Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
RAIS wa Zanzibar na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Amani Abeid Karume amesema hali ni shuwari Zanzibar na kuwataka wanasiasa katika Kisiwa cha Pemba kupingana kwa hoja na wale wasioweza kujenga hoja waondoke katika ulingo wa siasa.
Hayo ameyaeleza wakati akizungumza katika uzinduzi wa shule ya msingi ya Wingwi Mtemani katika Mkoa wa Kaskazini Pemba jana ambapo alisema kwamba kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa kutumia jukwaa la kisiasa kwa kueleza mambo ya vitisho kutokana na kushindwa kujenga hoja za maana.
Tupingane bila kupigana kwa maana tukipingana kwa hoja ndio demokrasia kama hoja zimeisha wewe tulia tu katafute mhogo na samaki wako wa tasi ule sio kuleta vitisho alionya Rais Karume.
Alisema kuwa Zanzibar imekuwa ni nchi ya amani na utulivu tokea miaka ya chuma hivyo mtindo uliojitokeza katika siku za karibuni wa kuchoma moto nyumba hauna maslahi kwa wananchi na badala yake aliwataka wanasiasa waliofilisika kufunga virago na kutafuta shughuli ya kufanya.
Zanzibar kuna amani tena utulivu wa kutosha wau wanafanya shughuli zao za kawaida na tunawalika wengine pia waje kutembelea visiwa hivi na wachane na wale watu wanaosema kuwa Zanzibar hakukaliki alisema Rais Karume.
Kaika hatua nyengine Rais Karume alivitaka vyombo vya habari hasa vya nje ya Zanzibar kuacha kuandika mambo ya uchochezi dhidi ya Zanzibar na badala yake vifanye kazi kwa mujibu wa maadili na taaluma ya habari.
Rais karume alisema kwamba katika siku za hivi karibuni habari nyingi zinazoandikwa kuhusu Zanzibar zimekuwa zikitiwa chumvi huku zikipambwa kwa vichwa cha habari mbali mbali kwa lengo la kuuza magazeti ikiwemo zile za Zanzibar kwawaka moto, nyumba zachomwa Zanzibar na mambo mengine na kusisitiza kuwa jukumu kubwa la vyombo vya habari ni kutoa elimu kwa kujenga jamii bora na sio kuchochea mifarakano.
Aidha aliwaonya wanafunzi kuacha kujiingiza katika mambo ya siasa kwani kwa kufanya hivyo wanaweza wakakubwa na matatizo mbali mbali ikiwemo ya kufikishwa katika vyombo vya sheria ikiwa watawasikiliza wanasiasa waliofilisika ambao wamekuwa wakiwaotosha.
Aliwataka wanafunzi hao kukataa kutumiwa na wanasiasa kwa kufanya udanganyifu kwenye vyeti vya kuzaliwa ili wajipatie vitambulisho vya mzanzibari mkaazi wanaweza wakajikuta wanaishia mahakamani na wanasiasa hawatawasaidia kitu zaidi ya kuwakimbia.
Aliwahimiza wenye sifa za kusajiliwa kupatiwa vitambulisho vya mzanzibari wende katika afisi za idara hiyo kwani kufanya hivyo watakuwa wanatetea haki yao lakini aliwakumbusha kuwa serikali haitawavumilia wale watakaofanya udanganyifu.
Wakati Rais Karume akitoa tahadhari hiyo tayari mwanafunzi mmoja wa kidatu cha tatu katika shule ya sekondari Kisiwani Pemba amemaliza kutumikia kifungo cha wiki mbili jela baada ya kupatikana na hatia ya kufanya udanganyifu wa cheti cha kuzaliwa katika wilaya ya wete mkoa wa kaskazini Pemba.
Ziara ya Rais Karume ni ya siku moja ya kufungua shule hiyo ya wingwi iliyoanza na wanafunzi 890 ambayo imejengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na michango kutoka kwa wadau mbali mbali ikiwemo serikali ya mapinduzi Zanzibar.
Awali akimkaribisha Rais Karume Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Haroun Ali Suleiman alisema kwamba serikali itaendelea na juhudi za ujenzi wa shule karibu na makaazi ya wananchi.
Waziri Haroun nae aliwaasa wanafunzi kuzingaia masomo na kuachana na vitendo vya kujihusisha katika mambo ya kisiasa sambamba na kutoa onyo kali kwa walimu kwamba serikali haitawavumilia watakaochanganya kazi na siasa.
Alisema kuna taarifa kwamba wapo baadhi ya walimu wanajishirikisha na siasa na hivyo kuwataka waachane na tabia hiyo kwani kufnaya hivyo kunaweza kuwasababishai matatizo katika kazi zao.
Nimepata taarifa kuwa wapo baadhi ya walimu wanajiingiza katika siasa lakini mimi nawaambia waache mambo hayo maana nasikia mwalimu mmoja ameshiriki kupiga watu mawe nasema isije ikawa kama mwaka 1995 nasema msiturudhise nyuma alisema Waziri huyo.
Alisema mwaka 1995 walimu wengi wlaifukuzwa kazi baada ya kudhaniwa wanajiingiza katika siasa lakini katika awamu hii ya Rais Karume hakuna mwalimu haa mmoja aliyefukuzwa kazi hivyo aliwataka kuachan ana kujishirikisha katika siasa ili waendelee na kazi zao wasije wakafukuzwa.
