Rais amchagua Abdala Mtonga kuwa Internal Auditor General

Bila kubadili katiba, tutaendelea kushuhudia uteuzi madudu! Wenzetu wakenya post kama hizi lazima mtu aombe na afanyiwe usaili.
 
Nilitaka kuchangia Kuhusu katibu Mkuu Kiongozi ajae nikamsahau jina nilipo anza kuandika tu Jamaa alikuwa RAS Morogoro majuzi kabla ya kupewa Katibu Mkuu TAMISEMI kabla ya hapo alianzia DED Masasi, anapanda vyeo kwa kasi ya ajabu sana hongera yake.
 
Ndugu zangu watanzania hivi tunachojadili hapa kweli kinaashiria "great thinking". Hatuwezi kweli kujadili sifa za mtu/kiongozi bila kugusia dini yake?

Nchi hii ni ya kila mtu na kuna mamilioni ya wananchi ambao hawaamini katika hizi dini mbili tunazopoteza muda mrefu kuzijadili.

Mimi nadhani huyu IAG anastahili kwa kuzingatia elimu na uzoefu alio nao. Tutampima kwa utendaji wake na siyo dini yake. Na ameteuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Kuhusu uwezo wa raisi na utaratibu uliotumika haya hayamhusu mteuliwa bali ni mfumo wetu wa kikatiba na kisheria.
 
Kuna tetesi zimezagaa kwamba JK amemteua bwana Abdala Mtonga kuwa internal auditor general.

Kama ni kweli nadhani uteuzi wake utakuwa mzuri maana jamaa alikuwa afisa masuhuri wa ofisi ya CAG na pia alikua mkaguzi wa kanda hapo hapo. Ni mtu safi asiyetaka ujinga ujinga kwenye utendaji wa kazi. Tatizo lake ni muoga kufanya maamuzi. Labda anaweza kuleta utofauti kwenye hii ofisi mpya iliyounda

============

Si tetesi tena, ni habari kamili...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amemeteua Bw. Mohammed A. Mtonga (52) kuwa Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali (Internal Auditor General).

Bw. Mtonga ni msomi mwenye Shahada ya Uzamili katika masuala ya Fedha (MSc in Corporate Finance) toka Chuo Kikuu cha Salford nchini uingereza.

Aidha Bw. Mtonga anayo Shahada ya Uhasibu ya CPA (T) inayotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) na Stashada ya Juu ya Uhasibu (Advanced Diploma in Professional Accountancy) toka Chuo cha Jamii Nyegezi ambacho kwa sasa ni Chuo Kikuu cha Mt. Augustine cha Mwanza.

Kabla ya uteuzi huu, Bw. Mtonga amekuwa na utumishi wa miaka 32 katika Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Heasabu ambapo amewahi kushika nyadhifa mbalimbali.

Nyadhifa alizowahi kushika Bw. Mtonga ni pamoja na Afisa Masuuli na Mkaguzi wa Hesabu wa Kanda. Pia amewahi kuwa Mkaguzi wa Hesabu Mkazi katika mkoa wa Lindi, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na Makao Makuu ya Jeshi (Ngome).

Uteuzi huu umeanza toka tarehe 06 Aprili, 2011.

Mbona hawajasema alisoma lini, haswa hiyo Msc? Nafikiria uwezo wake wa kutafsiri hizo IFRS maana experience yake haionyeshi kama alikuwa ana-deal na IFRS - ama nakosea?
 
Mbona hawajasema alisoma lini, haswa hiyo Msc? Nafikiria uwezo wake wa kutafsiri hizo IFRS maana experience yake haionyeshi kama alikuwa ana-deal na IFRS - ama nakosea?


Ama huu ukumbi wakati mwengine ni kichekesho kitupu.

Hivyo ni nani alieteuliwa, ikatolewa maelezo ya anachoweza kufanya?

Na hii Mkuu, wewe itakusaidia nini?

Wacheni hizo.
 
Mbona hamkuyasema hayo Mkapa alipokuwa Raisi, au kwa kuwa alikuwa Mkristo mwenzenu!? Mfumo Kristo Bwana! Mtu anakuwa na Chuki bila sababu kwa sababu rais Muislamu! Nchi hii yetu sote rais akiwa muislamu ataamua kadri ya uwezo wake na akiwa mkristo ataamua kwa kadri ya uwezo wake!:happy:

Mbona yamesemwa sana toka vyama vingi vianzishwe? Tatizo ni mfumo wa katiba yetu unaompa madaraka Rais kuteua kila kitu. Haya ni madai ya muda mrefu ya kumpunguzi Rais madaraka. Tatizo hizo dini zenu mlizorithi( maana hakuna aliyechagua kwa hiali yake kuwa na hiyo dini, inategemeana BABU wa Babu zenu walikutana na nani) zimewapumbaza. Ni ukoloni huo pia.
 
...yangu macho tu, tusubiri utendaji wake ndio tujadili vizuri.

