Rais Jakaya Kikwete analipwa mshahara na posho kiasi gani? na analipa kodi kiasi gani?

Tatizo kubwa la watanzania leo hii ni Katiba mbovu. Hili ni moja ya madhara ya katiba kuwa kimya.
 
Mshahara wa Rais wako unataka kuujua ili iweje? Hilo siyo suala la kutangazatangaza ovyo tu kwasababu linaweza kuharibu usalama wa taifa. Lazima tuwe na heshima kidogo kwa mambo ya kitaifa.
<br />
<br />
How? Uwazi wa mshahara wa mkulu utaharibu vipi usalama wa taifa? Na usalama wa taifa ni nini? Siri na ufisadi hauharibu usalama wa wanainchi? Kiuchumi, kiafya, kijamii etc?
 
Watanzania wanalipa kodi saana tu tena maskini ndio ulipa zaidi sababu hana namna ya kukwepa,mfano katika kilo moja ya sukari we pay more than 400/= as a tax,kenya wametuzidi tax collections sababu wana viwanda vingi vinazalisha na kuexport ,lakini hapa kwetu ni Bakharesa tu,viwanda vyengine vinazalisha bidhaa za kuuza mbagala tu,after all kama Watanzania wangekuwa hawalipi kodi hizo pesa za kununullia Radar,ndege ya Rais nk zimetoka wapi?
wamarekani wote wanajua ni wajibu wao kulipa kodi, je wabongo wangapi wanalipa kodi. Jifananishe na Kenya wewe sio kurukia America.
 
Kama mishahara ya Obama,cameron,Angella,Sarkozy,Jacob zuma n.k. inajulikana why not wa Jakaya mrisho kikwete?
kwanini msiseme mshahara wa rais tu. Kuna haja gani mpaka msipecify? au ndo maana hamkuuliza wa ben, ali na julias?
I doubt ni hii asking yenu. Nitahoji baada ya JK kutoka madarakani.
 
Mishahara ya viongozi wakubwa wote ni siri,sababu za kiintelijensia.Mapato ya Rais kwa mwaka ni makubwa mno.........labda katiba mpya ikipatikana itatusaidia kufumbua hilo fumbo.
<br />
<br />
Anaweza akawa anajilipa hata ka nusu bajeti ka wizara moja eti.
 
Bado tuko nyuma mno katika kuweka mambo kama haya wazi, sitashangaa kwamba ni haki ya kila mtanzania kujua mkuu wa nchi analipiwa nini, nalipwa kiasi gani kwa mwezi na familia yake inatugharimu kiasi gani kui maintain.
Sitashangaa vile vile magamba wakikurupuka na kudai eti kwa sababu za kiusalama hawataweza kuweka hizi info in public!
Ndio loopholes kama hizi ambazo wabongo inabidi tuwe makini, tusidanganyike na mambo ya usalama kwa wakuu wa nchi, huku nchi inatafunwa bila maelezo kama yalivyotokea meremeta!
 
Mshahara wa Rais wako unataka kuujua ili iweje? Hilo siyo suala la kutangazatangaza ovyo tu kwasababu linaweza kuharibu usalama wa taifa. Lazima tuwe na heshima kidogo kwa mambo ya kitaifa.
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Mkuu hilo sio jambo la kitaifa ni jambo linaloihusu jamii inayoonzowa na hao watu.nchi masikini kama tz haiwezekani viongozi wake wakawa na mishahara mikubwa zaidi ya nchi zilizoendelea.
 
mshahara wake unabadilika kila mwezi kutokana na amepigiwa kelele kiasi gani ?
kelele iko directly proportional na mshahara
 
Mshahara wa Rais wako unataka kuujua ili iweje? Hilo siyo suala la kutangazatangaza ovyo tu kwasababu linaweza kuharibu usalama wa taifa. Lazima tuwe na heshima kidogo kwa mambo ya kitaifa.

mpumbavu kweli wewe
 
Sasa unataka ili nini wewe mshahara wako mbona mkeo haujui hebu tokeni hapa ....................badala ya kuzungumzia jinsi gani utajiendeleza uinue kipato unataka uujue ili ? hivi CDM kwanini katibu mkuu mwingine hata pewa mshahara na marupurupu mengine kama slaaaaaa?????

Utajiandeleza vipi ikiwa hufahamu namna ya kile ukipatacho kinavyotumika..?
 