SOURCE:ZANZIBAR YETU WEB BLOG.
Hayo ameyaeleza wakati akizungumza katika uzinduzi wa shule ya msingi ya Wingwi Mtemani katika Mkoa wa Kaskazini Pemba jana ambapo alisema kwamba kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa kutumia jukwaa la kisiasa kwa kueleza mambo ya vitisho kutokana na kushindwa kujenga hoja za maana.
Tupingane bila kupigana kwa maana tukipingana kwa hoja ndio demokrasia kama hoja zimeisha wewe tulia tu katafute mhogo na samaki wako wa tasi ule sio kuleta vitisho alionya Rais Karume.
Alisema kuwa Zanzibar imekuwa ni nchi ya amani na utulivu tokea miaka ya chuma hivyo mtindo uliojitokeza katika siku za karibuni wa kuchoma moto nyumba hauna maslahi kwa wananchi na badala yake aliwataka wanasiasa waliofilisika kufunga virago na kutafuta shughuli ya kufanya.
Zanzibar kuna amani tena utulivu wa kutosha wau wanafanya shughuli zao za kawaida na tunawalika wengine pia waje kutembelea visiwa hivi na wachane na wale watu wanaosema kuwa Zanzibar hakukaliki alisema Rais Karume.
Kaika hatua nyengine Rais Karume alivitaka vyombo vya habari hasa vya nje ya Zanzibar kuacha kuandika mambo ya uchochezi dhidi ya Zanzibar na badala yake vifanye kazi kwa mujibu wa maadili na taaluma ya habari.
Rais karume alisema kwamba katika siku za hivi karibuni habari nyingi zinazoandikwa kuhusu Zanzibar zimekuwa zikitiwa chumvi huku zikipambwa kwa vichwa cha habari mbali mbali kwa lengo la kuuza magazeti ikiwemo zile za Zanzibar kwawaka moto, nyumba zachomwa Zanzibar na mambo mengine na kusisitiza kuwa jukumu kubwa la vyombo vya habari ni kutoa elimu kwa kujenga jamii bora na sio kuchochea mifarakano.
Aidha aliwaonya wanafunzi kuacha kujiingiza katika mambo ya siasa kwani kwa kufanya hivyo wanaweza wakakubwa na matatizo mbali mbali ikiwemo ya kufikishwa katika vyombo vya sheria ikiwa watawasikiliza wanasiasa waliofilisika ambao wamekuwa wakiwaotosha.
Aliwataka wanafunzi hao kukataa kutumiwa na wanasiasa kwa kufanya udanganyifu kwenye vyeti vya kuzaliwa ili wajipatie vitambulisho vya mzanzibari mkaazi wanaweza wakajikuta wanaishia mahakamani na wanasiasa hawatawasaidia kitu zaidi ya kuwakimbia.
Aliwahimiza wenye sifa za kusajiliwa kupatiwa vitambulisho vya mzanzibari wende katika afisi za idara hiyo kwani kufanya hivyo watakuwa wanatetea haki yao lakini aliwakumbusha kuwa serikali haitawavumilia wale watakaofanya udanganyifu.
Wakati Rais Karume akitoa tahadhari hiyo tayari mwanafunzi mmoja wa kidatu cha tatu katika shule ya sekondari Kisiwani Pemba amemaliza kutumikia kifungo cha wiki mbili jela baada ya kupatikana na hatia ya kufanya udanganyifu wa cheti cha kuzaliwa katika wilaya ya wete mkoa wa kaskazini Pemba.
Ziara ya Rais Karume ni ya siku moja ya kufungua shule hiyo ya wingwi iliyoanza na wanafunzi 890 ambayo imejengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na michango kutoka kwa wadau mbali mbali ikiwemo serikali ya mapinduzi Zanzibar.
Awali akimkaribisha Rais Karume Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Haroun Ali Suleiman alisema kwamba serikali itaendelea na juhudi za ujenzi wa shule karibu na makaazi ya wananchi.
Waziri Haroun nae aliwaasa wanafunzi kuzingaia masomo na kuachana na vitendo vya kujihusisha katika mambo ya kisiasa sambamba na kutoa onyo kali kwa walimu kwamba serikali haitawavumilia watakaochanganya kazi na siasa.
Alisema kuna taarifa kwamba wapo baadhi ya walimu wanajishirikisha na siasa na hivyo kuwataka waachane na tabia hiyo kwani kufnaya hivyo kunaweza kuwasababishai matatizo katika kazi zao.
Nimepata taarifa kuwa wapo baadhi ya walimu wanajiingiza katika siasa lakini mimi nawaambia waache mambo hayo maana nasikia mwalimu mmoja ameshiriki kupiga watu mawe nasema isije ikawa kama mwaka 1995 nasema msiturudhise nyuma alisema Waziri huyo.
Alisema mwaka 1995 walimu wengi wlaifukuzwa kazi baada ya kudhaniwa wanajiingiza katika siasa lakini katika awamu hii ya Rais Karume hakuna mwalimu haa mmoja aliyefukuzwa kazi hivyo aliwataka kuachan ana kujishirikisha katika siasa ili waendelee na kazi zao wasije wakafukuzwa.
SOURCE:ZANZIBAR YETU WEB BLOG.