serikali yetu ambako kunatufanya tuwe dhaifu, wavivu, wazito na kutegeana.
Angalia kama inavyojulikana, mtu mwembamba ni mwepesi mwenye uwezo wa kufanya mambo kwa haraka na ufanisi bila kuchoka, lakini mtu mnene kwanza ni mvivu, anafanya mambo pole pole, anapumua kwa shida na kila mara ni mwepesi kuugua na huishia kujiliwaza kwa kuendelea kunenepa na kula kwa ulafi akidhani kuwa akiongeza mlo, basi matatizo yatajipotelea.
Wewe ulikuwa mwana michezo, wasifu wako unasema ulikuwa mwanamichezo mahiri. Nafikiri utakubaliana nami kuwa staha yako ilikuruhusu si siku zile tuu, bali mpaka leo hii kuwa na siha ambayo inakuruhusu kukimbia bila kuchoka, kwa furaha na ukimaliza kufanya mazoezi una nguvu na upeo mzuri wa kufanya kazi na hulemewi na uchovu. Sasa ukiangalia mtu Kibonge, najua jibu unalo, mtu huyu ni goigoi, anategemea watu wengine wamsaidie au wafanye kazi kwa niaba yake na kwenye timu, mtu huyu kila siku yeye ni wa mwisho kwa maana hajiwezi, unene unamumbua na mbaya zaidi mtu huyu kila siku anavyoendekea kuwa mnono, ndivyo anavyoongeza uwezekano wa yeye kupata shinikizo na kuanguka chini puu, marehemu!
Sasa Serikali ya Tanzania ni kama huyu Kibonge, Bongisa, Bwanyenye ambaye akitembea tumbo, mat ako, mapaja, mikono na shingo vinanesanesa vikiwa vimejaa mafuta makubwa na hata uwezo wa kufanya kazi au kuaminiwa kuwa atafanikiwa ni haba. Unene wa Serikali yetu, kama vile unene wa Mwanadamu, ni wazi kuwa ni ziada isiyo na manufaa, ni ziada isiyo lazima na isiyo na ufanisi.
Serikali yetu imeiga mfumo wa Kikoloni, na hicho kilifanywa na Mkoloni ili kutudhibiti. Lakini sisi tumeendeleza utamaduni huu na hata kuufanya ni jambo la kisiasa na bila kufikiria, tumekuwa tunatumia pesa zaidi kujishibisha kwa kuipanua Serikali eti tukidai tunaongeza na kusambaza huduma za maendeleo kila kona.
Ukweli ni huu Mheshimiwa Kikwete, tatizo la sisi kushinda kupiga hatua za kimaana kimaendeleo ni kutokana na ukosefu wa Tija na uongozi Imara ambao uko tayari kufanya kazi kwa bidii na maarifa, kama vile mkimbiajiwa mbio ndefu anavyoweza kimbia kwa masaa mawili, sawa na mkimbiaji wa mbio fupi anayeweza kimbia mita 100 kwa Sekunde 9!
Tuna Mawaziri na Wizara nyingi kupita kiasi na hazina ufanisi. KUna makatibu wakuu wengi lakini hatuoni uwajibikaji. Tuna Wakuu wa Mikoa na wilaya ambao nao wamepewa wasaidizi wengi kwa majina ya Wakurugenzi, Waratibu na hata Wabunge, lakini kinachoishia ni matumizi kuongezeka lakini hakuna manufaa wala ufanisi.
Kama tukipunguza ukubwa wa Serikali yetu kwa asilimia nilizozipendekeza kwako hapo juu, basi bajeti na fedha ambazo zimeendelea kutumika kulea unono maiti wa Serikali, zingetumika kwa kupeleka maendeleo na huduma kwa wananchi, iwe ni Afya, Elimu, Maji hata kuboresha Miundo Mbinu.
Punguza Wizara, punguza Mawaziri, punguza Manaibu, punguza Makatibu na Wakurugenzi. Wazungu wanasema "Consolidate", basi unganisha chini ya mwamvuli mmoja na kuwa na watu maalumu kusimamia kila nyanja na utakayemteua kuwa kiongozi mkuu wa idara au wizara, ni bora ajue kuchapa kazi na si talalile na kubembea. Nawe uwe makini kumpumulia mtendaji huyu kwenye shingo yake, ukimdai ripoti na matokeo chanya. Wala usimruhusu akatumia madaraka au fedha kinyume na fungu au kilichopangwa.