Tusipoipigania katiba kwa nguvu zetu zote,basi huku kote itabaki kupiga domo tu kama kijiwe.
 
mbona wakichaguliwa wakristo sisi huwa hatusemi wala hakuna anayeandika ujinga unaohusiana na dini ya mtu.? kuweni wastaarabu kwani mawaziri na makatibu wakuu wapi ni wengi kati ya waisalm na wakristo? Nachukizwa na udini halafu mtu anajiita great thinker.
 
ha ha eti mbona mkapa aliongozwa na maaskofu watu hawakusema?ni zamu sasa ya mashehe nao kujitanua ikullu
 
Congratulations,

However, I have doubts on his anticipated performance! Sehemu zote alizopita zina madudu yake na kama ni muadilifu angekuwa ashatupwa. Nina uhakika PS na wakubwa wengine walikuwa wanafanya madudu na yeye anayakagua na kupitisha. Ndiyo sababu tuko hapa leo. Anyway, hata kwenye vilaza kuna aliye na afadhali.
 
Jamani, hii nchi siyo ya Waislamu na Wakristo pekee! Sisi tusio kwenye makundi hayo tutakwenda wapi? Idadi yetu inaongezeka kila kukicha kwani Ulokole na U-Ansar Sunna unasababisha wenye vichwa kujiuliza usahihi wa hizi "conventional religions" na hatima ya ubinadamu.
 
Mimi pia nahitaji hiyo sheria kwa kweli maana kama sielewi hivi, kwani Controller and Auditor General (CAG) pia anafanya audit kwa kuwa internal audit ni sehemu ya audit. Nahisi kama hatujuwi tunachofanya hapa sana sana tunazidi kumwongezea mzigo masikini mlipa kodi (nchi hii inaendeshwa kwa PAYE) pasipokuongeza efficiency yeyote kama tulivyofanya kwenye EWURA, SUMATRA na upuuzi mwingine unaofanana na huo.

Ni nani amesema kwamba tatizo letu ni kutokufanyika kwa audit? Hili si kweli kwani kila mwaka CAG anareport upotevu wa mabilioni na hakuna kinachofanyika, reports zake tunaishia kufungia vitumbua Kwamtogole.Tungekuwa serious kufanyia kazi reports na recommendations za CAG wala tusingehitaji ofisi mpya ya internal audit, huu ni upotevu wa pesa usio na sababu.

ndugu naomba nikubaliane nawe japo tupishane kidogo. Profession ya uhasibu imegawanyika sana,kuna kazi ndogo ndogo kuanzia petty cash book management,journal entries n.k mpaka consolided financial statements. Ivi yote haviwezi kuangaliwa na mtu mmoja,hata ikiwa ivo ndo balaa maana uozo utafichuzwa na uyo uyo mmoja. Lakini kwa kuweka checks and balances inakuwa rahisi kumanage fedha. Ni kama kazi za kisheria,haiwezekani kuwe na jaji katika ngazi ya kata au mahakama ya wilaya,huko kuna mahakimu. Sasa na uhasibu uko ivo,ili kupunguza errors CAG anakuwa na wawakilishi kila ngazi ktk ofsi za serikali hasa level ya mkoa,hapa hawa ukagua hesabu za ndani kabisa,na huitwa Internal auditors, hawa wanasimamiwa na Chief Internal auditor,huyu ndo mkuu,ila hawa wote wanawajibika kwa Chief ambaye ni CAG,yan controller and Auditor General. Kwa ivo ivo kazi zaenda. Naomba kusema kuwa hamna kazi isiyogawanyika,huwa kuna Delegation of powers. Hata rais mwenyewe ana wawaziri,msikitini kuna sheikh,imam n.k kanisani kuna askofu mkuu,maaskofu na mapadre/wachungaji,n.k n.k . Nadhan nimejaribu kueleza kwa uwezo wangu. Mwisho tumwombee bwn Mtongo aweze kuwa na maamuzi. Auditing is all about drawing conclusion whether statements show a true and fair view. Ts making a decision. All the best bwn mtonga.
 
Nimeisoma hii thread kwa makini sana nilichokiona ni chuki walionayo Wakristo dhidi ya Waislam sijui kwa nini, mnasema Waislam awajasoma kazi yao kuuza kahawa, akitokea mwenye elimu akachaguliwa mnasema kachaguliwa kwa Uislam wake.
Kweli sasa naweza kuamini ni vigumu kutofautisha Chadema na Kanisa
 
Nimeishoma hii thread kwa makini sana nilichokiona ni chuki walionayo Wakristo dhidi ya Waislam sijui kwa nini, mnasema Waislam awajasoma kazi yao kuuza kahawa, akitokea mwenye elimu akachaguliwa mnasema kachaguliwa kwa Uislam wake.
Kweli sasa naweza kuamini ni vigumu kutofautisha Chadema na Kanisa

we ritizi una matatizo yako,ni wapi na ni mchangia yupi kasema waislam hawakusoma?na nani kaweka neno kunywa/kahawa?? Kweli? Au ndugu unataka kutueleza reality? Aya endelezen chuki na ligi zenu!
 
Wakristo watalalama saaaana kwa sababu walisha zoea kubebwa na kujiona wo ndio wenye haki zaidi a waislam wa tanganyika.

Siku zote wanasahau kuwa nchi ni ya wote na kila mtu ana haki sawa. KUTESA KWA ZAMU , kwani nani mlitesa sana enzi za Nyerere na Mkapa.
 
Back
Top Bottom