MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,182
- 2,304
Ninafikiri wengi mtakubaliana na mimi kwamba tumejaliwa rais ambaye hapendi kuumiza kichwa kufikiri jinsi ya kutatua matatizo sugu ya wananchi wake kama umeme, Mauaji ya Arusha, migomo vyuo vikuu, matokeo mabaya ya kidato cha nne n.k. Ninafika mahali najiuliza hivi kama asipokuwepo nini kitaharibika kwa sababu uwepo wake au kutokuwepo kwake haku make any difference. Ingetosha tu kwa mawaziri wachache committed kuwepo na nchi ingekwenda tu.
Nasema hivi kwa sababu wakati nchi yetu imo katika matatizo makubwa yanayopelekea uchumi kwenda kombo ambapo tayari inflation imekwenda juu kutokana na shida ya umeme, rais huyu bado yuko kimya. Humsikii kabisa yeye kama baba wa familia ya nchi hii akiingilia kati na kutoa utatuzi wowote na badala yake ana katabia ka kutupia mawaziri wake mpira bila hata kuwapa hint ya nini kifanyike.
Rais wetu amekuwa mtu asiyependa kuumiza kichwa ktk kutatua matatizo makubwa ya watanzania bali yeye amekuwa akipendelea kufanya vitu virahisi rahisi ambavyo actually vilitakiwa vifanywe na wakuu wa Wilaya, wakuu wa mikoa au mawaziri.
Kwa mfano, wakati wabunge na mawaziri na watanzania wanaumiza vichwa jinsi ya kuondokana na matatizo ya umeme, yeye rais anapanda ndege kwenda kufukua nyayo za binadamu wa kale Ngorongoro.Baada ya kuzungukia miradi yake serengeti anarudi tena Tumbi kufungua kituo cha akina mama.
Hivi huyu amekuwa rais wa kufungua mikutano ,semina, kuhudhuria mazishi, kushuhudia matukio, kuwa mgeni rasmi n.k. Hivi vyote ni vitu rahisi ambavyo hata wakuu wa wilaya wengeweza kuvifanya na siyo rais anaomba Mungu ije barua ya mwaliko ili ajifanye yuko busy.
Hivi haya ndo tuliyomchagua ayafanye? ni kwa nini ni mwoga wa kuingilia kutoa solution badala ya vijembe kama rais? Hivi yeye kama rais aliyejidai capable uwezo wake umefika wapi katika kufanya tatizo la umeme historia, kushughulikia matatizo makubwa ya msingi yanayowakumba watanzania kwa sasa?
Kwani nini anawatega mawaziri ili waonekane hawawezi wakati ukweli ni kwamba anawatumia kama kinga huku akiwa hana kabisa dharira ya dhati ya kutatua tatizo husika?
Kwa nini ameshindwa kusimama katika nafasi yake kama rais wa nchi kuonyesha uwezo na uwepo wake?
Ninaomba ajue tunafuatilia kwa makini jinsi ambavyo amejiweka mbali na matatizo ya watanzania na kuamua kukaa mbali huku akiangalia matatizo ya watanzania kama movie ya vichekesho.
Naomba JK ujiulize kwa uaminifu kabisa kwa nini upo hapo kama kiongozi wa nchi wakati wa TZ wanakosa majibu ya matatizo yao kama umeme, kufeli kidato cha nne, mauaji Arusha N.k. Ina maana wewe uko busy kuliko Barak Obama wa US ambaye kila wakati siyo tu ana updated information za mambo yanayoendelea ktk nchi yake at his finger tips bali anayashughulikia kwa wakati muafaka.
Mkuu JK una viporo vingi sana vinavyosubiri majibu yako kama mtu mwenye mamlaka makubwa kuliko watu wote katika nchi hii. Hatuwezi kusubiri hadi utoe hotuba ya mwaka mpya tarehe 31/12/2011 tunahitaji utuambie wewe una solution gani kama rais. Tunataka tuone creativity au maadam wewe tatizo halikuhusu basi tukafilie mbali sisi.
Tunachotegemea sisi ni kwamba rais angekuwa yeye ndo anakula mfupa uliomshinda Ngeleja, Shukuru Kawambwa, Said Mwema, Pinda na mawaziri wengine.
Sasa mkuu wewe unafanya tu vitu vilaini na visivyo vya lazima na kuwaachia mawaziri vitu vyote vigumu bila msaada wowote?. Please JK take your position acha kukwepa majukumu kwani unadhalilisha cheo cha urais na unataka tuamini kwamba urais ni just symbolic na wala huna meno.
Ninavyoona JK unataka kuwa kama mfalme na siyo mtendaji mkuu wa serikali mwenye kufanya maamuzi makubwa na magumu kwa mustakabali wa nchi yetu na haswa watanzania wote.
Kwa ufupi tunashindwa kukuelewa. Kama ulijua urais mgumu kwa nini hukumwachia mtu mwingine basi agombee urais kuliko kutumia Ikulu kama kijiwe cha kupumzikia na kwenda kufanya matembezi ngorongoro, mikutanoni n.k.
Kwa ufupi mkuu JK ni jambo la wazi kabisa unawategea mawaziri na umewasukumia kazi zako zile ngumu na za kuumiza kichwa na za kwao rais ukachukuwa wewe.
Na ndiyo maana ninasema mkuu unaogopa majukumu yanayoumiza kichwa na badala yake unafanya vile vitu vyepesi then unajidai unaongoza nchi.
Hii nchi kwa sasa inajiongoza yenyewe kwa sababu umekimbia kiti na kama ni gari basi brake zimefeli tena likiwa linashuku mlima na hapa hatujui tutaangukia wapi.
