Rais Kikwete amteua bwana Sisco kuwa Balozi

Aliyekuwa mkuu wa itifaki Bwana Abdul Sisco amekuwa balozi mpya wa Tanzania Malyasia.

Rais pia ameteua mkuu mwingine wa itifaki.



Source: Ikulu, na habari zaidi tusubiri magazeti ya kesho!

Hongera sana Sisco. Mimi nakupongeza sana.

Lakini labda naomba kuuliza kidogo je kuna vigezo vyovyote vinavyotumika katika kuchagua mtu kuwa balozi?

Je mtu yeyote Tanzania anaweza kuwa Balozi?

Je kila mtu akipiga Mkwara akapewa madaraka, itakuwaje kama nafasi zitakuwa zimeisha? Si ndiyo mwanzo wa kushikana mashati?

A well deserved appointment for a Civil servant of his calibre!
Mwanadiplomasia!
But what are the motives for bringing this to Jukwaa la siasa?
Curious?

Rais Kikwete ateua Cisco, Biswaro mabalozi Malaysia, Brazil Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete amewateua mabalozi wapya kuiwakilisha Tanzania katika nchi za Brazil na Malaysia.



Taarifa iliyotolewa jana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imesema kuwa rais amemteua Balozi Joram Biswaro kuwa balozi wa Tanzania nchini Brazil na Balozi Abdul Cisco Mtiro kuwa balozi wa Tanzania nchini Malaysia. Uteuzi huo utaanza mara moja.

Kabla ya uteuzi huo, Balozi Biswaro alikuwa Mkurugenzi Idara ya Asia na Australia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Balozi Mtiro alikuwa Mkuu wa Itifaki katika wizara hiyo.



Pia Rais Kikwete amemteua Anthony Itatiro kuwa Balozi na Mkuu wa Idara ya Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Itatiro alikuwa Mnikulu katika ofisi ya Rais.

Ningependa kusahihisha tu kuwa Cisco Mtiro tayari alishateuliwa kuwa Balozi tangu enzi za Mkapa wakati alipokuwa anaiwakilisha Tanzania katika nchi zinazozungumza kifaransa kule West Africa na kituo chake cha kazi kilikuwa Nigeria

labda waandishi wetu wangeuliza hili wangeambiwa lakini ndio hivyo tena

Vile vile ningependa kuchukua fursa hii kuwaweka wazi kuwa HALISI si credible pamoja na sources zake kwani mwezi wa pili alikuja humu na thread iliyodai kuwa JK AMFUKUZA KAZI CISCO lakini nilipombana hakuweza kuja na jibu linaloeleweka
 
Naona neno breaking news sasa limeanza kuwa na maana tofauti, for hakika hii haiwezi kuwa breaking news, tuache utani jamani!
 

Ningependa kusahihisha tu kuwa Cisco Mtiro tayari alishateuliwa kuwa Balozi tangu enzi za Mkapa wakati alipokuwa anaiwakilisha Tanzania katika nchi zinazozungumza kifaransa kule West Africa na kituo chake cha kazi kilikuwa Nigeria

labda waandishi wetu wangeuliza hili wangeambiwa lakini ndio hivyo tena


Ndo nikasema sasa tunaanza ku-misuse breaking news!
 
game theory, heshima kwako.
hapana cisco hajapata kuwa balozi nigeria bali alikuwa huko kama afisa mwandamizi. hii ni mara ya kwanza kwa balozi cisco kupewa kituo (nchi) katika wadhifa huo.
 
How so? Please explain...
With all due respect Curious was the keyword and the answer I got was satisfying "perhaps because this is the most view thread in this forum",although dougbtful I agree with you;)

Having a problem for it being here NO! I was just in reference to some of the J.F members that some threads are better off in other forums kama hii, to Vibweka vya Wakubwa here also in reference to the thread P.Kalaghe ateuliwa balozi canada...In this sikuona uhusiano wowote wa kisiasa na ndio curiosity inaposimama;)
I did not think :rolleyes: such a Headline should be politicized or in this matter Cisco awa Balozi qualify to be in a political forum!
Hivyo tu!
 
game theory, heshima kwako.
hapana cisco hajapata kuwa balozi nigeria bali alikuwa huko kama afisa mwandamizi. hii ni mara ya kwanza kwa balozi cisco kupewa kituo (nchi) katika wadhifa huo.


