Rais Kabila Anusurika Kuuliwa

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
Watu tisa wamefariki dunia baada kundi la watu wenye silaha kuivamia ikulu ya jamhuri ya Kongo na kupambana na walinzi wa ikulu wakiwa na nia ya kumuua rais Joseph Kabila.
Kundi la watu wenye silaha wakiwa na bunduki na mapanga waliyavamia makazi ya rais wa Jamhuri ya Kongo, Jospeh Kabila wakiwa na nia ya kumuua rais huyo na kuipindua serikali yake.

Mapambano makali yaliyodumu takribani lisaa limoja yalizuka baina ya walinzi wa ikulu na kundi hilo ambapo watu saba toka kwenye kundi hilo waliuawa huku walinzi wawili wa ikulu nao wakipoteza maisha yao.

Rais Kabila na mkewe hawakuwepo ndani ya makazi hayo wakati shambulio hilo lilipotokea.

Waziri wa mawasiliano, Lambert Mende alijitokeza kwenye televisheni ya taifa na kusema kuwa hali sasa iko shwari.

"Hawa watu walitaka kumdhuru rais Kabila", alisema waziri Mende na kuongeza kuwa baadi ya watu toka kwenye kundi lililofanya shambulizi hilo waliuliwa na wengine walikamatwa na kutiwa mbaroni.

Rais Joseph Kabila alichaguliwa katika uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia mwaka 2006 na ana mpango wa kugombea tena katika uchaguzi ujao mwezi novemba mwaka huu.

Alirithi urais toka kwa baba yake, Laurent Kabila aliyeuliwa mwaka 2001.
 
Dah Inabidi kuongeza ulinzi sana kwake...Hawa Jamaa hawana mchezo.....Lakini habari zinasema bwana alikuwa kwenye makazi yake...
 
mambo ya kiintelijensia hayo lazima yatachanganya tu sijui mie nimesoma magazeti mengi wanasema hakuwepo sasa sijui si unajua sababu za kiusalama na kutaka kuonyesha kwamba jeshi halina udhaifu yawezekana alikuwepo ama hakuwepo!ila nashangaa inakuwaje wavamizi wafike mpaka ikulu ina maana ulinzi hautoshii nina maana ana walinzi wachache??
Dah Inabidi kuongeza ulinzi sana kwake...Hawa Jamaa hawana mchezo.....Lakini habari zinasema bwana alikuwa kwenye makazi yake...
 
mambo ya kiintelijensia hayo lazima yatachanganya tu sijui mie nimesoma magazeti mengi wanasema hakuwepo sasa sijui si unajua sababu za kiusalama na kutaka kuonyesha kwamba jeshi halina udhaifu yawezekana alikuwepo ama hakuwepo!ila nashangaa inakuwaje wavamizi wafike mpaka ikulu ina maana ulinzi hautoshii nina maana ana walinzi wachache??

Hii mambo ya congo bana...inawezekana kabisa mpango mzima ulikuwa kwenye hao hao presindental guards kama kwa baba yake ilivyo kuwa...inaweza kuwa kuna mtu kachomekwa..ndani ya systeam...ila ali miss target wakati wa kuvamia...kwani walifika mpaka ikulu..kama 50m ndio wakazuiwa kwenye road block hapo ndio shughuli ikaanzia..

Jamaa atagombea tena mwaka huu november na bado kuna upinzani upande wa mashariki mwaka DRC...ndio ambako hajakamanata sana..bado kuna internation peace keeper kwenye nchi..maneo ya Bunia,Goma Ben...haijatulia kabisa..I hope atajiongezea ulinzi..au apeleke wengine mafunzoni Ufaransa..
 
kweli madaraka ni gharama sana mie nilidhani ataogopa kugombea hivi kwanini CONGO haitawaliki tatizo kubwa ni nini yaani naona watu wanashindwa kua pamoja kabisa!na hali hii sijui kama itakuja kutulia!
Hii mambo ya congo bana...inawezekana kabisa mpango mzima ulikuwa kwenye hao hao presindental guards kama kwa baba yake ilivyo kuwa...inaweza kuwa kuna mtu kachomekwa..ndani ya systeam...ila ali miss target wakati wa kuvamia...kwani walifika mpaka ikulu..kama 50m ndio wakazuiwa kwenye road block hapo ndio shughuli ikaanzia..