Jamani ndugu zangu wana jf natamani sana kujua kiasi anacholipwa raisi ili niweze kupima eficient yake niweze kujua nnanyonywa kiasi gani kwani nnamuona raisi ka vile afanyi kazi yake ipasavyo amekua kama bendera ye anafuata tu upepo unapokwenda.
 
analipwa laki tatu mshahara sawa na tichaaaa.
Acheni utani basi kwenye ishu serious! Ni vyema mwananchi kujua mkuu wa nchi anapata kiasi gani toka kwenye jasho la watu wake na yeye anachangia kiasi gani kwenye jasho hili. Pia ningeshauri mishahara ya watumishi wote wa umma iangaliwe kujua kama kweli inakidhi mahitaji yao ili kupunguza ubadhirifu kwenye fedha za umma! Haiingii akilini Serikali inamlipa mtumishi wake laki tatu ambapo mtumishi huyu anaishi Dar es Salaam, ana familia (labda watoto wa3), amepanga, anawasomesha watoto, anajigharimia matibabu, analipa kodi, familia inakula, anasafiri kila siku kwenda na kurudi kazini, anachangia shughuli za kijamii na mambo mengine kibao. Je serikali imeshawahi kufikiria na kuainisha ni jinsi gani mtumishi huyu anavyopangilia matumizi ya huu mshahara? Kama bado basi serikali ijue wazi kuwa hili lina mchango mkubwa kwenye ufisadi na ufanisi duni wa sekta ya umma! Matokeo ya hili ni watumishi kuwepo kazini lakini ukweli hakuna wanachofanya huku serikali nayo ikijifanya inalipa mishahara ambayo haina tija yoyote kwa huyu mtumishi. Wanajamii, tulijadili hili kwa kina ili kuona mustakabali wa taifa letu unaelekea wapi.....
 
Wananchi tuna haki ya kujua mshahara na mapato ya raisi wetu, na Je analipa kodi kiasi gani? Obama anaweka mambo yote hadharani je sisi tunaficha nini? kwa nini mshahara wa raisi uwe siri wakati ni raisi wetu na tumempa ikulu yetu sasa kwa nini tusijue mshahara wake?

Usitarajie haya kwetu. Likitokea swala ambalo linawafavour wao, utasikia hata mataifa duniani wanafanya hivi. Ikitokea issue kama hii utasikia kiongozi huyuhuyu anasema 'kila nchi na utaratibu wake.
 
Kwa mujibu wa Jedwali la Pili la Sheria ya Kodi ya Mapato.........

EXEMPT AMOUNTS
(Made under section 10)
1.
The following amounts are exempt from income tax -
(a) amounts derived by the President of the United Republic or the President of the Revolutionary Government of Zanzibar from salary, duty allowance and entertainment allowance paid or payable to the President from public
funds in respect of or by virtue of the office as President;

Hata zile milioni 30 ambazo wabunge wote huwa wanapewa pindi wanapomaliza kipindi chao cha Ubunge pia huwa hazikatwi kodi. Hata zile posho za Wabunge pia hazikatwi kodi. Ila sisi wafanyakazi tunakatwa kodi kwa kwenda mbele!
 
Niliwahi kuambiwa kwamba mshahara anaolipwa Rais wa JMT ni mdogo kuliko mshahara anaokuwa analipwa Maximo, yule kocha wa Taifa Stars. Na wala siwezi kushangaa kusikia hivyo. Wanaweza kuuanika mshahara wa rais hapa na wote tukashangaa kwamba ni mdogo sana, na kwa mujibu wa sheria ya kodi ya mapato, rais hatakiwi kulipa kodi kutoka kwenye mshahara wake.

Lakini kumbukeni kwamba kwenye bajeti iliyopitishwa na Bunge kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012, ofisi ya Rais imetengewa Shs. 135 bilioni kwa ajili ya matumizi ya kitaifa/mbalimbali. Pesa hizi Mnyika alizihoji Bungeni lakini hakupewa ushirikiano wa kutosha toka kwa Wabunge wa Magamba. Fungu hili Rais anaweza kulitumia atakavyo, na kwa mujibu wa sheria, fungu hili huwa halikaguliwi na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali!
 
Huyu alijidai atataja mali zake akiingia madarakani hajaztaja mpaka leo!!! Itajakuwa mshahara???? Hehehe bado na zile pasenti za kina richmnd,jairo na wooote mafisadi angeanza na cha juu cha mikataba feki na kamishen za kina jairo hehehehehe kaz ipo
 
Niliwahi kuambiwa kwamba mshahara anaolipwa Rais wa JMT ni mdogo kuliko mshahara anaokuwa analipwa Maximo, yule kocha wa Taifa Stars. Na wala siwezi kushangaa kusikia hivyo. Wanaweza kuuanika mshahara wa rais hapa na wote tukashangaa kwamba ni mdogo sana, na kwa mujibu wa sheria ya kodi ya mapato, rais hatakiwi kulipa kodi kutoka kwenye mshahara wake.

Lakini kumbukeni kwamba kwenye bajeti iliyopitishwa na Bunge kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012, ofisi ya Rais imetengewa Shs. 135 bilioni kwa ajili ya matumizi ya kitaifa/mbalimbali. Pesa hizi Mnyika alizihoji Bungeni lakini hakupewa ushirikiano wa kutosha toka kwa Wabunge wa Magamba. Fungu hili Rais anaweza kulitumia atakavyo, na kwa mujibu wa sheria, fungu hili huwa halikaguliwi na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali!
Sasa kama hali iko hivi, hata asipolipwa chochote ana hasara gani?
 
Back
Top Bottom