Rais Kikwete asaini Muswada wa Katiba

Kwa hiyo swala zima la Katiba Mpya ni la KISIASA! - Ndio mguu tuloanza nao na ajabu watu wameshindwa pia kutazama hapa.

Unfortunately ndio hali tuliyonayo sasa. Na ndio maana nilisema makosa yalifanyika bungeni. Waziri mkuu na Spika walikuwa na every opportunity ya kuunganisha watanzania na kuifanya hii katiba iwe ya kitaifa - beyond party politics, but they both decided to look away!

Na kama hii katiba itaandikwa kwa kufuata kila kilichopo kwenye hii sheria Tanganyika ndio watakuwa loosers. CUF wanaungana na CCM kwenye hili sio kwa sababu wameambiwa wafanye hivyo na CCM ila kwa sababu inaonekana (after all these years) kukamilisha uhuru wa Zanzibar toka kwa -wakoloni' - Tanganyika. Huu ni mkakati wa Zanzibar wa kuondokana na kadhia hii ya 'kunyonywa' na Tanganyika. Wabunge wengi wa CUF wanatoka Zanzibar, na tutambue CUF Zanzibar sawa na CUF Tanganyika. Wakina Mh Barwan na Magdalena Sakaya sijui kama wanaelewa couldn't care less about Tanganyika?

Unless kufanyike marekebisho makubwa na muundo wa muungano upewe kipaumbele kwenye uundwaji wa hii katiba mpya, CCM watajikuta wapo upande mwingine wa historia! Majuto mjukuu!
 
Hivi kulikuwa na haja gani ya makubaliano kati yake na chadema. Hivi ni kwanini kikwete hawezi kamwe kuwasikiliza wananchi? Hivi ni kwa nini kikwete anatuchukulia hivi watanzania? Hakika siamini kama duniani kote kuna kiongozi wa nchi mpenda mzaha ktk mambo ya msingi kama kikwete. Kwa kweli hii hali imenisikitisha sana.

Mkuu wananchi unaozungumzia wewe ni wapi hao? na wanasemaje kuhusu mswaada huo? maana kwa mtazamo wa watu ni kwamba Jukwaa la katiba/CDM ni wananchi lakini ukumbuke kuwa hakuna utafiti unaoonyesha maoni ya wananchi kwa percentage ambayo itaonyesha majority wanataka nini na JK amekataa. ukumbuke kuwa kuna uwakilishi Bungeni una reflect pia maoni ya wananchi. watu wamekuwa wakitumia "wananchi" kama ngao yao ya kukubaliwa maoni yao
 
..nadhani sasa maandamano ya CDM yamehalalishwa.

..hakuna shaka kwamba Raisi amepuuza mawazo na ushauri wa CDM.

..CDM sasa wanaweza kuja kwetu wananchi na kusema Bungeni walisimangwa, na Ikulu walipuuzwa.
 
Ninaamini Jk aliwaambia chadema kwamba atasaini ili mchakato uanze na maoni yao kayachukua ili kuyafanyia kazi wakati wa kipindi cha kuchukua maoni kwa wananchi
 
Guys this is politics. Hivi kuna mtu yeyote mwenye akili yake alidhani kuwa JK hatasaini muswada ule?. Asinge saini angewasha moto mkubwa sana na wabunge wake wa CCM waliokuwa wakitoa povu ili kuwakomoa CDM. The movie is simple, saini muswada iwe sheria halafu peleka bungeni marekebisho ili ku-accomodate hoja za watu wengine. Ingekuwa ni provocation kama angesaini muswada kabla ya kukutana na CDM.

Kitu pekee ambacho anaweza kukichelewesha ni kuanza utekelezaji wa sheria kama kuteua wajumbe wa kusikiliza maoni. Kama atateua tume hiyo basi ni dhahiri kuwa hakuna la maana litakalofanyika. Kama mna kumbukumbu nzuri hata sheria ya uchaguzi aliitia saini kama huu muswada alioutia leo kabla ya kufanya marekebisho.

JK angeonekana ni msaliti mkuu kwa wabunge wa CCM kama asingeutia saini muswada huu, kitu ambacho kingemuweka pabaya kwenye kupitisha sheria zingine huko mbeleni.

Tusihofu wala ku-spin this out of control, issue si kuzuia muswada kutiwa saini issue ni kuzuia sheria mbaya kuanza kutumika. Haiingii akilini hata kidogo serikali hiyohiyo ipeleke muswada bungeni na wabunge wake waipishe halafu iwasaliti wabunge hao kwa kutousaini muswada huo. Ingekuwa sheria hii imeanzia bungeni JK alikuwa na sababu ya ku-VETO.