Jamaa atagombea tena mwaka huu november na bado kuna upinzani upande wa mashariki mwaka DRC...ndio ambako hajakamanata sana..bado kuna internation peace keeper kwenye nchi..maneo ya Bunia,Goma Ben...haijatulia kabisa..I hope atajiongezea ulinzi..au apeleke wengine mafunzoni Ufaransa..
 
I cant imagine eti watu watoke kwenda kuvamia ikulu....i cant think of it at this era.
 
I cant imagine eti watu watoke kwenda kuvamia ikulu....i cant think of it at this era.

Anything is possible now.. Watu wamechoka maisha ya mulo mmjoa kwa siku. Na Congo with all its richness...utashanga saana cku utaenda Kinshasa..umaskini wakutisha, na hapo ni mji mkuu. Sasa fikiria miji mingine kama bukavu, goma n.k..??
 
Tatizo la huyu jamaa (Comrade Kabila Jr.) hajui kusoma alama za nyakati au sijui ni ubishi wakee tuu, raia wameisha mchoka lakini yeye amebakia kuwa king'ang'anizi sita shangaa nikisikia kafanyiwa kitu mbaya kama babake!
 
Mwanangu sio tatizo lake tu kila kiongozi mwafrica akiishakaa hataki kutoka unakumbuka ya kibaki wa kenya!!mie sijawahi kusikia kama msumbiji kuna matatizo kama haya ya kung'ang'ania madaraka sijui kwanini hawa jamaa mie naona akiondoka vizuri itasaidia sana hata kujenga mshikamano kwa raia wake hata hapa kwetu tanzania CCM wasingekua wanatumia ubabe mie nadhani watu bado wengi tu wangekua wanakipenda chama ila kwa sasa wanakichukia sababu kimekua kinatumia ubabe mwingi kwenye maamuzi na kuwakandamiza watu wa hali ya chini ama kweli taabu tu
Tatizo la huyu jamaa (Comrade Kabila Jr.) hajui kusoma alama za nyakati au sijui ni ubishi wakee tuu, raia wameisha mchoka lakini yeye amebakia kuwa king'ang'anizi sita shangaa nikisikia kafanyiwa kitu mbaya kama babake!
 
kweli madaraka ni gharama sana mie nilidhani ataogopa kugombea hivi kwanini CONGO haitawaliki tatizo kubwa ni nini yaani naona watu wanashindwa kua pamoja kabisa!na hali hii sijui kama itakuja kutulia!

Basicaly Congo juu ya utajiri mkubwa wa Madini mbali,Misitu,Mito...pande za kusini(North Kivu) na mashariki tena ambako kuna copper na jicho la mmarekani liko uko..then kuna Uraniu, nchi una utajili mwingi wa asili sana...ambao bado haujaanza hata kutafitiwa..

So yote haya kila mwanasiasa anatama awa ontop either kwa nguvu au democrasia...achilia mbali majeshi ya nchi zingine kuingia na kufanya vurugu..na kuchukua miti na hata dhahabu...kupita north ambako uganda,burundi na rwanda zinashabihiana.

So west countries ambako lina watu wao wengi sana...wanafanya mambo mbali mbali kujua nini kinapatikana zinaweza zenyewe kwa zeneyewe kuwa na makundi..kama nchi zinazo msaport Jean Mbemba...na za Kabila...so zinakuwa zina mpa uwezo flan flan achukue mamlaka ili weweze kuingia kirahisi...etc...Ndio issue kuu...Uku.
 
Watu tisa wamefariki dunia baada kundi la watu wenye silaha kuivamia ikulu ya jamhuri ya Kongo na kupambana na walinzi wa ikulu wakiwa na nia ya kumuua rais Joseph Kabila.
Kundi la watu wenye silaha wakiwa na bunduki na mapanga waliyavamia makazi ya rais wa Jamhuri ya Kongo, Jospeh Kabila wakiwa na nia ya kumuua rais huyo na kuipindua serikali yake.

Mapambano makali yaliyodumu takribani lisaa limoja yalizuka baina ya walinzi wa ikulu na kundi hilo ambapo watu saba toka kwenye kundi hilo waliuawa huku walinzi wawili wa ikulu nao wakipoteza maisha yao.