Sasa kama kuna mchemsho, huu ni wa nani Ikulu, CMB au nani hii...........................

JK appoints envoys to Malaysia, Brazil

A Correspondent Daily News said:

Friday,November 09, 2007 @00:02

PRESIDENT Jakaya Kikwete has appointed Dr. Joram Mukama Biswaro to serve as ambassador to Brazil and Mr Abdul Cisco Mtiro as High Commissioner to Malaysia, in changes that saw Mr Anthony Itatiro become the Chief of Protocol. Formerly the State House Comptroller, Mr Anthony Itatiro replaces Mr Cisco as the Chief of Protocol.

He will hold the rank of ambassador, a statement from the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation said yesterday. The appointments are with immediate effect. Before the appointment, Ambassador Dr Biswaro, a career diplomat and journalist, was a Director of Asia and Australasia in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation.

He also served as the Acting Director for Africa and Middle East and Director for Africa. Dr Biswaro, who holds a PhD in Regional Integration and a Masters of Arts in Diplomacy degree from the Washington University, is also fluent in Portuguese and served in various capacities as a Foreign Service Officer in Tanzania missions in Mozambique and Ethiopia.

He also studied BA in International Relations at the University of Dar es Salaam and Post-graduate Diploma in Conference Diplomacy at the Institute of Social Studies (ISS). He also holds a Diploma in Journalism from the then Tanzania School of Journalism (TSJ). Ambassador Itatiro, a career diplomat joined the Foreign service in 1982 and was in 2000 appointed Deputy Chief of Protocol, before being posted to the Democratic Republic of Congo, as the Acting Head of the Mission and Charge de Affaires.

In 2004, he was appointed by the President to be the Deputy State House Comptroller and Comptroller in 2006. He holds a BA in International Relations from the University of Dar es Salaam and a post-graduate Diploma in International Relations and diplomacy. Ambassador Mtiro is a graduate in International Relations from the University of Dar es Salaam.
 
sidhani kama kuna mchemsho katika taarifa hiyo. mtu anaweza kuteuliwa balozi kama wadhifa/cheo (waweza kuwa balozi lakini huna kituo nje ya nchi), na pia baada ya kuwa balozi wa wadhifa/cheo anaweza kuteuliwa tena kuwakilisha nchi katika nchi nyingine ( hapo tena inaweza semwa "ateuliwa kuwa balozi nchini malaysia")
 
Joram Mukama Biswaro ..kapambwaaaaaa halafu
Mshikaji kaambulia sentensi moja, ngoja niende shule na mimi:

"Ambassador Mtiro is a graduate in International Relations from the University of Dar es Salaam."

Shule muhimu sana!
 
naomba nikusahihishe ndugu yangu GAME THEORY ni kwamba sisco aliposhindwa uchaguzi wa temeke na mrema alipata post ya kwenda ubalozini nigeria akiwa afisa wa mwandamizi wa mambo ya nje na hakuwa balozi kamili,lakini aliporudi nyumbani baadaye aliteuliwa kuwa mkuu wa itifaki na kwa mujibu wa utaratibu wa mambo ya nje ili uwe mkuu wa idara kwanza ni lazima uwe na cheo cha ubalozi,hivyo sisco alipandishwa kutoka afisa mwandamizi wa mambo ya nje na kuwa balozi and then akapewa ukuu wa itifaki kama ilivyo kwa itatilo ambaye alikuwa mnikulu,lakini sasa kapandishwa kuwa balozi na moja kwa moja kapewa ukuu wa itifaki
 
Amepangiwa kituo cha kazi??? au ameteuliwa kuwa balozi???.