Mkuu hapo nakubaliana na wewe 100%. Inawezekana kabisa Rais amejaribu kuangalia prons and cons za pande zote, yaani kusani tofauti na matarajio ya wabunge wa chama chake na wabuge waliopinga muswada huo kupitisha sheria hiyo. Nadhani ndo maana kama umesoma vizuri tangu ile resolution ya iliyosomwa na ikulu jana kuna provision ya kuurekebisha muswada huo ambayo na leo imewekewa uzito wake.

Baada ya kusema hayo naomba niseme kuwa hii nadharia itakuwa proved iwapo tu rais hatateua tume angalao mpaka tutakapoona imetolewa nafasi ya mijadala na hatimaye mabadiliko(maboresho) kwenye sheria hii ilopitishwa.

In meantime lets give him the benefit of doubt. Its just a matter of time then soon tutakuwa na haki ya kusema kuwa rais wetu ni msanii e.t.c. Otherwise naona wengi humu tunajadili CDM na CCM na sio namna itakayosaidia kupatikana kwa katiba bora.
 
Hapo kwenye red; kwa TZ, na hasa kwa CCM ndio hivyo Mkuu. Tena si wao (CCM) tu, bali pia vyombo vyetu vya kisheria vinatuaminisha hivyo. Rejea Hukumu ya Mahakama ya Rufaa juu ya suala la mgombea binafsi lilivyoamuliwa na jopo la Majaji 7 chini ya Uongozi wa Jaji Mkuu wakiwapo wazee na "marafiki" kadhaa wa mahakama akina Prof. Palamagamba Kabudi. Habari ndio hiyo!
Unajua wakati nimesikia JK atakutana na Ujumbe wa CDM, nilitoa ki hint humu kwamba CDM hawatakuwa wamewakilishwa na Ujumbe wa viongozi wao pekee nikitegemea wao watanisoma na pengine kufikiria kupeleka ujumbe ulokuwa na watu kutoka vyama vingine, taasisi na kamati za katiba zilizoundwa. Nilitegemea sana wataambatana na watu kama Salim, Warioba na wataalam kwenye maswala kama haya. Lakini ndio hivyo tena imeshakuwa...
 
kwani watatunga katiba kimyakimya? mie nafikiri kuna hatua fulani watenda kwa wananchi kwa kura za maoni, hapo si mnaweza ipiga chini katiba iliyotengenezwa na tume?

ama hakuna tena kura ya maoni ?
 
kama Jk angekuwa na lengo baya tangu mwanzo asingepoteza muda kuwasilikiza chadema hapo tuwe wakweli ndio maana kautia saini baada ya kupokea hoja za chadema na kuomba wananchi washirikiane na tume itakayoundwa kwa ajili hiyo
 
baada ya kutia saini hatua itakayofuta ni kuunda tume ya kupokea maoni ya wananchi ikiwemo chadema wanaweza kupeleka maoni yao hata kama wamemkabidhi Rais
 
Wakuu zangu hii ndio imetoka, tukubali matokeo hakuna cha kurekebisha lolote mpira ndio umeanza na filimbi imeshapigwa. Muda wa Mapumziko ni baada ya dakika 45..Ukicheza rafu kadi ya njano ukiendelea nyekundu..

Kifupi, CDM imeadhirika wala sii kidogo ila tu kama wananchi na taasisi zao watachukua hatua tofauti..
Unaona sasa! Hicho Chadema walichokuwa wanapigania ni kwa maslahi yao au ya Watanzania wote ukiwemo wewe. Wewe unaona ni Chadema wameadhirika wakati siku zote unalia nchi inaelekea kubaya....hujui chanzo? Kama mawazo ya wasomi ni haya na kule vijijini itakuwaje?
 
baada ya kutia saini hatua itakayofuta ni kuunda tume ya kupokea maoni ya wananchi ikiwemo chadema wanaweza kupeleka maoni yao hata kama wamemkabidhi Rais

Mkuu mbona unataka kupotosha. CDM hawakupeleka maoni ya Katiba iwe vipi, CDM wamepeleka maoni ya mchakato wa kupata katiba uwe vipi, ikiwemo hilo la uundwaji wa tume.

Sasa sidhani kama tume itakayoundwa itakuwa na mandate ya kupokea maoni ya mchakato huo uwe vipi. Huku ni kuchangia bila kujua unachangia nini mkuu.
 

Aidha, kutiwa saini kwa Muswada huo ili uwe Sheria ni hatua kubwa na muhimu katika safari ya kutungwa kwa Katiba mpya ya Tanzania kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais Kikwete katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa wananchi Desemba 31, mwaka jana, 2010.