Rais Kabila na mkewe hawakuwepo ndani ya makazi hayo wakati shambulio hilo lilipotokea.

Waziri wa mawasiliano, Lambert Mende alijitokeza kwenye televisheni ya taifa na kusema kuwa hali sasa iko shwari.

"Hawa watu walitaka kumdhuru rais Kabila", alisema waziri Mende na kuongeza kuwa baadi ya watu toka kwenye kundi lililofanya shambulizi hilo waliuliwa na wengine walikamatwa na kutiwa mbaroni.

Rais Joseph Kabila alichaguliwa katika uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia mwaka 2006 na ana mpango wa kugombea tena katika uchaguzi ujao mwezi novemba mwaka huu.

Alirithi urais toka kwa baba yake, Laurent Kabila aliyeuliwa mwaka 2001.


CORRECTION:
1. Tukianza na Headline:
RAIS KABILA ANUSURIKA KUUWAWA SIO KUULIWA

2. Katika kiswahili hakuna wingi wa saa, (yaani huwezi kusema masaa) ni SAA hata kama ni 1000

3. Usiseme Mapambano makali yaliyodumu takribani lisaa limoja
Sema Mapambano makali yaliyodumu takribani saa moja

Tusaidiane kukuza kiswahili chetu kwa kukitumia kwa ufasaha: hapo kwenye masaaa wengi wanapata sana taabu hata waandishi na watangazji wa redio, mpaka kwenye matangazo ya kampuni za simu utasikia ONGEA KWA MASAA 24
Asanteni kwa kunisikiliza.
 
hahaaaaaaaaam haaya bwana malenga wetu
CORRECTION:
1. Tukianza na Headline:
RAIS KABILA ANUSURIKA KUUWAWA SIO KUULIWA

2. Katika kiswahili hakuna wingi wa saa, (yaani huwezi kusema masaa) ni SAA hata kama ni 1000

3. Usiseme Mapambano makali yaliyodumu takribani lisaa limoja
Sema Mapambano makali yaliyodumu takribani saa moja

Tusaidiane kukuza kiswahili chetu kwa kukitumia kwa ufasaha: hapo kwenye masaaa wengi wanapata sana taabu hata waandishi na watangazji wa redio, mpaka kwenye matangazo ya kampuni za simu utasikia ONGEA KWA MASAA 24
Asanteni kwa kunisikiliza.
 
Niliwahi kudokeza kwenye thread yangu moja on Jukwaa la Siasa kuwa marais kama Mugabe, Kabila, Museveni, CCM wakae mkao wa kufuturu maana saa ya ukombozi yaja na wala si mbali mtasikia mambo yakiitikia. Kama kakoswakoswa basi ujue yuko njiani kwenda kuonana na baba yake soon.
 
Basicaly Congo juu ya utajiri mkubwa wa Madini mbali,Misitu,Mito...pande za kusini(North Kivu) na mashariki tena ambako kuna copper na jicho la mmarekani liko uko..then kuna Uraniu, nchi una utajili mwingi wa asili sana...ambao bado haujaanza hata kutafitiwa..

So yote haya kila mwanasiasa anatama awa ontop either kwa nguvu au democrasia...achilia mbali majeshi ya nchi zingine kuingia na kufanya vurugu..na kuchukua miti na hata dhahabu...kupita north ambako uganda,burundi na rwanda zinashabihiana.

So west countries ambako lina watu wao wengi sana...wanafanya mambo mbali mbali kujua nini kinapatikana zinaweza zenyewe kwa zeneyewe kuwa na makundi..kama nchi zinazo msaport Jean Mbemba...na za Kabila...so zinakuwa zina mpa uwezo flan flan achukue mamlaka ili weweze kuingia kirahisi...etc...Ndio issue kuu...Uku.

Nakubaliana na wewe....its all bout western countries interests and this hurts......tunakufa sisi,wao wachukue madini wakaendeleza kwao sisi watuletee misaada......sasa yule Mbemba ile kesi iliisha? ataweza gombea tena kweli na ile kesi yake kama bado ipo? i also think Kabila is not strong enough!
 
Back
Top Bottom