Quote:
Halisi3rd May 2007, 10:29 AM
Kwanza baada ya Kalaghe kuna habari kwamba, Abdul Cisco Mtiro naye atapangiwa kituo, na huenda ikawa ni katika nchi za kiarabu. lakini Habari ni kwamba, Kalaghe alikua na uhakika wa kuula na kwamba alishawaambia watu kwamba asipopewa nafasi "ATALIPUA MABOMU" ya wakubwa. SIna hakika ni mabomu gani, lakini kama hivyo ndivyo basi ni hatari kwa MASLAHI YA TAIFA KAMA MTU ANAKU NA JEURI KAMA HIYO. TUKATAE, TUKUMBUKE ENZI ZA MWALIMU JK, ambaye hakukubali hata mara moja kuwa MTUMWA.

JAMBO LINGINE NAOMBA WANA JF MUNISAIDIE, Wale mabalozi waliotangazwa kuiteuliwa akiwamo bwana MAharange aliyehamishwa kutoka DRC, wameshaapishwa? kama bado kwanini? Kuna habari kwamba hawajaapishwa kwa sababu hawajateuliwa!!!! If that is true, again ITAKUWA INATISHA

Source:Halisi 3rd May 2007, 10:29 AM
Title of thread: PETER KALAGHE ATEULIWA BALOZI CANADA (baada ya kushindwa kupandisha website ya IKULU

Wakati mwingine tuwe tunakubali kwamba JF ni kiboko, kuliko hata any news media in Tanzania. Thanks Mwanamalundi, BRAVO JF
 
Hivi jamani, ni kusema Mtiro kapanda cheo au kashushwa?
Ipi nafasi bora!
 
bush_TZAmb_600.jpg
 
Cisco mtiro ni rafiki mkubwa wa JK. Kabla hata ya uchaguzi wa 2005, Cisco alipewa ahadi ya kuwa balozi wa Tanzania Marekani iwapo JK atashinda urais. Hili suala lilikuwa limeshajulikana i.e. kwamba cisco ataenda kuwa balozi Washington D.C na alikuwa analizungumza wazi. What happened after that? kama kawaida, before balozi hajateuliwa, jina lake linapelekwa department of state/wizara ya mambo ya nje for scrutiny. Habari za kuaminika ni kwamba jina la Cisco halikurudi na hii huwa ina maana kwamba US state department hawajamkubali. As a result, akateuliwa mwingine kwenda US na cisco akawa anasubiri kituo kingine kipya.

Sababu za Cisco kukataliwa zipo wazi miongoni mwa maafisa wa foreign affairs Tanzania. Wanachosema wanadiplomasia wengi ni kwamba CIsco alikuwa close na uongozi wa wizara ya mambo ya nje (uongozi wa prior to 2005), uongozi ambao mataifa mengi kama marekani yalikuwa very disappointed na shughuli na mienendo ya maafia wake. Mabalozi kadhaa akiwepo wa marekani alifikia hatua ya kuandika memos to Mkapa on these matters.

Tukianzisha sheria ya bunge ku scrutinize wateule wote wa rais tutapunguza uteuzi wa mafisadi na wahuni ambao wote kwa pamoja hayati nyerere alisema tuwakwepe kama ukoma.
 
Cisco mtiro ni rafiki mkubwa wa JK.

Tukianzisha sheria ya bunge ku scrutinize wateule wote wa rais tutapunguza uteuzi wa mafisadi na wahuni ambao wote kwa pamoja hayati nyerere alisema tuwakwepe kama ukoma.

Very good observation mzee.
 
Joram Mukama Biswaro ..kapambwaaaaaa halafu
Mshikaji kaambulia sentensi moja, ngoja niende shule na mimi:

"Ambassador Mtiro is a graduate in International Relations from the University of Dar es Salaam."

Shule muhimu sana!

...............kazi muhiimu ! huyo Itatiro mavyeti yoote hayo kwani anaenda chuo kufundisha !?
 
Kuna upotoshaji hapo juu.Mtu akishakua charge de"Affaires anakua na cheo cha juu kwa hiyo kupewa Cheo cha Ubalozi si jambo la ajabu
 
Back
Top Bottom