Tena watendaji hawa usiwape madaraka wafanye kazi tuu, bali wajue kujibana na kuweka akiba na si kufuja kila senti kisa fedha zipo!
Punguza utitiri wa Watendaji wa Mikoa na Wilaya! hakuna maana ya kuwa na kivuli cha kila cheo kutoka Waziri Mkuu, Mkoa na Wilaya! Huku ni kuongeza matumizi yasiyo na maana. Leo kuna DC, DDD, DEO, DRD, na DDDDDD kila sehemu sawa na RC, RDD, RAO, na RRRRR nyingi.
Kila kazi na cheo tunachokitengeneza, kinahitaji mshahara, gari, nyumba, marupurupu, watumishi na mambo megine mengi tuu. Hayo ni gharama hasa ukizingatia kuwa mfumo huu tumeutumia tangu tupate Uhuru na hatupigi hatua kama Taifa bali kama wateuliwa wa nafasi hizi, tunapata maendeleo kibinafsi ya kuwa matajiri, lakini Taifa linazidi kukwama kwenye tope la mfinyanzi wa Umasikini!
Hata Ubunge, nao tumeufanya ni suala la kuzidiana kura na si suala la kuleta maendeleo. Hivi kwa nini kuna wilaya ambazo zimemegwa vipande na kuunda magharibi na mashariki?
Je Iramba, Same, Rungwe, Arumeru na nyinginezo kama Kinondoni ilivyogawanywa kuwa Kawe, Ubungo na Kinondoni, zimeleta maendeleo gani ukifanya utafiti wa kina kama si kuongeza matumizi?
Kama waliopewa madaraka na dhamana ya kuongoza wakati wilaya hizi zikiwa ni kitu kimoja si Magharibi, Mashariki, Kusini au Kaskazini walishindwa kazi na kuleta matunda, kwa nini waliendelea kuaminiwa kuwa iko siku watafanikiwa hasa kwa wale ambao wamekaa kama Wawakilishi na Watendaji zaidi ya miaka 20 na bado wanang'ang'ania eti wataweza kazi?
Ni wakati wa kufanya mambo kisayansi na kuelekea katika mfumo wa kisasa kama vile uzalishaji mali ulivyoongezeka kutumia teknolojia ambako kumepunguza gharama na uwingi wa watu kufanikisha kazi.
Hebu fikiria mishahara, nyumba, magari na marupurupu mengine, gharama za kiofisi, samani, na vifaa vya maofisi tunazozitumia kisa tuna watu wengi lakini hakuna ufanisi?
Kazi ya wewe kuratibu na kupunguza Serikali tena sasa hivi itakuwa ni Rahisi! Tuna Kompyuta na mtandao wa kompyuta ambao utafanikiwa pindi huu mkonge wa nyuzi optiki ukikamilika na hata ule mradi wa Vitambulisho vya Taifa.
Naomba ulitafakari hili unapojiandaa kuanza ngwe yako ya pili ya Utawala (nasikitika kukubali huna mshindani iwe ni ndani ya chama chako CCM au nje kupitia Upinzani mpaka dakika hii nikikuandikia salamu hizi) baada ya uchaguzi, basi uanze kampeni mpya ambayo itatumia sayansi kuboresha kauli mbiu yako ya Ari, Kasi na Nguvu Mpya!
Wafundishe Watanzania kwa matendo kuwa tunaweza Kukaza Mkanda, Kubana Matumizi na kupunguza Ukubwa wa Serikali na kupata mafanikio hata yakatiririka katika nafsi zetu kama mtu mmoja mmoja, familia na jamii kwa ujumla.
Kama Obama alivyosema "ndiyo, tutaweza" naamini nawe ukiwa na nia ya kizalendo bila woga au kujishuku na kutokujiamini, nawe utaweza pamoja na mapingamizi utakayopata kutoka kwa wale kupe, mbung'o na hata mchwa kama Mzee Mwinyi alivyotuambia majuzi ambao ni wanyonyaji na wamezoea vya kunyonya na vya urahisi na ndio maana wamenenepa kupita kiasi na kila siku wana mashinikizo na viugonjwa vinavyowalazimu kuiacha Muhimbili na kukimbilia India Bondeni na Ulaya Ulaya kwa matibabu.
Mchungaji anakuambia Mheshimiwa, kama Mwalimu Nyerere alivyosema na kutukumbusha, Uwezo tunao, Sababu tunayo, je mwenzangu utajumuika na kuwa na Nia hii ambayo ninayo? Waswahili walisema penye Nia kuna Njia!
"Ndiyo, Tutaweza" Yes, We Can!