Pamoja na kutiwa saini hiyo bado Serikali itaendelea kusikiliza maoni na mawazo ya wadau na wananchi mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha sheria hiyo.

Hivyo, Mheshimiwa Rais Kikwete anatoa wito kwa mwananchi yoyote mwenye maoni ama mawazo ya namna ya kuboresha Sheria hiyo, ajisikie yuko huru kutoa maoni yake na Serikali itasilikiza na kuchukua hatua zipasazo.

I am shocked beyond belief........................hivi hao chadema alikutana nao kufanya nini wakati sheria yenyewe ni mbovu?

some leaders never learn............................................mpaka hapo tutakapowachomoa kutoka kwenye kalawati kama kadaffi..........
 
Mkuu hapo nakubaliana na wewe 100%. Inawezekana kabisa Rais amejaribu kuangalia prons and cons za pande zote, yaani kusani tofauti na matarajio ya wabunge wa chama chake na wabuge waliopinga muswada huo kupitisha sheria hiyo. Nadhani ndo maana kama umesoma vizuri tangu ile resolution ya iliyosomwa na ikulu jana kuna provision ya kuurekebisha muswada huo ambayo na leo imewekewa uzito wake.

Baada ya kusema hayo naomba niseme kuwa hii nadharia itakuwa proved iwapo tu rais hatateua tume angalao mpaka tutakapoona imetolewa nafasi ya mijadala na hatimaye mabadiliko(maboresho) kwenye sheria hii ilopitishwa.

In meantime lets give him the benefit of doubt. Its just a matter of time then soon tutakuwa na haki ya kusema kuwa rais wetu ni msanii e.t.c. Otherwise naona wengi humu tunajadili CDM na CCM na sio namna itakayosaidia kupatikana kwa katiba bora.

thanks brother
 
safi sana... JK siku zote kiongozi mzuri anafanya maamuzi sahihi na sio kupelekwapelekwa na kikundi cha watu flani nazungumzia (CDM HAPA)

wewe nayeye wote haziwatoshi ndomaana unampasapot,au wewe nimmoja katiya watoto wakenn?
 
Unajua wakati nimesikia JK atakutana na Ujumbe wa CDM, nilitoa ki hint humu kwamba CDM hawatakuwa wamewakilishwa na Ujumbe wa viongozi wao pekee nikitegemea wao watanisoma na pengine kufikiria kupeleka ujumbe ulokuwa na watu kutoka vyama vingine, taasisi na kamati za katiba zilizoundwa. Nilitegemea sana wataambatana na watu kama Salim, Warioba na wataalam kwenye maswala kama haya. Lakini ndio hivyo tena imeshakuwa...

Mkuu wangu kwa kweli kuilaumu CHADEMA kwamba walikataa kuwashirikisha makundi mengine kwenda kumwona Rais nadhani tutakuwa tunawaonea bure; kwanza sio kazi yao na pia sidhani kama hayo makundi mengine wakiwamo hao wazee ulowataja wangekubali kirahisi hivyo na ukizingatia kigezo cha muda.

Mimi nadhani adui namba moja katika hili ni Bunge letu. Hiki kinapaswa kuwa chombo cha kuwaunganisha wananchi wote kwa kuweka utaifa mbele badala ya vyama na itikadi lakini halikufanya hivyo. Walikuwa na kila mamlaka ya kikatiba kuitaka serikali ifanye chochote kwa maslahi ya wote, lakini hawakufanya hivyo. Badala ya kujadili hoja wakaishia kujadili watu!

Adui nambari moja wa taifa hili kwa sasa ni Bunge hili la kishabiki; Bunge lililopewa uwezo wote na wananchi badala yake likajigeuza kuwa Bunge la kutetea maslahi yao na ya wachache. CHADEMA wala Serikali hawapaswi kulaumiwa.
 
Unaona sasa! Hicho Chadema walichokuwa wanapigania ni kwa maslahi yao au ya Watanzania wote ukiwemo wewe. Wewe unaona ni Chadema wameadhirika wakati siku zote unalia nchi inaelekea kubaya....hujui chanzo? Kama mawazo ya wasomi ni haya na kule vijijini itakuwaje?

Kubali usikubali CDM wameingia choo cha kike
 
Kama maoni yatawasilishwa bungeni kama schedule of amendments,kuna guarantee gani kwamba maoni hayo yanaweza kupitishwa au kuridhiwa na bunge ambalo majority ni wa CCM?Je tuna uhakika milango yote ya ghiliba kutoka chama tawala itakuwa imefungwa?

Kungekuwa na madhara gani kama isingesainiwa na marekebisho yakafanywa kwa kuaminiana?nauliza hivyo kama mtanzania asiye na taarifa kamili....
 
Back
Top Bottom