Polisi na Mabomu ya machozi ndio mtindo mpya uliobaki wa kuongoza nchi.
Please rudi kwenye kiti uongoze nchi au declare umeshindwa tujue moja ila kwa namna nchi inavyokwenda ni kama haina rais kwa sasa
Nasema hivi kwa sababu wakati nchi yetu imo katika matatizo makubwa yanayopelekea uchumi kwenda kombo ambapo tayari inflation imekwenda juu kutokana na shida ya umeme, rais huyu bado yuko kimya. Humsikii kabisa yeye kama baba wa familia ya nchi hii akiingilia kati na kutoa utatuzi wowote na badala yake ana katabia ka kutupia mawaziri wake mpira bila hata kuwapa hint ya nini kifanyike.
Rais wetu amekuwa mtu asiyependa kuumiza kichwa ktk kutatua matatizo makubwa ya watanzania bali yeye amekuwa akipendelea kufanya vitu virahisi rahisi ambavyo actually vilitakiwa vifanywe na wakuu wa Wilaya, wakuu wa mikoa au mawaziri.
Kwa mfano, wakati wabunge na mawaziri na watanzania wanaumiza vichwa jinsi ya kuondokana na matatizo ya umeme, yeye rais anapanda ndege kwenda kufukua nyayo za binadamu wa kale Ngorongoro.Baada ya kuzungukia miradi yake serengeti anarudi tena Tumbi kufungua kituo cha akina mama.
Hivi huyu amekuwa rais wa kufungua mikutano ,semina, kuhudhuria mazishi, kushuhudia matukio, kuwa mgeni rasmi n.k. Hivi vyote ni vitu rahisi ambavyo hata wakuu wa wilaya wengeweza kuvifanya na siyo rais anaomba Mungu ije barua ya mwaliko ili ajifanye yuko busy.
Hivi haya ndo tuliyomchagua ayafanye? ni kwa nini ni mwoga wa kuingilia kutoa solution badala ya vijembe kama rais? Hivi yeye kama rais aliyejidai capable uwezo wake umefika wapi katika kufanya tatizo la umeme historia, kushughulikia matatizo makubwa ya msingi yanayowakumba watanzania kwa sasa?
Kwani nini anawatega mawaziri ili waonekane hawawezi wakati ukweli ni kwamba anawatumia kama kinga huku akiwa hana kabisa dharira ya dhati ya kutatua tatizo husika?
Kwa nini ameshindwa kusimama katika nafasi yake kama rais wa nchi kuonyesha uwezo na uwepo wake?
Ninaomba ajue tunafuatilia kwa makini jinsi ambavyo amejiweka mbali na matatizo ya watanzania na kuamua kukaa mbali huku akiangalia matatizo ya watanzania kama movie ya vichekesho.
Naomba JK ujiulize kwa uaminifu kabisa kwa nini upo hapo kama kiongozi wa nchi wakati wa TZ wanakosa majibu ya matatizo yao kama umeme, kufeli kidato cha nne, mauaji Arusha N.k. Ina maana wewe uko busy kuliko Barak Obama wa US ambaye kila wakati siyo tu ana updated information za mambo yanayoendelea ktk nchi yake at his finger tips bali anayashughulikia kwa wakati muafaka.
Mkuu JK una viporo vingi sana vinavyosubiri majibu yako kama mtu mwenye mamlaka makubwa kuliko watu wote katika nchi hii. Hatuwezi kusubiri hadi utoe hotuba ya mwaka mpya tarehe 31/12/2011 tunahitaji utuambie wewe una solution gani kama rais. Tunataka tuone creativity au maadam wewe tatizo halikuhusu basi tukafilie mbali sisi.
Tunachotegemea sisi ni kwamba rais angekuwa yeye ndo anakula mfupa uliomshinda Ngeleja, Shukuru Kawambwa, Said Mwema, Pinda na mawaziri wengine.
Sasa mkuu wewe unafanya tu vitu vilaini na visivyo vya lazima na kuwaachia mawaziri vitu vyote vigumu bila msaada wowote?. Please JK take your position acha kukwepa majukumu kwani unadhalilisha cheo cha urais na unataka tuamini kwamba urais ni just symbolic na wala huna meno.
Ninavyoona JK unataka kuwa kama mfalme na siyo mtendaji mkuu wa serikali mwenye kufanya maamuzi makubwa na magumu kwa mustakabali wa nchi yetu na haswa watanzania wote.
Kwa ufupi tunashindwa kukuelewa. Kama ulijua urais mgumu kwa nini hukumwachia mtu mwingine basi agombee urais kuliko kutumia Ikulu kama kijiwe cha kupumzikia na kwenda kufanya matembezi ngorongoro, mikutanoni n.k.
Kwa ufupi mkuu JK ni jambo la wazi kabisa unawategea mawaziri na umewasukumia kazi zako zile ngumu na za kuumiza kichwa na za kwao rais ukachukuwa wewe.
Na ndiyo maana ninasema mkuu unaogopa majukumu yanayoumiza kichwa na badala yake unafanya vile vitu vyepesi then unajidai unaongoza nchi.
Hii nchi kwa sasa inajiongoza yenyewe kwa sababu umekimbia kiti na kama ni gari basi brake zimefeli tena likiwa linashuku mlima na hapa hatujui tutaangukia wapi.
Polisi na Mabomu ya machozi ndio mtindo mpya uliobaki wa kuongoza nchi.
Please rudi kwenye kiti uongoze nchi au declare umeshindwa tujue moja ila kwa namna nchi inavyokwenda ni kama haina rais kwa sasa